Wasanii wa nyimbo za Injili acheni kumpigia Mungu kelele

Setfree

JF-Expert Member
Dec 25, 2024
2,689
3,698
Naongea na nyinyi mnaojiita wasanii wa nyimbo za Injili (Gospel Artists), vikundi vya kwaya na bendi. Nyinyi mnaotunga na kuimba nyimbo za Injili, nyimbo za sifa na kuabudu lakini maisha yenu ni ya mchanganyo! Maisha ya uvuguvugu. Nyinyi mnaopenda kumwimbia Mungu lakini dhambi hamtaki kuziacha. Mnaimba sana kwenye matamasha ya Injili, kanisani na kwenye mikutano ya Injili, lakini hamtaki kuacha matendo haya ya kidunia yaliyoandikwa katika Wagalatia 5:19-26 BHN

Basi, matendo ya kidunia yanajulikana: Uzinzi, uasherati, ufisadi; kuabudu sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, choyo, mabishano, mafarakano; husuda, ulevi, ulafi na mambo mengine kama hayo.

Kwa kufanya hayo mnasababisha Jina la Mungu linatukanwa. Kwa kutenda hayo, tambueni leo kwamba nyimbo zenu ni kelele mbele za Mungu, na wala hataki kusikia sauti za vinanda vyenu.
Amosi 5:23 SRUV
Niondoleeni kelele za nyimbo zenu; kwa maana sitaki kuzisikia sauti za vinanda vyenu.

Basi, tubuni, mkamrudie Mungu ili yeye afute dhambi zenu, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kutoka kwake Bwana(Matendo 3:19).

Mkitubu na kurejea kikamilifu, nyimbo zenu zitapata kibali mbele za Mungu.

Yeyote anayesikia maneno haya bila kuyazingatia na kuyafanya, anafanana na mtu mjinga aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga. Mvua ikanyesha, mito ikafurika, pepo kali zikavuma na kuipiga nyumba hiyo, nayo ikaanguka kwa kishindo kikubwa(Mathayo 7:24-27)

Blessed and wise is the one who receives the message of this thread with discernment and applies it with diligence.
your_browser_is_not_able_to_play_this_audio
 
Umeanza kutoka kwenye mstari sasa,utakata wasiimbe MAWE Yaimbe si ndio?

Maana maandiko yanasema msipo sifu MAWE yatasifu
 
Umeanza kutoka kwenye mstari sasa,utakata wasiimbe MAWE Yaimbe si ndio?

Maana maandiko yanasema msipo sifu MAWE yatasifu
Kila alitajaye jina la Bwana(kwa kuimba au kwa maneno) na auache uovu.
2 Timotheo 2:19 SRUV
Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye mhuri huu, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila alitajaye jina la Bwana na auache uovu.
 
Kila alitajaye jina la Bwana(kwa kuimba au kwa maneno) na auache uovu.
2 Timotheo 2:19 SRUV
Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye mhuri huu, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila alitajaye jina la Bwana na auache uovu.
Sawa mama nimekubali
 
Umeanza kutoka kwenye mstari sasa,utakata wasiimbe MAWE Yaimbe si ndio?

Maana maandiko yanasema msipo sifu MAWE yatasifu
Usisome mstari mmoja tu wa Biblia ukaishia hapo. Soma Maandiko haya kwa makini ujue ni kina nani walioambiwa wakiacha kumsifu Yesu MAWE yatapaza sauti(yatapiga kelele).

Luka 19:28-40
Na alipokwisha kusema hayo, alitangulia mbele akipanda kwenda Yerusalemu. Ikawa alipokaribia Bethfage na Bethania, kwenye mlima uitwao wa Mizeituni, alituma wawili katika wale wanafunzi, akisema, Nendeni mpaka kijiji kile kinachowakabili, na mtakapoingia ndani mtaona mwana-punda, amefungwa, ambaye hajapandwa na mtu ye yote bado, mfungueni mkamlete hapa. Na kama mtu akiwauliza, Mbona mnamfungua? Semeni hivi, Bwana anamhitaji. Na wale waliotumwa wakaenda wakaona kama alivyowaambia. Na walipokuwa wakimfungua mwana-punda, wenyewe waliwaambia, Mbona mnamfungua mwana-punda? Wakasema, Bwana ana haja naye. Wakampeleka kwa Yesu, wakatandika nguo zao juu ya mwana-punda, wakampandisha Yesu. Na alipokuwa akienda walitandaza nguo zao njiani. Hata alipokuwa amekaribia matelemko ya mlima wa Mizeituni, kundi zima la wanafunzi wake walianza kufurahi na kumsifu Mungu kwa sauti kuu, kwa ajili ya matendo yote ya uwezo waliyoyaona, wakasema, Ndiye mbarikiwa Mfalme ajaye kwa jina la Bwana; amani mbinguni, na utukufu huko juu. Baadhi ya Mafarisayo waliokuwa katika mkutano wakamwambia, Mwalimu, uwakanye wanafunzi wako. Akajibu, akasema, Nawaambia ninyi, wakinyamaza hawa, mawe yatapiga kelele."

Umeona? Waliokuwa wakimsifu Yesu katika tukio hilo ni kundi zima la Wanafunzi wa Yesu. Mafarisayo walipomwambia Yesu awakanye waache kumsifu ndipo alipowajibu "wakinyamaza hawa[wanafunzi], mawe yatapiga kelele."

Jiulize sasa, je hao wanafunzi wa Yesu wanaotajwa hapo walikuwa wazinzi? Walikuwa walevi?

Mungu hapendezwi na watu vuguvugu.
Ufunuo 3:16 SRUV
Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.

TUBU LEO
 
Ubarikiwe sana
 
Hata kelele za furaha waache?
Kama ni kelele za furaha kwa ajili ya kumfurahisha Mshana Jr , ruksa!
Lakini kama wana lengo la kumpigia Bwana kelele za furaha, sharti kwanza wauache uovu.
2 Tim 2:19
Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye muhuri hii, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila alitajaye jina la Bwana na auache uovu.
 
Yaani Kama Mimi Ni Mkristo ila Kuna Muimbaji nikimuona tu namuelewa mpaka nimeacha kusikiliza nyimbo zake nisije nikamchukulia Sheria mkononi.
Anaitwa" Bella Kombo" Namuelewa.... saaaa.... Mungu aniepushie Dhambiiiii
Ni pisi kali haswa anasura kama ya cocastic
 
nimeipenda hii ndugu mshana jr
Kama umeipenda hiyo, hii hapa👇 je, unaichukia?
Zaburi 32:11 BHN
Furahini na kushangilia kwa sababu ya Mwenyezi-Mungu enyi waadilifu; pigeni vigelegele vya shangwe enyi wanyofu wa moyo.

Ni nani amefikia viwango vya kuimba na kupiga kelele kama Daudi?

Daudi alipofanya dhambi tu Bwana alimkemea.
Katika 2 Samweli 12:1-14, tunaona Nabii Nathani akimwendea Daudi na kumkaripia kwa dhambi aliyotenda ya uzinzi na uuaji.

Sikiliza anavyokemewa:
2 Samweli 12:9-13
“Kwa nini umemdharau Bwana, ukafanya yaliyo maovu machoni pake? Umempiga Uria Mhiti kwa upanga, nawe umemtwaa mkewe awe mke wako; umemwua kwa upanga wa wana wa Amoni.”

“Basi sasa, upanga hautaondoka nyumbani mwako milele, kwa sababu umenidharau, ukamtwaa mke wa Uria Mhiti awe mke wako.”


Daudi alitubu, akasamehewa.
Daudi akamwambia Nathani, Nimetenda dhambi juu ya Bwana. Nathani akamwambia Daudi, Bwana naye ameiondoa dhambi yako; hutakufa.”

No matter how great a singer you are—like David—God will not tolerate your sins.
cc: Mshana Jr
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…