Wewe!Yupi umemficha kati yao?
Punguza stress mkuu.Hii ilishapostiwa muda humu, idelete bwana mkubwa. Unatujazia server tu.
Yanga na Pacome wasingeweza kuacha hiyo fursa ya kuitwa kwa mara ya kwanza ndiyo maana ishu ikabuma wakaona we nenda tu hii nafasi ni adimu.
Ni klabu yenyewe iliyosema ameenda kuangaliwa na madaktari wa timu ya taifa, wewe hilo linakuingia akilini kweli mchezaji anaitwa kwa mara ya kwanza, tena anaitwa baada ya mwingine kuachwa kutokana na kuwa majeruhi, halafu aende kuangaliwa majeraha yake? Kama alikwenda akiwa majeruhi basi mliwadanganya kuwa yuko fit kiafya ili fursa isimpite, vyovyote iwavyo kuna udanganyifu ulifanyika.
Mengine nitakujibu baadae nikitulia.
Washamba sana utopolo.Mikwara.wanadhani mamelodi wanaingizwa mjini kwa cheap politics kama hizi,kesho mkijichanganya mechi inaishia hapahapa kwa mkapa
Ili kuwa proffesional alipaswa kuzungumza katika tone gani kufikisha ujumbe kuwa baadhi ya wachezaji hawajawasili?Kocha ana utoto sana hayo sio maneno ya kuongea kwenye press kubwa kama hiyo..
Yanga inaonekana kituko na uongozi was yanga unaonekana ni mbovu kuwai kutokea
Inawezekana kaulizwa swali, na pia inawezekana kuulizwa kwa hilo swali nae akatumia nafasi ya kucheza mind game.Kocha ana utoto sana hayo sio maneno ya kuongea kwenye press kubwa kama hiyo..
Yanga inaonekana kituko na uongozi was yanga unaonekana ni mbovu kuwai kutokea
Ni sahihi ni mind game, ingekuwa kweli hawapo asingeliongelea kabisa. Hayo maneno ya mind game na ukizingatia kocha wa Mamelod kamzungumzia Aziz Ki kama mchezaji hatari.Mi nimetafsiri kama mind game, siamini kama viongozi wanaweza kurusu Diarra na Aziz Ki wasiwe sehemu ya mchezo wa kesho, itakuwa hatuko serious na hizo national team, viongozi kuruhusu waende games za kirafiki wakati tuna mechi muhimu
Hata mm nimetafsiri hivyoNi sahihi ni mind game, ingekuwa kweli hawapo asingeliongelea kabisa. Hayo maneno ya mind game na ukizingatia kocha wa Mamelod kamzungumzia Aziz Ki kama mchezaji hatari.
Niachie basi, utaniua 🙈Wewe!
kwakweli nimemsikiliza kwa makini na amekata tamaa kabisa gamondi,nami pia nishakata tamaaStephen Aziz Ki na Djigui Diarra bado sijawaona kambini na walipaswa kuwa wamerejea kutoka kwenye majukumu yao ya timu zao za taifa”
- Kocha Miguel Gamondi, Yanga Afrika.
Yapi maoni yako??
Umetumia akili na nguvu nyingi kumjibu na kumuelewesha huyo dunduka empty set,hana anachokijua anaendeshwa kwa hisia na udaku ndio maana MO na kikundi chake wakina Jaribu Tena na Mangungu wanawachezea 5imba watakavyo.Mbona umeandika uongo na maelezo yaliyojaa hisia zako?
Yanga wangetaka wachezaji wao wasiitwe kwenda kwenye timu zao za taifa wangetoa statement kwenda kwenye hizo timu kuwa wachezaji wake hawawezi kwenda na hata wangezingizia majeruhi. Kwani kwa akili yako walioitwa wote walienda? Si kuna wachezaji wa vilabu vingine wameitwa na hawakuenda na sababu ikiwa majeraha. Hivyo hata kwa Pacome na wengineo Yanga wangetaka wasiende wangetoa taarifa kuwa Pacome ni majeruhi na hakuna kitu wangefanywa na hizo nchi.
Kuhusu kuvaa jezi za Mamelod aliyekataa ni waziri wako wa michezo na hakukataa za Mamelod pekee bali za timu zote za pinzani (Al Ahly na Mamelod) je wewe ulimsikia kiongozi gani wa Yanga akikataza?
Kuhusu Diarra na Aziz Ki kutofika kama ni kweli bado, huwa inatokana na mazingira magumu ya ndege kuja Tanzania.
Kuhusu majeruhi, pengine mchezo wa mpira umeanza kufatilia juzi hapa. Mchezaji kupona jeraha ni swala moja ila kuwa fit ni swala lingine. Kocha alichokiongelea hapo ni ishu ya fitness ya mchezaji kucheza kwenye ngumu. Nyie mnawaona tu uwanjani Aucho yupo mazoezini au Pacome yupo mazoezini na wenzake ila je anatimamu wa asilimia mia? Hilo ndilo linaloongelewa na kocha.
Kuwa mwanamichezo, sio kila mara unakuwa unatawaliwa na akili za kishabiki shabiki hata kufanya reasoning inakushinda