Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 11,208
- 19,001
Jinsi masuala ya muungano yanavyoshughulikiwa na kwa sasa, ni mtu kipofu wa akili tu ndio hataona kwamba kadiri siku zinavyopita mbegu za uhasama kati ya Tanzania bara na Zanzibar inazidi kuota mizizi, majani ya chuki yakizidi kuchanua. Ni kiongozi mjinga tu asieweza kuona kwamba jinsi haya mambo ya muungano yanakoenda, yanaweza kusababisha mgongano (confrontation) mkubwa sana kati ya wakazi wa Zanzibar walioko bara na wakazi wa bara walioko Zanzibar.
Badala ya kujibu hoja zinazowekwa mezani, viongozi wameamua kwa makusudi kuwashambulia wale wanaozitoa, bila kuona kuwa kwa kufanya hivyo wanazidi kuchochea uhasama kati ya Tanzania bara na Zanzibar. Kwa kumfurahisha nani?
Kama Tanzania bara wanaona kwamba kwao kero kubwa ya muungano ni kutokuwa na serikali ya Tanganyika, kwa nini hawasikilizwi? Wakati wa Nyerere huenda kulikuwa na sababu za msingi kuwa na serikali mbili, lakini ni wazi hilo halikubaliki kwa sasa, na huwezi kulilazimisha likaendelea kuwapo bila kuleta madhara.
Muungano tunaweza kulazimishwa uendelee kuwapo kwa kutumia nguvu ya dola, lakini haitazuia watu kuanza violence (kupigana) uhasama unaojitokea ukizidi kukua. Amini nawaambieni, huu muungano mnaodai uko imara unaweza kuvunjwa kwa nguvu na kuleta hali ya machafuko bara na visiwani. Watanzania bara walioko visiwani wataondolewa kule kwa nguvu, na wa-Zanzibar walikoko bara wataondolewa huku kwa nguvu, na hata kupoteza mali au uhai wao. Ndilo tunalosubiri? Au tunadhani haliwezi kutokea Tanzania, vitu kama hivyo vinatokea Rwanda tu?
Muungano ulifanyika zaidi ili Zanzibar kusiwe na counter-revolution ya Waarabu (wajomba) walipopinduliwa na kuchinjwa, na kwa Tanganyika kulinda usalama wake katika kuwa kitovu cha kupigania uhuru wa Afrika. Sasa hizi sababu sio hoja tena. Kama imefikia mahali Watanzania hawautaki muungano, basi ni bora uvunjwe kwa utaratibu na kuelewana, watu waulizwe je ungependa kubaki bara au kurudi visiwani, au ungependa kubaki visiwani au kurudi bara nk. Labda tuanze na "Referendum", wananchi ndio tuamue kidemokrasia kama tunataka au hatutaki muungano, sio serikali ituamulie kwa maslahi yake, au maslahi ya serikali ya Mapinduzi Zanzibar, au maslahi ya CCM.
Tusione aibu kukaa chini na kutafakari kuuvunja muungano, kama kuwa na serikali moja au tatu haiwezekani, kwa sababu mfumo wa muungano uliopo sasa hivi unazidi kukuza uhasama kati ya Tanzania bara na Zanzibar. Mwaka 1982 Senegal na Gambia waliungana na kuwa nchi moja ya Senegambia. Iliposhindikana, waliuvunja muungano, mwaka 1989. Juzi hapa Uingereza imejitoa kwenye muungano wa Ulaya. Kwa hiyo Tanzania haitakuwa ya kwanza kuvunja muungano. Muungano ni mkataba.
Badala ya kujibu hoja zinazowekwa mezani, viongozi wameamua kwa makusudi kuwashambulia wale wanaozitoa, bila kuona kuwa kwa kufanya hivyo wanazidi kuchochea uhasama kati ya Tanzania bara na Zanzibar. Kwa kumfurahisha nani?
Kama Tanzania bara wanaona kwamba kwao kero kubwa ya muungano ni kutokuwa na serikali ya Tanganyika, kwa nini hawasikilizwi? Wakati wa Nyerere huenda kulikuwa na sababu za msingi kuwa na serikali mbili, lakini ni wazi hilo halikubaliki kwa sasa, na huwezi kulilazimisha likaendelea kuwapo bila kuleta madhara.
Muungano tunaweza kulazimishwa uendelee kuwapo kwa kutumia nguvu ya dola, lakini haitazuia watu kuanza violence (kupigana) uhasama unaojitokea ukizidi kukua. Amini nawaambieni, huu muungano mnaodai uko imara unaweza kuvunjwa kwa nguvu na kuleta hali ya machafuko bara na visiwani. Watanzania bara walioko visiwani wataondolewa kule kwa nguvu, na wa-Zanzibar walikoko bara wataondolewa huku kwa nguvu, na hata kupoteza mali au uhai wao. Ndilo tunalosubiri? Au tunadhani haliwezi kutokea Tanzania, vitu kama hivyo vinatokea Rwanda tu?
Muungano ulifanyika zaidi ili Zanzibar kusiwe na counter-revolution ya Waarabu (wajomba) walipopinduliwa na kuchinjwa, na kwa Tanganyika kulinda usalama wake katika kuwa kitovu cha kupigania uhuru wa Afrika. Sasa hizi sababu sio hoja tena. Kama imefikia mahali Watanzania hawautaki muungano, basi ni bora uvunjwe kwa utaratibu na kuelewana, watu waulizwe je ungependa kubaki bara au kurudi visiwani, au ungependa kubaki visiwani au kurudi bara nk. Labda tuanze na "Referendum", wananchi ndio tuamue kidemokrasia kama tunataka au hatutaki muungano, sio serikali ituamulie kwa maslahi yake, au maslahi ya serikali ya Mapinduzi Zanzibar, au maslahi ya CCM.
Tusione aibu kukaa chini na kutafakari kuuvunja muungano, kama kuwa na serikali moja au tatu haiwezekani, kwa sababu mfumo wa muungano uliopo sasa hivi unazidi kukuza uhasama kati ya Tanzania bara na Zanzibar. Mwaka 1982 Senegal na Gambia waliungana na kuwa nchi moja ya Senegambia. Iliposhindikana, waliuvunja muungano, mwaka 1989. Juzi hapa Uingereza imejitoa kwenye muungano wa Ulaya. Kwa hiyo Tanzania haitakuwa ya kwanza kuvunja muungano. Muungano ni mkataba.