Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,359
- 11,238
Hamas imetoa tangazo rasmi la kukubali mapendekezo ya kusitisha vita na kuachia baadhi ya madai yao.
Tangazo hilo limeleta furaha kubwa kwa watu wa Gaza na hata Israel japo limekuja huku Israel imeshatoa tangazo la kuhamisha watu mashariki ya Rafah tayari kurudia mashambulizi yale ya nguvu yaliyozoeleka kuanzia kaskazini mpaka Khani Younis.
Dalili za Hamas kukubali kusitisha vita zilikwishaonekana na majibu ya Netanyahu hayakuwaridhisha wananchi wengi wa Israel wakiongozwa na kiongozi wa upinzani,Yair Lapid.
Viongozi wa Hamas wakiungwa mkono na nchi zinazosimamia upatanishi wamemlaumu sana Benjamin Netanyahu kuwa kwa hamu yake ya kuendeleza vita akitaraji kubadili upepo kuwa ndiye kikwazo katika juhudi hizo za kumaliza vita.
Kwa tangazo hili rasmi la Hamas ni lazima kwa Israel kufuta mpango wa kuivamia Rafah au kuendelea na kushindwa moja kwa moja.
Hatua ya kuendelea kuinjgia Rafah na kuuwa mamia ya maelfu ya watu tena kunahatarisha zaidi kuwavuta Misri na Jordan kuvunja mikataba ya amani waliyowekeana na Israel.
Gideon Levy ambaye ni mwandishi mashuhuri wa gazeti la Haaretz amesema Hamas wamecheza sana kwa hatua waliyochukua ambapo wameiwacha serikali ya Israel ikiwa imeduwaa.
Tangazo hilo limeleta furaha kubwa kwa watu wa Gaza na hata Israel japo limekuja huku Israel imeshatoa tangazo la kuhamisha watu mashariki ya Rafah tayari kurudia mashambulizi yale ya nguvu yaliyozoeleka kuanzia kaskazini mpaka Khani Younis.
Dalili za Hamas kukubali kusitisha vita zilikwishaonekana na majibu ya Netanyahu hayakuwaridhisha wananchi wengi wa Israel wakiongozwa na kiongozi wa upinzani,Yair Lapid.
Viongozi wa Hamas wakiungwa mkono na nchi zinazosimamia upatanishi wamemlaumu sana Benjamin Netanyahu kuwa kwa hamu yake ya kuendeleza vita akitaraji kubadili upepo kuwa ndiye kikwazo katika juhudi hizo za kumaliza vita.
Kwa tangazo hili rasmi la Hamas ni lazima kwa Israel kufuta mpango wa kuivamia Rafah au kuendelea na kushindwa moja kwa moja.
Hatua ya kuendelea kuinjgia Rafah na kuuwa mamia ya maelfu ya watu tena kunahatarisha zaidi kuwavuta Misri na Jordan kuvunja mikataba ya amani waliyowekeana na Israel.
Gideon Levy ambaye ni mwandishi mashuhuri wa gazeti la Haaretz amesema Hamas wamecheza sana kwa hatua waliyochukua ambapo wameiwacha serikali ya Israel ikiwa imeduwaa.