Kyenyabasa
JF-Expert Member
- Mar 8, 2023
- 248
- 712
Mimi si mwanasiasa ila ni Mtanzania ninayenufaika na siasa. Kwa umri wangu mdogo, nimeona vyama vingi vikifa ikiwemo CUF, chama ambacho nilikipenda sana, ila baadaye nikaanza kuvutiwa na smartness ya Chadema, ingawa si mwanachama.
Kwa mtazamo wangu, Chadema imejengwa kwenye msingi imara sana, hivyo si rahisi kuiangusha. Kuhusu maridhiano, naunga mkono kwa sababu harakati bila mazungumzo zinaweza zisikupatia kile unachostahili, hasa kama yule unayepambana naye ana nguvu nyingi pia.
Kwa hali ilivyo, maridhiano yakizaa katiba mpya, basi Mbowe, anayebezwa, atakumbukwa miaka mingi mbele, na hiki ndicho wahafidhina wengi ndani ya CCM na Chadema hawataki kitokee, kwa sababu kitainyanyua sana jina la Mbowe. Mengine yote yasemwe, ila maridhiano ni kete muhimu sana.
Chadema ni watundu mnooo huwezi kuwameza kirahisi, ndio maana nimewafananisha na msumari wenye kutu. Hawa watu ni wahuni, huwezi kuwaua kirahisi. Maslahi ya Chadema na CCM yabaki kwanza chini, ila ya Tanzania yetu yawekwe mbele.
Hongera Samia na Mbowe.
Kwa mtazamo wangu, Chadema imejengwa kwenye msingi imara sana, hivyo si rahisi kuiangusha. Kuhusu maridhiano, naunga mkono kwa sababu harakati bila mazungumzo zinaweza zisikupatia kile unachostahili, hasa kama yule unayepambana naye ana nguvu nyingi pia.
Kwa hali ilivyo, maridhiano yakizaa katiba mpya, basi Mbowe, anayebezwa, atakumbukwa miaka mingi mbele, na hiki ndicho wahafidhina wengi ndani ya CCM na Chadema hawataki kitokee, kwa sababu kitainyanyua sana jina la Mbowe. Mengine yote yasemwe, ila maridhiano ni kete muhimu sana.
Chadema ni watundu mnooo huwezi kuwameza kirahisi, ndio maana nimewafananisha na msumari wenye kutu. Hawa watu ni wahuni, huwezi kuwaua kirahisi. Maslahi ya Chadema na CCM yabaki kwanza chini, ila ya Tanzania yetu yawekwe mbele.
Hongera Samia na Mbowe.