Viongozi wa Yanga SC ni muda wenu sasa kutoa ufafanuzi kwa mashabiki kwa nini Pacoume hachezi na wakati alishapona majeraha

NALIA NGWENA

JF-Expert Member
Oct 6, 2016
10,377
12,935
Pacoume ni moja kati ya mchezaji pendwa katika kikosi cha Yanga SC, siyo pendwa kwa kocha bali hata kwa mashabiki kutokana na kipaji chake cha kusakata kabumbu .

Cha kushangaza kumetokea sintofahau kila kukicha msemaji wa yanga Ally kamwe ansema kuwa Pakome yupo tayali na ni mzima wa afya lakini kila yanga wakicheza hata kwenye SUB au benchi jina lake halipo kabisa.

SWALI; je Yanga Sc kuna kitu kipo nyuma ya pazia juu ya Pacoume kinachofanya asicheze??
na kama hakuna mbona kupitia msemaji wa Yanga SC anadanganya mashabiki kuwa kocha ndiyo ana maamuzi ya kumchezesha ila hali yake ipo salama na kocha hamchezeshi??

Viongozi wa Yanga Sc mnapaswa kutolea ufafanuzi juu ya mchezaji Pacome na siyo kuwaeleza mashabiki maneno ya propaganda kama aliiomba dakika 20 kwenye dabi na kocha alimnyima mara Pakome yupo safi kiafya sasa mashabiki wanashindwa kuelewa kwa uzushi wa propaganda huo.
 
Back
Top Bottom