Tongue blister
JF-Expert Member
- Jun 19, 2009
- 362
- 11
Nimejaribu kujiuliza lihi swali kila wakati bila kupata majibu yaliyo sahihi , Huwa najiuliza Rais wetu aliwaza nini au huwa anawaza nini pale ambapo huwa teuwa wana jeshi wastaafu kuwa wa wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya ?
Labda kwa ufahamu wangu mdogo mnaweza kunisaidia katika kupata majibu yaliyo sahihi.Tukizingatia pia kwamba wapo pia Vijana wengi wasomi wenye kuijua siasa na wenye uwezo wa kuongoza nchi ndani ya Tanzania wanaishio bila ajira .
Je ni yapi basi mafanikio ambayo tumeyaona yameletwa na viongozi hao shupavu kutoka majeshini ? Na je kuna ukaribu gani ktk ya waheshimiwa hao na wananchi wa kawaida wa kule Geita ama wa Kule Newala mkoani Mtwara ?
Nimejaribu kutazama baadhi ya posts ambazo zimekuwa zikizungumzia maeneo mbali mbali yenye matatizo ya kimaendeleo nikagundua kwamba ukiyafuatilia kwa ukaribu maeneo hayo utaambiwa mbunge wao ni mwana jeshi au mkuu wa wilaya pale ni mwana jeshi au hata Mkuu wa mkoa.
Swali langu ni Je …Rais huwa ana jaribu kufikiri nini katika kuwa Teuwa wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa wana jeshi ?
Labda kwa ufahamu wangu mdogo mnaweza kunisaidia katika kupata majibu yaliyo sahihi.Tukizingatia pia kwamba wapo pia Vijana wengi wasomi wenye kuijua siasa na wenye uwezo wa kuongoza nchi ndani ya Tanzania wanaishio bila ajira .
Je ni yapi basi mafanikio ambayo tumeyaona yameletwa na viongozi hao shupavu kutoka majeshini ? Na je kuna ukaribu gani ktk ya waheshimiwa hao na wananchi wa kawaida wa kule Geita ama wa Kule Newala mkoani Mtwara ?
Nimejaribu kutazama baadhi ya posts ambazo zimekuwa zikizungumzia maeneo mbali mbali yenye matatizo ya kimaendeleo nikagundua kwamba ukiyafuatilia kwa ukaribu maeneo hayo utaambiwa mbunge wao ni mwana jeshi au mkuu wa wilaya pale ni mwana jeshi au hata Mkuu wa mkoa.
Swali langu ni Je …Rais huwa ana jaribu kufikiri nini katika kuwa Teuwa wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa wana jeshi ?