Ujenzi: Nimefanya uchunguzi kwanini watu wengi wanashindwa au kuchelewa kuwa na kwao

Jinsi ya kupunguza gharama za gypsum board.
Piga hesabu unahitaji boards ngapi. Mfano unahitaji 50pcs. Nunua 20pcs kwanza. Mwambie fundi aweke nzima nzima,yaani aweke sehemu zinazoingia nzima nzima nyumba nzima. Zile sehemu zinazohitaji vipande aziache kwanza.
Utashangaa nzima zinaingia 20 au pungufu.
Zile sehemu zinazohitaji vipande nenda hardware ongea nao wakuuzie damaged boards(hizi huwa zinakuwa zimemeguka kidogo wakati wa kumshusha mzigo hawawezi kuuza kwa wateja wa kawaida) hizo utauziwa moja 5000-7000. Unanunua kama 30pcs ndio unaenda kuweka sehemu zinazohitaji vipande.
Hesabu iko hivi
Boards nzima 50 ni 50*14,000=700,000
Kwa njia hii nilioshauri
Board nzima 20 ni 20*14,000=280,000
Damaged board 30*6000=180,000
Total 460,000
700,000-460,000=240,000
Umeokoa 240,000.
mkuu kama una dondoo nyingine ya kupunguza matumizi please just share tujifunze,
hii ya gypsum nimeipenda.
 
Yaan umeongea point wadada wana matumizi sana lkn sasa ivi kichwa kina muuma baada ya serikali kikomaa na manunuzi ya mfumo hahaha
kabisa kiongozi Hawa baadhi hao huwa hawajilewei kabisa

utakuta mtu ananyumba hiyo laki 6 matumizi labda laki nne inasimama 1m kwa mwezi ....
bado gharama za urembo na makorokocho mengine ,keshi atakuja kulia na kusema hivi kwann mie siendeleei nakosea wapi na kilio shuuu ,
.sasa mpe ushauri akapange nyumba uswahili hataki ili ajimake ajenge hata chumba kimoja ....
Nilichogundua wengi kinachowagharimu maisha ya show off wakati ndani kwa ndani wanaumia kuyaishi hayo maisha ...
Mtu atataka akapenge nyumba zima na hana famili atataka kukaaa upanga ama mikochoni wakati zipo nyumba huko uswahilini bei cheee na unaweza fanya vitu vingine vya maendeleo
 
Nikupongeze kwa hatua hiyo mkuu,tatizo siyo kupata rejected gypsum tatizo ni kupata zinazofanana zote quality unayoitaka unless ukubali kuchanganya tofauti tofauti,hii idea nilikutana nayo mtaani ila mimi nilikuwa nataka gypsum za GYPROC hizi zinatoka Turkey nilipopeleleza kama nitaweza kununua nzima kadhaa kisha nichanganyiwe na ambazo zimeharibika kidogo nikaambiwa kwa brand hiyo kupata mbovu siyo rahisi kutokana na zinafungwa imara sana siyo rahisi kupata damage so wakasema za hivyo nitapewa za hapa hapa za Kichina hizi zinazotengenezwa Kisarawe.

Kama siyo mtu wa kuchagua sana hilo ni wazo zuri sana kama ukilifuata una-save pakubwa.
Nashukuru pia kwa output yako kama nilivyosema mimi ujenzi wangu umekua kama kutafuta tenda..kabla sijafanya maamuzi huwa nacheki idea tofauti kupata itakayo nifaa..labda nikuulize kwani hizi za mchina huwezi pata grade nzuri inayoikaribia ya mturuki?? ntafollow up..chengine naomba ushauri nataka niweke uzio kwenye nyumba..kati ya ukuta wa matofari na nyaya(senyenge) ipi inakaa vizuri zaidi
 
Nashukuru pia kwa output yako kama nilivyosema mimi ujenzi wangu umekua kama kutafuta tenda..kabla sijafanya maamuzi huwa nacheki idea tofauti kupata itakayo nifaa..labda nikuulize kwani hizi za mchina huwezi pata grade nzuri inayoikaribia ya mturuki?? ntafollow up..chengine naomba ushauri nataka niweke uzio kwenye nyumba..kati ya ukuta wa matofari na nyaya(senyenge) ipi inakaa vizuri zaidi

Mchina quality nzuri zipo hazikosekani ila zinakuwa zinapishana bei kidogo sana na za Turkey,hilo la fence nadhani ya tofali ndo the best.mara nyingi wanaoweka kuta za senyenge huweka kwa ajili ya kuzuia watu wasikatishe katishe hovyo kwenye makazi yao otherwise hakuna kingine.

Ukuta wa tofali huzuia walio nje wasiweze kuyasoma mazingira ya ndani wakati senyenge huonyesha picha nzima ya ndani na ni rahisi kukatwa.
 
Haha mkuu haiwezekani eti?!

Jenzi zinatofautiana kati ya mkoa na mkoa,sijaona alipofafanua kwamba huu ujenzi amefanya sehemu gani ya Tanzania ila kuna sehemu kama Mbeya na Tanga wanajengea zile tofali za kuchoma moja Tsh 100/= inaweza kuwa ni huko.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hawa Mwanza na Mara wanajenga hivyo uki compare na blocks ipi ni cheap?
 
Kweli kabisa maana unaweza kuwa na pesa na ukaelewana na Fundi kuanzia msingi mpaka kupaua ukajua kazi iliyobakia ni kidogo kumbe finishing ni zaidi ya msingi mpaka kupaua.Hahaaaa ujenzi konyo ndo maana wenye nyumba baadhi wanekera wapangaji.
Finishing ni mchezo sasa, Unaenda dukani unarudi na vitu vichache lakini imekamua milion mfano vifaa vya plumbing vya awali
 
Vitu vinavyotumika physically ndio unatakiwa usi-gamble. Mfano tiles ambazo kila siku zinakanyahwa,vyoo,taps,vifaa vya umeme etc. Ila vitu kama boards kuwa nyembamba hamna athari yoyote kwasababu hazikai pale juu ili mtu akanyage.
Mabati na mbao inabidi kuangalia sana quality kuliko savings.
Board zikiwa fake au nyembamba shida ni bati likipitisha maji zikapata maji ni janga la kitaifa
 
Board zikiwa fake au nyembamba shida ni bagi likipitisha maji zikapata maji ni janga la kitaifa
Bati likipitisha maji hata board iwe nene itashuka. Seriously unaweka board nene kuzuia maji yaliyopita kwenye bati? Aisee
 
Nashukuru pia kwa output yako kama nilivyosema mimi ujenzi wangu umekua kama kutafuta tenda..kabla sijafanya maamuzi huwa nacheki idea tofauti kupata itakayo nifaa..labda nikuulize kwani hizi za mchina huwezi pata grade nzuri inayoikaribia ya mturuki?? ntafollow up..chengine naomba ushauri nataka niweke uzio kwenye nyumba..kati ya ukuta wa matofari na nyaya(senyenge) ipi inakaa vizuri zaidi
Hapo umetumia field ya procurement, inaleta tija sana, na ndiyo maana serikali wana sheria zinazoongoza manunuzi public procurement act hii sheria hata lrivate wangeitumia kwa ulazima ingewaletea tija sana kwenye shughuli zao za kioffisi
 
Bati likipitisha maji hata board iwe nene itashuka. Seriously unaweka board nene kuzuia maji yaliyopita kwenye bati? Aisee
Unaweka board bora na imara unene sio tija, bati sio guarantee kukaaa miaka na miaka isje kupitisha maji, ila maji hayo yakikutana na board za kifamba zinapukurika kama unga usibishe prondo nimeshaona yamewatokea watu
 
Unaweka board bora na imara unene sio tija, bati sio guarantee kukaaa miaka na miaka isje kupitisha maji, ila maji hayo yakikutana na board za kifamba zinapukurika kama unga usibishe prondo nimeshaona yamewatokea watu
Hakuna board ya kuzuia maji. Uweke board nene au nyembamba maji yakivuja hayakusaidii kitu. By the way hio nene ina mm ngapi na hio nyembamba ina mm ngapi?
 
Board zikiwa fake au nyembamba shida ni bati likipitisha maji zikapata maji ni janga la kitaifa
Nope!!!

Mkuu board hata ikiwa imara kiasi gani ikipata maji kidogo tu inashuka au inachafuka vibaya sana ndo maana inashauriwa kuhakikisha kwanza kabla ya kupachika haya madude uhakikishe upauaji uliofanyika ulikuwa mzuri?usubiri angalao mvua heavy mbili zinyeshe ukague banda lako kama sivyo hasara utaipata.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kipato kidogo na wategemezi lukuki ndiyo chanzo kikuu ya kufeli kwa wengi - mtu unaanza na mshahara wa 650,000/= Tshs kwa mwezi take home baada ya kumaliza ka degree kako pale Mlimani..- Kodi, Umeme, Maji, msosi, mavazi, nauli humo humo...bado wadogo zako, wazazi wako na mandugu wengine wenye shida ndogo ndogo...bado ununue godoro, kitanda, feni, jiko la gesi nk

No saving...unajikuta unafanya kazi miaka 10, at age of 37 ndiyo unaanza kutafuta kiwanja......mpaka uhamie kwako una 50 - kibabu.
 
Wahindi hawajengi mijumba kama yenu na wanaishi Safi tu
Wahindi sio watanzania maana wakisema wajenge kikinuka wanaacha majengo yao hapa. Kwa hiyo wanabaki kuishi kwenye apartments na nyumba za nhc huku wakifanya investments. Mambo yasipokuwa mambo wanaliquidate wanasepa.
 
Kwa wakazi wengi wa mjini kuna jambo moja ambalo limekuwa kizungumkuti sana kwa watu wengi hasa sisi wa uchumi mdogo.

Hakuna mtu anayependa kuishi kwenye Nyumba za kupanga hivyo kila mtu anapenda kujenga awe na kwake, mahala ambapo atakuwa huru kufanya anavyotaka yeye.

Nimefanya uchunguzi ni kwanini watu wengi wanashindwa au kuchelewa kuwa na kwao.

1. Watu wengi wanaogopa kujenga, yaani mtu anakuwa anasubiri awe na pesa nyingi ndio aanze ujenzi.
Mara nyingi kadiri mtu umri unavyoongezeka na majukumu nayo huongezeka hivyo kipato hakitaruhusu uwe na pesa nyingi

2. Watu wanatamani vitu ambavyo hawana uwezo navyo. Jirani yangu kuna mama alipata pesa yake kiasi akaamua kwenda kuanza ujenzi kwenye kiwanja chake, pasipo kufanya tathmini ya uchumi wake alianzisha msingi wa jumba kubwa kiasi kwamba pesa aliyokuwa nayo yote iliishia kwenye msingi.

Mpaka sasa anajikongoja lakini kutokana na ukubwa wa nyumba basi imesogea mpaka kwenye madirisha ndani ya miaka kama mitano sasa. Lakini ukipiga hesabu vizuri ni kwamba pesa aliyokwisha tumia angeweza kujenga nyumba ndogo angalau ya vyumba viwili na sebule na leo angekuwa anaishi kwake.

So tukadirie haya mambo
Ukitaka kujenga anza hata mimi nilikua na woga kwamba hela nlonayo haitoshi ila nikaanza na Sasa Niko kwangu japo haijaisha ila kila nipatacho namaliza then naendelea naamini si muda itaisha.ni nyumba kubwa ya kutosha isiyo na mbwembwe
 
Back
Top Bottom