Utabiri wa Kijinga- Kinachoenda kutoka Kenya hivi karibuni

ecolizer baba

Member
Sep 29, 2010
88
310
Wasalamu ndugu zangu. Poleni na majukumu.

Nimekaa na kutafakari sana juu ya mwenendo wa Sasa za Kenya kwa hivi Sasa hasa baada ya kuonekana dhahiri kuwa mhimili wa Mahakama na ule wa Serikali wana uhasama. Yote haya ni kwa sababu ya kufutwa kwa matokeo ya Urais.

Jana tumeona Haki Mkuu David Maraga akilalamika hadharani huku akilituhumu jeshi la polisi kwa kushibdwa kutoa ulinzi kwa Majaji wa Mahakama ya juu.

Lakini pia tumeona kile kinachoitwa kuwa ni shtaka la kutaka DCJ Mwilu na Isaack Laneola wachunguzwe kwa kile kibachodaiwa kuwa ni kuwa na mawasaliano kati yao na watu wa NASA ikihusishwa na suala zima la kesi ya matokeo ya urais.

Maoni yangu juu ya hayo mambo mwili:

1. CJ David Maraga anazidi kufanya makosa. Yule ni Mwanasheria tena nguli. Ndiye reference ya mambo yote ya kisheria kwa Kenya sahivi. Hakupaswa kufanya press ya aina ile ya kulituhumu jeshi la Polisi na serikali. Haya ni makosa makubwa. Alipaswa kuongea na Rais Uhuru Kenyatta na kumueleza juu ya uhitaji wao wa ulinzi na kumuambia kuwa IGP ameshindwa kutekekeza maombi yao. Rais Kenyatta akishindwa kuwapa ushirikiano ndio angetoka before the public. But kile alichokifanya sio sawa. Amegeuka kuwa mwanasiasa badala ya kusimamia professionalism.!!

2. Tuhuma dhidi ya DCJ na Laneola kama ni za kweli huenda Mahakama ya nchini Kenya ikaingia kwenye tope zito. Na hii huenda ikafanya wananchi wakapoteza imani nayo. Lakini pia heshima ambayo ilikuwa imejijengea hivi karibuni kimataifa huenda ikafutika.

Sasa kutokana na malalamiko ya Maraga huenda watu wenye nia ovu wakatumia mwana huo kuwadhuru Majaji halafu Jubilee na serikali yake wakahusishwa. Hii ikitokea, believe me hali ya kisiasa itachafuka kwa sababu akina Raila watapata loop hole ya kulazimisha serikali ya nusu mkate.

Tuendelee kuwaombea wakenya katika kipindi hiki kigumu.

Naomba kuwasilisha.
 
KAMA SI YALE MASHITAKA (waliyofutiwa wale wakuu) KULE ICC....
TUNGEONA MAAFA MAKUBWA KUPATA KUTOKEA NCHINI KENYA
WAKENYA KUWENI WAVUMILIVU MSUBIRI KURUDIA KURA
MUNGU AWAPE AMANI..
 
Wakenya watamaliza matatizo yao wenyewe. Acha wapigane tu maana ndiyo jadi yao.
 
Wasalamu ndugu zangu. Poleni na majukumu.

Nimekaa na kutafakari sana juu ya mwenendo wa Sasa za Kenya kwa hivi Sasa hasa baada ya kuonekana dhahiri kuwa mhimili wa Mahakama na ule wa Serikali wana uhasama. Yote haya ni kwa sababu ya kufutwa kwa matokeo ya Urais.

Jana tumeona Haki Mkuu David Maraga akilalamika hadharani huku akilituhumu jeshi la polisi kwa kushibdwa kutoa ulinzi kwa Majaji wa Mahakama ya juu.

Lakini pia tumeona kile kinachoitwa kuwa ni shtaka la kutaka DCJ Mwilu na Isaack Laneola wachunguzwe kwa kile kibachodaiwa kuwa ni kuwa na mawasaliano kati yao na watu wa NASA ikihusishwa na suala zima la kesi ya matokeo ya urais.

Maoni yangu juu ya hayo mambo mwili:

1. CJ David Maraga anazidi kufanya makosa. Yule ni Mwanasheria tena nguli. Ndiye reference ya mambo yote ya kisheria kwa Kenya sahivi. Hakupaswa kufanya press ya aina ile ya kulituhumu jeshi la Polisi na serikali. Haya ni makosa makubwa. Alipaswa kuongea na Rais Uhuru Kenyatta na kumueleza juu ya uhitaji wao wa ulinzi na kumuambia kuwa IGP ameshindwa kutekekeza maombi yao. Rais Kenyatta akishindwa kuwapa ushirikiano ndio angetoka before the public. But kile alichokifanya sio sawa. Amegeuka kuwa mwanasiasa badala ya kusimamia professionalism.!!

2. Tuhuma dhidi ya DCJ na Laneola kama ni za kweli huenda Mahakama ya nchini Kenya ikaingia kwenye tope zito. Na hii huenda ikafanya wananchi wakapoteza imani nayo. Lakini pia heshima ambayo ilikuwa imejijengea hivi karibuni kimataifa huenda ikafutika.

Sasa kutokana na malalamiko ya Maraga huenda watu wenye nia ovu wakatumia mwana huo kuwadhuru Majaji halafu Jubilee na serikali yake wakahusishwa. Hii ikitokea, believe me hali ya kisiasa itachafuka kwa sababu akina Raila watapata loop hole ya kulazimisha serikali ya nusu mkate.

Tuendelee kuwaombea wakenya katika kipindi hiki kigumu.

Naomba kuwasilisha.
Mkuu, kwa uelewa wangu hii mihimili mitatu ya nchi inafanya kazi sawa, ndiyo maana jaji mkuu anapaswa kupigiwa salute na IGP kama alivyo spika wa Bunge, hivyo basi, Jaji mkuu hapaswi kuomba ulizi toka kwa rais, yeye anaviagiza vyombo vya ulinzi wa ndani ya nchi, isipokua jeshi bila kupitia rais wa nchi, mamlaka hayo amepewa kikatiba, mara kwa mara unamsikiaga Job Ndugai, huku kwetu akiamrisha polisi wamtafute wabunge fulani fulani na kuwapeleka kwenye kamati za bunge, hata mwananchi wa kawaida akilikosea heshima bunge, spika anao uwezo kisheria kuliagiza jeshi la polisi kumsaka na kumkamata ili apelekwe mbele ya bunge, bila kuomba kibali cha rais, lengo ni kuifanya mihimili hii iwe huru isitegemee fadhila za rais.

Kuhusu hotuba aliyotoa Maraga, kwanza katiba inamruhusu, kama inavyoruhusu mihimili ile mingine miwili, lakini anapozungimza ajikite kuzungumzia muhimili wake tu mazungumzo yajikite katika kuelimisha wananchi katika suala zima la kuheshimu katiba na utawala bora, kufuatia matamshi yaliyotolewa na rais na naibu wake, yaliyopelekea wafuasi wao kuandamana na kutoa vitisho, lisingekuwa jambo la busara kukaa kimya, kwa sababu ni vizuri akawafahamisha wananchi na dunia nzima nini kinaendelea na baadhi ya hatua alizochukua.
 
watanzania wamemwaga povu kweli aisee...kama hukubaliani na mtoa mada inabidi upite kimya kimya...sio kusema kuwa wakenya wanawachukia watz...nani amesema hilo? kuna vuta nikuvute kati ya hizi nchi mbili ila haijafikia chuki...tungekuwa tulisha pigana kitambo ila twaishi kwa amani tu...peace
 
Acha upuuzi kuita forum za kijinga,kwani wewe upo kwenye forum yanani siyawa Tz!? Ficha upumbavu wako.
Mkuu tofautisha hili ni jukwaa la siasa la Kenya sisi watanzania tuna jukwaa letu la siasa, kwa hiyo heshimu maoni yake na umjibu kwa busara
 
Mkuu tofautisha hili ni jukwaa la siasa la Kenya sisi watanzania tuna jukwaa letu la siasa, kwa hiyo heshimu maoni yake na umjibu kwa busara
Mkuu Mimi naheshimu maoni yake kabisa nawala sina tatizo juu ya hilo,yeye ndio hana busara Na ndicho kilichonikela yeye ataitaje forum zenu za kijinga inamaana ametutusi watumiaji wa Jukwaa la siasa na jukwaa la hoja mchanganyiko nasi ni wajinga sababu forum ni za kijinga!?Wawe na adabu kila mtu amuheshimu mwenzie
 
Mkuu Mimi naheshimu maoni yake kabisa nawala sina tatizo juu ya hilo,yeye ndio hana busara Na ndicho kilichonikela yeye ataitaje forum zenu za kijinga inamaana ametutusi watumiaji wa Jukwaa la siasa na jukwaa la hoja mchanganyiko nasi ni wajinga sababu forum ni za kijinga!?Wawe na adabu kila mtu amuheshimu mwenzie
Pole mkuu. Tuliza presha. Hapa sote tunakuja kujiburudisha tu.
 
Tuwaombee wakenya? Watatulipa? Acha wafu wazike wafu wao.

Mbona Kuna mambo mengi Tu ya kuombea Tz;
 
Nonsense CJ David Siyo mjinga kutoa press conference. Kenyata mwenyewe keshamtisha wewe ulitarajia amwambie halafu afanye nini?
 
Commercial break kidogo..sonko usiwaumize Dada zetu
FB_IMG_1505930389502.jpg
 
Back
Top Bottom