Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
3,355
12,991
Screenshot 2024-09-08 140136.png


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amevitaka Vyombo vya Usalama vilivyopo chini ya Wizara hiyo kujiandaa na chaguzi zinazokuja ikiwemo Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika mwaka huu (2024) na Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani (2025) huku akivitaka vyombo hivyo kuacha milango wazi kwa wananchi wanaofika katika ofisi zao kutoa malalamiko mbalimbali.

Ametoa kauli hiyo mkoani Kilimanjaro wakati akifunga Semina Elekezi kwa Wakuu wa Vyombo vya Usalama,Viongozi Waandamizi na Washiriki wa semina ambapo mada zilizolenga kuwajenga viiongozi hao waandamizi ziliwasilishwa na watoa mada kutoka taasisi mbalimbali za serikali.

Screenshot 2024-09-08 140123.png

Screenshot 2024-09-08 140210.png

Screenshot 2024-09-08 140156.png
Pia soma: Ally Mohamed Kibao auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana

‘Wizara hii ina vyombo ambavyo vimebeba taswira ya Serikali kwa maana nyingine vimebeba taswira ya wananchi,kwahiyo tukiwa tunayatambua hayo na tukitembea na dhana ya 4R tutaenda kuibeba dhana hiyo hasa kipindi hiki ambacho tunaelekea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu hapo mwakani kwahiyo mjue kwamba wizara hii ni tegemeo kubwa sana na tuhakikishe tunaingia katika uchaguzi nchi yetu ikiendelea kubaki salama," alisema Masauni.

Pia soma: LIVE - Uzi Maalum wa Matukio ya Kiusalama kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
 
Wanawaza uchaguzi mkuu! Sisi tunataka mambo ya kutekana yakomeshwe vinginevyo hakuna haja ya kuwa na jeshi la polisi! Mtu amefanya kosa apelekwe polis sio kutekwa na kuuliwa! Nchi inaingia kwenye laana hii
 
Mungu wa mbinguni amrehemu hayati Mwinyi

Kwamba Watu wanauwana katika Mazingira ambayo wewe ni Msimamizi Mkuu wa sekta Hiyo

Inasikitisha sana

Kwako Pascal Mayalla
 
Mungu wa mbinguni amrehemu hayati Mwinyi

Kwamba Watu wanauwana katika Mazingira ambayo wewe ni Msimamizi Mkuu wa sekta Hiyo

Inasikitisha sana

Kwako Pascal Mayalla
Ni muhimu kiongozi madhubuti kujizatiti na kuwajibika iliwezekana field kabisa kusimamia taasisi zake za kiuchunguzi kuhakiisha ukweli juu ya matukio yanayolalamikiwa unabainika na wahusika wote wanatiwa nguvuni bila hata moja kuponyoka.

Dhana ya kujiuzulu nadhani haina maana sana zaidi ya sifa za kihistoria tu,

Lakini pia kujiuzulu nadhani ni kwa wale waliochoka kuhudumu kwenye nafasi zao, waliochoka malalamiko na lawama, na ambao wamekosa mawazo mapya, mipango na fikra mbadala wa kujiondoa kwenye mikwamo kadha wa kadha kwenye taasisi wanazo zisimamia, lakini pia kukatishwa tamaa na sintofahamu za za mara kwa mara hususani za aina hii.

Ni muhimu kutokukata tamaa bali kujizatiti kudeal na kila changamoto na huo ndio uongozi
 
Back
Top Bottom