Dr Matola PhD
JF-Expert Member
- Oct 18, 2010
- 58,956
- 101,371
Ni kwa vile tu hamjui, usalama wa Taifa hawana power of arrest.Watu wanatumia hii kazi kututishia tishia yani hata raia wa kawaida nao wanatutishia ni tiss ilimradi tu tuishi kinyonge.....
Akiingia kwenye 18 zako mletee defender anawekwa ndani na hawezi kujitambulisha Polisi kama yeye ni usalama atatumia network yake kujichomowa ndani ya nondo.
Kuna dereva mmoja wa usalama alikuwa anafanya deal za kubeba wahamiaji haram siku yake akaingia kwenye 18 za Polisi akawekwa ndani Moshi, RSO alivyokwenda akaitwa chemba akachukuwa kitambulisho chao akamuacha apambane na hali yake na kibarua kiliishia hapo.
Usalama ni tofauti na wengi mnavyowachukulia, hao wanaowababaisha mitaani ni Uvccm wanashona vikaunda suti vyao nyeusi na kujifanya usalama wakati ni green guard wa maccm tu.