usilete ujuaji kwa daktari siku nyingine utamuua ndugu yako , yupo mtu x alienda kituo x hapa dar akakutwa na ugonjwa x wa macho akashauriwa operation tena ilikuwa anafanyiwa bure ila analipia kitanda na huduma ya chakula jumla 100k kwa siku 2 akampigia rafiki yake daktari akampoteza akamwambia akanunue dawa x bila kumuona , asee kaamka siku ya 2 jicho limeanza haribika kajifanya kuvimba akaamka next day jicho limeanza ozaa , kaenda mhimbili wanamwambia ni la kutoa tu , jamaa ss hv ni chongo , TUHESHIMU MADAKTARI , UKIPIMA CHUKUA DAWA HAPO HAPO MAANA KUNA SWALA LA QUANTITY NA DURATION VITAKUZINGUA TU
Hii sidhani kama nilikujibu wewe ,nadhani ilikuwa ni wrong tagSio Tu hela Mkuu namiliki pia Vituo vya Afya kadhaa..
Karibu!
Ulifanikiwa kupona hiyo typhoid?Kisa cha pili
Usiku mmoja niliumwa tumbo, asubuhi kulivyokucha tu nikaibukia kwenye kituo cha Afya.
Nikaandikishwa dirishani nikapewa maelekezo kuwa nikamuone daktari chumba fulani.
Daktari akaniuliza kinachonisumbua nikamjibu kuwa ni tumbo pale pale akaniambia hiyo ni Typhoid.
Nikambishia nikamuambia Typhoid haiwezi kuwa kwasababu nina miaka mingi nakunywa treated water na hata vyakula vibicho kama chumbari huwa sili.
Akaniambia hata kama unaepuka njia hizo bado njia za kuweza kupata Typhoid ni nyingi kwa mfano ukawa unakula migahawani.
Nikashangaa kusikia hoja ya aina hiyo kutoka kwa Doctor ikabidi nimuulize hao wadudu wanapenya vipi mpaka wakweza ku survive kwenye chakula ambacho kishakuwa boiled?
Maana yake hata ule ushauri wa kiafya kuwa tunywe maji yaliyo chemshwa basi hauwezi kuwa na impact yeyote kwenye kuzuia wadudu enezi wa Typhoid.
Doctor akaniambia Typhoid unaweza kuipata kwa njia nyingi hata kupitia maji ya chooni unayotumia kutawaza.
Hapo ndio nikabaki mdomo wazi. Akaniambia nenda maabara chumba kinachofuata ukapime.
Nikapima damu, majibu niliyosomewa na Doctor ni kuwa nina vidonda vya tumbo pamoja na Typhoid.
Wakanitajia gharama za dawa kuwa ni 25,000 nikawaambia sawa ila mi kwa saizi sina hiyo hela ila naombeni mnipe hiyo tipoti ya vipimo niondoke nayo ili nikipata hela niende duka la dawa niwaoneshe hiyo report wanipe dawa.
Wakakataa wakaniambia hawatoi ripoti ya vipimo na kama sina hela basi nirudi tu nyumbani nijipange, siku nikapata nitarrjea hapo wanipe hizo dawa.
Sikuridhika na majibu yao ya vipimo hususani ya kuniambia nina Typhoid. Nilipotoka hapo nikaenda kwenye kituo cha Afya Cha Arafa.
Sababu ya kwenda kwenye hicho kituo ni kutokana na kushawishiwa na rafiki yangu kuwa hicho ndio kituo kinachotoa huduma bora kwasababu mke wake alihudiwa hapo.
Kufupisha stori
Niliandikiwa vipimo viwili hapo Arafa
Kipimo cha kwanza kilisema nifanyiwe checkup ya Ultra Sound kuangalia damage ya tumboni
Kipimo cha pili kilikuwa ni damu. Vipimo vyote kwa ujumla niliambiwa nilipie 25,000.
Lakini nilipimwa kipimo kimoja tu ambacho ni cha damu. Hakukuwa na Ultra Sound na wala pesa yangu niliyolipia kwa ajili ya kipimo hicho haikurudishwa.
Nilipofika kwa daktari akaniambia vipimo vimeonesha nina vidonda vya tumbo akaniambia nenda dirisha la dawa
Nilipoenda kwenye dirisha la dawa niliambiwa nilipie 99,000.
Nikasema hiyo hela sina kwa sasa ila naombeni ripoti ya vipimo wakaninyima
Kwa bahati nzuri niliwahi kupiga picha ripoti ya maabara ila ile ya kwa Doctor sikuweza kuipata.
Almost Miezi minne now nimeweza kutibu vidonda vya tumbo kupitia maoni ya wana JF bila kutumia midawa yao ya kausha damu.
Hali ni mbaya kila.sehemu😂Bro, huku mitaani kuna vizahanati vingi sana vya kuganga njaa. Ukijichanganya unapigwa pesa tu.
Pole sana MkuuSiyo kila mahala kuna vituo vya afya au hospitali, kingine ni urasimu mkubwa, juzi nilienda hospital kubwa tuu ya rufaa nikatumia siku nzima Mpaka kumuona daktari.
Pamoja na kuwa na Bima ya afya bado nikaambiwa hivi vipimo 2 itabidi ulipe cash!! Kila nikijaribu kujua ni vipimo gani hivyo sikupata jibu. Kwenda kulipia hivyo vipimo nikaambiwa 180,000, ambayo muda huo sikuwa nayo.
Kwenye bima nikaambiwa nipime full blood picture tuu, ambayo niliwaeleza kwamba nimeifanya few days ago Kwenye hospital nyingine. Yaani siku ikaisha hivi hivi...