Adhabu ya Kunyonga Hadi Kufa imepitwa na wakati?

SA, hapo kwenye red unakusudia kusema nini? Hiyo rule inaanzia wapi? Pengine hii ni mojawapo ya 'chicken-egg' dilema...wapi haki hiyo ya kuishi inaanzia - kwa muuwaji au kwa aliyekwisha uwawa? Kama tukisema haki ya kuishi haiwezi kunyang'anywa.....je wanaonyang'anya wenzao haki hiyo wafanywe nini?
Muuaji na aliyuawa wanahaki ya kuishi. Kwa sheria ilivyo sasa anayenyang'anya mwenzie haki hiyo naye ananyang'anywa.Sasa hii inasidia nini?
 
Muuaji na aliyuawa wanahaki ya kuishi. Kwa sheria ilivyo sasa anayenyang'anya mwenzie haki hiyo naye ananyang'anywa.Sasa hii inasidia nini?
Kwa sheria ilivyo sasa anayemnyang'anya mwenzie haki hiyo kinyume cha sheria na yeye ananyang'anywa haki hiyo kisheria. Hili kwa kiasi fulani linaleta sense of justice kwa wale waliopoteza mpendwa wao. Pia kwa kiasi fulani linapunguza watu kujichukulia sheria mikononi mwao na pia mauwaji ya visasi.
 
Ningekuwa katika nafasi nzuri ya kuchangia iwapo tu, miongoni mwetu atanifafanulia swali hili; Ni vipi haki ya kuishi ya mtu aliyeuwawa makusudi na "mwendawazimu" flani itazungumzwa katika lugha ya kueleweka ilhali tunampa muuaji nafasi ya kuishi no matter kazi zipi atafanya akiwa kifungoni ilhali yupo hai?
 
Kwa sheria ilivyo sasa anayemnyang'anya mwenzie haki hiyo kinyume cha sheria na yeye ananyang'anywa haki hiyo kisheria. Hili kwa kiasi fulani linaleta sense of justice kwa wale waliopoteza mpendwa wao. Pia kwa kiasi fulani linapunguza watu kujichukulia sheria mikononi mwao na pia mauwaji ya visasi.

Kaka, kwa kuleta relief kwa waliompoteza mpendwa wao inawezekana na wakati mwingine haitokei (hilo siwezi liongelea sana)Lakini hii ya kusema eti itapunguza kuchukua sheria mkononi sidhani. Kuna wimbi la matukio ya kusikitisha sana sasa hivi, mtu kaiba kuku basi anapigwa mawe mpaka afe, kaiba simu ya kitochi hali kadhalika!

Bado unadhani hukumu ya kifo imesaidia? (as a matter of fact its not enforced......why???)
 
Ningekuwa katika nafasi nzuri ya kuchangia iwapo tu, miongoni mwetu atanifafanulia swali hili; Ni vipi haki ya kuishi ya mtu aliyeuwawa makusudi na "mwendawazimu" flani itazungumzwa katika lugha ya kueleweka ilhali tunampa muuaji nafasi ya kuishi no matter kazi zipi atafanya akiwa kifungoni ilhali yupo hai?
Issue inakuja kama kweli unadhani kufa kwake huyu muuaji kutasaidia kurudisha haki ya aliyemuua sababu kama ameua watu kumi je yeye kufa kifo kimoja ni sawa na wale kumi aliyowauwa?, na je unadhani kifo ndio adhabu kubwa kwa huyu mtu?, kifo ingekuwa ni adhabu basi wote mwisho wa siku tutapata hii adhabu sababu hakuna atakaebaki hai maisha
 
Kwa sheria ilivyo sasa anayemnyang'anya mwenzie haki hiyo kinyume cha sheria na yeye ananyang'anywa haki hiyo kisheria. Hili kwa kiasi fulani linaleta sense of justice kwa wale waliopoteza mpendwa wao. Pia kwa kiasi fulani linapunguza watu kujichukulia sheria mikononi mwao na pia mauwaji ya visasi.
Kwahiyo una-advocate an eye for an eye.., ukitaka mtu mkono na wewe ukatwe mkono? huoni kwamba hapa jamii itapata hasara badala ya kilema mmoja basi watakuwa na vilema wawili?, huoni kwamba ingefaa zaidi kama huyu aliyekata mkono afanyishwe kazi na matunda ya kazi zake yaweze kumtunza aliyemdhuru?
 
Hii issue ni ngumu sana, mara nyingine huwa nakaa nafikiria naona kama adhabu ya kifo sio nzuri, kwa sababu mhusika anaponyongwa kimsingi waliodhurika na matendo yake hawapati chochote na yeye pengine anaweza asipate nafasi ya kujifunza na kujuta kwamba nilichokifanya hakikuwa sawa, lakini mara nyingine unafikiri unaona kuna watu akili zao ni mboovu na adhabu yao ni hiyo hamna kitu kingine, mfano majambazi wanaovamia na kuua labda familia nzima watu kama hao unadhani utawafanyaje?


Adhabu ya kifo ni sawa kwa mtu aliyeua kwa makusudi,na ukweli ni kuwa adhabu hiyo haitekelezwi mara moja kama adhabu ya kifungo,ni lazima mtu aliyehukumiwa kunyongwa akae kwa muda gerezani ili apate adhabu ya kisaikolojia kwanza itakayomfanya a repent before his/her execution ( Hii ni nafasi ya kujifunza kwa mnyongwaji).Mambo mengine yote haya sijui haki ya kuishi ni propaganda tu za wanaharakati,kwa nini kama hivyo muuaji hakuzingatia haki hiyo? Mimi naona the punishment should fit the crime committed.

Mtuhumiwa anaponyongwa kijamii ni faraja kuwa katendewa haki kwa mujibu wa kosa alilotenda, ndugu wa aliyeuawa pia watafarijika ingawa hakuna manufaa ambayo ni material.Ukweli ni kuwa hadi mahakama inatoa adhabu ya kunyongwa inakuwa imejiridhisha,ingawa si kweli kuwa kila inapotoka adhabu hiyo mtuhumiwa kaua kweli wakati mwingine ni kutopata utetezi mzuri wa kumnasua kwenye tuhuma. Mwisho wauaji waendelee kupunguzwa ili tuwe na jamii ya wapenda haki.
 
Adhabu ya kifo ni sawa kwa mtu aliyeua kwa makusudi,na ukweli ni kuwa adhabu hiyo haitekelezwi mara moja kama adhabu ya kifungo,ni lazima mtu aliyehukumiwa kunyongwa akae kwa muda gerezani ili apate adhabu ya kisaikolojia kwanza itakayomfanya a repent before his/her execution ( Hii ni nafasi ya kujifunza kwa mnyongwaji).Mambo mengine yote haya sijui haki ya kuishi ni propaganda tu za wanaharakati,kwa nini kama hivyo muuaji hakuzingatia haki hiyo? Mimi naona the punishment should fit the crime committed. Mtuhumiwa anaponyongwa kijamii ni faraja kuwa katendewa haki kwa mujibu wa kosa alilotenda, ndugu wa aliyeuawa pia watafarijika ingawa hakuna manufaa ambayo ni material.Ukweli ni kuwa hadi mahakama inatoa adhabu ya kunyongwa inakuwa imejiridhisha,ingawa si kweli kuwa kila inapotoka adhabu hiyo mtuhumiwa kaua kweli wakati mwingine ni kutopata utetezi mzuri wa kumnasua kwenye tuhuma. Mwisho wauaji waendelee kupunguzwa ili tuwe na jamii ya wapenda haki.

Kama ni faraja au la hii ni debatable alafu Kifo ni adhabu kubwa?, nani ambae hatakufa..., hii ni njia ya sisi wote na ni kwamba huyu anatangulia nadhani kuna adhabu ambazo zinatesa zaidi ya kifo
 
Kaka, kwa kuleta relief kwa waliompoteza mpendwa wao inawezekana na wakati mwingine haitokei (hilo siwezi liongelea sana)Lakini hii ya kusema eti itapunguza kuchukua sheria mkononi sidhani. Kuna wimbi la matukio ya kusikitisha sana sasa hivi, mtu kaiba kuku basi anapigwa mawe mpaka afe, kaiba simu ya kitochi hali kadhalika! Bado unadhani hukumu ya kifo imesaidia? (as a matter of fact its not enforced......why???)
Nilikuwa na maana kama jamii inaamini ni haki kwa aliyeuwa makusudi kunyongwa, wauwaji wakipewa 'adhabu' tofauti na kifo, jamii itaacha kutumia mahakama kupata haki hiyo na hivyo watu kujiamulia wenyewe. Kimsingi sikubaliani na watu kuuwawa kiholela kwa makosa kama wizi wa simu nk lakini vitendo hivyo ni dalili tosha kuwa kwa kiasi fulani jamii imepoteza imani na justice system.
 
Kama ni faraja au la hii ni debatable alafu Kifo ni adhabu kubwa?, nani ambae hatakufa..., hii ni njia ya sisi wote na ni kwamba huyu anatangulia nadhani kuna adhabu ambazo zinatesa zaidi ya kifo

Suala la kuwa nani hatakufa si hoja hata kidogo.Jiue mwenyewe si kumuua mtu mwingine, Inaelekea ujawahi kumuona mtu aliyehukumiwa kunyonga anavyopata mateso ya kisaiokolojia ni mateso makubwa kuliko unavyofikiria wewe. Adhabu ya kifo ni adhabu kubwa zaidi ndio maana inaitwa Capital Punishment.
 
Kwahiyo una-advocate an eye for an eye.., ukitaka mtu mkono na wewe ukatwe mkono? huoni kwamba hapa jamii itapata hasara badala ya kilema mmoja basi watakuwa na vilema wawili?, huoni kwamba ingefaa zaidi kama huyu aliyekata mkono afanyishwe kazi na matunda ya kazi zake yaweze kumtunza aliyemdhuru?

Uchumi...Ndio maana pale mwanzo nikasema suala hili inategemea unaliangalia kutokea upande gani! Aliyedhurika yupi?

Mfano, wewe una watoto wawili wadogo say below 7yrs, siku mmoja unarudi home unakuta mwendawazimu mmoja kwa sababu zake amewachinja wanao wote na zaidi kambaka mkeo....say ukawa na subra ya kutafuta haki mahakamani, hiyo adhabu unayoisema haiwezi kuwa relevant kwako kwa sababu wewe huwategemei watoto wako kiuchumi. Labda katika mfano huu wewe kama muathirika ni adhabu gani ungeona muafaka?
 
Uchumi...Ndio maana pale mwanzo nikasema suala hili inategemea unaliangalia upande gani! Aliyedhurika yupi? Mfano, wewe una watoto wawili wadogo say below 7yrs, siku mmoja unarudi home unakuta mwendawazi mmja kwa sababu zake amewachinja wanao wote na zaidi kambaka mkeo....say ukawa na subra ya kutafuta haki mahakamani,hiyo adhabu unayoisema hawezi kuwa relevant kwako kwa sababu wewe huwategemei watoto wako kiuchumi. Labda katika mfano huu wewe kama muathika ni adhabu gani ungeona muafaka?

Mimi siungi mkono adhabu ya kifo. Na pia ni mzazi. Nina binti mdogo. Ninampenda kuliko hata maisha yenyewe. Sasa siku mtu aje aniulie kinyama binti yangu....sina shaka kabisa kuwa nitabadili mtazamo wangu kuhusiana na suala hili.

Jitu hilo yaani liendelee kuishi, kuhema na kupumua na kula wakati mwanangu hataweza kupata tena fursa hiyo? Mweh! Ngumu sana kuikubali hiyo hali.

Kwa hiyo wakati mwingine inategemea, kama mtu hujawahi kuuliwa kinyama yule umpendaye kikwelikweli nadhani unaweza ukawa na mtazamo tofauti kabisa. Subiri yakukumbe ndo utaweza kuwa na ile niitayo 'a balanced perspective on the issue'.
 
kiiman ni hukumu nzito lkn sheria zetu wanaadam hutunga kwa kutojal saana iman bali zinaangalia maslah ya nchi zetu lkn cku zote kifo hakimuadabishi mtu,anaefanya makosa cku zote anapaswa kupewa adhabu itajayomfanya ajutie alichokifanya adhabu ziko nyingi na ni kali mno
 
kiiman ni hukumu nzito lkn sheria zetu wanaadam hutunga kwa kutojal saana iman bali zinaangalia maslah ya nchi zetu lkn cku zote kifo hakimuadabishi mtu,anaefanya makosa cku zote anapaswa kupewa adhabu itajayomfanya ajutie alichokifanya adhabu ziko nyingi na ni kali mno

Unajuaje kama hizo adhabu nyingine zitamfanya ajutie maovu yake? Atakuambia kuwa najuta kumuua fulani na fulani? Au?
 
Uchumi...Ndio maana pale mwanzo nikasema suala hili inategemea unaliangalia kutokea upande gani! Aliyedhurika yupi? Mfano, wewe una watoto wawili wadogo say below 7yrs, siku mmoja unarudi home unakuta mwendawazimu mmoja kwa sababu zake amewachinja wanao wote na zaidi kambaka mkeo....say ukawa na subra ya kutafuta haki mahakamani,hiyo adhabu unayoisema haiwezi kuwa relevant kwako kwa sababu wewe huwategemei watoto wako kiuchumi. Labda katika mfano huu wewe kama muathirika ni adhabu gani ungeona muafaka?

Mkuu first of all Justice... Hakuna Justice ambayo itakuwa equivalent na maisha ya unayempenda kwahiyo kwangu mimi sitajisikia vizuri au haueni kwa mtu aliyenitendea mabaya kunyongwa au kifo chake..na kwangu mimi kunyongwa kwangu mimi kufanya hivi ni kumfanya huyu mtu akimbie hukumu yake na suffering. Pia nina uhakika mtu anaweza akapata punishment kubwa zaidi akiwa hai kuliko kunyongwa ambayo inakatisha suffering..

Kuhusu kufanya watu wapunguze maovu sababu ya kuogopa kosa hii ilishaonekana kwamba sio kweli angalia a following extract from wikipedia

[h=3]The deterrence issue[/h]Supporters of the death penalty often cite deterrence as a reason to keep or reinstate the punishment.[SUP][citation needed][/SUP] However, a study comparing Hong Kong, a city-state without the death penalty, and Singapore, a city-state that uses the death penalty frequently and swiftly, and has a similar culture and murder rate to Hong Kong, found no evidence that Singapore's death penalty deterred crime relative to Hong Kong.
 
Jitu hilo yaani liendelee kuishi, kuhema na kupumua na kula wakati mwanangu hataweza kupata tena fursa hiyo? Mweh! Ngumu sana kuikubali hiyo hali.

Kwa hiyo wakati mwingine inategemea, kama mtu hujawahi kuuliwa kinyama yule umpendaye kikwelikweli nadhani unaweza ukawa na mtazamo tofauti kabisa. Subiri yakukumbe ndo utaweza kuwa na ile niitayo 'a balanced perspective on the issue'.

Depends na perspective ya mtu mwingine anaona kumuua huyu mtu ni kumpa adhabu ndogo sababu labda angeumia zaidi kwa kupata kifungo, kazi ngumu na mateso... . Na kama wewe in that instant ukimkuta anafanya hayo mauaji na ukamuua hata sheria haitakuhukumu(wala hakuna mtu atakaekulaumu) sababu unaweza ukasema sababu ya hasira na passion ulikosa ile mens rhea (guilty mind) kwahiyo hautahukumiwa kwa mauaji..., ingawa baada ya muda kupita hio itakuwa ni revenge...,

Alafu hio ya kusubiri yakukumbe ndio utoe hukumu hapo hautatoa views ambazo ziko balanced sababu utakuwa unasukumwa na motive za revenge.
 
kumwadhibu anayekuwa ametenda kosa, lakini pia ni kutoa funzo kwa wanaobaki, wajue kuwa kosa fulani lina implication fulani, and let me tell you broda, it works out!

Mkuu baada ya kufanya research kidogo nimeona kwamba it does not work angalia extract hapo chini:-

Is not a deterrent; crime rates have not gone down.
In fact, the murder rate in the US is 6 times that of Britain and 5 times that of Australia. Neither country has the DP. Texas has twice the murder rate of Wisconsin, a state that doesn't have the DP. Texas and Oklahoma have historically executed the most number of DR inmates, yet in 2003 their state murder rates increased, and both have murder rates higher than the national average.
 
Depends na perspective ya mtu mwingine anaona kumuua huyu mtu ni kumpa adhabu ndogo sababu labda angeumia zaidi kwa kupata kifungo, kazi ngumu na mateso... . Na kama wewe in that instant ukimkuta anafanya hayo mauaji na ukamuua hata sheria haitakuhukumu(wala hakuna mtu atakaekulaumu) sababu unaweza ukasema sababu ya hasira na passion ulikosa ile mens rhea (guilty mind) kwahiyo hautahukumiwa kwa mauaji..., ingawa baada ya muda kupita hio itakuwa ni revenge...,

Kwa kweli mimi mtu atakayeniulia mwanangu sidhani kama naye anastahili kuendelea kuhema, kupumua, kula na kushiba na kunya. Ikiwa juu yangu kuamua adhabu yake basi itakuwa ni kifungo cha miaka kadhaa (michache sana) kikiambatana na kazi ngumu halafu kifuatiwe na yeye kuuliwa tu kwa sababu hastahili kuendelea kuishi na kuvuta oksijeni ya bure.

Alafu hio ya kusubiri yakukumbe ndio utoe hukumu hapo hautatoa views ambazo ziko balanced sababu utakuwa unasukumwa na motive za revenge.

Sasa yakiwa hayajakukumba ndiyo utakuwa huna hata msingi wa opinions zako kuhusiana na adhabu hiyo. Na usifikiri kila aliyeuliwa mpendwa wake huunga mkono hii adhabu. Wengine bado huendelea kuipinga. Ndiyo maana nikasema, yakishakukuta hata ukitoa maoni kuhusiana na adhabu angalau unakuwa unaongea kwa mamlaka fulani. Iwe unaunga mkono au kupinga. Usije shangaa wewe sasa unaipinga lakini pindi mpendwa wako atakapouliwa kinyama ukajikuta unabadili kabisa mawazo yako.

Trust me, this is an extremely personal issue, sensitive, and touchy.
 
Sasa yakiwa hayajakukumba ndiyo utakuwa huna hata msingi wa opinions zako kuhusiana na adhabu hiyo. Na usifikiri kila aliyeuliwa mpendwa wake huunga mkono hii adhabu. Wengine bado huendelea kuipinga. Ndiyo maana nikasema, yakishakukuta hata ukitoa maoni kuhusiana na adhabu angalau unakuwa unaongea kwa mamlaka fulani. Iwe unaunga mkono au kupinga. Usije shangaa wewe sasa unaipinga lakini pindi mpendwa wako atakapouliwa kinyama ukajikuta unabadili kabisa mawazo yako.

Mkuu there is a good reason kwanini polisi hawaruhusiwi kupeleleza kesi zinazowahusu au daktari kumfanyia operation mtu wa karibu sana na yeye..., Sababu hata decision na maamuzi yao yatakuwa calculated na yatakuwa tofauti na ingekuwa otherwise..., Kwahiyo kama sasa hivi naona death penalty haifai takuwa sipo sawa kubadilisha mawazo yangu itakapo-work against me.... Au unaona its okay tuwaachie watu waliotendwa ndio watunge sheria.....?

Inabidi maamuzi yetu yawe regardless kwamba yamenikuta mimi au sio mimi na yasiwe driven by emotions and revenge..,
 
Adhabu ya kifo ni sawa kwa mtu aliyeua kwa makusudi,na ukweli ni kuwa adhabu hiyo haitekelezwi mara moja kama adhabu ya kifungo,ni lazima mtu aliyehukumiwa kunyongwa akae kwa muda gerezani ili apate adhabu ya kisaikolojia kwanza itakayomfanya a repent before his/her execution ( Hii ni nafasi ya kujifunza kwa mnyongwaji).Mambo mengine yote haya sijui haki ya kuishi ni propaganda tu za wanaharakati,kwa nini kama hivyo muuaji hakuzingatia haki hiyo? Mimi naona the punishment should fit the crime committed. Mtuhumiwa anaponyongwa kijamii ni faraja kuwa katendewa haki kwa mujibu wa kosa alilotenda, ndugu wa aliyeuawa pia watafarijika ingawa hakuna manufaa ambayo ni material.Ukweli ni kuwa hadi mahakama inatoa adhabu ya kunyongwa inakuwa imejiridhisha,ingawa si kweli kuwa kila inapotoka adhabu hiyo mtuhumiwa kaua kweli wakati mwingine ni kutopata utetezi mzuri wa kumnasua kwenye tuhuma. Mwisho wauaji waendelee kupunguzwa ili tuwe na jamii ya wapenda haki.

Kujifunza maana yake nini? Mimi nadhani unajifunza upate ufahamu ili uutumie kwa maisha ya baadaye, sasa kama atajifunza halafu anaenda kunyongwa huko kujifunza kunamsaidia nini?
 
Back
Top Bottom