KERO Barabara ya Kwa Barikiwe - Kinzudi ni kero, najiuliza wasimamizi walisinzia wakati kinamwagwa kifusi

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,323
5,493
Barabara ya Kwa Barikiwe - Kinzudi ni kero, najiuliza wasimamizi walisinzia wakati kinamwagwa kifusi cha gadeni tena kipindi hiki cha mvua?

Hali ya Barabara Africana njia ya kuanzia kwa "Kwa Barikiwe" kuelekea Kinzudi ni mbaya mamlaka zitusaidie hata kukwangua matope maana ni kero kwelikweli sio kwa watembea kwa miguu bali hata wenye magari, Bajaji, pikipiki na Watumiaji wote tunapata tabu.

Kero hii imechangiwa na waliomwaga udongo wakituaminisha ni kifusi, lakini ukweli usemwe, kilichowekwa sio kifusi cha kuweka kwenye barabara ya aina hiyo, kile ni kifusi cha gadeni (bustani) maana udongo mtupu.

Kifusi hicho kimemwagwa kwenye kipindi hiki cha mvua, najiuliza wahusika walikuwa wanalenga nini, ni kweli barabara hiyo ilikuwa na changamoto ya mashimo lakini ndio watuwekee kifusi cha aina hiyo? Hivi Mbunge na wasaidizi wake ikiwemo Diwani hawalioni hili jamani!

Kuna ambao kabisa tumepaki magari, maana watu tokea juzi magari yanaharibika yakipita kwenye njia hiyo, Wafanyabiashara wa maeneo ya juu Kinzudi wanapata changamoto kupata mizigo, Wanafunzi wetu hasa wanaosoma Shule ya Msingi Kinzudi na wengine wanapata tabu, bodaboda na Bajaji wameanza kupandisha bei wengine wanasitisha ruti badala yake wanashusha abiria kwa Barikiwe Center kutokana na ubovu wa barabara hiyo, jambo ambalo ni kero.

Hali hii ikiendelea hivi mambo yatazidi kuwa mabaya, hatua zichukuliwe, Viongozi wawajibike kutuwezesha kuwa na mazingira Bora ya kupita.

photo_2024-04-18_15-09-37.jpg

kIC.jpg

KKKKKKK.jpg

KKKKK.jpg

KKKK.jpg
 
Sisi wapiga Kura ndio wajinga tuandamane kuwaondoa hawa wahuniiiiii,anzeni pale mtaani kwenu
 
Mkuu wa mkoa, mkuu wa wilaya, mwenyekiti wa serikali za mitaa, mbunge, diwani na tarura wapo wanaangalia tu.

Nchi yetu sote, lakini matatizo yanapotokea wao hawaonekani. Wako busy na tozo, huku barabara zinawashinda kutengeneza.

Hizi kero zimekua nyingi kila mahali, but no body cares about it.
 
Nchi yetu ina ufala mwingi sana,hapo linaweza kupita greda tu,sifa zote zikaenda kwa Mama 😀
 
TARURA iangaliwe upya kabisa, sijui kwanini wanaweka udongo uletao matope kwenye barabara nyingi hasa za Dar, hii imekuwa ni hatari sana kipindi cha mvua sbb barabara hizo hufa na kuwa matope mabaya sanaaaaa, na TARURA wako wanaona, na sio mara ya kwanza wanaweka udongo mbaya sana tena clay soil kabisa na mvua zikinyesha barabara hizo hazifai, ni bora wasiweke vifusi kabisa ila wachonge na kuweka mitaro tu

TARURA waangaliwe upya, kuna hatari barabara zote wakaua kwa matope, soil type wanazoweka ni udongo haufai kabisa, bora wachonge tu barabara waache hivyo na waweke mitaro pembeni ya hizo barabara.. na hii ndio sbb barabara zingine zikiwekwa lami, zinakatika kwa chini wakati wa mvua au hubonyea sbb ya udongo mbovu
 
Back
Top Bottom