Abidjan: Omba Omba wapigwa Marufuku ili Kupambana na Fujo za Mjini

Dalton elijah

JF-Expert Member
Jul 19, 2022
216
478
1712255570273.jpg


Jiji kuu la Ivory Coast, Abidjan limetangaza kupiga marufuku ombaomba ili kupambana na "fujo za mijini".

"Ili kupambana na fujo za mijini, biashara za kutembea kwenye barabara kuu, kuombaomba kwa namna zote, na matumizi ya mikokoteni sasa yamepigwa marufuku rasmi katika wilaya nzima," alisema naibu gavana Vincent N'cho Kouaoh katika taarifa kwa AFP siku ya Alhamisi.

"Hatua hii inalenga kuboresha hali ya maisha ya watu, kuhakikisha usalama wa watu na mali, na kuboresha ufanisi wa polisi na kazi zao," alisema.

Mwanzoni mwa Machi, gavana wa Abidjan, Ibrahim Cisse Bacongo, alisema "anachukia vitu fulani" kama "wafanyabiashara wa kutembea" na "ombaomba" na alitaka "kupata njia mbadala".

Mwaka 2013, Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamed Bakayoko, alipiga marufuku kuombaomba kwenye makutano ya barabara lakini alishindwa kudhibiti tukio hilo.

Marufuku ya hivi karibuni imekuja baada ya kuondolewa kwa wingi wa ombaomba wa maeneo hatarishi na mitaa ya mabanda huko Abidjan.

Kulingana na Taasisi ya Taifa ya Takwimu, idadi ya watu wa Abidjan iliongezeka kutoka milioni tatu hadi
milioni sita kati ya mwaka 1998 na 2021.

Chanzo: Trt Swahili.
 
Back
Top Bottom