Wamiliki wa Hotel zilizoko ufukweni, marufuku kulipisha kiingilio

Kuna siku nakumbuka huko kigamboni nimetoka tu baharini niko beach mchangani nikafwatwa na walinzi wakaniambia umeingiaje,kumbe wanalipia bwana
 
Hivi hawaongezagi thamani? Wanatoza tu pesa hawaweki taa, kusafisha fukwe, kutunza miti ya kupumzikia, muziki, parking e.t.c?

Kama hawaongezi thamani ni kweli hakuna sababu ya tozo. Ila kama wanaongeza thamani kuna haja ya kulifikiria hili upya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi sidhani kama ni hivyo...hutozwi kuogelea unatozwa kutumia huduma za hoteli hiyo. Kwa mfano ukiweza kupaa angani ukatua baharini usawa na hiyo hoteli ya whitesands na kuendelea na mambo yako na baada ya hapo ukapaa ukaondoka zako hakuna mtu anayetakiwa kukuchaji. Ukitumia huduma nyingine zozote zilizowekwa na hoteli hiyo ni lazima ugharamie.

Mfano hai: Kule kigamboni kuna beach kama tatu zinafuatana..Kipepeo, Sunrise na South Beach..ukiweza kupita vichochoroni ukaingia baharini ukaogelea hadi usawa wa South beach hakuna mtu atakudai..na kwa kuwa zinapakana waweza kuendelea kuogelea usawa wa hoteli yoyote hapo.

Utakapotoka majini na kwenda kukaa umbali wa hizo mita 60 nje ya bahari (kisheria) au kutumia viti au chochote ambacho kiliwekwa na hoteli hiyo kwa ajili ya watu wake ni lazima utadaiwa.

Huo ni mtazamo wangu!

Uko vizuri. Nadhani kiingilio inayozungumzwa ma wanachochajiwa ni kwajili ya huduma wanayotoa. Kama Viti,Ulinzi,Bafu , Vyoo na sehemu zingine ,atumizi ya Swimming Pool. Tatizo watoa matamko hawajafanya utafiti.
 
ee37b72ca3182652846a470a68bdee80.jpg
http://
Wamiliki wa Hotel za kitalii zilizoko katika fukwe mbalimbali nchini wamepigwa marufuku kutoza wananchi kiingilio wanapoenda kupumzika na kuogelea katika fukwe hizo.

Marufuku hiyo imetolewa na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC).

Mwanasheria wa NEMC, Manchari Heche alisema kuwa kwa mujibu wa sheria, fukwe zote ni mali ya umma hivyo hakuna anayepaswa kuzitumia kwa biashara akiwatoza fedha wananchi.

“Fukwe zote ni mali ya umma kwa sababu kuna mipaka yake, hivyo kitendo cha kuwatoza wananchi fedha kuingia katika fukwe hizo ni kosa kisheria na wanaofanya hivo wanapaswa kuacha mara moja,” alisema Heche.

Baadhi ya hotel zilizoko katika fukwe hususan jijini Dar es Salaam zimekuwa zikitoza wananchi kiingilio cha kati ya shilingi 10,000 na 40,000 kwa kutembelea fukwe hizo kupunga upepo na kuogelea.

Katika hatua nyingine, Heche aliwataka wawekezaji wote waliojenga katika fukwe za bahari kuhakikisha wako umbali wa mita 60 kutoka Baharini, kinyume cha hapo nyumba na hotel zao zilizo chini ya umbali huo zitabomolewa.

Chanzo: Dar24

Tunataka manispaa husika watengeneze barabara za kuingia kwenye fukwe, kama ramani za mji husika sinavyo onyesha, lakini kwakiwango kikubwa hili jambo lina sum is sana watu wanakwenda ufukweni.
 
Kama Kila mtu ataenda na bites na/au drinks zake maintenance ya facilities Kama w/c itakuwaje?
 
Back
Top Bottom