Yanayojiri Kesi ya Mbowe na Kauli tata za Serikali - Katiba Mpya ni Hitaji la Dharura sana

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
31,693
41,728
Kauli hii ni rasmi ya serikali:

IMG_20211126_221549_007.jpg


Ukichanganya na mfano wa kauli kama hizi (kwenye kesi ya Mbowe) zenye kutokea upande wa serikali:

1. Mahakama si mama yako,
2. Waraka wa mshitakiwa kama nyenzo yake kujitetea ni "takataka,"
3. Mtake msitake mawakili wa serikali ni mawakili wa mahakama,
4. Washitakiwa rumande au magereza hawana haki zozote,
5. Washitakiwa hawaruhusiwi kuletewa chakula au chochote cha kunywa isipokuwa jumamosi tu,
6. "Sisi tunaingia mahabusu mpaka ndani kuonana nao, ninyi ni kuwabakia nje."
7. Nk

Kwa hakika ni kauli tata, zenye kukosa staha na zenye kujaa ukakasi kuhusiana na haki za msingi za watu.

Tuko katika mazingira ambayo serikali iko kwenye mvutano na raia wake. Mbaya zaidi serikali inahusishwa moja kwa moja kwenye kunyima watu haki ikiwamo kuwabambikizia kesi na hata hukumu.

Vipi serikali ndani ya sufuria basi itegemewe kututendea haki kina yakhe nje ya sufuria hili?

IMG_20211119_091739_123.jpg


Hivi ni kweli kuwa wakuu wetu hawa hawaioni hali hii ya kutokuwepo kwa uhalali?

Hivi waheshimiwa hawa wakiwamo Rais Samia, Mpango, Majaliwa, Jaji Mkuu, Spika na wengine wote wanaiona hali hii kuwa ni muafaka kabisa?

Hivi waheshimiwa hawa wanapokuwa wanasali wanategemea kuiona pepo hii hii tunayofunzwa kuiona tukiwa tumemtendea jirani yetu kama ambavyo mtu ungependa kutendewa nafsi yako?

Kwa hakika zikizingatiwa pia kauli kama hizi kwa mustakabala mwema wetu sote, mahusiano mapya baina ya serikali na watu wake ni jambo la dharura sana.

Ama hakika tofauti na hapo tunakoelekea kama jamii, itakuwa ni kudhamiria kupaelekea njia panda, kusikokuwa na tija kwa yeyote.
 
Kuna siku ngumi zitapigwa Mahakamani. Au Jaji kufokewa na Mawakili wa upande ule uliojimilikisha Mahakama.
 
Hata msopompa kura atakuwa rais tu. Hivi unafahamu kwamba kwa katiba yetu hii rais SSH anaweza kuwaua wasukuma wote na bado asishitakiwe popote?

Anayetangaza mshindi ni yeye. Akishatangazwa kwishney hairuhusiwi kuhoji popote.
 
ninyi pelekeni kesi mahakamani, atakayesema hupati fidia au unapata ni Mahakama, sio simbachawene.
 
ninyi pelekeni kesi mahakamani, atakayesema hupati fidia au unapata ni Mahakama, sio simbachawene.

Msingi wa hoja ni kauli tata za serikali tena viashiria vya faulo zaidi huko mahakamani.

Huko siyo kwa mama yetu. Hatukujua pia kumbe na mahakama nayo ilikuwa na mawakili dhidi yetu.

Tutashinda vipi kama upande wa mashtaka na mahakama wako upande mmoja dhidi yetu?
 
Msingi wa hoja ni kauli tata za serikali tena viashiria vya faulo zaidi huko mahakamani.

Huko siyo kwa mama yetu. Hatukujua pia kumbe na mahakama nayo ilikuwa na mawakili dhidi yetu.

Tutashinda vipi kama upande wa mashtaka na mahakama wako upande mmoja dhidi yetu?
hizo kauli ni za kawaida, ninyi ni wageni wa mahakama. hata mahakama huwa inaongea sana hivyo ata mawakili wa kujitegemea tunaongea sana hivyo wakati mwingine. au unataka nikuletee uamuzi wa mahakama ulioongea hivyo mle ndani? msisumbue akili kuumiza moyo kwa mambo ambayo ni ya kawaida. kesi ya mbowe isije kuwasababishia ugonjwa wa moyo ambao hata mbowe mwenyewe hata pata. ninyi msiojua sasa.
 
Kauli hii ni rasmi ya serikali:

View attachment 2025294

Ukichanganya na mfano wa kauli kama hizi (kwenye kesi ya Mbowe) zenye kutokea upande wa serikali:

1. Mahakama si mama yako,
2. Waraka wa mshitakiwa kama nyenzo yake kujitetea ni "takataka,"
3. Mtake msitake mawakili wa serikali ni mawakili wa mahakama,
4. Washitakiwa rumande au magereza hawana haki zozote,
5. Washitakiwa hawaruhusiwi kuletewa chakula au chochote cha kunywa isipokuwa jumamosi tu,
6. "Sisi tunaingia mahabusu mpaka ndani kuonana nao, ninyi ni kuwabakia nje."
7. Nk

Kwa hakika ni kauli tata, zenye kukosa staha na zenye kujaa ukakasi kuhusiana na haki za msingi za watu.

Tuko katika mazingira ambayo serikali iko kwenye mvutano na raia wake. Mbaya zaidi serikali inahusishwa moja kwa moja kwenye kunyima watu haki ikiwamo kuwabambikizia kesi na hata hukumu.

Vipi serikali ndani ya sufuria basi itegemewe kututendea haki kina yakhe nje ya sufuria hili?

View attachment 2025315

Hivi ni kweli kuwa wakuu wetu hawa hawaioni hali hii ya kutokuwepo kwa uhalali?

Hivi waheshimiwa hawa wakiwamo Rais Samia, Mpango, Majaliwa, Jaji Mkuu, Spika na wengine wote wanaiona hali hii kuwa ni muafaka kabisa?

Hivi waheshimiwa hawa wanapokuwa wanasali wanategemea kuiona pepo hii hii tunayofunzwa kuiona tukiwa tumemtendea jirani yetu kama ambavyo mtu ungependa kutendewa nafsi yako?

Kwa hakika zikizingatiwa pia kauli kama hizi kwa mustakabala mwema wetu sote, mahusiano mapya baina ya serikali na watu wake ni jambo la dharura sana.

Ama hakika tofauti na hapo tunakoelekea kama jamii, itakuwa ni kudhamiria kupaelekea njia panda, kusikokuwa na tija kwa yeyote.
Aseee!
 
hizo kauli ni za kawaida, ninyi ni wageni wa mahakama. hata mahakama huwa inaongea sana hivyo ata mawakili wa kujitegemea tunaongea sana hivyo wakati mwingine. au unataka nikuletee uamuzi wa mahakama ulioongea hivyo mle ndani? msisumbue akili kuumiza moyo kwa mambo ambayo ni ya kawaida. kesi ya mbowe isije kuwasababishia ugonjwa wa moyo ambao hata mbowe mwenyewe hata pata. ninyi msiojua sasa.

Kwamba?

"... mawakili wa kujitegemea tunaongea sana hivyo wakati mwingine."

Wewe huoni sense ya inequality iliyopo kwenye mada hii?

Au humo kwenye sufuria, wewe ni hiyo njemba yenye vest nyeupe?

IMG_20211119_091739_123.jpg


Hiiiiii bagosha!
 
Kwamba?

"... mawakili wa kujitegemea tunaongea sana hivyo wakati mwingine."

Wewe huoni sense ya inequality iliyopo kwenye mada hii?

Au humo kwenye sufuria, wewe ni hiyo njemba yenye vest nyeupe?

View attachment 2025353

Hiiiiii bagosha!
sidhani kama wewe ni wakili kwasababu sijaona umeongea hoja yeyote yenye mashiko ya kisheria ndio maana niliandika hivyo. kwani wewe ni mwanasheria?
 
sidhani kama wewe ni wakili kwasababu sijaona umeongea hoja yeyote yenye mashiko ya kisheria ndio maana niliandika hivyo. kwani wewe ni mwanasheria?

Uko kwenye kukusanya taarifa mjomba?

Nisiache kukwambia huna ubavu, credibility wala moral authority ya kuwashauri mawakili wa utetezi kwenye shauri hili.

Zingatia, mada hapa ni kauli tata za serikali zisizokuwa na chembe ya afya.

Ushauri wako kama unakuwasha, peleka kwa bwana Chaula huko.

Huyo bwana ni wakili mzigo. He is doing more of disservice kwa serikali yenyewe kama unajali.
 
Kwamba?

"... mawakili wa kujitegemea tunaongea sana hivyo wakati mwingine."

Wewe huoni sense ya inequality iliyopo kwenye mada hii?

Au humo kwenye sufuria, wewe ni hiyo njemba yenye vest nyeupe?

View attachment 2025353

Hiiiiii bagosha!
Hako kajamaa kwenye sufuria kamekenua meno na hako kamalaya kamevaa bikini vinanchekesha sana yani sijui,,,, huyo mchoraji ni msenge aisee
 
Ndo tumejua kumbe na mahakama zina mawakili ambao ni wa jamhuri. Jaji alitakiwa amkemee sana huyo wakili wa serikali kwa maneno ya dharau dhidi ya mahakama. Shida ni kuwa naye jaji hakielewi.
 
Ndo tumejua kumbe na mahakama zina mawakili ambao ni wa jamhuri. Jaji alitakiwa amkemee sana huyo wakili wa serikali kwa maneno ya dharau dhidi ya mahakama. Shida ni kuwa naye jaji hakielewi.

Wamelewa madaraka. Sidhani kama mtu anaweza kuwaeleza vyema kuliko huyu:

IMG_20211119_091739_123.jpg


Cc: Dr Akili
 
Back
Top Bottom