Zanaco
JF-Expert Member
- Feb 17, 2016
- 1,611
- 1,590
Jumamosi ya Novemba 15, 1884, Kansela wa Ujerumani, Otto von Bismarck, aliitisha mkutano mkubwa kwa ajili ya kuligawa Bara la Afrika. Mkutano huo uliofahamika kama Berlin Conference, ulifanyika kwenye makazi yake huko Wilhelmstrasse, Berlin.
Mkutano huo ulilenga katika kuwaepusha wababe wa Magharibi kutumbukia vitani wakati wakigombania mali za Afrika. Mataifa 14 yalihudhuria, wakiwemo Ujerumani wenyewe, Uingereza, Marekani (wakiwakilishwa na Henry Morton Stanley), Himaya ya Ottoman (Dola ya Mtukufu Sultan , Denmark, Ufaransa, Muungano wa Austria na Hungary, Urusi, Ureno, Hispania, Muungano wa Sweden na Norway, Ubelgiji, Italia na Uholanzi.
Mkutano huu ndio uliosababisha ukoloni barani Afrika, kwani uliazimia katika kuligawa bara hili miongoni mwa wababe waliohudhuria, kwa faida yao. Baada ya mkutano huo, mataifa hayo yakatuma wawakilishi wao kuja Afrika kuchukua maeneo na mali.
Ujerumani ikamtuma kijana wa miaka 28, aliyeitwa Karl Peters, akiwa na vijana wenzake watatu; Dk. Karl Juhlke, Pfeil na August Otto.
Vijana hawa wakafunga safari hadi Afrika na kutia nanga Zanzibar na baadaye kuanza safari ya bara hadi walipofika Usagara ambako walikutana na Chief Mangungo katika Ikulu yake ya Msovero. Usagara kwa sasa ndio Kilosa.
Karl Peters akatumia ujanja, hila na ulaghai kuingia mkataba na kiongozi huyo wa kiafrika uliosababisha Ujerumani kuchukua eneo lake lote pamoja na watu wake.
Mkataba huo uliandikwa kijerumani na Chief Mangungo akamtumia mkalimani wake kutoka hapo hapo Msovero (Ramazan) ambaye na yeye wala hakuijua lugha hiyo.
Mkataba huo ulisomeka kama ifuatavyo:
“Mangungo amekubali kutoa himaya yake yote pamoja na watu wake na hadhi yake kwa Dk. Karl Peters, kama mwakilishi wa Umoja wa Ukoloni wa Kijerumani, kwa ajili ya matumizi ya moja kwa moja ya koloni la Kijerumani.
Dk. Karl Peters, kwa niaba ya jina la Umoja wa Ukoloni wa Ujermani anatangaza dhamira yake ya kuitwaa himaya yote ya Sultan Mangungo na haki zote kwa ajili ya Koloni la Ujerumani inayohusisha kila kona na amali za Mwenyi Sagara.”
Baada ya mkataba huu, Karl Peters akalichukua eneo lote lililokuwa chini ya Mangungo na kuliweka chini ya kampuni yake ya Deutsch-Ostafrika (German East Africa) ambayo ilikuwa ikimiliki eneo lote ambalo leo hii ni Tanzania Bara na Rwanda na Burundi.
Wakati machifu wengine, kama Mkwawa, walipigana na Ujerumani kukataa maeneo yao kuchukuliwa, Mangungo alilitoa eneo lake kirahisi kabisa.
Hayo yalitokea mwaka 1884. Hayo yalitokea karne ya 19. Hayo yalitokea kwa sababu Mangungo hakusoma, hivyo asingeweza kufua dafu mbele ya msomi, Daktari wa Falsafa, Karl Peters.
Baada ya karne zijazo kuna ubaya gani na sisi tukisomwa kama hawa akina Ramazani?
Ebu wasanii badala ya kutengeza move za mapenzi tutengezee move ya zaku elimisha Jamii kama hii mtauza nitanunua copy mbili nimuone Ramazan akipiga fix na kumzunguka Chief.
Mkutano huo ulilenga katika kuwaepusha wababe wa Magharibi kutumbukia vitani wakati wakigombania mali za Afrika. Mataifa 14 yalihudhuria, wakiwemo Ujerumani wenyewe, Uingereza, Marekani (wakiwakilishwa na Henry Morton Stanley), Himaya ya Ottoman (Dola ya Mtukufu Sultan , Denmark, Ufaransa, Muungano wa Austria na Hungary, Urusi, Ureno, Hispania, Muungano wa Sweden na Norway, Ubelgiji, Italia na Uholanzi.
Mkutano huu ndio uliosababisha ukoloni barani Afrika, kwani uliazimia katika kuligawa bara hili miongoni mwa wababe waliohudhuria, kwa faida yao. Baada ya mkutano huo, mataifa hayo yakatuma wawakilishi wao kuja Afrika kuchukua maeneo na mali.
Ujerumani ikamtuma kijana wa miaka 28, aliyeitwa Karl Peters, akiwa na vijana wenzake watatu; Dk. Karl Juhlke, Pfeil na August Otto.
Vijana hawa wakafunga safari hadi Afrika na kutia nanga Zanzibar na baadaye kuanza safari ya bara hadi walipofika Usagara ambako walikutana na Chief Mangungo katika Ikulu yake ya Msovero. Usagara kwa sasa ndio Kilosa.
Karl Peters akatumia ujanja, hila na ulaghai kuingia mkataba na kiongozi huyo wa kiafrika uliosababisha Ujerumani kuchukua eneo lake lote pamoja na watu wake.
Mkataba huo uliandikwa kijerumani na Chief Mangungo akamtumia mkalimani wake kutoka hapo hapo Msovero (Ramazan) ambaye na yeye wala hakuijua lugha hiyo.
Mkataba huo ulisomeka kama ifuatavyo:
“Mangungo amekubali kutoa himaya yake yote pamoja na watu wake na hadhi yake kwa Dk. Karl Peters, kama mwakilishi wa Umoja wa Ukoloni wa Kijerumani, kwa ajili ya matumizi ya moja kwa moja ya koloni la Kijerumani.
Dk. Karl Peters, kwa niaba ya jina la Umoja wa Ukoloni wa Ujermani anatangaza dhamira yake ya kuitwaa himaya yote ya Sultan Mangungo na haki zote kwa ajili ya Koloni la Ujerumani inayohusisha kila kona na amali za Mwenyi Sagara.”
Baada ya mkataba huu, Karl Peters akalichukua eneo lote lililokuwa chini ya Mangungo na kuliweka chini ya kampuni yake ya Deutsch-Ostafrika (German East Africa) ambayo ilikuwa ikimiliki eneo lote ambalo leo hii ni Tanzania Bara na Rwanda na Burundi.
Wakati machifu wengine, kama Mkwawa, walipigana na Ujerumani kukataa maeneo yao kuchukuliwa, Mangungo alilitoa eneo lake kirahisi kabisa.
Hayo yalitokea mwaka 1884. Hayo yalitokea karne ya 19. Hayo yalitokea kwa sababu Mangungo hakusoma, hivyo asingeweza kufua dafu mbele ya msomi, Daktari wa Falsafa, Karl Peters.
Baada ya karne zijazo kuna ubaya gani na sisi tukisomwa kama hawa akina Ramazani?
Ebu wasanii badala ya kutengeza move za mapenzi tutengezee move ya zaku elimisha Jamii kama hii mtauza nitanunua copy mbili nimuone Ramazan akipiga fix na kumzunguka Chief.