Wakati Mwingine unatamani kusikia Magazeti yetu yakiwa na vichwa vya habari zifuatazo

Raisi wa Tanzania Leo atafungua Canal Mkondo wa Bahari unaoziunganisha Bahari ya Hindi lake Victoria,Tanganyika na Nyasa Mkondo huo utazisaidia sana Nchi Masikini jirani na Tanzania Tajiri wa kila kitu kuweza kuwa na bandari zao. Wakati huo huo Tanzania Itatoa Mikopo ya kuondoa umasikini kwa raia wote wa nchi za africa Mashariki na kati pamoja na Africa ya Kusini msaada huo utasiniwa na maraisi wa nchi husika watakaofika Ikulu ya Dodoma Satellite City.

Waziri wa Digital atazindua Ubongo mpya wa binadamu wenye uwezo wa hali ya juu katika kutunza kumbukumbu ambao utakuwa replaced na ubongo wa Wananchi wote wa Tanzania huku Chuo Kikuu cha Technologia kikizindua Mabawa kwa ajili ya Binadamu ili nao waluke kama ndege.

Waziri wa Haki amesisitiza Binadamu wote ni Sawa na wana haki sawa hivyo mpango wa kuzisaidia Nchi zote Duniani kufanana kama Tanzania kiuchumi na Siasa safi na Maendeleo ni Lazima hivyo ameitisha Mkutano wa Wakuu wote Duniani wakiwepo al qaeda kushiriki mkutano huo ili dunia iwe salama Tanzania haiwezi kulinda dunia peke yake haswa na huu uvamizi wa mara kwa mara wa Aliens kutoka sayari za mbali maana Sayayari za karibu zote Tanzania inazitawala kwa Haki.

Chuo cha kilimo kinazindua mbegu ndogo ambazo zitazuia njaa na kurutubisha mwili mbegu hizo binadamu atakula mara moja kwa Miaka kumi ndipo atasikia njaa tekinolojia iliyotumika ni ya hali ya juu sana kwani hewa ya oxygen ikivutwa bakteria huvutiwa kwa wingi mbegu inawegeuza chakula njaa hupotea na mwili hukaa sawa na uchafu hutoka kwa njia ya ngozi.
 
Kuota kama kiongozi aliefoji vyeti atakufa kunaruhusiwa? na mm nataka niote sasa hivi.
 
Ndoto yako si mbaya ila bahati mbaya tulio wengi wala hatuna raghba na hayo mambo.

Sisi twapenda zaidi habari za akina Bashite, Gwajima, Koromije, na vyeti ghushi.

Hayo uliyoyaorodhesha ni magumu mno na ni mambo ya Wazungu huko Ulaya.

Ndivyo tulivyo!

Maendeleo hayaji kwa kuota. Mateja huota sana kwenda Marekani, lakini huishia Kwa Mtogole.

Maendeleo ni hatua. Hatua mojawapo muhimu kabisa ni kuwaondoa vihiyo na walioghushi vyeti katika korido za watoa maamuzi. Hao wana madhara makubwa kwa maendeleo, kuliko madhara ya ukimwi.
 
Ikiwa tuliowapa mamlaka ya kutuongoza ndio hawa wanaonunua vyeti vya watu wengine, hayo tutaendelea kusikia kwa nchi za wenzetu ambao wapo serious.

Wakati Mwingine unatamani kusikia Magazeti yetu yakiwa na vichwa vya habari zifuatazo.

1. Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam College ya Injinia wamefanikiwa kutengeneza daraja wakiwa wanafanya majaribio na daraja hilo litakaa miaka 50 ndiyo liweze kuhitajika kufanyiwa marekebisho. Ni daraja la kisasa kabisa kutokea.

2. Chuo cha Taifa cha Usafirishaji kitazindua helkopita mpya na ya kisasa kabisa mwezi huu ambayo imetengenezwa na wanafunzi wa chuo hicho na Rais ataenda kuizundua helkopita hiyo mwezi ujao.

3. Tanzania imeimarisha zaidi viwanda vyake ambayo ni nguzo ya viwanda vyote nchini. Viwanda hivyo viko chini ya Serikali ya Tanzania ambavyo ni vya Chuma, Kemikali na Injinia.

4. Tanzania inaweza kuwekewa vikwazo vya uchumi kwa kusisitiza kuwa viwanda vyake vya nyuklia ni kwa sababu ya nishati ya umeme tu na si vingine.

5. Msanii tajiri kuliko wote Afrika kutoka nchini Tanzania atafanya ziara kubwa nchini Marekani na Wasanii wa Marekani wanapigana kumbo ili angalau kumuomba wamshirikishe kwenye nyimbo zao.

6. Tanzania ndiyo nchi inayoongoza kwa kuwa na uchumi imara Afrika.

8. Tanzania ni nchi pekee Afrika ambayo kila Mtanzania ana uhakika wa kupata maji na umeme kwa kiwango cha asilimia themanini mijini na vijijini.

9. Rais wa Tanzania kesho atasafiri kwenda Mbeya na baadaye ataenda Kigoma kwa kutumia treni ya mwendo kasi.

10. Wakulima na Wafugaji nchini Tanzania hali zao kiuchumi ni imara zaidi kwa sababu serikali inawajali na kuwawezesha sana.

11. Madaktari kutoka Tanzania wamegundua dawa ya kuzuia kansa na ukimwi.

12. Rais wa Tanzania apewa zawadi ya Mo Ibrahim kuhusu utawala bora baada ya kukosa mshindi miaka mingi.

Natamani Magazeti yetu siku moja yaandike hivyo. Ni lini?. Sijui, lakini kwa Mwenyezi Mungu yote yawezekana. Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika.

02/03/2017.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Serikali ya Tanzania yasikia kilio cha wengi yapunguza kodi toka 18% mpaka 15%, n kufuta kodi kandamizi kwa wazawa wanaoanzisha biashara...
 
Serikali ya Tanzania yaongeza kima cha chini na kufikia laki 6 kwa mwezi. Pia wafanyakazi wote nchini ambao mishahara yao ni chini ya milioni moja hawatakatwa kodi kuanzia July 1, 2017.

Serikali ya Tanzania yasikia kilio cha wengi yapunguza kodi toka 18% mpaka 15%, n kufuta kodi kandamizi kwa wazawa wanaoanzisha biashara...
 
Leo ni 2/3/2017 zaidi ya miezi mitano tangu ajira zisitishwe.
Kesho nikiamka natamani nikute pm katekeleza alichosema.

"Kairuki atumbuliwa kwa kushindwa kutoa jibu muafaka la ajira"
-Atakiwa na yeye akajiajiri
-Kigwangala amfuatia nyuma
 
Ukiachilia mbali wananchi wanaopenda kula Ubuyu daily, Je viongozi wenye dhamana katika maeneo husika wamewekeza kiasi cha resource ili tufikie hatua hiyo ?

So far viongozi tulionao wamejikita kwenye udaku na vijembe wakiongozwa na Dr Yohana mwenyewe.

Na ndo maana kipindi cha nyuma Le Mutuz aliwahi kusema kitu kimoja very profound, kwamba, viongozi wetu nao ni reflection yetu sisi wenyewe wananchi.

Kitu ambacho ni kweli.

Hao viongozi hutoka miongoni mwa sisi wananchi. Huwa hawashushwi toka mbinguni au toka sayari ingine.

Hutoka humu humu kwenye jamii.

Uongo?
 
Lol! Hili nalo neno. Elimu ya kuunga unga na kuongoza nchi wapi na wapi! Ni lazima atumie vitisho ati!

Mtu hakuwahi kufaulu shuleni tangia shule ya msingi mapaka chuo, halafu anawaongoza wasomi
 
Nadhani kuna tofauti kati ya Hapa kazi tu na Hapa Kesi tu. Ila kama hakuna tofauti basi endelea kutamani.
 
Wakati Mwingine unatamani kusikia Magazeti yetu yakiwa na vichwa vya habari zifuatazo.

1. Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam College ya Injinia wamefanikiwa kutengeneza daraja wakiwa wanafanya majaribio na daraja hilo litakaa miaka 50 ndiyo liweze kuhitajika kufanyiwa marekebisho. Ni daraja la kisasa kabisa kutokea.
madaraja yanajengwa na makapuni ya ujenzi sio vyuo vikuu. vyuo vikuu kazi yao kuzalisha watalamu. wapi zitatoka pesa za majabio ya kutengezeza garaja la kisasa tena kubwa kiasi hichoo_O? hapa umewaza opp ndugu:p

2. Chuo cha Taifa cha Usafirishaji kitazindua helkopita mpya na ya kisasa kabisa mwezi huu ambayo imetengenezwa na wanafunzi wa chuo hicho na Rais ataenda kuizundua helkopita hiyo mwezi ujao.
hivi kumbe hata hizo dege tunazinunu kutoka vyuonio_O. vyuo vinazalisha wataalamu, na makapuni kuwatumia wataalamu ktk uzalishaji.

jiunge na makampuni upante uzoefu kutoka kwa wazoefu, kisha uchangie ubunifu wako kwa kushare na wazoefu.
 
Wakati Mwingine unatamani kusikia Magazeti yetu yakiwa na vichwa vya habari zifuatazo.

1. Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam College ya Injinia wamefanikiwa kutengeneza daraja wakiwa wanafanya majaribio na daraja hilo litakaa miaka 50 ndiyo liweze kuhitajika kufanyiwa marekebisho. Ni daraja la kisasa kabisa kutokea.

2. Chuo cha Taifa cha Usafirishaji kitazindua helkopita mpya na ya kisasa kabisa mwezi huu ambayo imetengenezwa na wanafunzi wa chuo hicho na Rais ataenda kuizundua helkopita hiyo mwezi ujao.

3. Tanzania imeimarisha zaidi viwanda vyake ambayo ni nguzo ya viwanda vyote nchini. Viwanda hivyo viko chini ya Serikali ya Tanzania ambavyo ni vya Chuma, Kemikali na Injinia.

4. Tanzania inaweza kuwekewa vikwazo vya uchumi kwa kusisitiza kuwa viwanda vyake vya nyuklia ni kwa sababu ya nishati ya umeme tu na si vingine.

5. Msanii tajiri kuliko wote Afrika kutoka nchini Tanzania atafanya ziara kubwa nchini Marekani na Wasanii wa Marekani wanapigana kumbo ili angalau kumuomba wamshirikishe kwenye nyimbo zao.

6. Tanzania ndiyo nchi inayoongoza kwa kuwa na uchumi imara Afrika.

8. Tanzania ni nchi pekee Afrika ambayo kila Mtanzania ana uhakika wa kupata maji na umeme kwa kiwango cha asilimia themanini mijini na vijijini.

9. Rais wa Tanzania kesho atasafiri kwenda Mbeya na baadaye ataenda Kigoma kwa kutumia treni ya mwendo kasi.

10. Wakulima na Wafugaji nchini Tanzania hali zao kiuchumi ni imara zaidi kwa sababu serikali inawajali na kuwawezesha sana.

11. Madaktari kutoka Tanzania wamegundua dawa ya kuzuia kansa na ukimwi.

12. Rais wa Tanzania apewa zawadi ya Mo Ibrahim kuhusu utawala bora baada ya kukosa mshindi miaka mingi.

Natamani Magazeti yetu siku moja yaandike hivyo. Ni lini?. Sijui, lakini kwa Mwenyezi Mungu yote yawezekana. Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika.

02/03/2017.
Hahahahahahahhahah hata shetani anaona kabisa haiwezekani.........
 
Back
Top Bottom