Sir John Roberts
JF-Expert Member
- Mar 1, 2017
- 11,792
- 21,149
Hii ndio inatakiwa safi sanaa
Ukiona hilo, ni kwa sababu leo angeshindwa kurudisha fomu akiwa mateka. CCM wamelikoroga wao wenyewe kwa kuleta majina yasiyokubalika na sasa wanaona ugumu wa kuwatetea majukwaani.Mtu mmoja ameuawa asubuhi hii na wengine wawili kufanikiwa kutoroka baada ya kujaribu kumteka mgombea udiwani wa kata ya Bwisha Ukara kwa tiketi ya CHADEMA.
Inadaiwa watu hao wamezingirwa baada ya mgombea huyo kupiga ukunga na ndipo walipozingirwa na kushushiwa kipigo ambapo mmoja ameuawa huku wawili wakifanikiwa kutoroka.
Hilo ni tukio la kwanza la mauaji yanayohusishwa na mambo ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 ambapo kunatabiriwa kuwepo kwa visa vingi vya vurugu kutokana na sintofahamu ambazo zimeanza kujitokeza.
Habari hii imethibitishwa na Katibu wa kanda ya Victoria- CHADEMA ndugu Zacharia T. Obad
Polisi wangemchukua na kumficha kisha kumuachia. Safi sana wakara huwa nawaaminia sana. Nyerere pia alikuwa na historia yao kwa upande wa 'mambo ya jadi'Hii roho mbaya ya kutekana inaonekana kushamiri. Kama waliweza kumthibiti wasingemua ili tujue ni akina nani waliowatuma.....
Mkuu Kiukweli ni mjinga tu ndio ataamini kuwa haya matukio yanaratibiwa na ccm, yaani wafanye huu utekaji na uuaji kwa makusudi kabisa huku wakijua kabisa lawama zitatupwa kwao na kuwapaka matope tena kwenye kipindi hiki cha uchaguzi?
Basi kama ni hivo watakuwa wapumbavu kweli kweli.
Ndio mana nikasema kuwa kama ni kweli wao ndio wanaratibu hayo basi watakuwa ni wapumbavu wa kiwango Cha lami.Wale wa Hai - Kilimanjaro waliorusha mawe ni chama gani ?
Hapa ndio upate majibu kuwa Ccm inahusika katika haya matukio na ndio wanaratibu 100%
Safi sana, wamkate na Lisu ili moto uwake rasmi,Hilo lingekuwa jema zaidi ni kukamata kipigo wataje waliowatuma
Hii ni lugha ambayo wana ccm wanaielewa sana.Safi sana.
Tukienda kwa Lugha hii hii ya matendo, hata nawao wataanza kua na hofu.
Wanaoamini usiwaite wajinga, ila wewe usiyeamini ndo tunajiuliza ni mtu wa aina gani. Uliuona umati uliojitokeza kutaka uongozi ndani ya CCM? umeshuhudia pesa iliyotumika na kiwango? Baadaye jiulize uelewa wa viongozi wa CCM.Mkuu Kiukweli ni mjinga tu ndio ataamini kuwa haya matukio yanaratibiwa na ccm, yaani wafanye huu utekaji na uuaji kwa makusudi kabisa huku wakijua kabisa lawama zitatupwa kwao na kuwapaka matope tena kwenye kipindi hiki cha uchaguzi?
Basi kama ni hivo watakuwa wapumbavu kweli kweli.
Sasa Kama kule kibiti walifanya watu wengine wabaya ndio maana jeshi likaingilia swali je kwanini walikuwa wanaua Wana CCM pekee na polisi?Mauwaji ya MKIRU yalikua ya tofauti sana sana na ndio maana jeshi liliingilia kati, huenda ilikua ni zaidi ya yale tuliyokua yunayajua, all in all tupendsne na kuheshimiana maana chaguzi zitapita ila maisha yatakuepo
Tunu ya kwanza ni haki. Taifa likipada mti wa haki litavuna tunda la amani! Kinachotokea sasa ni ushahidi tosha wa jinsi kusivyo na haki Tz. Bila haki hakuna Demokrasia. Lakini Mhe. Bashiru alisema wazi kweupe kuwa ccm kitatumia vyombo vya dola kubaki madarakani. Sitashangaa vurugu na mauaji zaidi kwa sababu waTz wachotaka ni haki. Hivi kuna mgombea kule Tunduma yupo ndani kwa kubambikiwa kosa la ujambazi wa kutumia silaha. Alikamatwa ili kuchunguzwa uraia lakini kufikishwa polisi kosa likabambikwa lingine, na polisi. Hii ndio maana ya kutumia vyombo vya dola kubaki madarakani.Mungu atuepushie huu ujinga, Tanzania ni nchi ya amani na naomba usiku na mchana amani, upendo , kuheshimiana kubaki kama mojawapo ya tunu zetu
Nani anashiba ndege, watu mtaani wana njaa na ughali wa bidhaa sokoni kama sukariHofu ya nini kama tumenunua ndege, flyover, madaraja na nchi ni uchumi wa kati?
Hebu jaribu kufikiri mara mbali mkuu kuna kitu hapa hakiko sawa.CCM siyo chama cha siasa tena bali ni genge la wahuni
Tangu lini genge la wahuni likawa na weledi na busara zaidi ya uhuni tu ??
WanaCCM wenzakoNani anashiba ndege, watu mtaani wana njaa na ughali wa bidhaa sokoni kama sukari