Ojuolegbha
JF-Expert Member
- Sep 6, 2020
- 795
- 504
UWT KUTOA MSAADA KWA WAATHIRIKA WA MAFURIKO RUFIJI NA KIBITI
Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) imeendelea na zoezi la ukusanyaji wa mahitaji muhimu kwa ajili ya kutoa misaada kwa waathirika wa mafuriko katika wilaya za Rufiji na Kibiti Mkoani Pwani.
Akizungumza na Wanahabari Aprili 15, 2024 katika ofisi za CCM mkoa wa Dar es salaam wakati wa zoezi la ukusanyaji wa misaada, Mwenyekiti wa UWT Taifa Ndg. Mary Pius Chatanda (MCC) ametoa wito kwa wadau mbalimbali kuendelea kutoa misaada.
“Naendelea kutoa wito kwa watu mbalimbali,mafuriko bado yanaendelea katika mikoa tofauti nchini,Watanzania wenzetu wanaishi katika mazingira magumu”.
Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) imeendelea na zoezi la ukusanyaji wa mahitaji muhimu kwa ajili ya kutoa misaada kwa waathirika wa mafuriko katika wilaya za Rufiji na Kibiti Mkoani Pwani.
Akizungumza na Wanahabari Aprili 15, 2024 katika ofisi za CCM mkoa wa Dar es salaam wakati wa zoezi la ukusanyaji wa misaada, Mwenyekiti wa UWT Taifa Ndg. Mary Pius Chatanda (MCC) ametoa wito kwa wadau mbalimbali kuendelea kutoa misaada.
“Naendelea kutoa wito kwa watu mbalimbali,mafuriko bado yanaendelea katika mikoa tofauti nchini,Watanzania wenzetu wanaishi katika mazingira magumu”.