DP World kuanza mchakato wa kuajiri, Wafanyakazi wa TPA wadaiwa kutakiwa kuchagua kwenda DPW au kubaki TPA

Hakuna haja ya kupanick wafanyakazi hicho ni kitu cha kawaida
Mashirika yote ya umma huwa na mikataba ya hali bora na wafanyakazi kupitia mabaraza yao ya wafanyakazi inayoainisha endapo kutatokea ajira kusimama au retrenchment mfanyakazi atalipwa nini na huwa sio siri iko wazi

Mwekezaji mpya akija aweza sema nachukua wafanyakazi wote au baadhi tu hawa ndio nitaendelea nao kwa mikataba mipya ila haruhusiwi.kuwashusha mishahara akiwachukua.Atakaokataa kuwachukua huachia kampuni yao wajue watawafanyaje kama hawana pa kuwapeleka huwataka wanaotaka kuondoka kwa hiari waandike barua kuondoka na malipo huwa makubwa kuliko akisubiri kustaafu kawaida

Kampuni binafsi wazoefu kwenye hili hasa za mafuta kila siku mwekezaji mpya huja utasikia leo kampuni inaitwa Caltex kesho anakuja mwekezaji mpya inaitwa BP keshokutwa inauzwa anakuja mwekezaji mwingine anaitwa Puma kila akija mpya mikataba ya wafanyakazi husainiwa upya anaowataka mwekezaji mpya asiowataka wanalipwa Chao wanaendelea na maisha.mengine Sema watu wa mashirika ya umma wanaona kitu kigeni lakini kitu cha kawaida sana akija mwekezaji mpya kampuni binafsi
 
20240322_193338.jpg
 
Mkuu mbona tangazo lipo wazi au mimi ndio sielewi? Huwezi kuwa mtumishi wa serikali halafu hapo hapo ukawa mtumishi wa DPW. Mumishi anachagua abaki TOA au aende DPW na huo ndio utaratibu na hao watumishi wamepewa elimu na muda wa kuchakata suala hili tangu mapema sana.

Kwa ninachofahu na nilichoelewa ni kuwa Ukiamua kwenda DPW utapewa terminal benefits zote kisha unaajiririwa DPW ambapo huko ni private sector na tunajua huko hakuna mbambamba ni kazi kwa kwenda mbele tofauti na serikalini ambako hata uharibu vipi basi unaangaliwa au watakuhamisha kitengo. Lakini private sector huwa wapo strictly.

Sasa hapo ni uamuzi na uchaguzi wa mwajiriwa mwenyewe abaki au aende lakini hakuna aliyetimuliwa wala kulazimishwa kuchagua atakacho
Bandari imekuwa kama Simba SC Wana Makolo 🐼
 
Kwahyo hakutakuwa na wajiriwa wapya??
Wanakuwepo critical areas
Ujue wawekezaji wakija huja na teknolojia mpya ambazo huhitaji wanaozijua na serikali haiwezi kubali waje nao wakati watanzania wapo wanaozijua wakati TPA ilikuwa ikiendeshwa teknolojia za zamani hawakuhitaji vijana wajua teknolojia mpya

Aliyesoma mfano computer technology miaka ya 1980 huwezi linganisha na aliyesoma computer technology na kumaliza digrii mwaka jana Wa mwaka jana yuko more current na yuko advanced kuliko obsolete technology ya TPA iliyopo hivyo wataajiri vijana wapya

Pili wa marketing wengi wa TPA mfano wamesoma kingereza tu na digrii za kingereza tu hawana third language kama kifaransa .Soko la TPA liko hadi Central Africa nchi ya kongo ambako lugha kuu kifaransa
Definitely wataajiri watanzania vijana wapya marketing officers wenye digrii za marketing lakini wanajua kifaransa kwa ajili ya kuwa marketing officers wao soko la Kongo tofauti na TPA ambayo ilikuwa haijali hilo kuwa na maafisa masoko wajua kifaransa ambako kuna wateja wengi mizigo ipitayo bandarini

Wapya wataajiriwa wala sio siri.Kuna maeneo wafanyakazi wa TPA waliopo hawawezi enea hata wajitutumue vipi
Degree zao na uzoefu wao haywezi fit kwenye teknolojia za kisasa na utendaji wa kibiashara za kimataifa wa kisasa uletwao na DP World

Mfano Dp world ni kampuni ya kimataifa Auditor na wahasibu wakuu lazima wawe na certification za kimataifa ili wakisaini document wanahisa wa DP World wawe na confidence ya kuanzia mhasibu mkuu au mkrugenzi wa fedha sio awe na Sifa za CPA ya Tanzania awe mhasibu au Auditor wanatakiwa wenye certification za kimataifa kama ACCA nk sio CPA (T) International shareholders wa kampuni yeyote ya kimataifa huhitaji wenye certification za kimataifa.Na wapo na serikali haiwezi kubali waajiri wa nje wakati Tanzania wapo.TPA ilikuwa haiwahitaji hao wenye certification za kimataifa .Hiivyo ajira mpya zitakuwepo

Watanzania wenye sifa za kimataifa ajira zitakuwepo nyingi vitengo vyote iwe IT ,uhasibu,masoko,procurements,Engineering,Port operations etc wataajiri tu hawana ujanja
 
Wale waliokuwa wakitetea kuwa DP World wakija hawatapunguza watu kazi njooni hapa mtueleze. Jamaa ndio wameishauziwa taratibu wanaanza kuondoa watu. Kiko wapi?

---
Tarehe 22 Oktoba, 2023 Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) iliingia Mkataba na Kampuni ya DP World ya Falme ya Dubai unaohusu uendeshaji wa Gati Na. 0 hadi 3 na Gati Na. 4 hadi 7 za Baridari ya Dar es Salaam kwa kipindi cha miaka thelathini (30). Kutokana na makubaliano hayo yanayohusisha usimamizi na uendeshaji wa maened tajwa, Watumishi wa Bandari ya Dar es Salaam wanapaswa kuchagua kati ya kubaki TPA au kusitisha mkataba wa ajira wa TPA na papo hapo kuajiriwa upya na Kampuni ya DP World.

Menejimenti imekamilisha zoezi la utoaji elimu kwa Watumishi wote wa TPA walio kwenye maeneo husika lililoanza Tarehe 4 hadi 19 Machi, 2024 kwa lengo la kuwapa Watumishi wote uelewa sahihi wa mabadiliko ya uendeshaji yanayoendelea Bandari ya Dar es Salaam. Pamoja na masuala mengine, elimu hii inahusisha mabadiliko ya uendeshaji wa bandari, utaratibu wa makabidhiano, utaratibu wa mtumishi kusitisha mkataba na TРА па раро hapo kuajiriwa upya na Kampuni ya DP World (KWA MTUMISHI ATAKAYEKUWA AMEAMUA KUFANYA HIVYO KWA HIYARI YAKE MWENYEWE BILA KUSHURUTISHWA), pamoja na stahiki ambazo zitatolewa na TPA kwa mtumishi atakayeamua kusitisha mkataba wa ajira wa TPA na kuajiriwa upya na Kampuni ya DP World.

Kwa msingi huo, nawajulisha Watumishi wa Bandari ya Dar es Salaam kuwa, makabidhiano kati ya TPA na Kampuni ya DP World yameanza kutekelezwa. Kwa kuwa zoezi la utoaji elimu kwa Watumishi limekamilika, Watumishi watakaoamua kuajiriwa upya na Kampuni ya DP World wanatakiwa kufika na kuorodhesha taarifa zao Jengo la TPA Makao Makuu, Ukumbi wa Mikutano Ghorofa ya 32 kabla au ifikapo Tarehe 29 MACHI, 2024.
Sijaona anaeondolewa, au huelewi ulichokibandika?
 
Back
Top Bottom