Historia ya Aziz Ali

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
21,031
30,372
Utangulizi

Aziz Ali alifariki mwaka wa 1950 miezi michache baada ya kutoka kuhiji Makka. Hata kwa mbali katika maisha yake haikumpitikia kuwa mali aliyoacha nyuma itakuja kutumika katika kupigania uhuru wa Tanganyika kwanza fedha zake zikitumika wakati wa TAA kisha TANU kupitia mwanae wa kwanza Dossa Aziz. Itoshe kusema tu gari alilomnunulia mwanae Nairobi mwaka wa 1947 kama kiliwazo baada ya kukataliwa katika masomo ya urubani kwa kuwa ni mtu mweusi, ndilo Dossa alilitoa kwa TANU mwaka wa 1954 kwa ajili ya kumsaidia Mwalimu Nyerere kufanya kazi zake kwa wepesi.


Aziz Ali

Aziz Ali amekuja Dar es Salaam mwanzo wa Vita Kuu ya Kwanza (1914-1918) akiwa askari katika jeshi la Wajerumani na baada ya vita aliajiriwa na Goa mmoja.

Mwajiri wake alipoondoka nchini alimwachia Aziz Ali gari mbili na hizi ndizo alizokuwa akifanyia biashara hapo mwanzo na kufungua kampuni ya ujenzi akaajiri mafundi.


Aziz Ali akiwa kijana

Kwa hakika jina lake hasa ni Ali Kidonyo.
Hili ndilo jina lake alilojulikana akiwa mtoto na kisha kijana kwao Tanga.

Hili Aziz alipewa na watu wa Dar es Salaam kwa hisani na wema wake.

Yeye alikuwa akitoa fursa kwa watu kumpa pesa kidogo kidogo kama malipo ya nyumba alizokuwa anawajengea na alikuwa mtu akishindwa kulipa akimpa muda hadi atakapoweza.

Nyumbani kwake mwezi Mtukufu wa Ramadhani alikuwa akitandika nje majamvi na kufuturisha hadi watu 100 asiowajua wakija wanafuturu na kuondoka.

Ndipo wakamwita "Aziz" yaani "Mpenzi." Ikawa wakimtaja jina wanatanguliza "Aziz," yaani "Kipenzi chetu Ali."

Kidonyo jina hili la kwao Tanga likafa kabisa.
Aziz Ali alikuwa mcha Mungu sana.

Alikataa kumwanzisha shule mwanae mkubwa Waziri maarufu kwa jina la Dossa hadi kwanza ahitimu Qur'an.

Hii ikapelekea Dossa kuanza shule darasa la kwanza akiwa na miaka 14 akawa darasa moja na Abbas Sykes mdogo wa tatu kwa rafiki yake Abdulwahid Sykes.
 

Attachments

  • IMG-20180330-WA0190.jpg
    IMG-20180330-WA0190.jpg
    31.3 KB · Views: 204
Asante kwa elimu nzuri Shekhe,Mwalim wetu Mohammed Said Ila nna Maswali 3..

1-Dossa alichangiaje uhuru wa tanganyika yaan nlitaka nijue Mchango wake

2- Dossa alikuwa na urafik na Nyerere na alimjuaje?

3-Nyerere baada ya kuwa Raisi wa Tanganyika Je Alimpa uongozi Dossa Azizi? Je alimtambua kwa mchango wake?
Maasalaam
 
Asante kwa elimu nzuri Shekhe,Mwalim wetu Mohammed Said Ila nna Maswali 3..

1-Dossa alichangiaje uhuru wa tanganyika yaan nlitaka nijue Mchango wake

2- Dossa alikuwa na urafik na Nyerere na alimjuaje?

3-Nyerere baada ya kuwa Raisi wa Tanganyika Je Alimpa uongozi Dossa Azizi? Je alimtambua kwa mchango wake?
Maasalaam
Ngoja aje
 
Utangulizi

Aziz Ali alifariki mwaka wa 1950 miezi michache baada ya kutoka kuhiji Makka. Hata kwa mbali katika maisha yake haikumpitikia kuwa mali aliyoacha nyuma itakuja kutumika katika kupigania uhuru wa Tanganyika kwanza fedha zake zikitumika wakati wa TAA kisha TANU kupitia mwanae wa kwanza Dossa Aziz. Itoshe kusema tu gari alilomnunulia mwanae Nairobi mwaka wa 1947 kama kiliwazo baada ya kukataliwa katika masomo ya urubani kwa kuwa ni mtu mweusi, ndilo Dossa alilitoa kwa TANU mwaka wa 1954 kwa ajili ya kumsaidia Mwalimu Nyerere kufanya kazi zake kwa wepesi.


Aziz Ali

Aziz Ali amekuja Dar es Salaam mwanzo wa Vita Kuu ya Kwanza (1914-1918) akiwa askari katika jeshi la Wajerumani na baada ya vita aliajiriwa na Goa mmoja.

Mwajiri wake alipoondoka nchini alimwachia Aziz Ali gari mbili na hizi ndizo alizokuwa akifanyia biashara hapo mwanzo na kufungua kampuni ya ujenzi akaajiri mafundi.


Aziz Ali akiwa kijana

Kwa hakika jina lake hasa ni Ali Kidonyo.
Hili ndilo jina lake alilojulikana akiwa mtoto na kisha kijana kwao Tanga.

Hili Aziz alipewa na watu wa Dar es Salaam kwa hisani na wema wake.

Yeye alikuwa akitoa fursa kwa watu kumpa pesa kidogo kidogo kama malipo ya nyumba alizokuwa anawajengea na alikuwa mtu akishindwa kulipa akimpa muda hadi atakapoweza.

Nyumbani kwake mwezi Mtukufu wa Ramadhani alikuwa akitandika nje majamvi na kufuturisha hadi watu 100 asiowajua wakija wanafuturu na kuondoka.

Ndipo wakamwita "Aziz" yaani "Mpenzi." Ikawa wakimtaja jina wanatanguliza "Aziz," yaani "Kipenzi chetu Ali."

Kidonyo jina hili la kwao Tanga likafa kabisa.
Aziz Ali alikuwa mcha Mungu sana.

Alikataa kumwanzisha shule mwanae mkubwa Waziri maarufu kwa jina la Dossa hadi kwanza ahitimu Qur'an.

Hii ikapelekea Dossa kuanza shule darasa la kwanza akiwa na miaka 14 akawa darasa moja na Abbas Sykes mdogo wa tatu kwa rafiki yake Abdulwahid Sykes.
wachana na mapicha picha ambayo hata wewe ukifa yatakuwa mengi tu japo haimanishi kuwa ndo ukweli na kujitoa.weka ushahidi/document za hivyo vitu alivyokuwa anafanya na sio picha zake kuelezea ngano.
 
wachana na mapicha picha ambayo hata wewe ukifa yatakuwa mengi tu japo haimanishi kuwa ndo ukweli na kujitoa.weka ushahidi/document za hivyo vitu alivyokuwa anafanya na sio picha zake kuelezea ngano.
Lukubuzo...
Adabu ni kitu cha bure.
Unaweza ukaeleza hayo yote kwa lugha ya kistaarabu na uungwana.

Ningependa sana kujua nini kimekughadhibisha kiasi umekuja na shari.
 
Utangulizi

Aziz Ali alifariki mwaka wa 1950 miezi michache baada ya kutoka kuhiji Makka. Hata kwa mbali katika maisha yake haikumpitikia kuwa mali aliyoacha nyuma itakuja kutumika katika kupigania uhuru wa Tanganyika kwanza fedha zake zikitumika wakati wa TAA kisha TANU kupitia mwanae wa kwanza Dossa Aziz. Itoshe kusema tu gari alilomnunulia mwanae Nairobi mwaka wa 1947 kama kiliwazo baada ya kukataliwa katika masomo ya urubani kwa kuwa ni mtu mweusi, ndilo Dossa alilitoa kwa TANU mwaka wa 1954 kwa ajili ya kumsaidia Mwalimu Nyerere kufanya kazi zake kwa wepesi.


Aziz Ali

Aziz Ali amekuja Dar es Salaam mwanzo wa Vita Kuu ya Kwanza (1914-1918) akiwa askari katika jeshi la Wajerumani na baada ya vita aliajiriwa na Goa mmoja.

Mwajiri wake alipoondoka nchini alimwachia Aziz Ali gari mbili na hizi ndizo alizokuwa akifanyia biashara hapo mwanzo na kufungua kampuni ya ujenzi akaajiri mafundi.


Aziz Ali akiwa kijana

Kwa hakika jina lake hasa ni Ali Kidonyo.
Hili ndilo jina lake alilojulikana akiwa mtoto na kisha kijana kwao Tanga.

Hili Aziz alipewa na watu wa Dar es Salaam kwa hisani na wema wake.

Yeye alikuwa akitoa fursa kwa watu kumpa pesa kidogo kidogo kama malipo ya nyumba alizokuwa anawajengea na alikuwa mtu akishindwa kulipa akimpa muda hadi atakapoweza.

Nyumbani kwake mwezi Mtukufu wa Ramadhani alikuwa akitandika nje majamvi na kufuturisha hadi watu 100 asiowajua wakija wanafuturu na kuondoka.

Ndipo wakamwita "Aziz" yaani "Mpenzi." Ikawa wakimtaja jina wanatanguliza "Aziz," yaani "Kipenzi chetu Ali."

Kidonyo jina hili la kwao Tanga likafa kabisa.
Aziz Ali alikuwa mcha Mungu sana.

Alikataa kumwanzisha shule mwanae mkubwa Waziri maarufu kwa jina la Dossa hadi kwanza ahitimu Qur'an.

Hii ikapelekea Dossa kuanza shule darasa la kwanza akiwa na miaka 14 akawa darasa moja na Abbas Sykes mdogo wa tatu kwa rafiki yake Abdulwahid Sykes.
Mkuu Maalim asante kwa simulizi hizi murua, nilikuwa napasikia tuu Mtoni kwa Aziz Ali, sikupata kumjua wala kumsikia mzee huyu!.

Tutafutie na habari za Musa Hassan wa jila la Msasani, na wazee wengine waliolipa jiji letu majina.

P
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom