Historia ya vitenge vya wax

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,598
215,331
1572399759769.png


Utamaduni wa kutengeneza vitenge kutumia wax ulianzia Indonesia katika kisiwa cha Java. Vitenge vilitengenezwa kwa kutumia kitambaa cha batiki. Wax ya nyuki ilipochanganywa na rangi za nguo iliimarisha ubora na haikutoka kirahisi hata iliponyeshewa na mvua.
Uzalishaji ulikuwa ni mdogo tu na vitenge vilitengenezwa kwaajili ya viongozi wa makabila na machifu.

Nerthalands ilipoichukua Indonesia kama koloni lake waliona utaratibu huu na kuchukua ufundi huu kuupeleka Holland katika miaka ya 1850. Makampuni yaliyoanzisha uzalishaji kwa mashine ni pamoja na Jean_Baptiste_Theodore_Prévinaire na Peter Fentener_van_Vlissingen. Wafanyabiashara hawa walikuwa na mategemeo ya kuwa uzalishaji wa mashine utatoa mali nyingi itakayoteka soko la Indonesia. Matokeo yalikuwa kinyume na matarajio yao. Walikosa soko kabisa.

Wakati huo huo Nerthalands ilichukua Pwani ya Dhahabu Afrika (The Gold Cost today’s Ghana). Na katika bidhaa ilizipeleka Ghana ni batiki wax print. Bidhaa hii ilipokelewa kwa kasi mno na Africa ilianza kutumia batiki wax kama vazi la kila siku.

Wakati huo Ghana walifuma nguo zao aina ya kente lakini hizi zilifumwa kwa mkono na zilikuwa ni alama ya ma machifu na viongozi wa jadi.

Mwaka 1854 mfalme Willem wa Nerthalands alianzisha kiwanda cha pamba katika mji wa Haarlem katika jitihada za kuokoa idadi ya raia wasio na kazi. Kiwanda hiki kilizalisha Hollandeise wax kwa wingi mno.

Mafanikio ya Wax Hollandeise yaliwavutia wafanyabiashara wengine. Ilikuja Scotish print jina lingine iliitwa English wax na Swiss wax.

Biashara iliposhamiri meli za Nertherland na Scotland zilipeleka vitenge Ghana miaka ya 1870-1930 kipindi hiki Netherland iliajiri watu kutoka Afrika Magharibi kwa wingi katika jeshi lake ili kupigania koloni la Indonesia. Askari hawa walijulikana kama Belanda Hitam. Wachache waliobahatika kurudi kutoka vitani walikuwa na fahari kuvaa suruali na shati la Wax Hollandeise. Belanda Hitam waliongeza umaarufu wa bidhaa hii.

Kitenge kizima ni yadi 12 lakini mauzo ya nusu kitenge yadi 6 hufanyika pia. Yadi sita ndiyo vipande vitabu. Afrika sasa wana viwanda vya kuzalisha vitenge vya wax. Mpaka sasa hivi majina maarufu ya vitenge vya wax ni imiwax, java print, roller print, na Le fancy. Uzalishaji wa kitenge kisicho na wax ni rahisi zaidi.

Vlisco ambayo ilikuwa Vlissingen ndiye mzalishaji mkubwa wa Wax Hollandeise aliyebaki na soko lake kubwa ni Afrika pamoja na Waafrika wanaoishi Ulaya na Marekani. Mwaka 2014 peke yake Vlisco ametengeneza faida ya €million 300.
 
Uzalishaji wa vitenge vya wax sikuhizi umebaki kama zamani ni classic collection. Vitenge vingi vya sikuhizi ni non wax print lakini technologia imeimarika kiasi cha kuwa non wax print ni nzuri tu.

Classic wax huuzwa €50 kwa yadi sita bei ya reja reja

Kuna vya €35

Vingi vya biashashara huuzwa €5, 10, 15, mpaka 20
 
Naomba siku moja atokee mtu anielewesha vitenge vya Kigoma huwa vinatoka wapi.

Bandari ipo Dar, na sio Congo wala Burundi wana kiwanda cha vitenge vya wax. Vitenge vya Kigoma huwa vinatoka wapi?
 
Naomba siku moja atokee mtu anielewesha vitenge vya Kigoma huwa vinatoka wapi.

Bandari ipo Dar, na sio Congo wala Burundi wana kiwanda cha vitenge vya wax. Vitenge vya Kigoma huwa vinatoka wapi?
Vitenge vya Kigoma vinatoka Ghana na Nigeria, wanabiashara kubwa sana na Congo. Kuna mchanganyiko wa Wax Hollandaise na Nigerian Wax pia Ghana ni wazalishaji wakubwa wa vitenge.
 
Vitenge vya Kigoma vinatoka Ghana na Nigeria, wanabiashara kubwa sana na Congo. Kuna mchanganyiko wa Wax Hollandaise na Nigerian Wax pia Ghana ni wazalishaji wakubwa wa vitenge.

Alaaa, hapo nimeelewa. Kama vinatoka Ghana na Nigeria, maana yake mzigo unapita Cameroon, Congo na hatimaye Burundi ndiyo vinaingia Kigoma.

La sivyo vinasafiri kupitia bahari ya atlantic mpaka Congo, then Burundi mpaka Kigoma.


Aiseeee.
 
Alaaa, hapo nimeelewa. Kama vinatoka Ghana na Nigeria, maana yake mzigo unapita Cameroon, Congo na hatimaye Burundi ndiyo vinaingia Kigoma.

La sivyo vinasafiri kupitia bahari ya atlantic mpaka Congo, then Burundi mpaka Kigoma.


Aiseeee.
Mkuu upande ule kuna biashara kubwa inaendelea. Kile kipindi cha miaka 18 ya kufunga mikanda baada ya vita ya Kagera wajanja waliingiza magodoro, shuka , dawa za meno mafuta ya kupikia bila kusahau vitenge kutoka Cameroon, Congo, Uganda mpaka Kagera.

Hii route ya Ivory Cost, kutokea Atlantic ocean inatumiwa na wachuuzi wengi.
 
View attachment 1248516

Utamaduni wa kutengeneza vitenge kutumia wax ulianzia Indonesia katika kisiwa cha Java. Vitenge vilitengenezwa kwa kutumia kitambaa cha batiki. Wax ya nyuki ilipochanganywa na rangi za nguo iliimarisha ubora na haikutoka kirahisi hata iliponyeshewa na mvua.
Uzalishaji ulikuwa ni mdogo tu na vitenge vilitengenezwa kwaajili ya viongozi wa makabila na machifu.

Nerthalands ilipoichukua Indonesia kama koloni lake waliona utaratibu huu na kuchukua ufundi huu kuupeleka Holland katika miaka ya 1850. Makampuni yaliyoanzisha uzalishaji kwa mashine ni pamoja na Jean_Baptiste_Theodore_Prévinaire na Peter Fentener_van_Vlissingen. Wafanyabiashara hawa walikuwa na mategemeo ya kuwa uzalishaji wa mashine utatoa mali nyingi itakayoua soko la Indonesia. Matokeo yalikuwa kinyume na matarajio yao. Walikosa soko kabisa.

Wakati huo huo Nerthalands ilichukua Pwani ya Dhahabu Afrika (The Gold Cost today’s Ghana). Na katika bidhaa ilizipeleka Ghana ni batiki wax print. Bidhaa hii ilipokelewa kwa kasi mno na Africa ilianza kutumia batiki wax kama vazi la kila siku.

Wakati huo Ghana walifuma nguo zao aina ya kente lakini hizi zilifumwa kwa mkono na zilikuwa ni alama ya ma machifu na viongozi wa jadi.

Mwaka 1854 mfalme Willem wa Nerthalands alianzisha kiwanda cha pamba katika mji wa Haarlem katika jitihada za kuokoa idadi ya raia wasio na kazi. Kiwanda hiki kilizalisha Hollandeise wax kwa wingi mno.

Mafanikio ya Wax Hollandeise yaliwavutia wafanyabiashara wengine. Ilikuja Scotish print jina lingine iliitwa English wax na Swiss wax.

Biashara iliposhamiri meli za Nertherland na Scotland zilipeleka vitenge Ghana miaka ya 1870-1930 kipindi hiki Netherland iliajiri watu kutoka Afrika Magharibi kwa wingi katika jeshi lake ili kupigania koloni la Indonesia. Askari hawa walijulikana kama Belanda Hitam. Wachache waliobahatika kurudi kutoka vitani walikuwa na fahari kuvaa suruali na shati la Wax Hollandeise. Belanda Hitam waliongeza umaarufu wa bidhaa hii.

Kitenge kizima ni yadi 12 lakini mauzo ya nusu kitenge yadi 6 hufanyika pia. Yadi sita ndiyo vipande vitabu. Afrika sasa wana viwanda vya kuzalisha vitenge vya wax. Mpaka sasa hivi majina maarufu ya vitenge vya wax ni imiwax, java print, roller print, na Le fancy. Uzalishaji wa kitenge kisicho na wax ni rahisi zaidi.

Vlisco ambayo ilikuwa Vlissingen ndiye mzalishaji mkubwa wa Wax Hollandeise aliyebaki na soko lake kubwa ni Afrika pamoja na Waafrika wanaoishi Ulaya na Marekani. Mwaka 2014 peke yake Vlisco ametengeneza faida ya €million 300.
Interesting
Good to know
 
1572455048117.jpeg


1572455440631.jpeg


Utengenezaji wa Wax Indonesia Java bado ni wa asili wanatumia mikono. Hii ni kazi ya kina mama kama ilivyo kusuka ukili na mikeka Pwani.
 
Back
Top Bottom