Wanawake wengi huondoka na Watoto wakidhani Wanaume watawafuata. Sijui nani aliwadanganya kuwa Mwanaume mtego wake ni Mtoto.

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
25,196
60,298
WANAWAKE WENGI HUONDOKA NA WATOTO WAKIDHANI WANAUME WATAWAFUATA. SIJUI NANI ALIWADANGANYA KUWA MWANAUME MTEGO WAKE NI MTOTO.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Watoto uliowazaa wanaumuhimu Kwa Mwanaume pale unapoishi naye. Weka akilini hiyo.
Weka na hii Hapa, Mwanamke anaumuhimu Kwa Mwanamke pale wanapoishi Pàmoja.

Zingatia, Wanaume wengi hujiona wanawajibu Kwa wale anaowaona. Yaani waliokaribu Yake ndîo Huona umuhimu waô kuliko waliombali, asiowaona. Kisaikokojia Mwanaume huchukua hatua na kufanya reactions Kwa Kuona. Yaani macho yanaathari kûbwa Kwa Mwanaume.

Ni Kosa la kiufundi Kwa Mwanamke kutokujua Saikolojia hii.
Hata ukiwa Mke WA Ndoa, kadiri unavyokuwa Karibu na Mumeo ndivyo wajibu wa Mwanaume huyo kwako unaongezeka.

Wanawake wengi hufanya Makosa ya kiufundi ndàni ya Ndoa. Mfano, wamegombana kidôgo na Mumewe anafungasha virago anaondoka.
Hilo ni Kosa la kiufundi.

Mwanaume hanaga Muda wa kukufikiri ukiwa Mbali naye. Weka akilini hiyo.

Mwanaume anakuwa na stress pale anapokuona hauna Raha, umenuna, au haujala kisa yeye hajatafuta Hana Pesa. Na wengi hufa mapema Kwa sababu hiyo.

Unapogombana na Mwanaume ukabaki hapohapo Usiku hawezi Kulala vizuri. Lakini ûkienda kwèñu au ukiondoka nakuhakikishia atalala usingizi mtamu na haitachukua Muda atakusahau.

Mwanaume anapokufukuza nyumbani kwàke lengo lake kuu ni awe na Amani na utulivu Kwa sababu ukiendelea kukaa pale Wakati mmegombana Moyo wake hautakuwa na furaha, kula hatakula Vizuri, Kulala hatalala, akienda Bar anakuwaza tuu wewe. Anawaza atarudije nyumbani.

Uchunguzi wangu unaonyesha Wanawake wengi yàani ya zaidi ya Asilimia 90% waliojaribu kukimbia Nyumba hawakupigiwa Simu na waume zào ili warudi.

Wanawake Baadhi Yao walirudi wènyewe Kwa aibu na Hasira kuwa hata wakiondoka Mwanaume Hana uhitaji kihivyo.

Wanaume hufuatilia Wake Zao wakiwa chini ya Mmiliki Yao yàani nyumbani Kwa Mume lakini Mke akishaondoka Mume anasahau kama yeye ni Mume na Uhuru wake huongezeka.

Kûna Wanawake hufikiri akiondoka na Watoto ndîo Mume atamfuata. Hilo ni Kosa kûbwa Sana.

Ndîo maana kûna Sheria ya kumlazimisha Mwanaume Kutoa huduma Kwa Watoto Kwa sababu nature ya Mwanaume husahau na kupoteza uthamani wa kitu kilichombali naye.
Hakuna Sheria za kulazimisha Mwanamke kuhudumia Watoto wake Kwa sababu naturally Wanawake wàpo hivyo.

Wanawake wengi waliokimbia na Watoto wamejikuta wakitelekezewa Watoto na wanahudumia wènyewe.

Alafu siô kwamba Wanaume wanafanya makusudi Nope! Yaani Ipo hivyo tuu.
Tenà Mwanamke akiwa na mdomo mchafu au anajifanya gangwe ndîo mambo huweza kuwa Magumu Kabisa.
Mwanamke anayependa Ligi hujikuta kwèñye shida zaidi.

Mtazamo wa Mama Kwa Mtoto ni tofauti Kabisa na mtazamo wa Baba Kwa Mtoto.

Wanawake wengi hufikiri Ile mtazamo waô juu ya Watoto waô ndivyo ulivyo Kwa Sisi Wanaume Jambo ambalo siô KWELI.
Ndîo maana Kesi za wababa waliotelekeza familia au Watoto waô zinaripotiwa kîla kukicha.

Wamama Matumaini ya Maisha Yao ya baadaye Yapo Kwa Watoto. Lakini Wanaume matumaini Yao ya baadaye hayapo Kwa Watoto isipokuwa Ñguvu zào wènyewe.

Kwanza Mwanaume ili awe Mwanaume hawezi kuwa na mtazamo wa kumtegemea yeyote Yule sembuse Mtoto aliyemzaa.

Wababa wengi huamini waô ndîo weñye baraka za Watoto waô. Hii ni tofauti na Wamama.
Kiutamaduni na kiroho Baba ndiye anayetoa Baraka Kwa kizazi chake. Mama hawezi Kutoa Baraka yoyote Kwa Mtoto ikashika.

Wanawake weñye Akili hujua kuwa Mtoto aliyemzaa Ipo Siku atahitaji maneno ya Baraka Kutoka Kwa Baba yake. Hivyo hata wakigombana vipi na Mzazi mwenza huhakikisha kuwa Mwanaume aliyezaa naye havunji mahusiano na Baba yake.

Wababa wengi hujua kuwa Mtoto lazima atamtafuta hasa akifika Umri wa kujitafutia Maisha ili apate Baraka Zake.
Na endapo hatamtafuta ni wazi Mtoto huyo hawezi kufika popote na kizazi chake kitakuwa hakina la maana lenye kufika mbali.

Watoto wengi wasio na Baraka za Baba hufanikiwa zaidi kwèñye Kazi za aibu na kujidhalilisha na kudhuru kama vile Muziki wa kukaa uchi, Madawa ya kulevya, Filamu za ngono, n.k.

Ni ngumu Sana tenà sana Mtoto kufanikiwa kwèñye ishu za maana kama hataweka mambo yake Sawa na Babaake.
Hiyo kijamii huitwa kukosa Radhi za Wazazi(na Hapa anayezungumziwa ni Baba).

Ni ngumu Sana Mwanamke kuwa mjeuri na kumfanyia visa Mwanaume alafu huyo Mwanaume ambariki Mtoto kabisakabisa yàani amkunjulie Roho yôte. Ngumu Sana.
Kwa sababu Watoto wengi hufuata mawazo na maonî ya mama zào.
Ni Watoto wachache Sana wenye Akili wanaojua nini chakufanya pale Wazazi wanapogombana na kuachana.

Siô ajabu, Mtoto anaweza akasoma Sana lakini asifanikiwe Sana. Yaani kivile.

Lakini chunguza Watu waliofanikiwa na wasio na mambo ya aibu na fedheha wengi waô wàpo vizuri na Wazee zào(Baba na Babu zào).

Chunguza waliofanikiwa lakini wanamambo ya aibu na fedheha kama ushoga, kucheza pono, kukaa uchi, kuuza madawa, Majambazi, wamamuziki wôte wakaauchi na watukanaji, wacheza Filamu wôte weñye mafanikio lakini wanatabia za hovyo Asilimia kûbwa wamegombana na Baba zao au hawakulelewa na Baba zào.

Acha nipumzike sasa

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa Sasa Dar es salaam
 
Mwanaume anayejitambua familia Yake iwe mbali au karibu ataihudumia Kadri ya uwezo wake.
Wapo wanawake tunawaona wanandoa zao wanaishi na wanaume nyumba moja na bado huduma baba hatoi...
 
Ni vizuri mwanaume kukaa na wanae unawahudumia vizuri ,kuliko mtoto akae na mama yake anatumika kama chambo ya kupiga vizinga vya reja reja.
Ila, tukiweka mbali ishu ya pesa. Tafiti zinaonesha watoto wa mzazi mmoja wengi wanaofanikiwa ni wale waliolelewa na baba zao kuliko mama. Nyingine zinaenda mbali kuangalia watu waliojela na waliodhurika na madawa ya kulevya, asilimia kubwa walitokea familia ya mzazi mmoja ambaye ni mama.

Malezi ya baba mwenye kutambua wajibu wake ni muhimu kwa ustawi wa familia na jamii
 
Ila, tukiweka mbali ishu ya pesa. Tafiti zinaonesha watoto wa mzazi mmoja wengi wanaofanikiwa ni wale waliolelewa na baba zao kuliko mama. Nyingine zinaenda mbali kuangalia watu waliojela na waliodhurika na madawa ya kulevya, asilimia kubwa walitokea familia ya mzazi mmoja ambaye ni mama.

Malezi ya baba mwenye kutambua wajibu wake ni muhimu kwa ustawi wa familia na jamii
Naunga mkono hoja ,mimi watoto wangu wote wapo kwangu , na hii imewapa nafasi mama zao kuolewa, japo mwanzo kulikua na vita ila sasa tupo vizuri mno na ninawapa nafasi ya kuwatembelea mama zao ,.
 
Naunga mkono hoja ,mimi watoto wangu wote wapo kwangu , na hii imewapa nafasi mama zao kuolewa, japo mwanzo kulikua na vita ila sasa tupo vizuri mno na ninawapa nafasi ya kuwatembelea mama zao ,.
Sauti ya baba kwa wanae inawapa kujiamini na kuwajengea nidhamu toka utotoni mpaka wanapojitegemea.

Pongezi nyingi kwako 👏
 
Back
Top Bottom