Hapo anatakiwa atafute tiba tu hakuna namna.Huwezi kuugua malaria ukajitibu kwa kulala kwenye neti,hutapona.Bamia zinasaidia kutokupata tatizo na sasa tatizo ameshalipata,kwa hiyo lazima ajitibu apone halafu ndiyo aendelee na huo utaratibu,vinginevyo atamaliza magunia bila kupona.
Ndiyo.Unaposema presha maana yake chanzo kikuu huwa ni kwenye moyo.Moyo wenyewe pamoja na mishipa yake mikuu inayotoa ama kuingiza damu kwenye moyo pamoja na mishipa mingine midogomidogo inayosambaza damu sehemu mbalimbali za mwili.Vyote hivi vinatakiwa kuwa kwenye utimamu wake,vinginevyo kasoro...
Madhara ya pombe ni makubwa sana kuliko wengi wanavyofikri.Mimi niko kwenye tiba kwa miaka kadhaa sasa,magonjwa mengi yanayowasumbua watu ni yale ya mtindo wao wa maisha ikiwemo unywaji wa pombe kupindukia.
Wewe unayedharau na kupuuza ujumbe huu ambao umekufikia bure kabisa bila malipo ni wazi...
TAMBUA UNYWAJI SAHIHI WA POMBE
Kitu cha msingi kwenye pombe siyo kujua aina ya beer au kilevi. Kitu cha msingi ni kujua percentage of pure alcohol (asilimia ya pombe halisi) na ujazo wake ( volume).
Unit moja ya pombe ni sawa na 10mls of pure alcohol or 8g of the same. Mwanaume hutakiwa kunywa...
Na hii ndiyo sababu kubwa hasa ya vijana wengi kuwa na kisukari. Asilimia ndogo sana ambayo inapata kisukari cha kurithi, lakini asilimia kubwa ni ulaji wa hivyo vitu ulivyovianisha. Kuna uhusiano mkubwa sana wa mlundikano wa mafuta mwilini na kisukari aina ya pili(type 2 diabate).
Ulaji wa vyakula vya mafuta kupindukia,jambo linalosababisha mafuta mengi mwilini na unene kupindukia.
Mambo haya huambatana na ugonjwa wa sukari ambao zamani uliwaandama watu wenye umri angalau miaka 50.
Lakini siku hizi mtu anakuwa na unene uliozidi akiwa na miaka michache.
Kwa historia ya muda ulioanza kupata shida hiyo,kuna uwezekano mkubwa ukawa na ugonjwa wa mifupa(Osteoporosis) ambao umeshindwa kuutibu muda mrefu na sasa umeendelea kujijenga na hatimaye unaonyesha kuwa limekuwa tatizo kubwa.Ugonjwa huu una sifa ya kupungua kwa molekuli ya mfupa na kuzorota kwa...
Namna ambavyo watu hutumia madawa kujitibu ni kama vile kutumia nyundo kubwa kuua buibui.Siku hizi watu wengi wananunua madawa kutoka katika maduka ya dawa bila kuwaendea wataalamu wa afya waliobobea.Wakati mwingine madawa ya kawaida kwenye maduka ya dawa yanaweza yasiwe mazuri na hata kuwa na...
UGONJWA WA BARIDI YABISI NI NINI?
Baridi yabisi ni neno la jumla kwa magonjwa au michakato mingine isiyo ya kawaida itokeayo kwenye viungo. Mamilioni ya watu ulimwenguni kote wanaugua aina fulani ya baridi yabisi.
Viungo vyetu na mishipa yetu, kama ilivyo misuli yetu, hudhoofika kadiri...
Dawa zipo tena za uhakika,isipokuwa wagonjwa wengi wanapenda kutapeliwa.Mfumo wa tiba una kanuni zake,haijalishi ni mitishamba.Mtu ana tatizo la miaka mitano lakini anataka atumie dawa siku mbili apone kweli!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.