Matajiri wakubwa Tanzania si wafanya biashara bali ni wanasiasa, viongozi wa serikali na ndugu zao, kuonyesha kwamba kuna kitu hakipo sawa

Sasa mkuu mtu kudhamin kampen za uraisi unadhani alikuwa hana hela?
Halafu hio ya kudhamin vyama au kampen ipo dunia nzima, kuanzia USA hadi andora, ni kawaida, usishangae kaka, dunia sio fair play ground, lazima kuna kuviziana kwa hapa na pale,
Sijasema dunia ni fair play wala sijasema kudhamini kampeni alikuwa hana hela. Mbona hujajibu kwanini Rais mstaafu Obasanjo alikuja kutatua mgogoro wa kiwanda cha Dangote?

Kwanza unalinganishaje Marekani wakati wadhamini wa Marekani ni kisheria inatambulika na mgombea anataja amepokea kiasi gani kutoka kwa nani. Wakati kwa Dangote na Obasanjo ni makubaliano binafsi sio kisheria.

Nilichosema ni kwamba biashara za Kiafrika zina mkono wa kisiasa, hapa unapinga kisha unasema Bakhresa alipewa ekari alime sukari kisa "ana uwezo". Tena mtu huyohuyo alipewa NMC miaka ya nyuma. Kampuni ya Mayanga Construction kipindi cha Magufuli ilikuwa inapewa tenda za ujenzi za fedha nyingi hadi inazidiwa, napo utasema "ina uwezo". Magufuli kafa na kampuni hatuisikii.

Kikwete alipoondoka kampuni ya Home Shopping Centre ikafunga biashara, wakati enzi za Kikwete ilikuwa inapiga hela sana. Hutaki kuelewa unakomaa wote hao wana uwezo.
 
Hapo unashindwa kutofautisha sera za kiuchumi za serikali na uamuzi binafsi wa kisiasa kwa biashara.

Hao Huawei vs Apple ni sera za kiuchumi za nchi zao kulinda data na kubaki na teknolojia muhimu ya mawasiliano. Hao kina Ambani na Tata Group ni sera za nchi India wana Make in India Initiative, mwanasiasa hafanyi single picking ya mtu na kumpendelea. Hao Tata waliisaidia India kwenye teknolojia ya nyuklia na kuunda silaha nyingi za kijeshi, sio ajabu wao kulindwa sababu hata upinzani wa maana pale India haina, ikipotea ni hasara kwa nchi. Ila ni ajabu kwa serikali kuchagua muuza mchele mmoja kati ya 20 na kumpa haki ya kuagiza kutoka nje yeye tu.

Bakhresa kupewa eka zote hizo sio shida. Kama aliweza kupewa kiwanda cha National Milling kuzalisha unga anashindwaje kupewa eneo azalishe sukari. Ndio siasa zenyewe ninazosema.
Fuatilia hio India unayosema haina picking up ya wanasiasa, Fuatilia ufalme wa Jio unavyowekwa na wanasiasa,

Huawei haikuwa kulinda data wala blabla, ingekuwa kulinda data wangeifungia kutumika USA, Kwanini waliiwekea vikwazo vya kuiua kabisa?

Same kwenye nchi zetu, kingine, hakuna utajiri wa huruma, et tumtoe mtu nanjilinji aje tumpe kiwanda mjini aendeleze, hapana, utajiri ni connection, utajiri ni kuchangamkia fursa, utajiri sio siasa kwamba uanze kulalamika sijui kwenda kwenye mikutano sijui nn, utajiri ni lobbying zinazofanywa kwenye vyumba vya siri,

Mengine yote ni kutafuta justification, india nenda tofauti na serikali kama una hela umeisha,
USA biden anamnyima tender za EV Elon Musk kisa wanatofautiana, inabidi ujue utajiri ni mgumu, ni kumtumia yeyote aliye mbele yako, awe mwanasiasa au lah,

Utajiri sio wa kugawana kama chai, ni ujanja ujanja, na kupiga kazi sana kwa maarifa

Hakuna mbinu nyingine, tukiendekeza siasa za cdm kwamba ccm ndo wametuzuia tusiwe matajiri, nakuahidi, hata tuwaweke cdm nao wataendelea hivi hiv tu
 
Sijasema dunia ni fair play wala sijasema kudhamini kampeni alikuwa hana hela. Mbona hujajibu kwanini Rais mstaafu Obasanjo alikuja kutafuta mgogoro wa kiwanda cha Dangote?

Nilichosema ni kwamba biashara za Kiafrika zina mkono wa kisiasa, hapa unapinga kisha unasema Bakhresa alipewa ekari alime sukari kisa "ana uwezo". Tena mtu huyohuyo alipewa NMC miaka ya nyuma. Kampuni ya Mayanga Construction kipindi cha Magufuli ilikuwa inapewa tenda za ujenzi za fedha nyingi hadi inaheremewa, napo utasema "ina uwezo". Magufuli kafa na kampuni hatuisikii.
Kikwete alipoondoka kampuni ya Home Shopping Centre ikafunga biashara, wakati enzi za Kikwete ilikuwa inapiga hela sana. Hutaki kuelewa unakomaa wote hao wana uwezo.
Usiseme biashara za Africa, hio ipo dunia nzima,
Siasa zinaplay part, kuanzia USA mpaka China mpaka Andora,

Usiwalaumu wafanya biashara,
France wamemuahidi Elon $1B kama ataenda jenga kiwanda ufaransa, umeona sasa, that is how world work, just live with it or be killed with it
 
Fuatilia hio India unayosema haina picking up ya wanasiasa, Fuatilia ufalme wa Jio unavyowekwa na wanasiasa,
cdm kwamba ccm ndo wametuzuia tusiwe matajiri, nakuahidi, hata tuwaweke cdm nao wataendelea hivi hiv tu
Kwahiyo mkuu unanipinga kwamba utajiri hauna mkono wa kisiasa au unaniunga mkono. Maana nilichosema unakataa, ila maelezo yako yanakikubali.
 
Usiseme biashara za Africa, hio ipo dunia nzima,
Siasa zinaplay part, kuanzia USA mpaka China mpaka Andora,

Usiwalaumu wafanya biashara,
France wamemuahidi Elon $1B kama ataenda jenga kiwanda ufaransa, umeona sasa, that is how world work, just live with it or be killed with it
Hakuna sehemu nimelaumu wafanyabiashara mzee. Nimeelezea kinachotokea, wewe unakomaa ku-sugarcoat uhalisia kwa kuuita "uwezo".

France kumpa Musk $1 billion sijasikia, ila hata wakimpa wana faida kama nchi. Kiwanda cha Tesla kikichopo Ujerumani kitagharimu $4 za ujenzi tu. Bado faida ya kodi na ajira. Hapo France ikitoa $1 inakuwa ni investment, uchumi huo.

Na bado huo sio mfano sahihi na Obasanjo & Dangote. Kama Ufaransa ingemwambia Musk njoo ujenge kiwanda alafu tutapiga marufuku mshindani wako kuuza bidhaa kama zako, au tutakutoza kodi kiduchu kuliko wapinzani wako hapo ndio ingekuwa mfano sawa na Dangote & Obasanjo.
 
Nakuunga mkono,
Ila nataka ufute kauli ya Africa, useme utajiri duniani una mkono wa wanasiasa
Nikisema duniani nitataja hata nchi zisizousika. Duniani nchi nyingine zina mahakama independent za usuluhishi wa kibiashara huwezi waletea huo ujinga wa kumchagua fulani auze unga wa muhogo peke yake, akina fulani pekee ndio waagize sukari.

Kule unasema fulani pekee ndio anaweza unda meli za kivita, kwakuwa amefirisika na madeni serikali inalipa madeni yake ili kuokoa uwezo wa jeshi la maji kuendelea kupata melivita. Vitu vinavyoeleweka na hakuna anayepinga.
 
Hakuna sehemu nimelaumu wafanyabiashara mzee. Nimeelezea kinachotokea, wewe unakomaa ku-sugarcoat uhalisia kwa kuuita "uwezo".

France kumpa Musk $1 billion sijasikia, ila hata wakimpa wana faida kama nchi. Kiwanda cha Tesla kikichopo Ujerumani kitagharimu $4 za ujenzi tu. Bado faida ya kodi na ajira. Hapo France ikitoa $1 inakuwa ni investment, uchumi huo.

Na bado huo sio mfano sahihi na Obasanjo & Dangote. Kama Ufaransa ingemwambia Musk njoo ujenge kiwanda alafu tutapiga marufuku mshindani wako kuuza bidhaa kama zako, au tutakutoza kodi kiduchu kuliko wapinzani wako hapo ndio ingekuwa mfano sawa na Dangote & Obasanjo.
Kupiga marufuku wapinzani wako si ndio kesi za BYD vs Tesla,
Apple Vs Huawei, au wew unaona hizo kesi zipoje?

Alichofanya Obasanjo kuzuia cement ya nje ya Nigeria, ni sawa na alichofanya USA kwa huawei, au alichofanya China kwa Google na WhatsApp,

Hizo ni common practice dunia nzima
 
Ni kawaida kwamba katika nchi nyingi matajiri wakubwa utakuta ni wafanya biashara, lakini sio Tanzania. Kwa sasa wanaoongoza kwa kuwa matajiri wakubwa Tanzania ni wanasiasa waliopo madarakani au waliokuwa madarakani huko nyuma. Halafu wanafuatiwa na viongozi wa serikali, pamoja na ndugu zao.

Imefikia kwamba hata ukiwa mfanya biashara, ili utajirike kwa haraka lazima uwe na connection na wanasiasa na viongozi wa serikali, kuanzia connection za ofisi ya raisi, makamu wake au mawaziri. Hata vjana wadogo kabisa wenye hizi connections sasa wanaibukia kuwa na fedha nyingi sana za kufuja na kuishi maisha ya anasa sana.

Inatokea pia kwamba kikundi hiki cha matajiri wa kisiasa uongozi wanalinda sana himaya yao, mara nyingi kwa kutumia vyombo vya dola kama polisi, na sasa hata wanajaribu kutumia jeshi la ulinzi, JW. Hawataki watu wengine wa "kawaida" wawe kama wao. Kwa hiyo wanajaribu kuendelea umiliki wa himaya zao kwa kuwekeza katika watoto wao ili kuja kuwarithisha kuwa "wenye nchi" pamoja na utajiri wao. Hii ni kutia ndani kuendelea kufanya ufisadi mkubwa ili hata vizazi vyao vya baade viendelee kuwa katika neema ya kuwa tofauti na Watanzania wa kawaida.

Wengi wasichojua ni kwamba tatizo kubwa la serikali kukataa uraia pacha sio suala la "usalama wa nchi", bali ni usalama wa hiki kikundi kuona Watanzania walioko nje wana uhuru wa mawazo na upeo wa kuona wanachokifanya. Ndio maana hawataki watu wa diaspora wapewe nafasi ya kuja kuwa tishio kwa himaya yao. Wanawaogopa sana watu wa diaspora na wanaona kuwapa uraia pacha ni kuleta hatari ya kuondolewa katika "ufalme wao". Hawa "wenye nchi" wanajua watu wa diaspora hawana "political illiteracy" ambayo wameijenga katika Watanzania wanaoishi nchini. Wanadiaspora wana macho na wanaona, na wanaogopwa.

Lakini nataka nitoe tahadhari kwa watu hawa, kwamba katika jamii yoyote ile, hali kama hii iliyopo Tanzania huwa haidumu. Kuna wakati itafikia critical point, na kutakuwa na mlipuko mkubwa ambao ni namna fulani ya mapinduzi, ili kuliondoa tabaka hili la "wenye nchi" katika hii himaya yao ambayo kwa sasa wanaifurahia sana na kujaribu kuilinda kwa kila namna. Hili ndilo lililotokea nchi kama Tunisia na Misri, na si muda mrefu litatokea Tanzania, hali ikiendelea hivi.
Siasa na ajira za taasis kama TRA zinazalisha milionea wapya kila siku.
 
Wataje hao wanasiasa wenye hela kumzidi Bakhresa, Mount Meru, Mo au Lake group,


Sometimes tusidanganyane sana, wanasiasa wana hela ila usiseme ndio wenye hela nying nchini, matajiri hii nchi ni wahindi na waarabu
Unataka utajiwe majina ya watu hili iweje?.Au ukapigie porojo kwenye vijiwe vya kahawa.
 
Ni kawaida kwamba katika nchi nyingi matajiri wakubwa utakuta ni wafanya biashara, lakini sio Tanzania. Kwa sasa wanaoongoza kwa kuwa matajiri wakubwa Tanzania ni wanasiasa waliopo madarakani au waliokuwa madarakani huko nyuma. Halafu wanafuatiwa na viongozi wa serikali, pamoja na ndugu zao.

Imefikia kwamba hata ukiwa mfanya biashara, ili utajirike kwa haraka lazima uwe na connection na wanasiasa na viongozi wa serikali, kuanzia connection za ofisi ya raisi, makamu wake au mawaziri. Hata vjana wadogo kabisa wenye hizi connections sasa wanaibukia kuwa na fedha nyingi sana za kufuja na kuishi maisha ya anasa sana.

Inatokea pia kwamba kikundi hiki cha matajiri wa kisiasa uongozi wanalinda sana himaya yao, mara nyingi kwa kutumia vyombo vya dola kama polisi, na sasa hata wanajaribu kutumia jeshi la ulinzi, JW. Hawataki watu wengine wa "kawaida" wawe kama wao. Kwa hiyo wanajaribu kuendelea umiliki wa himaya zao kwa kuwekeza katika watoto wao ili kuja kuwarithisha kuwa "wenye nchi" pamoja na utajiri wao. Hii ni kutia ndani kuendelea kufanya ufisadi mkubwa ili hata vizazi vyao vya baade viendelee kuwa katika neema ya kuwa tofauti na Watanzania wa kawaida.

Wengi wasichojua ni kwamba tatizo kubwa la serikali kukataa uraia pacha sio suala la "usalama wa nchi", bali ni usalama wa hiki kikundi kuona Watanzania walioko nje wana uhuru wa mawazo na upeo wa kuona wanachokifanya. Ndio maana hawataki watu wa diaspora wapewe nafasi ya kuja kuwa tishio kwa himaya yao. Wanawaogopa sana watu wa diaspora na wanaona kuwapa uraia pacha ni kuleta hatari ya kuondolewa katika "ufalme wao". Hawa "wenye nchi" wanajua watu wa diaspora hawana "political illiteracy" ambayo wameijenga katika Watanzania wanaoishi nchini. Wanadiaspora wana macho na wanaona, na wanaogopwa.

Lakini nataka nitoe tahadhari kwa watu hawa, kwamba katika jamii yoyote ile, hali kama hii iliyopo Tanzania huwa haidumu. Kuna wakati itafikia critical point, na kutakuwa na mlipuko mkubwa ambao ni namna fulani ya mapinduzi, ili kuliondoa tabaka hili la "wenye nchi" katika hii himaya yao ambayo kwa sasa wanaifurahia sana na kujaribu kuilinda kwa kila namna. Hili ndilo lililotokea nchi kama Tunisia na Misri, na si muda mrefu litatokea Tanzania, hali ikiendelea hivi.
Muda utaongea oneday
 
Nyie ndio mnaamini Bakhresa aliuza kahawa pale msikitini akaanzisha kiwanda cha kusaga nafaka taratibu hivyo hadi akawa bilionea. Upewe mashine ya kusaga tuone kama utapata hata utajiri wa milioni 50. SAS anawatazama uko.

Au mnakuja kwa mzee Gulam Dewji na mwanae Mo mnasema walipambana, ni sawa walipambana. Ila hata wewe tukikupa vile viwanda vya nguo bure kwenye ubinafsihaji, na ukavitumia kama dhamana kukopea mabilioni nje, na tukakupa mashamba ya mkonge sawa na bure miaka 20 baadae huwezi shindwa kuwa bilionea mkubwa.
Huwezi nipa klabu kubwa kwa hela za "maandishi" billioni 20, alafu nikiulizwa nimeziweka akaunti gani na zimetumikaje nafoka nakulalamika ninavyopata hasara. Baadae ukarudi ukakuta sipo bilionea.

Sasa hayo yote huwezi yapata bila mkono wa kisiasa au kuwa na wanasiasa nyuma. Katafute mmiliki wa Kagera kiwanda cha sukari nani, mmiliki wa Mtibwa nani alafu ujue kwanini sukari Tanzania haitoshelezi kwa uzalishaji ila serikali haitaki kuagiza nje tena kwa bei nafuu.

Nilishtuka baada ya serikali ya Magufuli kukisumbua kiwanda cha Dangote kuhusu either makaa ya mawe au clinker (sikumbuki ni kipi hapo) ghafla Rais mstaafu wa Nigeria, Olisegun Obasanjo akafanya ziara binafsi kwa private jet kuonana na Magufuli. Baada siku chache mambo ya Dangote cement yakatulia. Nikaenda kufuatilia kwanini suala linamhusu Dangote alafu Olisegun ndio aje binafsi wakati ana tiketi ya kidiplomasia anaweza kuja kitaifa.

Kiufupi iko hivi, Dangote alitokea familia ya uwezo ila akaongezea kuwa na political and military connection, Nigeria ilitawaliwa na military rulers. Akafanya awe na haki ya kuagiza mchele na sukari nje na kuuza kwa faida kubwa (sababu kwa kutumia siasa aliua ushindani). Baadae Nigeria ikafanya uchaguzi kutafuta kiongozi wa kiraia iachane na utawala wa kijeshi, Dangote akafadhili uchaguzi mkuu wa Olisegun Obasanjo na akashinda.
Obasanjo akaleta sera ya viwanda kwa kiqsi fulani, ghafla Dangote akaanza kujenga viwanda na ghafla akawa bilionea maradufu. Ukifuatilia biashara za Dangote huwa zinapewa subsidiaries, exclusive rights, mara ndio zinakuwa kipaumbele na sera kuu ya serikali. Kwa sasa ana refinery, ni usanii mtupu unaendelea. Dangote ni GSM wa Obasanjo. Na Marais wa Nigeria huwa wanaachiana na kulindana, mnyororo unaendelea na ukitaka kuingia hapo kati wanufaika wako tiyari muingie vita ya wenyewe kwa wenyewe.

Biashara za Afrika zina mkono mkubwa wa kisiasa. Hata pale Misri ni hivihivi, Sudan ni hivi, Somalia baada ya kuharibika ile miaka ya 90 waliokuwa wanahamia Nairobi na Dar kujenga mahoteli na kuanzisha biashara kubwa ni wanasiasa wao waliotoroka. South Africa pale hao ndio kabisa wanafanya biashara ikulu.
Biashara ambayo haina innovation nyuma ni vigumu itengeneze utajiri wa haraka. Biashara za kawaida kama unga na simenti inataka uwekezaji mkubwa (sijui hela utapata wapi), sera rafiki kwako mfanyabiashara hiyo (nani ataweka sera za kuku-favour) na ulinzi (dhidi ya sheria, kesi, upinzani, ushindani). Hivyo vyote vinapatikana kwenye siasa za Kiafrika.

Hao wote uwezo mkubwa kibiashara wanao, kisha tag ya kisiasa ndio inakuja.
Umeeleza vyema
 
Back
Top Bottom