Halmashauri ya Jiji imeshindwa kumsimamia Mkandarasi kuzoa taka kwa wakati Mitaa ya Kariakoo

BigTall

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
425
1,071

Hili siwezi kukaa nalo lazima niliseme maana alihitaji uelewa zaidi wa kibobezi. Mimi nafanya harakati zangu za kutafuta riziki mitaa ya Kariakoo sasa nina mwaka mmoja na miezi kadhaa lakini kuna jambo naomba nililete hapa jukwaani wana JF tusaidiane kulipazia sauti.

Kama tunavyojua kwenye maeneo ya mikusanyiko kumekuwepo na kawaida ya kuzalishwa taka, hali ambayo inasababisha wasimamizi wa maeneo kuweka utaratibu wa kukusanya taka hizo ili zisilete athari za kiafya kwa wananchi.

Nasikitishwa sana na hali inayoendelea Kariakoo sehemu ambayo ni mlango wa Jiji hata Nchi kwa jumla hususani kwenye sekta ya biashara ili linadhibitishwa na ripoti za Mamlaka ya Mapato (TRA) kuhusu mapato yanayokusanywa.
photo_2024-04-18_07-51-38.jpg

photo_2024-04-18_07-50-44.jpg
Licha ya Halmashauri ya Jiji kuweka Mkandarasi (Kajenjere), lakini anashindwa kutimiza jukumu la kuzoa uchafu kwa wakati kwenye maeneo mengi na kupelekea kero ya harufu kwenye baadhi ya Mitaa.

Lakini kibaya zaidi mkandarasi na Jiji wameshindwa kuweka maeneo rafiki ya kurundika taka zinazozalishwa hususani taka zinazotokana na vyakula.

Kumekuwepo na utaratibu wa wafanyabiasha hususani Mama ntilie ikifika jioni wanachukua uchafu na kuulundika kwenye maeneo ambayo mkandarasi ameyahalalisha kama maeneo rasmi ambapo asubuhi magari ufika kuchukua uchafu huo.

Utaratibu huu unaratibiwa kwenye maeneo yasiyo rafiki ni maeneo ambayo kuna shughuli za kibiashara na tumekuwa tukikumbana na kero maana kuna wakati uchafu huo unaweza kukaa siku hata mbili bila kuzolewa au wakati mwingine watu wanamwaga taka mapema saa 10 muda ambao bado shughuli za kijamii zinaendelea kwenye maeneo hayo.

Hali hii ni kero kubwa kwetu hasa mvua ikinyesha uchafu huo unatoa harufu mbaya huku nzi na wadudu wengine vyote vinakuwa sehemu hizo huku uchafu unaendelea kuzagaa kiholela kwa sababu unarundikwa tu sehemu ya wazi, hali ambayo inaweza kupelekea magonjwa ya mlipuko.

Nasikitika kwa kuwa kila wakati uliowekwa kiutaratibu Watu Kajenjere wanafika kuzoa taka lakini wao hawatupi huduma bora, kama hali itaendelea hivi itafika wakati nasisi tutakuwa wagumu kutoa pesa ya taka maana kuna wakati mteja anataka kuja dukani kwako anaona eneo hilo limezungukwa na uchafu.

Kama Mkandarasi au Jiji wanashindwa kusimamia suala hili mfano kuweka miundombinu rafiki ya wananchi kumwaga taka na kuziondoa kwa wakati bila kupelekea kero kwa wananchi basi hawana kudi kuwajibika kama sio kuwajibishwa maana Kariakoo ni sehemu kwa maendeleo ya Taifa yetu inatakiwa kuwa na mazingira rafiki yanayovutia watu sio kukimbiza watu.
 
Kitu chochote kuwepo sehemu sio mahala pake maana yake ni uchafu, Sasa uwepo wa biashara bila mpangilio tayari unaona maana halisi, hivyo ni vigumu sana kupata mazingira ya usafi kariakoo!! Cha muhimu sasa ni utashi wa kisiasa na mengine yafuaye!! Kwanza uongozi wa mkoa ujue maana ya uchafu na waanzie hapo kufanyia kazi
 
Hata kuchanga inayokusanywa inaachwa muda mrefu, hasa pale mtaa wa uhuru na nyamwezi
 
Tatizo wakazi wenyewe ni wachafu mno!! Nadhani umasikini na uchafu vinaenda pamoja.
Hakuna wakazi Kariakoo. Wachafuzi wakubwa wa mazingira ni wafanyabiashara wa mitaani waliohalalishwa na serikali.

Pili kasi ya usafi haiendani na msongamano mkubwa wa watu, magari, vitoroli,bajaji na bodaboda.

Uzembe wa Manispaa na uongozi wa mitaa kutosimamia usafi wa mazingira. Wenyewe wanawahi kupanga fremu kila sehemu wazi.
 
Hakuna wakazi Kariakoo. Wachafuzi wakubwa wa mazingira ni wafanyabiashara wa mitaani waliohalalishwa na serikali.

Pili kasi ya usafi haiendani na msongamano mkubwa wa watu, magari, vitoroli,bajaji na bodaboda.

Uzembe wa Manispaa na uongozi wa mitaa kutosimamia usafi wa mazingira. Wenyewe wanawahi kupanga fremu kila sehemu wazi.
Kwani shida ya uchafu kwa Dar ni kariakoo tu?!! Mitaa yote tu isipokuwa sehemu chache wanakoishi wenye kipato cha kati na juu.
 
Wanatakiwa waweke large garbage bins kwa ajili ya kukusanya taka...ikifika jioni gari liwe linapita kubeba
 
Back
Top Bottom