Tujadili: Nini kinajenga mashaka kwa Rais Samia?

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Aug 24, 2011
54,484
123,107
Sarakasi zilizotokea kwenye kumpitisha Samia kuwa mgombea wa CCM kwenye uchaguzi Mkuu ni za kutia aibu kubwa sana.
Lakini nimekuwa najiuliza nini hasa sababu ya CCM kumpitisha bibi harusi huyu mlango wa nyuma? Kwa nini haiwezekani fomu zikatolewa kwa wote wenye nia na kupigiwa kura? Nini sababu ya wao kufanya hivyo. Katika majukwaa inatajwa Samia kufanya makubwa katika utawala wake. Si hayo makubwa yataleta kura za bwerere kabisa?

Nje ya hapo kumekuwa na mambo mengi ya hovyo kabisa kulazimisha kila kitu kiwe cha Samia. Mabango kila mahali, huwezi kufanya sherehe ya kiserikali bila bango la Samia, ajabu mpaka kwenye muhimili wa Mahakama sherehe zao zina mabango ya Samia......Sijui Samia Cup, Samia Urembo, Ndondi Vitasa vya Samia, Goli la Mama Samia, kila kitu kila mahali Samia.

Najiuliza kama mtu umefanya kazi vizuri ikaonekana, haya yote ya nini? Kwa nini unahangaika kiasi hiki kama KUKU MTETEA ANATAKA KUTAGA?
 
Mi nataka kuelimishwa katiba yetu inasemaje hiki kipengele, Rais akifariki makamu wa raisi anatakiwa aongoze kumalizia tu muhula au anamalizia na anaanza tena muhula mpya kama Rais samia.
"Endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais kufariki dunia, kujiuzulu, kupoteza sifa za uchaguzi au kutomudu kazi zake kutokana na maradhi ya mwili au kushindwa kutekeleza kazi na shughuli za Rais, basi Makamu wa Rais ataapishwa na atakuwa Rais kwa muda uliobaki katika kipindi cha miaka mitano..."

Ndivyo inavyoeleza Katiba ya Tanzania ya 1977, kifungu cha 37 (5).

Kwa hiyo hayo mengine nadhani ni utashi binafsi.
 
"Endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais kufariki dunia, kujiuzulu, kupoteza sifa za uchaguzi au kutomudu kazi zake kutokana na maradhi ya mwili au kushindwa kutekeleza kazi na shughuli za Rais, basi Makamu wa Rais ataapishwa na atakuwa Rais kwa muda uliobaki katika kipindi cha miaka mitano..."

Ndivyo inavyoeleza Katiba ya Tanzania ya 1977, kifungu cha 37 (5).

Kwa hiyo haya mengine nadhani ni utashi binafsi.
Ahsante mkuu nimeelewa
 
K
"Endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais kufariki dunia, kujiuzulu, kupoteza sifa za uchaguzi au kutomudu kazi zake kutokana na maradhi ya mwili au kushindwa kutekeleza kazi na shughuli za Rais, basi Makamu wa Rais ataapishwa na atakuwa Rais kwa muda uliobaki katika kipindi cha miaka mitano..."

Ndivyo inavyoeleza Katiba ya Tanzania ya 1977, kifungu cha 37 (5).

Kwa hiyo hayo mengine nadhani ni utashi binafsi.
Kumbe Katiba haijasema aendelee😄😄😄
 
IMG-20241007-WA0000.jpg
 
"Endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais kufariki dunia, kujiuzulu, kupoteza sifa za uchaguzi au kutomudu kazi zake kutokana na maradhi ya mwili au kushindwa kutekeleza kazi na shughuli za Rais, basi Makamu wa Rais ataapishwa na atakuwa Rais kwa muda uliobaki katika kipindi cha miaka mitano..."

Ndivyo inavyoeleza Katiba ya Tanzania ya 1977, kifungu cha 37 (5).

Kwa hiyo hayo mengine nadhani ni utashi binafsi.
Pia ni pale tuu Rais aliyetoka kabakiza kipindi kisichopungua miaka 3...na makamu wa Rais anayechukua nafasi yake atahesabika kama Naye kahudumu muhula kamili...na kama Rais kaondoka chini ya miaka 3 kumaliza muda wake...makamu wa Rais ataongoza kwa kwa kipindi cha mpito na kuitisha uchaguzi Mkuu...ambao pia na yeye anaweza kugombea, na akishinda huo utahesabika ni muhula wake wa kwanza...so as it stands, Samia ni muhula wake wa kwanza na ndio maana utawala wake unaitwa awamu ya sita.
 
Samia hakubaliki sababu ni:-
1. Mwanamke.
2. Mzanzibari.
3. Hana uwezo.

Haya anayajua na ndiyo chanzo cha mashaka yake.
La jinsia yake sidhani kama ni sababu, la Uzanzibari wake pia sidhani kama inaweza kua sababu. Wabara hatuna historia ya ubaguzi wa kimakabila, Wazanzibari wametapakaa everywhere in this country then why Samia abaguliwe kwa Uzanzibari wake? Hili sio kweli, nadhani hiyo point No 3 ndio inabeba HOFU kwa wote, yeye mwenyewe na chama chake, kibaya zaidi ni historia ya mtangulizi wake, yule jamaa kafanya kazi ya miaka 20 in 6 years of his rein, hilo ndio tatizo kubwa
 
Back
Top Bottom