DCI Boaz vipi, Mbona amekimbia kesi ya Mbowe?

HPAUL

JF-Expert Member
Jan 18, 2011
410
567
Leo upande wa mashtaka umefunga ghafla kesi ya ugaidi inayowahusu washtakiwa wanne akiwemo Freeman Mbowe.

Katika hali ya kushangaza shahidi muhimu ambaye akitajwa karibu kila siku na mashahidi wa upande wa serikali DCI Boaz hajaitwa mahakamani kutoa ushahidi.

Ikumbukwe huyu ndiye aliyepokea taarifa kutoka kwa Luteni Urio, juu ya kuwepo mipango ya ugaidi, na yeye aliye andaa mpango kazi wa awali wa kesi hii. Boaz alitakiwa kuja kuieleza mahakama ni kwa jinsi gani aliiona hii kesi ni ya ugaidi, alitakiwa kuunga mkono ushahidi wa Urio na kuthibitisha kwamba kweli Urio alifika ofisini kwake, maana hapo Kuna utata mkubwa, alitakiwa kuieleza mahakama ni kwa Nini alikubali mpango wa kuharibia maisha makomandoo watatu ambao walikuwa na kazi zao, warubuniwe na Urio kwamba Kuna kazi ya ulinzi VIP kumbe wanatumbukizwa shimoni na kubambikiwa ugaidi, kifupi bila Boaz kutoa ushahidi muunganiko wa kesi nzima unakosekana.

Hii haijatokea kwa bahati mbaya, pengine hii kesi ni mchongo hivyo kumleta DCI mahakamani na kudhalilishwa siku 3 mfululizo ni Kibatala itakuwa ni aibu kwa taifa, lakini majibu mazuri zaidi wanayo upande wa mashtaka.
 
Hii kesi ni bora tu Jamhuri wakakubali matokeo. Kiukweli wameshindwa vibaya! Maana kila anayekuja kutoa ushahidi, anaondoka akiwa hoi bin taaban!

Na yote hii ni kwa sababu ya ukosefu wa uhalisia wa mashtaka yenyewe!
 
Kama Jaji akijifanya hamnazo na akaamua kuwa hawa watu wanne "WANA KESI YA KUJIBU"...

Basi, iwe isiwe, wote waliokwepa kuja kutoa ushahidi kuthibitisha makosa ya washitakiwa kama waleta mashitaka [Jamhuri], then wajiandae kuwa mashahidi wa upande wa utetezi....

That means, hawajakikwepa kizimba cha mahakama. Na hata chief Hangaya kupitia kwa AG wake ajiandae kuja kujibu maswali kizimbani....

Mpaka hapo, one can easily predict what would be maamuzi sahihi ya Jaji Tiganga siku ya Ijumaa tarehe 18/2/2022 yatakuwaje...

To cut it short, ni kuwa, THE GAME IS OVER....!!
 
Ukweli ni kwamba baada ya Mbowe juzi kwenda pekee yake ofisi ya jaji pamoja na mawakili wa pande zote ndio hii kesi ilipoenda kumalizwa!!!
Kama Jaji akijifanya hamnazo na akaamua kuwa hawa watu wanne "WANA KESI YA KUJIBU"...

Basi, iwe isiwe, wote waliokwepa kuja kutoa ushahidi kuthibitisha makosa ya washitakiwa kama waleta mashitaka [Jamhuri], then wajiandae kuwa mashahidi wa upande wa utetezi. Which means, hawajakikwenda kizimba cha mahakama. Hata chief Hangaya kupitia kwa AG ajiandae kuja kujibu maswali kizimbani....

Mpaka hapo, one can easily predict what would be maamuzi sahihi ya Jaji Tiganga siku ya Ijumaa tarehe 18/2/2022 yatakuwaje...

To cut it short, ni kuwa, THE GAME IS OVER....!!
 
Wa Kwanza Kuna mtu anaitwa Dikison Matata anakugonga za ugoko alafu anaondoka,wa pili anaingia Mtobeswa anaku chanachana anaondoka,watatu anakuja msafisha njia wa bwana mista Malya Sasa huyu anakupaka. Grisi kila mahali unalainika Kama beringi Mwisho anaingia mzee wa kazi mheshimiwa Kibatala mtoto wa Dr Kibatala pale St Fransis fundi wakutumbua mishipa huyu ndio anakumalizia.
 
Ukweli ni kwamba baada ya Mbowe juzi kwenda pekee yake ofisi ya jaji pamoja na mawakili wa pande zote ndio hii kesi ilipoenda kumalizwa!!!
Likely, Yes...

Na mambo mengine ni huko Ubelgiji aliko Chief Hangaya kwa sasa na Tundu Lissu....

Wenye akili tunaelewa vizuri sana what's going on "behind the closed doors" si kwa kesi hii tu ya Mbowe bali kwa mambo mengi ya nchi yaliyoharibiwa na Mwendazake John Pombe Magufuli...!

Hiyo siyo "coincidence". Bali ni mpango mzima ulio kamili.
 
Wa Kwanza Kuna mtu anaitwa Dikison Matata anakugonga za ugoko alafu anaondoka,wa pili anaingia Mtobeswa anaku chanachana anaondoka,watatu anakuja msafisha njia wa bwana mista Malya Sasa huyu anakupaka. Grisi kila mahali unalainika Kama beringi Mwisho anaingia mzee wa kazi mheshimiwa Kibatala mtoto wa Dr Kibatala pale St Fransis fundi wakutumbua mishipa huyu ndio anakumalizia

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app

Kweni Kibatala ni mtoto wa Dr Kibatala aliyewahi kuwa St Francis Ifakara?
 
Sijui kwanini tunakubali kuhadaika kiurahisi hivi hiyo kesi haiwezi kuisha kiurahisi hivyo mark my words hawa watu watafungwa tu ingawaje ni ukweli mchungu ila watafungwa hii kesi imekaa vibaya hawawezi tumia gharama kubwa then wawaachie kiurahisi hivyo
Serikal huwa inapoteza sana tu. Tofauti ni kwamba watuhumiwa watakaa muda mrefu sana hadi serikal ije ikubali kunyanyua mikono juu si leo
 
Sijui kwanini tunakubali kuhadaika kiurahisi hivi hiyo kesi haiwezi kuisha kiurahisi hivyo mark my words hawa watu watafungwa tu ingawaje ni ukweli mchungu ila watafungwa hii kesi imekaa vibaya hawawezi tumia gharama kubwa then wawaachie kiurahisi hivyo
Hii kesi sitaki iishe maana kwenye committal utetezi wanewaweka, Sirro,Sabaya, na AG, wasipofuta tunao hao
 
Back
Top Bottom