Haya machinjio ya Nyama Wilayani Uyui (Tabora) ni hatari kwa Afya

Nyakijooga

Senior Member
Dec 9, 2018
138
229
Huu ndio muonekano wa maeneo ya kuchinjia vitoweo katika Kata ya Goweko ambapo pia ni kwa ajili ya maeneo mbalimbali ikiwemo Kata ya Nsololo, Wilaya ya Uyui Mkoani Tabora.

Taarifa ninazozijua ni kuwa Serikali ilitoa zaidi ya Shilingi Milioni 25 kwa ajili ya machinjio hayo kwa ajili ya kata hizo mbili tangu Mwaka 2013.

Hadi sasa hakuna kinachoendelea na baadhi ya fedha za mradi zilipigwa, uonekano wa machinjio hizo na kiasi cha fedha ambacho inadaiwa kimetumika ni tofauti, japo viongozi waliopita walijaribu kufatilia ila huwa mambo yanaishia njiani bila kupata suluhisho la suala hilo.

Kutona na hiki unachokiona kwa sasa wauza nyama wanachinjia kwenye eneo la TRC ambapo awali yalikuwa makazi ya Watu, baada ya TRC kuwalipa fidia ili kupisha ujenzi wa Reli ya Kisasa ya SGR.

Eneo hilo wanalofanyia shughuli za machinjio ya Wanyama hakuna mkaguzi anayekagua usalama wa nyama.
WhatsApp Image 2024-05-16 at 09.42.21_f5e09675.jpg

WhatsApp Image 2024-05-16 at 09.42.24_da07347d.jpg

WhatsApp Image 2024-05-16 at 09.42.22_6f6c41c9.jpg


DIWANI AULIZWA
JamiiForums imewasiliana na Diwani wa Kata ya Goweko ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Uyui, Shabani Katalambula anaelezea:

Suala la fedha sina uhakika nako labda aulizwe Mkurugenzi Mtendaji ndio msimamizi wa fedha, mimi nimeingia Udiwani Mwaka 2014 sikuwahi kuona Mradi huo umetengeza fedha.

Ninachokumbuka kwenye miaka ya 2010 kulikuwa na fedha zimetengezwa zinzotokana na mapato ya ndani kama sijakosea.

Pamoja na hivyo kuna changamoto kadhaa ikiwemo ya maji pamoja na kwamba wakati wa ujenzi walikosea upande wa Kibra.

Taarifa nilizozipata kwa miaka hiyo, walipofika Waislamu kuangalia wakagundua kuna hicho changamoto kidogo.

Hivyo, Wachinjaji wanachinja pembezoni mwa eneo hilo, pembeni ya eneo hilo la Machinjio yaliyejengwa

Kuhusu suala la Afya wapo maafisa ambao huwa wanakagua, unajua wafugaji wetu sio wakubwa kama ilivyo wale wa mijini, Halmashauri yetu ya Uyui haijafikia kiwango hicho cha kuwa na machinjio makubwa.

Pia soma - Mradi wa Machinjio ambao hautumiki, DC w Uyui asema wametenga Tsh. 14m hadi 24m kuuboresha
 
Hii Halmashauri nayo ni changamoto .full kufisidi hela za Halmashauri...toka enzi za Nsekela mdogo wa manunuzi+ ufuska kwa waalimu wapya..

Yaani hiyo Halmashauri bila kupata madiwani wa UPINZANI,itaendelea kudidimia
 
Ni kwann serikali isione ipo haja ya kupambana kuweka umakini na nguvu kubwa ktk miradi midg midg inayoanzishwa ktk mazingira ambayo ni kwaajili ya kutoa huduma bora , nasio bora huduma.

Matukio haya yanailazimisha serikali kuja kuzalisha migogoro midg midg mfano mimi mwananchi , ninatafuta uwanja wa kununua mwenyekiti akaona machinjio yanaeneo kubwa sana pasipo kujali kuwa eneo hilo nikubwa coz lipo kwaajili ya kukizi maitaji ya soko kwakokosa huko uelewa, abamega kipande kwa nia nzuri aidha kujenga ofisi za serikali na baadae hupelekea mgogoro baina ya taasisi au watu wanaokinzana katk utekelezaji wa mjukumu.

Muhimu miradi inapoanzishwa ipewe kipaumbele itasaidia sana , sio kuanzisha miradi isiyo kamilika
..
 
Back
Top Bottom