Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,865
- 4,692
Salaam
Kumekuwa na tabia za Viongozi wa kiasa nchini kwetu kujiweka mbele sana kwenye majanga kama mafuriko na mengine.
Kwanza, ni matumizi mabaya ya pesa za umma viongozi wengi kujazana sehemu moja ya tukio jambo ambalo kiongozi mmoja anayehuaika anaweza kutangulia kusimamia eneo lake.
Pili, tabia hii inasababisha Wataalamu na Wananchi kuwazingatia wao zaidi kuliko kuokoa na kutatua matatizo ya Wananchi.
Tafadhali viongozi waache tabia za kuleta siasa na kutaka kuonekana sana wakati wa majanga. Waachie Wataalamu na baadaye waje wao kutazama utatuzi wa tatizo ulipofikia.
Nawasilisha