PureView zeiss
JF-Expert Member
- Sep 5, 2016
- 9,332
- 30,681
Afisa mifugo wilayani Handeni mkoani Tanga (Jina lake bado halijafahamika) amefariki dunia baada ya kumgonga ndege aina ya Bundi na pikipiki aliyokuwa akiendesha yenye namba za usajili STM 0232 . Ajali hiyo imetokea asubuhi ya leo Ijumaa, Mei 17 2024 eneo la Sindeni, Handeni jirani na kona ya PRS 2.
Mashuhuda walioshuhudia ajali hiyo wamesema baada ya dereva huyo kumgonga bundi pikipiki yake ilipoteza mwelekeo na kuanguka na dereva huyo kupasuka kichwa. Na bundi huyo baada ya kugongwa alikufa papo hapo.
Mkuu wa wilaya ya Handeni, Albert Msando amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa haamini kama ajali hiyo imetokana na imani za kishirikina.
#CloudsDigitalUpdates
Mashuhuda walioshuhudia ajali hiyo wamesema baada ya dereva huyo kumgonga bundi pikipiki yake ilipoteza mwelekeo na kuanguka na dereva huyo kupasuka kichwa. Na bundi huyo baada ya kugongwa alikufa papo hapo.
Mkuu wa wilaya ya Handeni, Albert Msando amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa haamini kama ajali hiyo imetokana na imani za kishirikina.
#CloudsDigitalUpdates