Tuziombe nchi rafiki na taasisi za fedha hususani World Bank na African Development Bank waahirishe au kutusamehe baadhi ya madeni wanayotudai

Dr Akili

JF-Expert Member
Aug 21, 2011
4,955
4,329
Rais wetu anakubalika sana kimataifa na ameweza kutufungua kimataifa. Ni rais pekee, executive president, mwanamke barani Afrika na wengi wako tayari kumsaidia ili kuonesha ulimwengu hasa wa Afrika kwamba wanawake wanaweza, tena sana tu kuliko wanaume wengi.

Wengi wanapenda kuona rais wetu anaipaisha kiuchumi na kiusalaama nchi yetu ya Tanzania ili iwe mfano kwa nchi zingine za Afrika ili nazo ziwe zinachagua akina mama kwenye nafasi hizi za ukuu wa nchi. Wakina mama ni wapole, wana huruma, hawapendi vurugu na ni watu makini sana.

Bahati mbaya rais wetu ameingia madarakani kipindi ambacho nchi inakabiriwa na athari kubwa za kiuchumi zilizosababishwa na janga la mlipuko wa covid 19. Pia ni kipindi ambacho mikopo ya fedha tuliyokopa miaka mingi ya nyuma ikawa ndiyo imeiva (mature) na kupaswa kuanza kuilipa. Karibu theluthi moja ya bajeti ya nchi inabidi itumike ku service madeni hayo! Na kama hayo hayatoshi yamezuka madhara ya kiuchumi kutokana na vita ya Russia na Ukraine.

Hizi tunatumaini marafiki zetu waliotukopesha enzi hizo pamoja na benki kama World Bank na African Development Bank watatuelewa na kuweza kuahirisha ulipaji wa baadhi ya madeni hayo kwa angalao miaka mitano. Baadhi yake wanaweza hata kutusamehe kabisa marafiki zetu. Hiki ni kitu cha kawaida ambacho hutokea baina ya mkopaji na mkopeshaji hali inapokuwa ngumu.

Hili likikubalika litatuwezesha kupata karibu TZS 6 trillion kila mwaka kutoka kwenye makusanyo yetu itakayoelekezwa kwenye ujenzi wa miradi mikubwa ya SGR, JNHPP na Chuma cha Liganga - Mchuchuma. Haya yatawezesha nchi yetu kuwa nchi ya viwanda ya mfano kwenye bara la Africa.
 
Kuziomba zitukopeshe tena pesa za kutuwezesha kukabiliana na athari za covid 19 haisaidii sana in the long term bali ni kuongeza mzigo baadaye.
 
Mama anaomba sana, halafu hela zinawekwa mifukoni mwa wenye vyeo.Mimi naona wasitusamehe,mikopo haina tija.
 
Tatizo mikopo mingi iliyochukuliwa na awamu ya 4 na 5 ilikuwa ya kibiashara. Hawakutaka mikopo yenye masharti mengi kutoka kwa "mabeberu". Sasa mikopo ya kibiashara haina mswalie mtume.

Pitia hapa kuna uchambuzi mzuri sana wa hali ya deni la taifa.

Deni la taifa - The Chanzo
 
Rais wetu anakubalika sana kimataifa na ameweza kutufungua kimataifa. Ni rais pekee, executive president, mwanamke barani Afrika na wengi wako tayari kumsaidia ili kuonesha ulimwengu hasa wa Afrika kwamba wanawake wanaweza, tena sana tu kuliko wanaume wengi.

Wengi wanapenda kuona rais wetu anaipaisha kiuchumi na kiusalaama nchi yetu ya Tanzania ili iwe mfano kwa nchi zingine za Afrika ili nazo ziwe zinachagua akina mama kwenye nafasi hizi za ukuu wa nchi. Wakina mama ni wapole, wana huruma, hawapendi vurugu na ni watu makini sana.

Bahati mbaya rais wetu ameingia madarakani kipindi ambacho nchi inakabiriwa na athari kubwa za kiuchumi zilizosababishwa na janga la mlipuko wa covid 19. Pia ni kipindi ambacho mikopo ya fedha tuliyokopa miaka mingi ya nyuma ikawa ndiyo imeiva (mature) na kupaswa kuanza kuilipa. Karibu theluthi moja ya bajeti ya nchi inabidi itumike ku service madeni hayo! Na kama hayo hayatoshi yamezuka madhara ya kiuchumi kutokana na vita ya Russia na Ukraine.

Hizi tunatumaini marafiki zetu waliotukopesha enzi hizo pamoja na benki kama World Bank na African Development Bank watatuelewa na kuweza kuahirisha ulipaji wa baadhi ya madeni hayo kwa angalao miaka mitano. Baadhi yake wanaweza hata kutusamehe kabisa marafiki zetu. Hiki ni kitu cha kawaida ambacho hutokea baina ya mkopaji na mkopeshaji hali inapokuwa ngumu.

Hili likikubalika litatuwezesha kupata karibu TZS 6 trillion kila mwaka kutoka kwenye makusanyo yetu itakayoelekezwa kwenye ujenzi wa miradi mikubwa ya SGR, JNHPP na Chuma cha Liganga - Mchuchuma. Haya yatawezesha nchi yetu kuwa nchi ya viwanda ya mfano kwenye bara la Africa.
Beberu kwenye kupiga hela hana cha umama we mama. Mwache mama agawe tu mali zetu .
 
Rais wetu anakubalika sana kimataifa na ameweza kutufungua kimataifa. Ni rais pekee, executive president, mwanamke barani Afrika na wengi wako tayari kumsaidia ili kuonesha ulimwengu hasa wa Afrika kwamba wanawake wanaweza, tena sana tu kuliko wanaume wengi.

Wengi wanapenda kuona rais wetu anaipaisha kiuchumi na kiusalaama nchi yetu ya Tanzania ili iwe mfano kwa nchi zingine za Afrika ili nazo ziwe zinachagua akina mama kwenye nafasi hizi za ukuu wa nchi. Wakina mama ni wapole, wana huruma, hawapendi vurugu na ni watu makini sana.

Bahati mbaya rais wetu ameingia madarakani kipindi ambacho nchi inakabiriwa na athari kubwa za kiuchumi zilizosababishwa na janga la mlipuko wa covid 19. Pia ni kipindi ambacho mikopo ya fedha tuliyokopa miaka mingi ya nyuma ikawa ndiyo imeiva (mature) na kupaswa kuanza kuilipa. Karibu theluthi moja ya bajeti ya nchi inabidi itumike ku service madeni hayo! Na kama hayo hayatoshi yamezuka madhara ya kiuchumi kutokana na vita ya Russia na Ukraine.

Hizi tunatumaini marafiki zetu waliotukopesha enzi hizo pamoja na benki kama World Bank na African Development Bank watatuelewa na kuweza kuahirisha ulipaji wa baadhi ya madeni hayo kwa angalao miaka mitano. Baadhi yake wanaweza hata kutusamehe kabisa marafiki zetu. Hiki ni kitu cha kawaida ambacho hutokea baina ya mkopaji na mkopeshaji hali inapokuwa ngumu.

Hili likikubalika litatuwezesha kupata karibu TZS 6 trillion kila mwaka kutoka kwenye makusanyo yetu itakayoelekezwa kwenye ujenzi wa miradi mikubwa ya SGR, JNHPP na Chuma cha Liganga - Mchuchuma. Haya yatawezesha nchi yetu kuwa nchi ya viwanda ya mfano kwenye bara la Africa.
Wala hata wakifanya hivyo huwezi ukaona matokeo chanya yoyote wakati hicho kidogo ulichonacho kimekushinda kukitunza, kila leo utasikia ni upotevu wa mabilioni serikalini tu, mala kifaa cha milioni 20, kinanunuliwa kwa milioni 130, hapo utegemee nini?kila mwaka ripoti ya CAG, imejaa upigaji tu, na mambo yanaachwa kama yalivyo tu!!
Hata leo hii wafute madeni yote na ubakie unawadai wewe, kama trilioni 30, ni mwaka mmoja tu, wewe ndio utakuwa unadaiwa tena!!!!tatizo kubwa la nchi za kiafrika ni ufisadi tu, pesa nyingi inapotelea huko.Inshu sio kuwa mama, inshu ni je unaweza kusimamia matumizi ya serikali yako kwa kuweka mifumo imara?!!na tatizo la Afrika ni kushindwa kujenga mifumo imara ya kiuongozi, badala yake anataka yeye ndio awe mtu wa kusimamia kila kitu, mfano jiwe, eti "naogopa kwenda nje kwani mafisadi wataiba pesa" kweli hii ina logic?!!
 
Tunakopa kimya kimya then tunakuja kutamba kwenye majukwaa huku mnatanua kwapa eti tunajenga kwa pesa za ndani!! Deni ni kulipa
 
Back
Top Bottom