Wazungu wakitujibu na kusema ukweli tusisema tunabaguliwa wala kudharauliwa

Hivi huko Uingereza kuna demokrasia? Mfalme kwa maana ya malkia anatawala miaka nenda rudi halafu unasema ndiyo demokrasia?
Mfalme/malkia ni mtawala asiye na madaraka ndiyo maana kuna Prime Minister wa chama kinachotawala na ndiye mwenye kuamua kama kwenda vitani kama alivyofanya Tonny Blair kwenye vita ya Iraq ingawa mtu kama Prince Charles mwana wa mfalme alipinga. Chama tawala na siyo malkia kinaamua nchi za kufadhili na nchi za kujenga nazo urafiki si Malkia.
 
ni wewe ndo unaamini hvyo7bu ushajitengenezea mqzingira ya kukata tamaa au kunyenyekeanyenyekea binadamu wenzako na maisha yako yatakuwa hvyo mpaka kabulini
lakini mimi naamini ipo siku wazungu watakuwa chini yetu na watatupigia magoti JUHUDI nikiziazisha mimi kizazi changu kitaziendeleza Hata hao wamalekani wenyewewe walitawaliwa no juhudi zao ndo zimewafikisha hapo walipo
so usikate tamaa sisi BLACK ndio tunaongoza kwa vipaji lukuki duniani na wengi wetu tuna SUPERBRAIN Ila watu kama wewe ndo huzizima ndoto zetu kwa kuamini mzungu ndo kilakitu
CHINA ilotoka wapi leo hii ipo wapi ni juhudi zao na MATUMAINI yao ndo leo yamewafikisha pale
So naamini ipo siku itafikia
 
Kuna umaskini wa kutisha na kuogofya sana Zimbabwe. Ila hatuna namna wazungu walituwahi.

Sasa hivi Azerbaijan ndio nchi pekee ya kiislam ina ubalozi na Israel (kuna kipindi pia Mauritania ilishawahi) na ipo karibu na Iran yani wanakula shavu ya uhakika kutoka magharib kwaajil ya iyo diplomasia.

Kuna kipindi Iran na Cuba walikubali kabisa nakusema tunakomaa ila tunaumia.

Oil rich gulf states saudi Arabia uae Kuwait Qatar Bahrain siyo wajinga kuwakumbatia wazungu wanafaham umuhim wao.

India kaamua kukomaa na wazungu(magharib) ndio maana anapiga hatua. Hasim wake Pakistan haelewek ila ni rafiq dhid ya ugaid anapigwa support kiaina. Ni China pekee yake ndiye anajiamin ila mwenzake Urus ana nguvu ila ana feel the pinch

Brazil aegemei upande wowote anajtahid sana kuwa neutral ndio maana anaunafuu mzuri.

Morales na Bolivia yake hoi licha ya akiba ya kutosha ya Lethium. Anayetia huruma sasa hivi ni Venezuela na mafuta yake hayamsaidii. Venezuela kwishaaa!!
 
Waafrika tunataka kuanzisha ugomvi wa mawe wakati tunaishi kwenye nyumba ya vioo.Wazungu wakitujibu na kusema ukweli tutakuwa wapole na kujiona sisi si kitu.

Kwa mfano,ukimuuliza Mugabe ndege iliyomfikisha Addis Ababa imetengenezwa na Waafrika au Wazungu atakuwa na jibu gani?

Tujiuluze tu hata lugha zetu za kiafrika sisi wenyewe tunazithamini?Mbona karibu kila mahali barani Afrika ni kingereza na kifaransa tu?Wakitubeza kwa kushindwa hata kuthamini lugha zetu tutawajibu nini?Hata hiyo speech Mugabe kaitoa kwa lugha gani?

Nchi ya kiafrika ikikumbwa na njaa,huwa hatusubiri wazungu watusaidie?

Janga la Ebola huko Afrika Magharibi ni kina nani walitoa fedha kusaidia kukabiliana na tatizo hilo?


Viongozi wa kiafrika wakiiba hela katika nchi zao huficha katika nchi nyingine za kiafrika au huficha katika nchi za Ulaya?Wazungu wakilisema hili na kutudharau watakuwa wametuonea?

Jamani,yako mengi sana ya aibu kuhusu sisi wa Afrika na ndio maana wanatudharau hivyo ni bora kwanza tukajirekebisha kabla ya kujitia kimbelembele.

Tulichofanikiwa Waafrika ni kutoa wacheza soka tu kwenda Ulaya ila mambo mengine yote yametushinda ikiwa ni pamoja na hata kujitawala wenyewe kwa wenyewe.Hata DEMOKRASIA TU IMETUSHINDA!

Ngozi nyeusi ni shida kwani hata hizi dini zetu bado zimetoka kwa hao wazungu na hata video za Yesu zinaonyesha Yesu si mtu mweusi.

Alafu hata wapigania uhuru wa nchi za kiafrika walisomea nchi gani na kwa msaada wa watu gani zaidi ya hao wazungu?

Mugabe na vingozi wengine wa Kiafrika mpaka leo hii wanatibiwa na kufia Afrika au Ulaya?

Waafrika tunatafuta usawa kwasababu za kibinadamu tu lakini sio kwasababu za kuwa na viwango(standards)-hivi ndivyo mimi ninavyoamini na nitaendelea kuamini hivyo mpaka siku naingia kaburini.

Tujisahihishe kwa mengi kabla ya kuanza kubwabwaja na kutafuta usawa.
Hakuna kitu kibaya kama utumwa wa fikra.
Makamanda feki wa chadema kaa kulamba miguu wazungu mtakuja kuigawa nchi yenu kwa wazungu bure bure.
 
Wazungu ni binadamu kama sisi, wana udhaifu mwingi tu. Tusitake kuwalamba sana miguu yao, washenzi tu. Kwamba sayansi yote inatokana na vichwa vyao sio hoja ya kutufanya tukaishi kwa kuwaogopa kila kukicha. Mugabe anayo mamlaka ya kimaadili ya kuwaambia kile ambacho kinawakilisha mawazo na hisia za waafrika walio na uzalendo na bara lao. Mugabe ni mzee wa miaka 91, asipoongea yeye nani mwingine azungumze kwa niaba ya bara letu?. Tusiwe watumwa wa kimawazo kupita maelezo, tunayo haki ya kuwa na haki na kuwaambia wazungu kile tunachoona kinafaa kutamkwa.

Hakuna kitu kibaya kama mtu mweusi unaingia kwenye basi ukiwa ulaya halafu kuna mpumbavu mmoja anaanza kuigiza mlio wa sauti ya nyani. Unakatiza kwenye korido ya kituo cha treni mtoto mdogo tu wa kizungu anaanza kukucheka na kukukejeli. Umekaa na rafiki yako ndani a mgahawa, mnakunywa juice na kucheka huku mkikumbushana story za nyumbani ghafla katoto kadogo hata akajafikisha miaka mitano kanakuiteni nyinyi nyani halafu kanamuonyeshea mama yake kwa kidole kuelekea upande mliokaa. Yapo matukio mengi ya kishenzi ambayo mtu mweusi anakutana nayo nje ya Afrika.

Sioni kosa kwa mzee Mugabe kuwapa vidonge vyao hao wakoloni. Naunga mkono juhudi za serikali katika kukusanya kodi na kutafuta njia za kuongeza pato la ndani la Taifa. Kujitegemea kunaongeza jeuri ya utaifa, ombaomba inaongeza dharau. Mugabe yuko sahihi kabisa kuongea maneno anayoyaamini.
acha matusi wewe bila mzungu leo ungekuwa kwenu shitindi huko ,kuanzia asubuhi unapoamka mpaka unalala maisha yako asilimia 95 yanaendeshwa na mzungu .
 
acha matusi wewe bila mzungu leo ungekuwa kwenu shitindi huko ,kuanzia asubuhi unapoamka mpaka unalala maisha yako asilimia 95 yanaendeshwa na mzungu .
Bwana mdogo mimi naishi Dar , hao wazungu pamoja na kuchangia maendeleo lakini wasikufanye ukawa mtumwa wa mawazo. Wanaokumbukwa baada ya kufa mara nyingi ni kwa sababu katika uhai wao waliacha identity, waliacha legacy. Utaweza vipi kukumbukwa miaka mingi ijayo ikiwa wewe kila siku unawanyenyekea wale kutawala?.
 
Swali dogo tu kwako NDAGLA pamoja na lugha uliotumia:Hivi mtu akisimama mbele ya watu na kusema mimi naitwa "Bitozi Nyangema" na mwingine akijita "Paul Peter".Ni nani atasababisha watu wacheke au kuguna?Unafikiri ni kwanini?Na kwa hili tutalamu wazungu?
 
Malkia hatawali uingereza acha kupotosha kunguni .kuna vyama vingi na kwa sasa david camerron ndio waziri mkee .
Ndugu yangu Malkia ndiye Head of State...Cameron akiteua baraza la mawaziri ni lazima aende kwa malkia kumfahamisha...Hiyo ndiyo katiba ya Uingereza ingawa hawana katiba iliyoandikwa.
 
Kuwaabudu wazungu na kukiri kuwa wana akili nyingi kuliko sisi ni upumbavu uliopitiliza. Shida ziliwapa wazungu nguvu ya kuumiza vichwa vyao na kutoka nje ya nchi zao. Afrika ina kila kitu,raha zinanyamazisha fikra. Mugabe ni miongoni mwa viongozi wachache sana wa maana waliotokea Afrika.Baba wa akili hanyenyekei wanaume wenzie bali huzungumza nao kwa hekima. China na Korea kaskazini haziwahi kuwanyenyekea hao wanaoabudiwa na wapumbavu. Sijaona China inavyokwama. Wazungu wamekubaliana wanaume kwa wanaume waoane,wanawake kwa wanawake waoane. Wazazi wasiwaadhibu watoto hata wakikosea lakini watoto hata wakiwaua wazazi wao hawafungwi kwa kuwa ni watoto. Mali inarithishwa kwa mbwa au paka. Ndiyo aina ya ustaarabu tuige toka Ulaya? Mwafrika mwamwona dhalili Obama anaitawala Dunia leo;je Obama si Mwafrika? Tukijiamini tutajitawala na kuitawala Dunia.
 
Kuwaabudu wazungu na kukiri kuwa wana akili nyingi kuliko sisi ni upumbavu uliopitiliza. Shida ziliwapa wazungu nguvu ya kuumiza vichwa vyao na kutoka nje ya nchi zao. Afrika ina kila kitu,raha zinanyamazisha fikra. Mugabe ni miongoni mwa viongozi wachache sana wa maana waliotokea Afrika.Baba wa akili hanyenyekei wanaume wenzie bali huzungumza nao kwa hekima. China na Korea kaskazini haziwahi kuwanyenyekea hao wanaoabudiwa na wapumbavu. Sijaona China inavyokwama. Wazungu wamekubaliana wanaume kwa wanaume waoane,wanawake kwa wanawake waoane. Wazazi wasiwaadhibu watoto hata wakikosea lakini watoto hata wakiwaua wazazi wao hawafungwi kwa kuwa ni watoto. Mali inarithishwa kwa mbwa au paka. Ndiyo aina ya ustaarabu tuige toka Ulaya? Mwafrika mwamwona dhalili Obama anaitawala Dunia leo;je Obama si Mwafrika? Tukijiamini tutajitawala na kuitawala Dunia.
Tukubali tukatae, "nature" ndio iliamua hali iwe hivi kati ya sisi na hawa wenzetu.Ni ukweli unaoumiza ingawa hatutaki kuukubali.
 
Swali dogo tu kwako NDAGLA pamoja na lugha uliotumia:Hivi mtu akisimama mbele ya watu na kusema mimi naitwa "Bitozi Nyangema" na mwingine akijita "Paul Peter".Ni nani atasababisha watu wacheke?Unafikiri ni kwanini?Na kwa hili tutalamu wazungu?

Yeyote anaweza sababisha watu kucheka/kutokucheka inategemea hadhira yake ni ya watu wanaojitambua kwa kiwango gani or wamekulia tamaduni zipi or anajitambulishia wapi.

Nyangema atachekwa akijitambulisha kwenye watu wenye mindset kama yako lakini kwangu sioni kichekesho kwa wote.

Wazungu lazima walaumiwe kwa kulazimisha ku-install apps za android kwenye windowsphone matokeo yake wametengeneza breed yenye mindset chakavu.
 
Mtoa post ukumbuke hata kabla ya chuo cha kwanza cha bologna afrika kwenye Timbuktu empire kulikuwa kuna chuo kinaiywa Timbuktu university masomo Kama medicine mathematics astronomy hadith na geography na inakadiliwa karibu wanafunzi 20000 toka barani afrika walikusanyika hapo
University of Timbuktu - Wikipedia, the free encyclopedia. Utafoati Kati ya mwafrika na mzungu ni mdogo sema wenzetu serious Sana katika ufuatiliaji was na kutafuta njia za kutatua matatizo yao.
 
Yeyote anaweza sababisha watu kucheka/kutokucheka inategemea hadhira yake ni ya watu wanaojitambua kwa kiwango gani or wamekulia tamaduni zipi or anajitambulishia wapi.

Nyangema atachekwa akijitambulisha kwenye watu wenye mindset kama yako lakini kwangu sioni kichekesho kwa wote.

Wazungu lazima walaumiwe kwa kulazimisha ku-install apps za android kwenye windowsphone matokeo yake wametengeneza breed yenye mindset chakavu.
Nakuongezea na hii:Hata siku yako ya kuzaliwa au ya mwanao ikifika mnakusanyana sebuleni huku mkiimba ule wimbo maarufu wa birthday ambao uko kwa lugha ya kingereza.

Utasikia,tena huku wewe mwenyewe ukichekelea: "Happy birthday to you x 2.......".

Kama unabisha hebu tuandikia wa kwetu wa kiswahili unaoutumiga zaidi ya huu wa kizungu kama upo.
 
Waafrika tunataka kuanzisha ugomvi wa mawe wakati tunaishi kwenye nyumba ya vioo.Wazungu wakitujibu na kusema ukweli tutakuwa wapole na kujiona sisi si kitu.

Kwa mfano,ukimuuliza Mugabe ndege iliyomfikisha Addis Ababa imetengenezwa na Waafrika au Wazungu atakuwa na jibu gani?

Tujiuluze tu hata lugha zetu za kiafrika sisi wenyewe tunazithamini?Mbona karibu kila mahali barani Afrika ni kingereza na kifaransa tu?Wakitubeza kwa kushindwa hata kuthamini lugha zetu tutawajibu nini?Hata hiyo speech Mugabe kaitoa kwa lugha gani?

Nchi ya kiafrika ikikumbwa na njaa,huwa hatusubiri wazungu watusaidie?

Janga la Ebola huko Afrika Magharibi ni kina nani walitoa fedha kusaidia kukabiliana na tatizo hilo?


Viongozi wa kiafrika wakiiba hela katika nchi zao huficha katika nchi nyingine za kiafrika au huficha katika nchi za Ulaya?Wazungu wakilisema hili na kutudharau watakuwa wametuonea?

Jamani,yako mengi sana ya aibu kuhusu sisi wa Afrika na ndio maana wanatudharau hivyo ni bora kwanza tukajirekebisha kabla ya kujitia kimbelembele.

Tulichofanikiwa Waafrika ni kutoa wacheza soka tu kwenda Ulaya ila mambo mengine yote yametushinda ikiwa ni pamoja na hata kujitawala wenyewe kwa wenyewe.Hata DEMOKRASIA TU IMETUSHINDA!

Ngozi nyeusi ni shida kwani hata hizi dini zetu bado zimetoka kwa hao wazungu na hata video za Yesu zinaonyesha Yesu si mtu mweusi.

Alafu hata wapigania uhuru wa nchi za kiafrika walisomea nchi gani na kwa msaada wa watu gani zaidi ya hao wazungu?

Mugabe na vingozi wengine wa Kiafrika mpaka leo hii wanatibiwa na kufia Afrika au Ulaya?

Waafrika tunatafuta usawa kwasababu za kibinadamu tu lakini sio kwasababu za kuwa na viwango(standards)-hivi ndivyo mimi ninavyoamini na nitaendelea kuamini hivyo mpaka siku naingia kaburini.

Tujisahihishe kwa mengi kabla ya kuanza kubwabwaja na kutafuta usawa.

NB:Nyie mnaonishambulia nijibuni swali hili dogo tu: Hivi siku yenu ya kuzaliwa au ya watoto wenu ikifika na mkakusanyika pale sebuleni, ule wimbo maarufu wa siku ya kuzaliwa (birthday),huwa ni wa lugha gani?Wa lugha yetu uko wapi?
Mpumbavu wewe unayewapa masifa wazungu waliokutawala.nakuita tena mpumbavu kwa kushabikia utumwa na ukibaraka,na huu upumbavu wako hautakuisha karibuni kwa kuwa umejipanga kuwatetea watu kwa rangi zao na kuwapa utukufu wa bandia !sasa nenda kalime mashamba yao ya ngano huko north carolina ama kapalilie bangi wanazolima mexico kwa kuwa huko ndio size yako wewe mpumbavu wa siku,na ninyi jamii forum mkishindwa kuondoa upumbavu huu kwenye hii mitandao na ninyi ni mmoja wa hawa wapuuzi.
 
Mpumbavu wewe unayewapa masifa wazungu waliokutawala.nakuita tena mpumbavu kwa kushabikia utumwa na ukibaraka,na huu upumbavu wako hautakuisha karibuni kwa kuwa umejipanga kuwatetea watu kwa rangi zao na kuwapa utukufu wa bandia !sasa nenda kalime mashamba yao ya ngano huko north carolina ama kapalilie bangi wanazolima mexico kwa kuwa huko ndio size yako wewe mpumbavu wa siku,na ninyi jamii forum mkishindwa kuondoa upumbavu huu kwenye hii mitandao na ninyi ni mmoja wa hawa wapuuzi.
Kukubali mapungufu na kujirekebisha kutakusaidi kulikoni kujifanya mbishi wakati unapotea.Hotuba ya Mugabe itachochea tu ubaguzi duniani.Wazungu wakimjibu unadhani ni nini kitatokea?
 
Kukubali mapungufu na kujirekebisha kutakusaidi kulikoni kujifanya mbishi wakati unapotea.Hotuba ya Mugabe itachochea tu ubaguzi duniani.Wazungu wakimjibu unadhani ni nini kitatokea?
Salary,

Inasikitisha kwa karne hii kukutana kijana anayeabudu wazungu kama.wewe,pengine historia ya afrika hauijui,tumekuwa na umasikini huu sababu ya wizi wao wazungu,
Ulishajiuliza kwanini walimuua ghadafi ili walibia wafie majini kama mamba na wengine kuenda kusafisha choo zao ulaya?
Ulishajiuliza kwanini wakombozi wote wa.afrika wanawachukia wazungu kuanzia kwa nkurumah,Kaunda, nyerere,ghadafi,Lumumba jk,?
Je wao na sisi nani anabagua mwingine?unawaogopa kuwambie ukweli ? Kwani hawajui?
Jitambue ondokana na utumwa
 
Back
Top Bottom