Utaibiwa kizembe kwasababu ya tamaa zako. Kitu pekee utakachokula bure mjini ni mate yako tu

RIGHT MARKER

Senior Member
Apr 30, 2018
150
520
MHADHARA (89)✍️
Kitu pekee utakachokula/utakachomeza bure mjini ni mate yako tu. Lakini vingine vyote ni gharama. Hakuna cha bure, ni lazima ulicholishwa utalipia kifedha, kiroho, kimwili, kihisia, kiakili, n.k - kama hutolipia leo utalipa hata baadae.

Punguza au acha kabisa tamaa, uzembe, uroho, na shida zisizokwisha mbele ya jasho la wenzako.

1. Hujawahi kubeti wala kucheza mchezo wowote wa bahati nasibu. Unatumiwa ujumbe wa simu (SMS) kuwa umeshinda shilingi milioni 50, hivyo ili kupata hela yako tuma kianzio cha pesa kiasi fulani au piga simu namba "hii", na wewe unaingia mkenge 👁️Umerogwa au una wazimu?

2. Unaishi kwenye nyumba yako uliojenga. Unatumiwa ujumbe wa simu (SMS) isemayo "hiyo hela ya kodi ya nyumba tuma kwenye namba hii" - na wewe unatuma hela halafu baadae unalalamika umeibiwa 👁️Umerogwa au kuna michepuko umeipangishia nyumba?

3. Umetumiwa ujumbe wa simu (SMS) ya huduma za mikopo ya fedha. Kwasababu ya tamaa au shida unafuata maelekezo yao, lakini baadae unaambiwa tuma kwanza kianzio cha hela ili uingiziwe hela uliyokopa. Unachukua hela ndani kwako unatuma ili ukopeshwe hela 👁️Huo ni ukichaa au umerogwa?

4. Unakutana na watu wanakwambia kuwa wanauza madini (dhahabu) yenye thamani ya shilingi milioni 500, lakini wanataka kukuuzia wewe kwa shilingi milioni tatu (3) ili wewe ukauze upate hizo hela, na wewe unaingia mkenge mchana kweupe.

RIGHT MARKER
Dar es salaam.
 
MHADHARA (89)✍️
Kitu pekee utakachokula/utakachomeza bure mjini ni mate yako tu. Lakini vingine vyote ni gharama. Hakuna cha bure, ni lazima ulicholishwa utalipia kifedha, kiroho, kimwili, kihisia, kiakili, n.k - kama hutolipia leo utalipa hata baadae.
Hata mate yenyewe unaweza ukameza bure yakakupalia, ukapelekwa hospitali ukatoa hela.
 
Watanzania wengi bado ni wendawazimu,hao hawana tofauti na wale mchungaji wao sijui nabii anawapostia picha ya nyumba au gari kwenye mtandao anaandika “andika amen kesho utaendesha gari yako au utaamkia kwenye nyumba yako”

Kweli kama mazuzu yanaandika na ku-post tena yakiwa bado yamelala kwenye chumba kimoja cha giza alichopanga na kazi maalumu hana na kufanya kazi ngumu hataki,yaani mpaka leo wapo watu wanaamini kuandika ”Amina” watapata hela watapata wenza wa maisha even watapata magari na nyumba.

Maisha haya hao tu wanaoamka saa 11 alfajiri na kulala saa sita usiku kwenda kukaza kufanya kazi ngumu kwa akili zao zote na nguvu zao zote haijawa rahisi kupata walivyo navyo(na siyo wote waliofanikiwa) leo just ku-type amen unataka upate mali kama siyo kutaka kuolewa mjini hapa ni nini?
 
Ongezea na hii
Umemuona Demu ukamtamani aka kumpenda na wewe bila kufikilisha akili anakwambia ananjaa,ajala toka Jana , Vocha, Kodi, umeme imeisha, Mama anaumwa. Nk
Usikia Akisema
"Nihudumie kwanza ndo niamini kua unanipenda, Mwanaume kama anihudumii Mimi hiyo sio type yangu"
 
Back
Top Bottom