Nominee
JF-Expert Member
- Sep 5, 2017
- 465
- 1,265
UTANGULIZI:
Ni jumapili ya tarehe 14/03/2010,Mida ya saa 10 jioni vinasikika vilio vya uchungu ndani ya nyumba kuukuu iliyopo maeneo ya uswahilini kata ya Mpambano wilayani Majita.Ni kilio hiki ndicho kinachowafanya majirani wasogee karibu na nyumba ya Mzee Mohammed kuangalia kuna nini kimetokea. "Eeeh mungu we....e...eee...we, nimekukosea nini mja wako hadi yote haya yanikute mimi tu, kwa niiii.....ni umeamua kunichukulia na huyu tena?, Baba Abdul amka,ooooooh mimi jamaaaani ntabaki na naaaaaani, amka mume wangu, amka, amka amka pliiiiiiz". Ni kilio cha kwiki na chenye kuhuzunisha cha mama huyu mjane ndicho kilichowashitua majirani hadi kusogea hapo. Mama Abdul alikuwa amepoteza mume wake kwa homa ya kupooza. Ni takribani wiki mbili zimepita tangu amzike mwanae mpendwa Abdul Mohammed, Mpelezi machachali ndani ya idara ya usalama wa taifa la BEIRAD kwa homa hiyohiyo ya kupooza. Ni huzuni kuu kupoteza wale uwapendao tena ndani ya wiki mbili tu. Mohammed Ismail almaarufu kama Mzee Mohammed ni miongoni mwa wazalendo ndani ya BEIRAD ambaye alilitumikia taifa kwa jasho na damu kuhakikisha kuwa usalama wa Raia na nchi kwa ujumla unalindwa dhidi ya mafedhuri wataka mali na umaarufu usio na maana. Akiwa chini ya uangalizi wa boss wake, Professor John Kluger anatumwa missions mbalimbali na zote anazikamilisha kwa ufanisi wa hali ya juu na hapo ndipo anapopewa fursa ya kumfundisha mwanae "Abdul Mohammed" ili aje kumrithisha fani yake.
JE,NINI KIMEWAKUMBA MTU NA BABA YAKE?. Usiikose simulizi hii kila siku za jumatatu, jumatano na jumamosi.
Ni jumapili ya tarehe 14/03/2010,Mida ya saa 10 jioni vinasikika vilio vya uchungu ndani ya nyumba kuukuu iliyopo maeneo ya uswahilini kata ya Mpambano wilayani Majita.Ni kilio hiki ndicho kinachowafanya majirani wasogee karibu na nyumba ya Mzee Mohammed kuangalia kuna nini kimetokea. "Eeeh mungu we....e...eee...we, nimekukosea nini mja wako hadi yote haya yanikute mimi tu, kwa niiii.....ni umeamua kunichukulia na huyu tena?, Baba Abdul amka,ooooooh mimi jamaaaani ntabaki na naaaaaani, amka mume wangu, amka, amka amka pliiiiiiz". Ni kilio cha kwiki na chenye kuhuzunisha cha mama huyu mjane ndicho kilichowashitua majirani hadi kusogea hapo. Mama Abdul alikuwa amepoteza mume wake kwa homa ya kupooza. Ni takribani wiki mbili zimepita tangu amzike mwanae mpendwa Abdul Mohammed, Mpelezi machachali ndani ya idara ya usalama wa taifa la BEIRAD kwa homa hiyohiyo ya kupooza. Ni huzuni kuu kupoteza wale uwapendao tena ndani ya wiki mbili tu. Mohammed Ismail almaarufu kama Mzee Mohammed ni miongoni mwa wazalendo ndani ya BEIRAD ambaye alilitumikia taifa kwa jasho na damu kuhakikisha kuwa usalama wa Raia na nchi kwa ujumla unalindwa dhidi ya mafedhuri wataka mali na umaarufu usio na maana. Akiwa chini ya uangalizi wa boss wake, Professor John Kluger anatumwa missions mbalimbali na zote anazikamilisha kwa ufanisi wa hali ya juu na hapo ndipo anapopewa fursa ya kumfundisha mwanae "Abdul Mohammed" ili aje kumrithisha fani yake.
JE,NINI KIMEWAKUMBA MTU NA BABA YAKE?. Usiikose simulizi hii kila siku za jumatatu, jumatano na jumamosi.