Hii hapa Ibara ya Katiba ya Tanzania aliyoigusia Lissu mkutanoni. Je, alikuwa sahihi?

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,209
25,548
Ni Ibara ya 99 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Inabeba dhana ya utaratibu wa kutunga Sheria kuhusu mambo ya fedha. Ibara husika ina ibara ndogo 3. Tafadhali someni Ibara hii na mjiridhishe iwapo Wakili Msomi mwenzangu Tundu A.M. Lissu alikuwa sahihi au la kwenye hoja yake ya kuhusu 'mamlaka ya Rais kikatiba na masuala ya kodi/tozo'.

Nainukuu:

99.-(1) Bunge halitashughulikia jambo lolote kati ya mambo yanayohusika na ibara hii isipokuwa kama Rais amependekeza kwamba jambo hilo lishughulikiwe na Bunge na pendekezo hilo la Rais liwe limewasilishwa kwenye Bunge na Waziri.

(2) Mambo yanayohusika na ibara hii ni haya yafuatayo:- (a) Muswada wa Sheria kwa ajili ya lolote kati ya mambo yafuatayo:-

(i) kutoza kodi au kubadilisha kodi kwa namna nyingine yoyote isipokuwa kupunguza;

(ii) kuangiza kwamba malipo au matumizi ya fedha yafanywe kutokana na Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali au mfuko wa Serikali mwingine wowote au kubadilisha kiwango hicho na namna nyingine yoyte isipokuwa kupunguza; Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

(iii) kuagiza kwamba malipo au matumizi ya fedha yafanywe kutokana na Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali au mfuko wa Serikali mwingine wowote wakati ikifahamika kwamba fedha iliyomo katika mifuko hiyo haikupangiwa itolewe kwa ajili ya malipo au matumizi hayo, au kuagiza kwamba malipo au matumizi yanayofanywa kutokana na mifuko hiyo yaongezwe;

(iv) kufuta au kusamehe deni lolote linalotakiwa lilipwe kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano;

(b) hoja au mabadiliko yoyote ya Hoja kwa ajili ya lolote kati ya mambo yaliyoelezwa katika aya ya (a) ya ibara hii ndogo.

(3) Masharti ya ibara hii yatatumika kwa muswada wowote uliowasilishwa kwenye Bunge au Hoja yoyote iliyotolewa katika Bunge na Waziri au Naibu Waziri.
 
Hiyo ibara ya 99 [1] inaonesha vile Rais hastahili kukwepa lawama kuhusu masuala yanayohusiana na kodi, kwasababu yeye ana mamlaka ya kupendekeza analoona ni sahihi, na hilo pendekezo lake kupelekwa bungeni kama taarifa na Waziri husika kujadiliwa.

Hili sote ni mashahidi, kwani tumeona mara kadhaa pale ambapo malalamiko ya tozo yakiwa mengi, Samia humuagiza Mwigulu wakajadili bungeni na kuona namna gani wanaweza kufanya ili kupunguza makali ya tozo kwa mwananchi, mfano wa hili ulitokea hivi karibuni ambapo walipunguza baadhi ya tozo.

Hivyo, kwangu mtu kusema kwamba Rais hatakiwi kulaumiwa kwenye hili napinga, tumeona Rais kwa mamlaka yake anaweza kurekebisha kisheria pale ambapo ataona hapajakaa sawa, lakini akiamua kukaa kimya, basi anafanya hivyo kwa mapenzi yake.
 
Tundu lissu yuko sahihi kabisa. Serikali pekee kupitia waziri ndio inaweza kupeleka muswada wa maswala ya fedha.
Bunge halina uwezo wa kukaa na kufanya hivyo.
 
Ni Ibara ya 99 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Inabeba dhana ya utaratibu wa kutunga Sheria kuhusu mambo ya fedha. Ibara husika ina ibara ndogo 3. Tafadhali someni Ibara hii na mjiridhishe iwapo Wakili Msomi mwenzangu Tundu A.M. Lissu alikuwa sahihi au la kwenye hoja yake ya kuhusu 'mamlaka ya Rais kikatiba na masuala ya kodi/tozo'.

Nainukuu:

99.-(1) Bunge halitashughulikia jambo lolote kati ya mambo yanayohusika na ibara hii isipokuwa kama Rais amependekeza kwamba jambo hilo lishughulikiwe na Bunge na pendekezo hilo la Rais liwe limewasilishwa kwenye Bunge na Waziri.

(2) Mambo yanayohusika na ibara hii ni haya yafuatayo:- (a) Muswada wa Sheria kwa ajili ya lolote kati ya mambo yafuatayo:-

(i) kutoza kodi au kubadilisha kodi kwa namna nyingine yoyote isipokuwa kupunguza;

(ii) kuangiza kwamba malipo au matumizi ya fedha yafanywe kutokana na Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali au mfuko wa Serikali mwingine wowote au kubadilisha kiwango hicho na namna nyingine yoyte isipokuwa kupunguza; Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

(iii) kuagiza kwamba malipo au matumizi ya fedha yafanywe kutokana na Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali au mfuko wa Serikali mwingine wowote wakati ikifahamika kwamba fedha iliyomo katika mifuko hiyo haikupangiwa itolewe kwa ajili ya malipo au matumizi hayo, au kuagiza kwamba malipo au matumizi yanayofanywa kutokana na mifuko hiyo yaongezwe;

(iv) kufuta au kusamehe deni lolote linalotakiwa lilipwe kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano;

(b) hoja au mabadiliko yoyote ya Hoja kwa ajili ya lolote kati ya mambo yaliyoelezwa katika aya ya (a) ya ibara hii ndogo.

(3) Masharti ya ibara hii yatatumika kwa muswada wowote uliowasilishwa kwenye Bunge au Hoja yoyote iliyotolewa katika Bunge na Waziri au Naibu Waziri.
Ushauri, wengi humu JF ni ma layman wa sheria, hivyo nyinyi wenzetu mànguli wabobezi na wabebovu, mkituletea vifungu vya katiba na sheria humu, msiishie to cut and paste tuu, tusaidieni kwa kutufafanulia kwa lugha ya wananchi what does kifungu hicho mean?.
P
 
Ushauri, wengi humu JF ni ma layman wa sheria, hivyo nyinyi wenzetu mànguli wabobezi na wabebovu, mkituletea vifungu vya katiba na sheria humu, msiishie to cut and paste tuu, tusaidieni kwa kutufafanulia kwa lugha ya wananchi what does kifungu hicho mean?.
P
Uko sahihi kabisa,haina maana kama mtu umeona mapungufu kwa jicho la kisheria halafu unakuja kutubwagia kama lilivyo bila kutusaidia sisi maamuma wa sheria nini mapungufu na ilitakiwa iwe vipi.
 
Ni Ibara ya 99 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Inabeba dhana ya utaratibu wa kutunga Sheria kuhusu mambo ya fedha. Ibara husika ina ibara ndogo 3. Tafadhali someni Ibara hii na mjiridhishe iwapo Wakili Msomi mwenzangu Tundu A.M. Lissu alikuwa sahihi au la kwenye hoja yake ya kuhusu 'mamlaka ya Rais kikatiba na masuala ya kodi/tozo'.

Nainukuu:

99.-(1) Bunge halitashughulikia jambo lolote kati ya mambo yanayohusika na ibara hii isipokuwa kama Rais amependekeza kwamba jambo hilo lishughulikiwe na Bunge na pendekezo hilo la Rais liwe limewasilishwa kwenye Bunge na Waziri.

(2) Mambo yanayohusika na ibara hii ni haya yafuatayo:- (a) Muswada wa Sheria kwa ajili ya lolote kati ya mambo yafuatayo:-

(i) kutoza kodi au kubadilisha kodi kwa namna nyingine yoyote isipokuwa kupunguza;

(ii) kuangiza kwamba malipo au matumizi ya fedha yafanywe kutokana na Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali au mfuko wa Serikali mwingine wowote au kubadilisha kiwango hicho na namna nyingine yoyte isipokuwa kupunguza; Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

(iii) kuagiza kwamba malipo au matumizi ya fedha yafanywe kutokana na Mfuko Mkuu wa Hazina ya Serikali au mfuko wa Serikali mwingine wowote wakati ikifahamika kwamba fedha iliyomo katika mifuko hiyo haikupangiwa itolewe kwa ajili ya malipo au matumizi hayo, au kuagiza kwamba malipo au matumizi yanayofanywa kutokana na mifuko hiyo yaongezwe;

(iv) kufuta au kusamehe deni lolote linalotakiwa lilipwe kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano;

(b) hoja au mabadiliko yoyote ya Hoja kwa ajili ya lolote kati ya mambo yaliyoelezwa katika aya ya (a) ya ibara hii ndogo.

(3) Masharti ya ibara hii yatatumika kwa muswada wowote uliowasilishwa kwenye Bunge au Hoja yoyote iliyotolewa katika Bunge na Waziri au Naibu Waziri.
sasa unawezaje kuwa mkuu wa taasisi halafu usiwe na mamlaka ya kufanya hivyo? Hawa jamaa wanataka tuwe na rais ambaye mamlaka yake ni madogo kuliko mamlaka ya MC wa sherehe ya harusi
 
Ibara ya 99 inasema wazi.
Bunge limefungwa mikono katika mambo yote yaliyotajwa isipokuwa tu labda kama Rais ataamua kulishirikisha katika mambo hayo. Kama asipolishirikisha, maana yake limefungwa mikono!
Mfumo wa vyama vingi ni luwa Rais na wabunge wachaguliwe kwa kura, Rais apate mawaziri ndani ya hilo kunde. Ilani ya Uchaguzi ndiyo inayotawala sheria za kutungwa, kwa vile ndiyo iliyowashawishi wapiga kura kuchagua Chama hicho. Iliyoyasema ni sawa na ndivyo inavyotakiwa kuwa. Akitaka hoja yake tundulissu aipeleke kwa Mbunge wake.
 
LISSU ana akili kubwa hata wewe Mselewa unajua hilo. Yuko sahihi maana Rais ndiye anayeweza kuuma na kupuliza. Akiamua kuuma tu hakuna kitu atafanywa maana hakujatolewa room ya Mtu mwingine kuomba rejea. Yaani hata bunge ambalo ndo chombo kikuu cha wananchi lazima lisubiri mapendekezo ya Rais.
 
Ushauri, wengi humu JF ni ma layman wa sheria, hivyo nyinyi wenzetu mànguli wabobezi na wabebovu, mkituletea vifungu vya katiba na sheria humu, msiishie to cut and paste tuu, tusaidieni kwa kutufafanulia kwa lugha ya wananchi what does kifungu hicho mean?.
P
Mbona kaka unajitoa? Halafu, hicho kifungu nilichokiweka hakihitaji tafsiri yoyote ya kisheria...kinajieleza chenyewe. Kukitafsiri ni kutaka kukiharibu. Kwangu mimi, vifungu vya kutafsiriwa ni vile vinavyofanya marejeo kwenye vifungu vingine na hivyo kulazimisha visomwe kwa pamoja.
 
Lisu alikuwa na maana kwamba sheria iliyopitishwa na bunge kuhusu tozo, ni batili kwa sababu waziri wa fedha hakupeleka waraka maalumu wa mhe Rais bungeni na kuusoma kama katiba inavyotaka kufanyika kabla ya sheria kupitishwa
 
Ushauri, wengi humu JF ni ma layman wa sheria, hivyo nyinyi wenzetu mànguli wabobezi na wabebovu, mkituletea vifungu vya katiba na sheria humu, msiishie to cut and paste tuu, tusaidieni kwa kutufafanulia kwa lugha ya wananchi what does kifungu hicho mean?.
P
1. Kwanza mimi namshangaa ndugu Petro E. Mselewa kulileta hili Kwa njia ya swali, kwamba, ".....ibara yenyewe ni hii, nyie mnaonaje?"

2. All in all, ibara iko very clear kwa yeyote kuelewa maana yake hata yule ambaye hajui au kusoma sheria.

Na kwamba mambo ya fedha na Kodi na tozo zote hakuna mtu au chombo kingine chochote (likiwemo Bunge) chenye mamlaka kuamua au kupinga kilichoamuliwa na Rais.

Ndiyo wabunge hawana uwezo wa kuikataa bajeti ya serikali na wakithubutu kufanya hivyo, Rais anafuta au kulivunja Bunge lote kufumba na kufumbua yu

Hii ndiyo mamlaka ya ki - Mungu aliyonayo huyu mtu aitwaye Rais wa Tanzania!
 
Back
Top Bottom