Sawa usituangusheHakuna shaka mkuu simulizi zangu zote zinafika mwisho
Sawa usituangusheHakuna shaka mkuu simulizi zangu zote zinafika mwisho
Hapo kwenye PAA! nini kimeendelea?SEHEMU YA 18
“Boss mwenyewe unarudi kutoka kazini “ Aliongea Steve baada ya Peter kufika nyumbani na kumkuta rafiki yake .
“Yeah nishakuwa boss saivi nafanya kazi katika kampuni kubwa tena benki hela zinakokaa , lazima unite boss .”
“Yeah , ila unabahati sana , unajua washikaji kila ninae mwambia kuwa unafanya kzi kwenye ile benki hakuna hata mmoja ambae ana niamini “
“ Usiwalazimishe kuamini , vipi lakini mambo yako ya field ?“
“Field iko vyema nimepata kwenye kampuni moja ya Telecom kule Posta ndiko ninako fanyia “
“ Anhaa kumbe tuko upande mmoja “
“Yeah , mrembo Rania na kisasi chako umefikia wapi au ndo unambwela “
“Kisasi kinaenda kiurahisi sana tofauti na nilivyofikiria , yaani si tumii hata nguvu”
“Eii.... wewe jamaa muongo sana , yule Rania ni mgumu wewe utampataje kirahisi hivyo , hebu acha Kamba zako hizo “
“Shida yako husadiki , ila nataka nikirudi kutoka Tanga nikuonyeshe uone kama nadanganya au wewe ndio mwenye ugonjwa wa kuto kuniamini “
“Acha wee waenda tanga kufanyae tena? “
“Naenda kwa ajili ya kazi huko na boss “
“Mhmh! , kweli naona ushaanza kuaminika kiasi hicho mpaka unaenda na boss”
“Sio kuaminika ni kwamba mfumo mpya wa ulinzi bado haueleweki kwa IT wengi kwa hio natakiwa kuurekebisha mimi mwenyewe “
“Halafu yule boss wako ana lishepu hilo , yule nakubali ani bemende “
“Aaaa… mke wa mtu yule na ni kama mama yako yule”
“Ana umama gani , hivi unafikiri yule akikutega upo chumbani nae utachomoka kama wewe ni mwanaume rijali , lazima uingie ndo utajua huyo sio mama yako ni umri tu ila tuyaache hayo”
“ Sema huyu mshikaji wako una mpango gani nae au ndo umemfanya House boy“
“ Masumbuko nina malengo nae nataka nikirudi nimfundishe kusoma na kuhesabu halafu nimtafutie biashara ya kufanya”
“Peter wewe hata usijisumbue kuniletea mwalimu au kutaka kunifundisha kwani sitaelewa kitu” Aliongea masumbuko na kumfanya Peter amwangalie huku akisogea pale kwenye sofa alipo kaa .
“Sikia Masumbuko , sijui alie kuambia kuwa huna uwezo wa kusoma na kuelewa ,ila mimi nina fahamu kabisa kuwa wewe unaweza ukasoma na kuelewa ,sema haujapata mwalimu mzuri kwa hio kuanzia sasa jua wewe una akili na unaweza kusoma na ukaelewa umesikia? “
“Ndio nimekuelewa “ Alijibu Masumbuko kwa heshima kwani hakuwahi kumuona Peter akiwa kwene hali hio ya kuwa siriasi
“Naona mshakuwa ndugu kamili kwa sasa “
“ Yeah , yaani nafurahi sasa hivi nyumbanii kuna mtu ambae naweza kumuongelesha wakati wote , nimechoka kuishi mwenyewe , hivi wewe Steve unajisikiaje unatoka shule unarudi nyumbni huku ukijua kabisa hakuna mtu , na hata pale unapokuwa na tatizo huna mtu wa kusema huyu ni ndugu yangu naweza kumuita au kumpigia simu kumuomba msaada “
“Ndio ni maisha magumu sana kiufupi sipatii hata picha lakini cha kumshukuru Mungu ni kwamba bado kakuweka hai na kukupigania mpaka sasa”
“Ndio , nilikuwa nampenda sana mama yangu na nitaendelea kumpenda daima huko aliko , alinipigania yeye mwenyewe kanikuza kwenye mazingira magumu mpaka alipo patwa na umauti , ila naamini siku moja tu nitakuja kumpata alie husika na ajali ile”
“Peter rafiki yangu kwanini usisahau yote hayo ile ilikuwa ni ajali ya kawaida tu kama polisi walivyo sema , kwanini unataka kuweka visasi moyoni , mimi nikajua ulikwisha sahau”
“ Hapana Steve siwezi kusahau kabisa yaani , na hakuna mtu wa kunishawishi , nakaa kimya tu kutokana na kwamba sitaki kisasi kifute ndoto zangu kwani naamini hata mama hatofurahia kabisa akiniona naishi kwa ajili ya kulipiza kisasi”
“Kwa hio Peter kumbe mama yako alikufa kwa ajali”Aliuliza masumbuko
“ Ndio ni story ndefu Masumbuko sipendi kuikumbuka kabisa “
“Hata mimi mama yangu alikufa kwa ajali “ Aliongea Masumbuko na kumfanya Peter amwangalie kwa maswali .
“Alikufa kwa ajali gani ??”
****
“ Nakuona unavyo mfanya mtoto akolee rafiki yangu “
Aliongea Lea akiwa amejilaza pembeni kwenye viti vya kuegamia huku akiwa ameshikilia kikombe cha pombe (Solo cup) Pembeni yake kushoti akiwepo Sebastiani akiwa amekaa mkao kama wake wote alikuwa wamevaa mavazi ya kuogela huku wakimwangalia Stella alie kuwa katika Swimming pool akiogelea kwa ustadi mkubwa ,alikuwa akizama na kwenda kuibukia mbeleni , kiufupi alikuwa kama kivutio siku hio katika eneo hilo kwani uzuri alio kuwa nao wa maji ya kunde ulikuwa ukivutia sana na shepu ambayo mungu amembariki nayo ilizidi kufanya kuonekana mzuri na hata pale alipo kuwa akiingia na kuibuka kwenye maji alifanya kuonekana kama malaika
“Huyu mwanamke mzuri sana , nimeona wanawake wazuri ila huyu ni kiboko , yaani hata huyu bwana wako namuona fala kumuacha kimwana kama huyu”
“Aacha hizo ujue Sebastian kwani kuwa mzuri ndio kupendwa ,ingekuwa wanawake walio na sura mbaya hawaolewi sasa”.
“Acha wivu wewe.. kiufupi pale haumfikii hata kwa dawa , Stella mzuri na pia ana roho nzuri , na ndio maana anazidi kuwa mzuri , sio kama wewe”
“Sikia seba.. huo utani sitaki , yote nilio yafanya nimefanya kwakuwa nampenda sana James na ningemkosa ningekuwa mwehu , mimi ni tofauti na Stella huoni hata hali yake kwa sasa ni nzuri , mimi nisingeweza roho yangu nyepesi”
“Hahaha.. kwahio ulijuaje kama Stella ataweza .. hio ndio roho mbaya ninayo zungumzia sasa, kujijali mwenyewe pasipo kumjali mwingine”
“Sikia seba utaniudhi sasa hivi , jishaue tu na wakati mimi ndio nakufanya uwe na Stella , fikiria tu siku atakavyojua ulikuwa kwenye mpango wa kumuachanisha na boyfriend wake sijui atakufanya nini”
“Basi yaishe mrembo ee , nilikua natoa ya moyoni , lakini nina furaha maana sasa hivi ninae Stella nahisi Dunia yote yangu , japo hajanikubalia ila naamini atanikubalia tu”.
“Halafu seba hivi utakuwa mzito mpaka lini , wewe unavyo endelea kuamini , utajikuta mtoto sio wako , wewe humuoni alivyokuwa mzuri wewe haya tu zembea”
“Kwa hio wewe nataka nifanyaje , na wakati unaona Stella mwenyewe bado anaonekana ana majonzi sema anajikaza kuonekana yupo sawa”
“Ndio maana nakwambia jitahidi umsahaulishe mtoto huyo na jijengee mazingira akuone mwanaume wa tofauti na wengine , mfanye akuamini “
“Najitahidi sana ”
“Bado.. , sasa sikia Stella jambo ambalo lina muumiza kwa sasa ambalo ni kama udhaifu wake mkubwa ni kumfunga Masumbuko huyo rafiki yako , lakini kumbuka akimpata Masumbuko basi na wewe umekamatika na Stella hatokuamini tena na anaweza akakufunga na wewe, maana anaijua sana sheria na utakuwa umekosa kila kitu na mimi sipo tayari kwa hilo”
“Sasa nifanyaje mbona kama unanitisha , mimi akinikamata nakuunganisha”
“ Huo ndio utakuwa umama sasa , hautokuwa mwanaume wewe inabidi ufikiria namna ya kujitoa kwenye kesi ili hata Masumbuko siku atakayo kamatwa wewe hautahusika moja kwa moja, anza kutengeneza ushahidi wa lile tukio kuwa haukushusika na pia tafuta ushahidi au hata kwa kuutengeneza ili umfanye Masumbuko kuwa na hatia moja kwa moja”
“Seba nimefurahi kweli leo asante kwa kunileta hapa , unajua nilikuwa nasikia Sea breeze ila sikujua kuwa pako vizuri kama hivi” Aliongea Stella na kuwafanya Lea na sebastiani kukanyamaza.
“ Ni kweli Stella yaani pazuri ,tupigeni picha basi” Aliongea lea huku akimsogela Stella aliekuwa akijifuta maji na taulo .
“Seba kaa na Stella basi niwapige picha” Aliongea lea na kuwafanya Stella amwangalie Sebastian na Sebastian alimwangalia Stella na kisha wakatabasamu kwa pamoja na kwa ushawishi wa Lea basi walikubali na kupigwa picha na Stella”
“Nitawatumia hizi” Aliongea Lea huku akitabasamu sana maana zilitoka kama alivyokuwa anataka .
****
Huku nyumbaani kwa Mama Rania alionekana Najma akitoka kwenye chumba chake akipiga miayo akielekea chini kwenye sebule yao na muda huo ilikuwa ni muda wa saa saba mchana .
“Hi! dad good afternoon!” Alisalimia Najma baada ya kumuona baba yake wakati tu alipofika sebuleni wakati huo baba yake alikuwa akiingia na sijui alifata nini maana siku hioo alionekana kuwahi kurudi jambo ambal sio kawaida yake .
“Naona leo umewahi , maana nakuona ukirudi saa sita au saa saba usiku “
“Leo kuna kitu nimerudi kuchukua mara moja na nitarejea baada ya muda kidogo , wewe mbona haujatoka kwenda kwenye mandalizi ya ufunguzi wa kampuni yako”.
“Nimetoa tu maagizo kwa wafanyakazi wangu siku hizi sipendi hata kutoka”
“Unaonekana kuwa na jambo maana si kawaida yako my princess“
“Yeah dadie ni juu ya yule mkaka , I am head over heels for him, please help me to find him dadii please “ (Ninamuwaza yeye tu baba )Akijidekeza kwa baba yake .
“My daughter nafanya kila njia kuhakikisha nina mpata and very soon tu utasikia taarifa ya kufurahisha maana timu yangu ipo uraiani huko inamtafuta “
“Asante sana dad ndio maana nakupenda I real love you dad “ Aliongea Najma maana alikuwa na uzungu mwingi yaani alikuwa hamuogopi baba yake kabisa ,watoto wengi wa kiafrika kumwambia baba ya kuwa wapo kwenye mapenzi ni swala gumu sana na kwao linaonekana kama ni utomvu wa nidhamu , ila kwa maisha ya wenzetu uzunguni huko ni swala la kawaida , pia baadhi ya familia za kiafrika washaathirfika na tamaduni za kizungu .
“Vipi na dada yako , unataka kuolewa kabla yake?”
“Dada naye anaanza kuwa kama mimi tu “ Alingea Najma nakumfanya Samir kumwangalia kwa mshangao , huku wakikaa kwenye masofa ya hapo sebuleni .
“Unamaanisha nini kuwa anaanza kuwa kama wewe?”
“Siku hizi hata si muelewi kuna mkaka nadhani kaanza kazi kwenye benki yetu sasa kila saa dada anamzungumzia mara amsifie na hata wakati mwingine usiku anaota akiongea huku akilitaja jina lake”
“Sasa yeye anakuwaje kama wewe , wewe si mwanaume unaempenda ,wewe ni tofauti na Rania “
“ Hata kama Dady nataka niende hapo kazini kwao nikwamuone huyo mwanume anae mchanganya dada yangu yukoje koje huyo “ Alingea Najma na kumfanya baba yake mapigo kuongezeka maana alijua kama ataenda basi anaenda kukuutana na Peter mwanaume anae mtafuta .
“Sikia unaonaje tukienda wote,mimi na wewe ,ninataka kumuona huyo mwanume kama kweli anamfaa mwanangu Rania maana nawajua wanaume waongo sana “
“Sure dad , nitakuambia siku nikipanga kwenda kumuona ili twende wote “
“Hapana Najma mimi nina kazi nyingi so nitakuambia siku nzuri ya kwenda”
“Sawa dad , but I cant wait , better make it soon dady “
“Worry out my daughter , but promise we do this together right “(Usijali mwanangu lakini hii ni ahadi ua sisi kwenda pamoja )
“Yess dady “
Samir alijikuta akitoka hapo huku akijifuta jasho maana anaona kazi inazidi kuwa ngumu watoto wake wanamchanganya vibaya .
“Nisipo fanya kitu hawa wapuuzi watakutana na inaweza kuleta matatizo kwa wote , inabidi nifanye kitu mapema kabla jambo baya halijatokea ,sina jinsi inabidi Rania aolewe na Hemedi , halafu anisaidie kumwangamiza Peter ili hawa mapacha wanaojifanya wanajua kupenda , nawaletea habari ya kifo tu”Alijiwazia huku akiingia chumbani kwake kwa ajili ya kuchukua kitu kilichomrudisha nyumbani .
SEHEMU YA 19
Samiri alikuwa kweli amedhamiria kumfanya Rania aolewe , aliamini njia ya kumuepusha na Peter ni ndoa .
Hivyo hakuwa na jinsi zaidi kumkubali rafiki yake awe mkwe, sababu hakuwa na cha kupoteza Ramia aolewapo na Hemedi , pia mali zake zingekuwa salama kuliko watoto wake kuwa na mahusiano na kijana Peter .
Alishangaa wakati mwingine ni kwanini alikuwa akimchukia sana Peter na kujithamini wapi chuki hio imetokea mpaka kuwa na nguvu ya kutomtaka kijana huyo kuingia katika maisha ya wanae , lakini hisia zake zilimwambia Peter hakuwa mtu sahihi kwa wanae zaidi ya maslahi na pia hakuamini kama kijana huyo alikuwa na mapenzi ya dhati kwa wanae , lakini pia aliona hatari ilioko kwa kijana huyo kupendwa na familia yake yote .
Siku hio wakati akiwa nyumbani alijihisi kuboreka kubakia hpo kwa muda mrefu ,lakini pia hata ile muwashawasha wa kwenda kutembea uliongezeka mara baada ya kuona meseji ya mchepuko wake Amanda , aliingia bafuni na kujiswafi .
Na kisha akaanza kujiandaa lakini wakati anachukua ufunguo ndio Mama Rannia alikuwa akiingia kutokea kazini.
Mwana mama huyu japo mume wake alikuwa akimnunia ila hakuacha kuonyesha heshima kwa mume .
“Haa ! Mume leo naona umewahi kurudi kazini”
“Ndio kuna kitu nilifuata ila ninaondoka na nitachelewa kurudi”
“Sawa mimi kesho nasafiri kikazi , unaonaje leo ukiwahi kurudi nyumbni mume wangu nimekumisi sana mpaka najisikia vibaya jamani”
Samiri wala hakujibu neno lolote zaidi ya kufungua mlango lakini kutokomea lakini sekunde mbili mlango ulifunguliwa tena na alikuwa ni Samiri , Mama Rania alimwangalia.
“Nimesahau kukutakia safari njema”
Aliongea na kisha alifunga mlango ,mwanamama huyu chozi lilimtoka na kujawa na hudhuni ,hakuamini kabisa mabadiliko ya mumewe kiasi cha kutomjali.
Alikaa kwenye kitanda akifikiria kosa gani amelifanya mpaka hali ya ndoa yake kufikia hatua hio , kuna muda alitamani hata kumfukuza Peter kazini ili hali ya ndoa yake irudi kama awali , lakini akikumbuka kuwa Peter alikuwa tegemezi katika kuimarisha ulinzi wa benki ,wazo alilitupilia mbali , ni zaidi ya mwezi yeye na mume wake kuishi kama dada na kaka
****
Ndani ya hoteli ya Coral Beach alionekana Lea siku hio ndani ya chumba kikubwa cha hadhi ya juu akiwa ameshikiliwa kiuno na James huku akiingiza mwiko wake ndani na kutoa huku kimwana huyo akitoa miliio ya kimahaba ,alionekana dozi anayopewa na james haikuwa ya kawaida .
James alikuwa akimkunja kama kambale na alionekana kubobea kweli kwenye mambo ya sita kwa sira kwani alionekana shughuli kuimudu vizuri takribani dakika kumi na tano walikuwa washamaliza na wote kufika ukingoni.
“Asante sana Hubby “ Aliongea Lea huku akimwangali James usoni aliekuwa akihema kama mbwa alie kimbia maili nyingi “
“Hauna haja ya kushukuru mpenzi wangu mimi hii ndo kazi yangu ya kuhakikisha kwamba nakuridhisha ili usije ukanitoroka ukaenda kwa wengine kwani nitaumia sana mpenzi , nimeumizwa na Stella sitaki kuumizwa na wewe tena”
“Usiwe na wasiwasi mpenzi kwa ninavyokupenda haitokuja itokee eti nakusaliti mpenzi wangu , mimi niwako tu peke yako , unavyo niacha ndivyo unavyo nikuta “
“Hata mimi nakupenda sana Lea na sipo tayari kuuona huu uso wako unatoa machozi kisa mimi kukusaliti , kwanza nataka ukimaliza tu chuo nakuoa”
“Kweli mpenzi , uko siriasi “
“Ndio kwani wewe hautaki kuolewa ,
“Nataka mpenzi ila unajua mapenzi yetu hayana uhuru kwani lazima kila siku tukifanya yetu tujifiche ili Stella asione , natamani kutembea na wewe kila mahali kuonyesha ulimwengu mzima kama napendwa na wewe james mwanume wa maisha yangu ”
Aliongea Lea kwa hisia kubwa na walianza akuchokozana tena, na kwa mara nyingine wakaingia kwenye tendo hilo la kuzini na walidumu kwa dakika kama ishirini , na kati yao hakuna hata mmoja alie kuwa akikumbuka kondomu walionekana kuaminiana.
“Vipi mpenzi lini tena warudi Kenya?”
“Kesho narudi ,nitakuwa huko kwa mwezi mmoja , halafu haujaniambia Stella anaendelaje kwa sasa , si rafiki yako?” Aliuliza James na lea kumuona bado anawasiwasi na hali ya Stella.
“Anaendelea vizuri tu wala hakuwazii , ngoja nikuoneshe maana saivi ana mpenzi mpya na hana habari na wewe “ Aliongea huku akimuonyesha baadhi ya picha ambazo zilimuonesha Stella akiwa kwenye kivazi cha kuogelea ,James alisisimka baada ya kuona umbile la Stella
Lea alikuwa akifanya kumuonesha James ,alimjunesha za Stella na Sebastian wakiwa kwenye pozi mbele ya Swimming pool
“Huyu ndio mpenzi wake mpya ?”
“Ndio huoni walivyo pendeza “
“ Hongera yake , nilijua tu kama hanipendi huyu mwanamke nilikuwa namwamini sana kumbe mchafu namna hii , sitokuja kumsamehe “
“ Usimchukie sana mpenzi , kwanza upo na mimi mwanamke ninaye kupenda , haina haja ya kumuwazia Stella tena” Aliongea Lea huku Stella akielekea bafuni akimwacha James.
James alishika simu yake na kuwasha data na kuangalia message za Watsapp, alijikuta akitabasamu baada ya kuona jumbe kutoka kwa jina la Business partner ,jumbe ya sauti (voice notes) , aliweka ‘Earphone’ masikioni na kusikiliza huku tabasamu pana likiwa limeupamba uso wake , inaonekana jumbe hio ilimfurahisha mno , pale alipomuona Lea anatoka bafuni ndio akajikausha na kuweka simu pembeni baada ya kufuta ule ujumbe .
****
Ilikuwa ni siku nyingine siku ambayo Mama Rania na kijana Peter walikuwa kwenye gari moja aina ya Range Rover Spot huku dereva akiwa Peter akiwa makini na usukani , pembeni yake alikuwa ni Mama rania alieonekana kusinzia, hakuwa na habari kabisa kwa alivyojiachia kwani sketi aliovaa ilikuwa imepanda mpaka kwenye mapaja ,ukizingatia pia kigauni alicho vaa kilikuwa chepesi sana , mwanamama huyu hayo ndio maisha yake ,alikuwa na uzungu mwingi hata kazini kwake.
Gari ilizidi kuyoyoma na ndani ya masaa manne gari ilikuwa ikipita sehemu moja inayoitwa Soni hapa ndio Mama rania alishtuka kutoka usingizini .
“Nimelala sana?”
“Yeah ndio tuko eneo moja linaitwa Soni na muda si mrefu tunafika lushoto mjini “
“ Aisee nimelala”
“Unaonekana kuchoka sana”
“Yeah nimechoka sana jana sikulala kabisa mpaka kuna kucha “
“Tatizo lilikuwa ni nini sasa ?”Aliuliza Peter huku akiwa makini zaidi na barabara kwani makona yalikuwa mengi .
“Mambo ya kawaida tu , halafu kuna baridi huku” Aliongea Mama Rania baada ya kupandisha kioo.
“Ndio huku ni juu milimani , milima ya Usambara , ni kuzuri kweli nishawahi kufika mara nyingi nyingi kuna baridi ,ila kuna maeneo mazuri ya kutembelea”
“Kumbe nipo na mwenyejii, basi inabidi unipeleke peleke hayo maeneo ya vivutio nikaone na mimi”
“Hilo hata usijali Boss”
Walitumia masaa machache sana kufika Soni, na moja kwa moja waliingia Lushoto mjini na kwakuwa ailikuwa mapema sana , waliingia kunywa chai kwenye mgahawa na baada ya hapo wakaanza ukaguzi ndani ya jengo hilo la benki , na Peter yeye akiwa na kazi ya kuweka mfumo mpya kwenye tarakishi pamoja na vimashine flani vya mtandao .
Kazi ilifanyika kwa masaa manne mpaka kuisha na iliisha mapema kabla hata ya muda ambao walipanga kuutumia , baada ya kazi zote hatimae waliondoka huku wote wakiingia kwenye gari na kuelekea kwenye hoteli moja maarufu sana ndani ya Lushoto ilio kuwa ikijulikana kama “IRENTE VIEW “ hii ni hoteli moja nzuri sana ilio kuwa ikimilikiwa na marehemu raisi mstaafu Benjamini mkapa , ilikuwa juu ya mlima na ukiangalia kwa chini unaona maeneno ya tambarare , kama nji za kwenda Moshi , Mazinde na baadhi ya maeneo mengine ni eneo zuri kweli kwa hoteli hio kuwepo .
:Jamani kuzuri huku , kuna mazingira safi hadi raha na hewa safi kabisa “ Aliongea Mama Rania wakati wakitoka kwenye gari baada ya kuingia ndani ya hoteli hio.
****
Tajiri Samir hakurudi nyumbani siku ambayo mke wake alikuwa amemuambia kuwa kesho yake atasafiri kikazi na wala hakujua kabisa mke wake alikuwa amesafiri kuelekea wapi Zaidi ya kujua yupo safari kikazi .
Usiku wa siku hio Mama Rania alimsubiri sana , alikuwa akitamani kupata haki yake ya ndoa na alikuwa kwenye hali mbaya sana , lakini Samir hakurudi kabisa kwani mchepuko ulikuwa umemshikilia sana siku hio .
“Umeamkaje mpenzi?” Aliuliza Amanda ,alikuwa amekaa kwenye Dressing table akijipodoa ,ilikuwa ni muda wa asubuhi na Samir ndio kwanza alikuwa akitoka usingizini .
“Jana umeniweza kweli yaani nimesahau kabisa kurudi nyumbani “
“Nipo hapa kwa ajili ya kukusahaulisha kuhusu mkeo maana najua upo kwenye wakati mgumu sana wewe ni familia yako “
“Ni kweli , ila yataisha tu ,”
“Vipi mke wako leo si atakuwa na presha huko”
“Kweli na anavyonipenda sidhani kama jana alilala, maana kila siku namkuta yupo macho ananisubiria , halafu aliniambia kuwa anasafiri kikazi”
“Masikini saivi atakuwa na mawazo safari nzima”Aliongea Amanda pasipo kujali kuwa anaye mfanyia hivyo ni mwanamke mwenzake na anaiharibu nda ya mwanamke mwenzie.
****
Sebastiani alikuwa ndio kwanza kutoka chuoni , aliingia ndani kwake na kisha akajirusha kwenye sofa lilipo ndani ya chumba chake .
“Stella unaninyima usingizi , ila nitakupata tu kwa namna yoyote ile upo ndani ya mawazo yangu sana , nakufikiria kila wakati” Alijiwazia sebastiani huku akiangalia feni inavyozunguka .
“Inabidi nikusaidie katika swala lako na Masumbuko na naamini kupitia hili lazima unipende mwenyewe”
Alinyanyuka na kuweka begi lake lilibeba tarakishi mpakato kwenye meza na kisha, alivua nguo zake na kuingia bafuni ,chumba chake kilikuwa ni self container , alimaliza kuoga na kuanza kujifuta maji , kuna wazo lilimjia ambalo lilimfanya atabasamu .
“Aliifuata simu yake na kisha akamtafuta Steve na kumuuliza yuko wapi na alijibiwa kuwa yupo kazini bado , aliuliza na kuhusu Masumbuko na kupewa jibu kuwa yupo nyumbani na Peter alikuwa mkoani kikazi . majibu hayo yalimfanya atabasamu na kuvaa nguo zake na kujiandaa haraka haraka .
“Hapa naenda kwa masumbuko kuchukua ushahidi au kuutengeneza na hivyo hana akili atajaa tu” Alijiongelesha huku akitabasamu kinafiki.
SEHEMU YA 20
Sebastian alipanda daladala na moja kwa moja alielekea Mbezi Beach nyumbani kwa Peter na Masumbuko , kutokana na muda huo kutokuwa na foleni kubwa , alitumia dakika arobaini na tano hivi kufika Mbezi Beach , alikuwa akipahafamu sehemu ambayo alikuwa akiishi Peter , alivuka barabara na kunyoosha juu kabisa mpaka nyumbani wanapoishi .
Masumbuko wala hakuwa na habari kwani muda huo alikuwa akiangalia muvi kama kawaida yake maana alikuwa akipenda sana TV.
Alisikia mlango unagongwa na akanyanyuka na kusogelea na kuchungulia kwanza ni nani anaye gonga na alivyo muona ni Sebastian kwanza aliogopa na kuanza kujishauri kufungua ama asifungue , lakini mlango ulizidi kugongwa ndipo alipo kata shauri na kufungua mlango .
“ Wewe fala nagonga hata haufungui , ulikuwa umelala nini?”
“Hamna nilikua najishauri nifungue au nisifungue “
“ Ulijua anaye gonga alikuwa mimi au? “
“ Ndio nilichungulia kabla ya kufungua”
“Sasa kwanini ulikuwa unajishauri kufungua , au ulikuwa unaogopa yale ya siku ile , yale yalipita na sina time nayo chukulia poa tu “
“ Unasema kweli ?”
“Ndio namaanisha , mimi siwezi kukosana na mwanaume mwenzangu kisa demu”
“ Asante sana , mimi hata siku ile sijui nilifikiria nini maana nilijikuta tu nimefanya vile “
“Vipi umefanya” Aliuliza huku akikaa kwenye sofa
“Si kukufanya uwe muhudumu”
“Hahaha... sema ulichonifanyia wewe boya ,ndio hivyo nimekusamehe maana Peter ni rafiki yangu na wewe pia umekuwa rafiki yangu kuanzia leo na kuendelea”
“Asante Sana”
“Peter yuko wapi?”
“Kasafiri “ Alijibu Masumbuko huku akikaa na yeye maana muda wote alikuwa amesimama . wakati huo Sebastian na yeye alikaa vizuri nakutoa simu yake akatachi akapangusa pangusa na kugusa ,ilikuwa simu janja ,kisha akamwangalia Masumbuko .
“ Masumbuko halafu unajua ile siku ulinishangaza sana hivi ulimla yule mwanamke ?”
“Ndio nilimpiga kitu safi mpaka akazimia nikaachana nae maana pale nilimpa kumbukumbu za masaa mawili”
“ Haha .. kwahio ni kama ulimpiga changa la macho na ukala kitumbua si ndio?”
“Yeah nilimbadilisha mawazo sijampiga changa la macho “
“Sasa kwani kuna utoafauti gani kati ya changa la macho na kumbadilisha mtu mawazo?”
“Mimi Sijui jibu wewe”
“Namaanisha si kama umembaka vile?”
“ Kwani kumbaka mtu inakuwaje kuwaje?”
“ Si kama kumfanya bila ya kujua anacho fanyiwa, hapo utakuwa umebaka mtu kwa sababu alikuwa hajui “
“Ndio nimembaka basi”
Basi Sebastian aliaga huku akimwambia Masumbuko kuwa amekuja kwa jili ya kuonana na Peter ila kwa sababu hakuwepo alisema atakuja siku nyingine .
Sebastian alifika geto kwake huku akitabasamu na kutoa simu yake na kuanza kuplay na hapo hapo ikaanza kusikika sauti ya Masumbuko .
”Ahahaha.. nimembaka basi , masumbuko wewe huna akili na utaenda jela bila ya kupenda fala wewe”Aliongea Sebastian huku akitoa ile memory kadi na kuweka kwenye kijiboksi hapo ndani . .
*****
Tajiri Samir alikuwa amedhamiria kwa silimia mia kuwa lazima afanye maamuzi mapema , kwani kila alipo fikiria kuwa Rania ashaanza kuwa na hisia na Peter alipata wasiwasi hali hio aliiona kama bomu linalotaka kulipuka na ni yeye tu ambae anaweza kulitengua .
Wakati akiwa ofisini kwake alitoa simu yake na kumpigia rafiki yake Hemedi na kumwambia kuwa jioni wakutane maeneo yao ya kukutania kwani ana jambo la kumwambia .
Basi baada yakufanya kazi na kumaliza tayari ilikuwa ni mida ya jioni ambayo alipanga kukutana na tajiri Hemedi katika hoteli ya Kilimanjaro kwani hapo ndipo makazi ya Hemedi akitaka kujivinjari na mwanamke yeyote yule .
Samiri alifika nakuegesha gari yake na kwakuwa aliambiwa na bwana Hemedi kuwa wakutane kwenye chumba alichokuwa anapendelea kuchukua hotelini hapo , basi Samir alipandisha juu kabisa mpaka kwenye chumba hicho.
Alifungua mlango na kuingia ,alimkuta Hemedi akiwa na mwanamke mmoja alie valia chupi tu , Hemedi baada ya kumuona rafiki yake alimruhusu yule mwanadada aondoke huku akimminya kalio .
Kitendo kile alikishuhudia Samir na kujikuta akipandwa na hasira hasa alipo fikiria kuwa huyo ndio mwanume ambaye anapaswa kumpa Rania kwa ajili ya kumuoa .
“ Niambie Samir , umefikiria juu ya ombi langu?” Aliongea huku akimimina pombe kwenye glass na kumpa Samir , huku Samir wakati huo alikuwa na hasira kila akifikiria vitendo vichafu vya Hemedi alijiona kabisa huyo hafai kabisa kumuoa mwanae.
“ Ndio nimefikiria”
“ Haya niambie baba mkwe”
“ Sikia Hemedi nimegundua wewe sio rafiki yangu umnafiki , unatumia nafasi ya matatizo yangu ili kumpata mwanangu , sasa mimi kama baba yake sipo tayari kwa hilo.”
“ Samir wewe ni rafiki yangu sana na tumesaidiana katika mengi na unanijua vizuri , kwani kuna shida gani ya mimi kumuoa mwanao?: na kwanza wewe unakuwa kwenye nafasi nzuri kwani Rania utampa mali zako na mimi sina shida na mali zake atazitunza na kumpa mwanae atakae mzaa na hakutakuwa na mgogoro wa mali zangu na watoto wangu wakubwa sasa hiko unacho kichukia ni kipi, mbona kuna watu wengi tu wazima wana oa mabinti “
“Sikia Hemedi wewe ni mnafiki sana na nia yako nishaijua wewe kwa kupenda kwako ngono najua unamtaka na mtoto wangu kwa ajili ya kumchezea , hivi na hio tabia yako kweli naweza nikakupa kweli mtoto wangu mimi si nina mchimbia kaburi mwenyewe “
“ Sikia Samir ni kweli unajua tabia yangu ila ni kuhakikishie kuwa nipo tayari kubadilika kwa ajili ya Rania kwasababu sijampenda Rania jana wala leo , ni muda mrefu sana na nilikuwa nikiogopa sana kukuambia hilo lisije lika leta athari kwenye urafiki wetu”
“ Kwa hio ulisubiri mpaka sasa ambapo nina matatizo ndio kuniambia kwakuwa unajua kabisa sitokuwa na jinsi?”
“ Sio hivyo rafiki yangu , ni kwamba sipo tayari kumuona Rania anampenda mtu mwingine na wakati mimi nipo hai , na isitoshe pia sitaki na familia yako kusambaratika na kuingia kwenye migogoro kisa mwanaume , tena mwanaume ambae hana mbele wala nyuma”
“ Hio sio sababu ya kutosha ya mimi kukupa mtoto wangu”
“Sababu kubwa ni hii hapa” Alivuta bahasha moja na kutoa picha na kuzimwaga mezani na hapo ndipo Samir aliona kama akili yake haifanyi kazi vizuri kwani aliona picha zikimuonesha Rania akibusiwa kwenye paji la uso na Peter”
“ Nadhani umeona sasa, hio nayo ni sababu kwani inanikasirisha sana kumuona mwanmke ninae mpenda akibusiwa hivyo na hio ni kwenye paji la uso kesho na kesho kutwa atabusiwa kwenye lipsi na kumpa kabisa kitumbua , nadhani kwa kiburi ambacho watoto wako wamerithi kutoka kwako sijui utamwambia nini akuelewe kuwa umemtafutia mchumba wa kumuoa”
Samir alijikuta akikaa chini na kunywa glass yote ya bia na kuisikilizia inavyo choma koo na kisha akatulia na kuanza kufikiria huku akiziangalia picha zilizo kuwepo hapo mezani , alipeleka mawazo yake kwa Rania na kufikiria ubishi wake na msimamo wake pale anapohitaji kitu , akamfikiria Nasma
ujeuri aliokuwa nao , akamfikiria Peter na yeye na kuanza kumpima sifa zake kama anafaa kuwa na mwanae hata mmoja aliona hafai.
“ Unajua Samiri wewe hata kuua mtu najua hauwezi , ila mimi nitakusadia kumpoteza kijana Peter kwajili ya kuwaokoa wanao “ Aliongea Hemedi na kumfanya Samir aliekuwa kwenye mawazo amwangalie na kujiuliza hitaji lake kuu ni nini , alijibu kuwa kujiambia kuwa hitaji lake kuu ni Peter kupotea katika uso wa Dunia ili kuiokoa familia yake.
“ Una uhakika juu ya hilo la kumpoteza Peter “
“ Ndio hilo naweza sana na lipo ndani ya uwezo wangu ,ni wewe tu kunipa baraka nimuoe mwanao na wewe utumie ubaba kumfosi mwanao nimuoe na mimi najua jinsi ya kumpata Rania kama ndio jambo ambalo lina kuumiza kichwa .
Samir alimwangalia rafiki yake huyo ambae dakika chache za nyuma alikuwa akimwamini sana katika kumwambia shida zake , kwake aliona mazungumzo hayo yalikuwa ni kama ya kibiashara.
“ Daah..! “ Aliongea Samiri na kukatishwa na simu ilokuwa ikitoa mlio wa sauti ikioonesha kuwa kuna mpigaji , alitoa na kuona ni namba ngeni .
“ Boss za siku nyingi!”
“ Salama nani mwenzangu?”
“ Ni mimi Krispine kutoka kampuni ya POPOTE TUNAFIKA , ulinipa kazi nifuatilie taarifa za yule mwanamke ,nimepata taarifa yake na mwanae”
“Uko wapi?”
“Nipo Ubungo”
“ Nakuja “
“Hili tutaongea siku nyingine Hemedi” Aliongea Samir na kisha kuondoka .
****
Tukiingia ndani ya mji wa Lushoto , alionekanna Mama Rania akiwa kwenye chumba chake ndani ya hoteli , baada ya kila mtu kuchukua chumba .
Chumba cha Peter kikiwa kipo mkabala na chumba cha Mama Rania , hoteli ilikuwa na mazingira ya kuvutia sana kwani chumba kilionekana kuwa kizuri mno .
Mama Rania alikuwa amekaa kwenye kitanda chake akionekana kuwa na mawazo , akiwa ameshikilia simu yake , ni kama alikuwa akisubiria mtu amtafute . na nikweli alikuwa akisubiria ujumbe ama simu kutoka kwa mume wake , kwani tokea alivyo ondoka jana yake nyumbani hakurejea kabisa , na mbaya Zaidi ni kwamba na yeye ameondoka bila ya kuonana nae , japo alikuwa akijua kuwa mume wake alikuwa akichepuka lakini hakuacha kumpenda mume wake na alitaka tu kujua hali ya mme wake kuwa anandeleaje .
Wakati akiwa kwenye mawazo akiwa amekaa kwenye sofa , jina la ‘My favourite Naa’ lilisomeka kwenye kioo cha simu yake janja ukiambatana na mlio wa sauti wa wimbo wa ‘Alan walker –Faded’, alikuwa ni mwanadada Nasma ,alitabasamu huku akiipokea na kuweka sikioni na kuanza kuongea na mwanae . alionekana kuna jambo la kufurahisha ambalo alikuwa akiongea na mwanae huyo maana hali yake ilibadilika na kuonekana kutabasamu .
Mama Rania alijikuta akitamani kupiga soga na Peter mara baada ya kumaliza kuongea na simu , kwani alikuwa amemzoea sana Peter na hususani akiwa kwenye hali ya mawazo mara nyingi mtu ambae amekuwa tabibu wake wa kumrudisha katika hali sawa alikua ni Peter , alinyanyuka kivivu na kuchukua kitenge chake na kujifunga huku akiwa amevalia kijisketi chake chepesi kwa ndani alitoka na kwenda mpaka kwenye chumba cha Peter , aligonga na kusubiria na baada ya muda Peter alifungua mlango hukua akiwa amevalia singlend na bukta lake .
“ Vipi naweza kuingia? “ Aliongea Mama Rania huku akimwangalia Peter usoni aliejifikiria kwa sekunde na kisha alimruhusu mama huyo na kuingia
“ Najihisi upweke kukaa mwenyewe nimeona nije unichangamshe
changamshe maana naona kama mawazo yananiandama”Aliongea Mama Rania
na Peter kwa akili yake ya haraka alijua kabisa mama huyo alikuwa akisumbuliwa na mawazo kwani kule njiani alikumbuka alimwambia kuwa hakulala kabisa usiku wa jana mpaka kunakucha .
“ Basi stori zilianza , na kama kawaida Peter kwakuwa alikuwa haishiwi na stori za uongo na kweli Mama Rania hali yake ya furaha hatimae ilikuwa imerudi kwa kiasi fulani , uzuri wa kile chumba ni kwamba kilikuwa na sehemu ya kukaa yaani kulikuwa na masofa(master suite room) ambayo yamepangwa na yalikuwa yakiruhusu watu kama watatu kukaa .
Baada ya kupiga stori kwa muda mrefu , huku hali ya hewa ya Lushoto ikizidi kuwapa kajiubaridi na kumfanya Mama Rania atoe ile khanga alio jifunga na kujifunika mabegani na wakati huo walikuwa wamehamia kwenye kungalia onyesho fulani la wanamuziki kutoka Marekani wakionyesha uwezo wa kwenye kuimba(Stage perfomance ) , sasa Peter alidhania mama Rania anapenda kile alichokuwa akiangalia kumbe mwenzake alikuwa ashalala muda na saa ilikuwa ikisoma saa nne usiku muda huo , Peter muda wote alikuwa akijua kuwa na mwenzake yupo makini kwenye kuangalia maana alikuwa akiona vijiaibu flani hivi vya kugeuka na kumwangalia Mama Rania usoni. Na hakujua kwa nini alikuwa na hali hio .
Baada ya dakika kadhaa alijikuta akigeuka na kumwangalia Mama Rania , hapo ndipo alipo gundua kumbe mwenzake ashapotelea usingizini muda mrefu huku akijiegamiza vibaya kwenye lile sofa ,Peter alimwangalia na kuona kweli boss wake kachoka , aliamua kunyanyuka lakini mara Mama Rania kwa jinsi alivyo kuwa ameegamia lile sofa alijikuta akielekea chini na Peter kwa uharaka wake alijikuta akichuchumaa na kumdaka na hapo Mama Rania ndipo alipo kuja kushituka akiwa kwenye kifua cha mwanaume na uso umekaribiana na wa Peter huku akihisi pumzi ya joto ya kijana , kwakuwa kijisketi alicho vaa kilikuwa kifupi kwani hizo ndio nguo zake , basi mapaja yote yalikuwa yamegusana na miguu ya Peter kwani alikuwa amevalia bukta .
Mama Rania alijikuta akihisi joto Fulani na pumzi ya Peter ilio kuwa ikimpumulia na kujikuta hisia za mapenzi zikimpanda na kwa upande wa Peter kama mwanaume rijali alikuwa akihisi joto la ajabu sana kutoka kwenye mwili wa Mama Rania na kujikuta dunguso yake kusimama wima na kugusa mapaja ya Mama Rania.
Mama Rania alijikuta akishusha mdomo wake taratibu kwa Peter , kisha lips zikagusana na kwakuwa Peter alikuwa mgeni alikuwa haelewi haelewi chakufanya alikuwa kama mtu aliepigwa shoto na kuhitaji kunasuliwa , Mama Rania alicharuka kwani hisia zilikuwa zimempanda kiasi kwamba kwa hali alio kuwa nayo shetani asingeweza kujizuia , na ukizingatia hajakutana na mwanaume kwa muda mrefu hali ilikuwa mbaya kwake alijisemea liwalo na liwe .
Mama Rania alimshika Peter mkono na kuushikisha kwenye mapaja yake karibu kabisa na kitumbua na kumfanya Peter ahisi msisimko wa ajabu sana na uliongezeka pale Mama Rania alipogusa dunguso ya Peter.
Peter alishindwa kabisa kujizuia kwani hisia zilikuwa zipo juu na ukizingatia kuwa hakuwahi kufanya kitendo hicho tokea azaliwe, basi kujikontrol ilikuwa ni ngumu sana kwa kijana kama Peter kwani alianza kabisa kutoa ushirikiano , Mama Rania alinyanyuka na kumuinua Peter huku wakipeana juisi ya mdomoni na mwanzoni Peter alikuwa hajui hatua ila muda ulivyo zidi kwenda alijikuta akianza kuwa fundi , Mama Rania alishusha nguo yake ya ndani pasipo kuvua ile sketi na kisha akatoa na sidiria na kijiblazia alichovaa, alichukua mkono wa Peter na kushikisha kwenye hazina yake na Peter alielewa somo na kutumbukiza kidole na kuanza kazi ya kusugua na kumfanya Mama Rania atoe miguno huku akijinyonga nyonga , Mama Rania aliona kama anacheleweshwa kwani wakati huo hata haikueleweka Peter alivua saa ngapi lile libukta ,wakati huo msumali ulikuwa dede na umetuna ,Mama Rania aliinama na kupandisha kile kijisketi juu kabisa na kumwachia Peter kazi na Peter mwenyewe hakuzubaa maana akili yake hapo ilikuwa haifanyi kazi vizuri , aliingiza mtwangio wake na kumfanya mama wa watu apanue mdomo na kukugugumia kwa utamu kama wote.
Baada ya nusu saa mbele Peter alionekana fahamu kumrudia huku Mama Rania akiwa hana nguo hata moja na Peter nae alivaa bukta lake haraka haraka na kuangalia pembeni kwani alianza kujutia kwa kile alichofnya , kwani aliona kabisa ashakwisha lala na mke wa mtu.
Kwa Mama Rania wala hakuwa hata na wasiwasi , tena tabasamu lilionekana likipamba uso wake , kwake kufika kileleni lilikuwa ni historia ya muda mrefu na histora hio ndio imejirudia siku hio akiwa na kijana mdogo Peter , alitambua wasiwasi aliokuwa nao Peter hivyo aliamua kumsogelea na kisha alimkumbatia huku akimwagia sifa kedekede .
Naam ! Liwalo na liwe .
****
Samiri aliendesha gari lake kwa haraka kubwa ili kuwahi sehemu ambayo amepanga kuonana na bwana Krispine ambae ni mfanya kazi wa kampuni ya kutafuta watu ijulikanayo kwa jina la “POPOTE TUNAFIKA” , alitumia muda wa saa limoja tu kutoka mjini Posta mpaka Ubungo Landmark Hotel , sehemu ambayo ndio alipo panga kukutana na bwana huyo .
“Za Siku Nyingi Boss” Alisalimia kijana mdogo kabisa alie valia suti yake safi kwa heshima kabisa , huku akiweka mkoba wake pembeni .
“ Salama kabisa namshukuru mwenyezi Mungu kwa kila hali”
“Nimechelewa kidogo kulikamilisha zoezi hili, kutokana na kwamba sikua na muongozo wowote katika kumtafuta ila nashukuru nimefanikiwa kumpata .
“Niambie anapatikana wapi?” Aliuliza Samir kwa shauku kubwa ya kutaka kujua sehemu ambayo anapatikana
“Kwa majina anaitwa Irene mshana ni mwenyeji wa mji wa Arusha sehemiu alipozaliwa:”Alipozi kidogo huku akifungua makaratasi yalio kuwa kwenye begi lake hilo .
“Alihamia jijini Dar kwa ajili ya kutafuta maisha baada ya mama yake kufariki kwa ugonjwa wa maralia , kuhusu taarifa za baba yake na ndugu kwa ujumla sijazipata .
Hapa jijini alikuwa akiishi maeneo ya Sinza mpaka alipo jifungua mtoto wa kiume ndipo alipo hama , na taarifa kwa sehemu alipo hamia hazijafahamika kwa undani Zaidi ,lakini nimefahamu kuwa alijifungua mtoto wa kiume lakini jambo la kusikitisha ni kwamba kwa utafutaji wa kampuni tumeweza kugundua kuwa mwanamama huyu alipoteza maisha yeye pamoja na mwanae.”
Samir alijikuta kwenye mshangao mkubwa sana na maumivu makali baada ya kusikia kuwa wote wawili walipoteza maisha hapo hapo .
“ Samir alijikuta akinyong`onyea baada ya taarifa hio kwani ilikuwa ni taarifa ambayo ilisikitisha mno mbali na mategemeo yake , hasa alipo sikia kuwa mwamke yule alijifungua mtoto wa kiume ambae anamtafuta usiku na mchana ili kuja kumrithisha mali zake kwani hakuwa na uhakika na maamuzi ya mali zake kuzirithisha kwa wanae wa kike .
“Ni hayo tu mheshimiwa na kama kuna jipya nitakalo libaini basi nitakuambia mapema iwezekenzvyo “ Aliongea bwana yule na kisha akapeana mkono na Samir na kisha kuondoka .
Alikaa chini na kujifikiria kwa muda huku akihuzunika kwa uzembe wake ,lakini mwishowe alikubaliana na hali halisi kwa kuona kwamba hayo yote yalikuwa mapenzi ya Allah.
Alijkuta akitoa simu yake na kumpigia tajiri Hemedi rafiki yake
“Una baraka zangu zote, nipo tayari kukupa mtoto wangu umuoe ila kwa masharti makuu mawili la kwanza ubadili tabia yako , kwani sipo tayri kumuona mwanangu akilia kwa kuumizwa na tabia yako ,na pili najua wewe ni mtu mwenye mtandao mkubwa sana kwa hio naomba umpoteze kijana Peter kwenye uso wa hii Tanzania maana sitaki kumuona akihusika na familia yangu “ Alisema maneno hayo Samir na kisha akaagiza chupa ya bia na kuanza kunywa hapo hapo hotelini na alipanga siku hio alewe chakari kutoa mawazo.
Wahenga wanasema”Majuto ni mjukuu” na “usiloijua ni kama usiku wa kiza kinene .
SEHEMU YA 21
Peter aliekuwa amegeuka upande wa dirishani alikuwa akiona hata aibu ya kumwangalia mama huyo , kwani kitendo walicho kifanya muda mfupi ulio pita kilikkuwa ni kitendo ambacho alikiona kama ushetani au dhambi kubwa sana japo hakuwa na dini , ila aliamini kuwepo kwa Mungu mhukumu wa watu wenye dhambi na yeye aliona kuwa amefanya dhambi kulaa na mke wa mtu, ilishangaza kwa yeye kujutia kwani moja ya malengo yake katika kisasi chake ni kutembea na familia nzima ya Samiri .
Peter aliitoa mikono ya Mama Rania na kisha kumgeukia na hapo ndipo alipo kosea kwani ile anageuka tu Mama Rania alikuwa tayari ashapeleka mdomo wake na kuanza kumyonya midomo , Peter aliannza kuleta ugumu lakini aliposhikwa dunguso yake na mikono milaini ya mama huyo alijikuta akinywea kama maji kwenye mtungi na kumuacha afanye kile anacho taka , mchezo uliendelea kwani walisogea mpaka kitandani na Peter kusukummwa kitandani na boss wake Shani au Mama Rania na kisha akamvua bukta na kutupa kwenye kona ,Mama huyu alishika kirungu na kuanza kuchezea jambo ambalo lilimfanya Peter awehuke kwani kitu anacho fanyiwa kilikuwa ni cha levo ya ktabu cha ‘Super Erotic Romance’ mama alikuwa akijua mambo kwani yeye alikuwa tayari ameolewa ukiachana na historia ya nyuma ya maisha yake kabla ya ndoa ,alijua mbinu jinsi ya kumpoteza mwanaume yeyote yule kwenye dunia ya mapenzi, Peter hakufurukuta kwani alikuwa kwenye sayari nyingine kabisa , sayari ambayo hakuna mtaalamu yoyote wa mambo ya anga amefanikiwa kuiona kwa Darubini .
“Liwalo na liwe” Aliongea Peter na kumshika Shani na kumgeuza hata Shani mwenyewe alishangaa kitendo hicho cha Peter kumgeuza kwanguvu kama mbogo . alimkunja kama kambale na kuingiza mtwagio wake maana ulikuwa mkubwa wa haja na kwakuwa Mama Rania katika kujifungua kwake kote ilikuwa ni kwa njia ya upasuaji basi eneo lake lilikuwa kama la binti mdogo .
Peter alimpelekea moto mama huyu Rwanda magere anaziiita Bakora za kimkakati , haikujulikana hata ujuzi alikuwa ameutolea (hivi vitu tunazaliwa navyo ni asili ) ,Mama Rania au ukipenda muite Shani alikunjwa na kukunjuliwa na kunyoooshwa na kupinduliwa , akafika kitonga akashuka akapanda tena akashuka akapanda tena na kushuka tena na kujikuta akiweka historia ya kuukwea na kuupanda mlima kitonga kwa mara kibao.
“Asante sana mpenzi , yaani hata siamini nikajua unajuwa kuchezesha vidole kwenye komputa tu kumbe hata kwenye mwili wa mtu uko vizuri ,umenifanyia kitu ambacho sitakaa chini na kuukosa uhondo huu “ Alijidekeza kabisa huku akitoa sifa zote kwa Peter huku akisahau kabisa mkononi ana pete ya ndoa .
Basi ukawa mwanzo na mwendelezo wa kupanda vilima na kushuka , siku tatu zote walizo kuwa katika jiji hilo la Lushoto kwaminajiri ya kufungua benki katika wilaya hilo uliambatana na ufunguzi wa mapenzi yao yasio na kibali mbele za Mwenyezi Mungu, walitembea kwenye vivutio vyote vya utalii vilivyopo ndani ya wilaya hio , huku kila siku wakirudi kupeana dudu , hata chumba alicho chukua Peter ilibidi akirudishe tu kwani alikuwa hakitumii tena, ilikuwa ni mwendo wa kupeana dudu tu , kiufupi sio Mama Rania sio Peter wote walinogewa , Peter alinogewa na vitu alivyo kuwa akipewa na mama huyo na Mama Rania na yeye alijikuta hata akimdharau mume wake kabisa na kuona sasa wako droo.
“Peter mpenzi wangu nakupenda sana , yaani natamani ungekuwa wewe ndio mume wangu “ Aliongea huyu kwa mapozi kabisa ukidhania ni binti wa miaka therathini au ishirini na hajawahi kuzaa kumbe ana mitoto tena mikubwa na mizuri kabisa ambayo ipo kwenye lika la kuolewa na kuwa na familia kama kijana Peter. .
“Nakupenda pia mpenzi , siku zote sikujua kumbe hii sehemu inanoga kiasi hiki” Huku akimshika na wakati huo walikuwa kwenye gari kuelekea hotelini wakitokea eneo moja linaitwa Mkuzi huko kwenye vivutio vya utalii , na mama Rania hakuwa hata na wasiwasi yaani alikuwa akijiona dunia nyingine kabisa na alitamani kabisa kutorudi nyumbni ,wakae tu huko hata mwezi mzima , na kwa Peter alikuwa amenogewa na yeye alitamani alekitumbua tu kwani utamu aliokuwa akihisi wakati akichovya kibuyu hicho cha asali haukuwa wakawaida laiti angejua kuwa mwanamke ambae ana mkunja kila siku na kumkunjua na kuonesha ubabe wake ni mwanamke alie husika na mauaji ya mama yake sijui angefanya nini na kwa Mama Rania na yeye laiti angejua kuwa mwanaume huyo alio kuwepo hapo ndio mtoto aliotoa maagizo kwa ajili ya kuuliwa na pia ni mtoto wa mume wake na kaka wa wanae sijui ingekuwaje .
“Vipi nikununulie ndizi naona zimeiva na zinavutia “ Aliongea Peter baada ya kufika eneo moja liitwalo Magamba .
“Ndio nunua “ Alijibu Mama Rania huku akijilaza kwenye kiti.
“Peter alitoa wallet yake kutoa hela kwa ajili ya kulipa , lakini ile anachomoa hela kulidondoka kitu kutoka kwenye waleti yake alinunua kwanza zile ndizi na kisha na kuziweka mbele na kisha aliinama na kuokota , alijikuta macho yakimtoka na hapo hapo akakumbuka siku ambayo Rania alimletea waleti yake .
****
Rania tokea Peter aondoke alijikuta kwenye wakati mgumu sana , kwani kila akikumbka tukiio la Peter kumbusu kwenye paji la uso mwili wote ulikuwa ukimsisimka , kila saa alikuwa akiangalia kidani cha holder ya funguo alicho pewa na Peter , huku akikumbuka maneno yake kuwa huo ni kama ushahidi wa wao kuwa marafiki, alijikuta akitabasamu usiku huo , huku akijiviringisha kwenye kitanda .
“Lakini yupo kimya sijui ujumbe wangu hakuupata?? “ Alijiongesha mwenyewe huku akionekana kabisa kuna ujumbe alimtumia Peter haikujulikana kamtumia kwa njia gani ila alionekan kabisa kuna ujumbe ambao alikuwa amemtumia Peter na alikuwa akisubiria majibu.
“Sis....” Ilisikika sauti ikiit na kumfnya Rania alie lala kugeuka na kuangalia mlangoni.
“Waoh!, Nasma.. karibu sana, leo umekuja kutusalimia jamani nimekumisije mdogo wangu” Kumbe alikuwa ni Nasma.
“Nimekumiss pia mrembo , leo nimekuja kabisa kulala na ndio maana unaniona usiku”
“That is great , karibu sana mdogo wangu yaani ungejua nilivyo kumiss wewe acha tu , sema majukumu ndio yananibana nimeshindwa kuja kukusalimia huko nyumbni kwako”
“Mewe muongo , ila nafurahi nimekuona , unazidi kuwa mzuri tu dada yangu”
“Ahahaha jamanii.. wakati wewe ndio mzuri katika familia yetu kuliko wote”
“Ahaha.. sio kweli wote tunalingana” Aliongea Nasma huku wakionekana kufurahia kuonana, kwani japo walikuwa wakiishi kwenye jiji moja lakini ni mara achache sana kwa wao kuonana ,Nasma yeye alikuwa kiishi sehemu yake , kutokana na kwamba yeye haelewani kabisa na baba,Nasma hakupenda ukoloni wa baba yake.
“Jamani chakula atayari , dada Najma anawasubiri”Aliongea mfanya kazi wa ndani akiwakaribisha kwenda kula achakula cha usiku.
“Najma mambo!” Alisalimia Nasma baada ya kumkuta pacha wake kwenye meza akiwasubiri maana ndio ulikuwa utaratibu lazima kuwasubiri watu wote wafike kwenye meza ndipo uanze kujipakulia na kama sio sheria hio Najma angekuwa ashajipakulia mapema mno..
“Safi nakuona karibu” Aliongea Najma kwa kujilazimisha .
“Hata mimi nakuona tokea miaka mingi tulipo achana tokea uende masomoni umebadilika na umezizi kuwa mzuri “
“Ndio ila najua si kushidi wewe” Aliongea najma huku akijipakulia chakula
“Halafu jamani baba siku hizi anachelwa “
“Nani anachelewa ?: , mimi hapa nimerudi “ Ilisikika sauti kutoka mlangoni na Samir alionekana akiingia huku amelewa chakali huku akiyumba yumba na kuwasogelea wanae .
“Watoto wangu warembooo.. naonaaa… leo mmekusanyika kunijadili .. mimi baba yenu , ..hiki kikao chenu tukipe jina gani vilee.. eti Nasma mtukutu ... aa... mimi nakiita kikao cha masimango”Aliongea Samir kilevi na kumfanya najma aamke na kumkalisha baba yake kwenye kiti .
“Dadii.. mbona uko hivi leo jamanii “.
“Nilikuwa nasherehekea”Aliongea
“Ulikuwa unasherehekea nini ?”
“Najma msaidieni baba aende chumbni kwake acha kumuuliza maswali”Aliongea Rania
“Nilikuwa nasherehekea kupatikana kwa mchumba wa Rania “Aliongea kilevi na kumfanya Rania ashituke na kumwangali baba yake huku Nasma na Najma wakimsadia baba yao apande ngazi kueekea juu chumbani
“Hii tabia ya baba kulewa kaanza lini Najma?”Aliuliza Nasma
“Mimi hata najua sasa , ila kaanza wiki ya tatu hii na leo kawahi “
Nasma ndio alikuwa kulwa na Najma alikuwa doto.
Basi walirudi na kuanza kupiga stori , huku Rania akiwahadithia kuwa yupo mbioni kupata mchumba jambo aambalo wadogo zake walishangaa huku wakitabasamu .
“Anaitwa nani huyo ?”
“Anaitwa Peter”Alijibu bila hata ya wasiwasi
“ Jamanii ..natamani kumuona , kwa hio mshaanza kuwa na mahusiano au ni mapenzi ya mtu mmoja “ Aliuliza Nasma
“ Bado ila naamini ana nipenda maana ashanipa zawadi na kasema yeye ni tofauti na wanaume waliopita , kasema hayuko tayari kuniacha”
“wow ! jamanii.., am so so happy for you sis..”Aliongea Nasma
“Na wewe Nasma vipi ?”
“ Yes , yes .. me too” Alijibu huku akijifumba uso kwa mikono na kumfanya Rania acheke na Najma kumwangalia huku akilazimisha tabasamu .
“Haha what ! ,So all of us we are in love , how if we arrange a day kukutanishana sisi wote na wapenzi wetu au mnaonaje? Aliongea Rania
“Kwa hio hata Najma ana mpezi tayari ?”
Hapo ndipo alipo haribu kwani Najma aliondoka bila ya kusema kitu na kukimbilia ndani kwake , alifika na kujikuta akianza kulia kilio cha kwikwi.
“Uko wapi , mbona sikuoni , mbon aunaufanya mtima wangu kuwa katika maumivu kwa kiasi hiki , nakupenda njoo unitoe kwenye haya haya mawingu ya sintofahamu” Aliongea Najma kwa hisia huku akitoa machozi laiti angejua mwanaume anae mlilia ni kaka yake angeacha mara moja, lakini ndo hivyo kosa si lake kupenda kosa linaanzia kwa baba kumtelekeza mwanamke huku ilihali akijua ni damu yake , sasa watoto wanakuja kumpenda mwanaume huyo huyo ,huku mama nae akinogewa na mwaname huyo huyo
“Wanaume wajibikeni na matendo yenu madhara yake yanakuja kuwa makubwa sana na ni kama haya yanayo onekana kwa familia hi ” Maneno ya mwandishi yanywe au yateme
“Halafu mbona na wewe umenuna ghafla “ Aliuliza Rania .
“Sijakutana na mpenzi wangu bado , kwani tumekutana mara moja tu na jina simjui” Aliongea Nasma nakumfanya na yeye kushangaa
“Mhmh! basi wewe na Najma mko sawa “
“Una maanisha nini dada ?”
“ Namaanisha na yeye amependa mwanaume ambae hamjui”
Nasma na yeye alishangaa huku akimuelewa pacha wake ni maumivu kiasi gani aliokuwa akipitia kwani alikuwa akijua ni jinsi gani inauma kumpenda mtu ambae bado haujamfahamu vizuri na huna namna ya kuonana huku ukisubiria bahati ya Mungu kuwakutanisha tena ..
****
Peter alijikuta akichukua ile picha na kuigeuza nyuma na kuona maneno yameandikwa , Mama Rania alikuwa akimuangalia hivyo aliamua kuweka ile picha kwenye waleti na kisha akaendela na safari .
walifika ndani na kisha waliagiza chakula na kuanza kula na kumaliza na kisha wakaanza kuangaliia movie huku wakiwa wamekaa kwenye pozi la kimahaba kabisa , hakuna hata mmoja alie kuwa na wasiwasi.
“Nikifika nataka kukununulia nyumba kubwa mpenzi”
“Unasema kweli?”
“Ndio natamani hata ya kuishi na wewe , ila nina mume nitakununulia nyumba na nitakuwa nakuja mara kwa mara kufurahia penzi letu”
“Asante mpenzi nakupenda sana”Huku wakianza kunyonyana na hata ile muvi ikaachwa kuangaliwa na kuanza kunyanduana na kijana huyu ambae kusudi la kwendca kufanya kazi kwenye benki anayosimamia mwanamama huyu ni kwa sabababu alitaka kulipiza kisasi kwa Samiri kwa kitendo cha kumdharau , na katka kisasi chake hicho alikuwa amedhamiria kulala na wanae wote ,lakini sasa anamkula mama mtu huku watoto wa mama huyu wakiliwazia penzi la Peter yaani kisasi kinajilipa chenyewe .
Kwa yaliokuwa yanafanywa na wawili hawa pamoja na historia zao ilikuwa ni jambo la kutisha kweli kweli ,Mama Rania hakumuona tena Peter kama mtoto , tena mtu ambae alikuwa anapaswa kutembea na mwanae Rania , alimuona kama mwanaume Tena mwanaume wa kukidhi haja zake zote .
Baada ya kumaliza kufanya waliokuwa wanafanya mambo ambayo \mnele za Mungu hayakuwa na kibali , Mama Rania alipotelea usingizini , na Peter alitumia wasaa huo kuangalia kile alichokuwa na hamu ya kuona muda wote
Ilikuwa ni picha ya mrembo Rania picha ambayo ilikuwa imekatwa kipande na kufanywa kama passport , huku ikimuonesha kimwana huyo kupendeza kweli kwa tabasamu lililopamba uso wake ,Aliangalia kwa sekunde kadhaa picha hio na kisha aliigeuza nyuma na kusoma vimaandishi vidogo vilivyoandikwa . “Najua ni kipindi kifupi nimekufahamu ila umekuwa na mchango mkubwa sana kwenye furaha yangu na umenitoa kwenye kiza kinene sana juu ya mtazamo wangu kuhusu wanaume nimegundua kuwa wewe ni mwanaume wa kipekee sana , na mwanume ambae ninaweza kuishi nae , nimetokea kukupenda sana Peter nipo tayari kuwa mpenzi wako naomba unikubalie na usinione mimi kama maaya ni hisia zangu juu yako nitasubiri jibu lako ni mimi rania nakupenda sana peter naomba unifikire na unipe jibu linalotoka ndani ya moyo wako sitaki kuumia tena”
Peter alijikuta jasho likimtoka huku akiwa haamini kwa kile anacho kisoma , kwa upande wake ilikuwa ni jambo ambalo angeshangilia kwani ni kitu alicho kuwa akikitaka kwa mrembo huyo kutoa bikra tu na kuondoka zake kwani aaatakuwa kashalipa kisasi , ila maneno yale yalimfanya apatwe kutokana na kwamba japo maandihi yale yalikuwa machache lakini aligundua kuwa yalikuwa yamebeba hisiaa nzito mno .
SEHEMU YA 22
“Nadhani ni wakati wa kutafuta mrithi wangu sasa nishachoka kuongoza kampuni nataka nibakie kwenye bodi tu ya kampuni” Aliongea Profesa Gladness.
“Sasa profesa utamwachia nani kampuni , wakati hakuna mtu ambae anafikia hata nusu yako”
“Mary ukiona natamka haya maneno jua nishapata mtu wa kukalia kiti changu”
“Ni yule mtu anae husishwa na viumbe kutoka sayari nyingine au kuna mwingine?”
“Kuhusu hilo nitaliweka wazi hivi karibuni haina haja ya kuwahi kuwaambia” Aliongea profesa Gladness bila ya kumtajia jina Mary kwani alikuwa ni shushu na hapo alikuwa yupo kiuchunguzi Zaidi kwa kile kilicho kuwa kinaendelea .Na uzuri wa profesa Gladness hakuwa akimuani mtu , na hio ndio slogani yake..
“Boss kuna wageni wako wamekuja kukutembelea “ Aliongea Mary na kumruhusu awaingize.
“ Haa…!! Mom .., dadii” Aliongea Gladness na kuwakumbatia wazazi wake ambao alikuwa ni Rafaeli na Nifani
“Mmerudi lini nchini ?”
“Ndio tumeingia leo hii nchini ,tumepitia KIA”
Gladness alifurahi sana kukutana na familia yake hio , kwani ni kipindi kirefu kidogo tokea wasafiri , kwani walikuwa wakila bata tu , na kutembelea nchi mbali mbali .
Basi familia hio walitoka na kwenda nyumbani kwa gladness sehemu ilo kuwa ikijulikana kama kijiji cha maroboti au Village G.
“UNAITWA RAFAELI MSWAKI UNAMIAKA 65 ,UFANYAJI KAZI WA TEZI YA MAFUTA MWILINI IMEPUNGUA KUFIKIA NUSU YA UZALISHAJI WAKE , PRESHA YAKO NI 137/88mmhg …, NGOZI ISHAANZA KUKUNJAMANA , UWEZO WA KUFANYA MAPENZI UMEPUNGUA KUFIKIA ROBO TATU,KWA MAKADIRIO UMEBAKISHA MIAKA SI CHINI YA KUMI KAMILI UTAKUWA USHAKUFA”
Ni baada ya kuingia tu ndani ya nyumba ya profesa Gladness na roboti lifahamikalo kwa jina la Nimrod lilimscan(skani) Rafeali na kutoa hayo maneno.
“ Nimrod tulia “ Aliongea Gladness na roboti hilo likiondoka zake huku lishaharibu hali ya hewa kwa kiherehera cha kumchunguza kila mgeni anaeingia nyumbani kwa Profesa Gladness.
“Daaa! Wewe mtoto maroboti yako yashaanza kunipa stress” Aliongea Rafeli kwani alikuwa hajui kuwa kabakisha miaka kumi mpaka kufariki kutokana na maneno na uchunguzi wa Nimrodi.
“Hapanna baba kuna muda mwingine yanakosea” Alijitetea gladness huku akimwangalia Rafaeli ambae alionekana kweli ashaanza kuwa mzee kibabu .
“Umesikia mke wangu huko ,nimebakisha miaka kumi tu kufa “
“Mume wangu bwana hayo ni maroboti “
“Kama ni maroboti basi ngja niliiite likuchunguze na wewe na wewe”
“ Hapana .. hapana .. mimi sitaki kujua nitakufa lini”
“Ahaha .. wewe si umesema hayo ni maroboti .. mbona unaogopa sasa”
“Ahahaha..mume wangu wewe anza kukaa na watoto wako vizuri na tumia muda mwingi kuwa nao “
“Ila limenidhalilisha lilivyo sema , siiwezi kazi ya chumbani vizuri .. hii dunia inavyo endelea hivi hatutaweza tunza siri kweli”
“Hahaha .. mume wangu ushakuwa babu tayari bhana “
“Na wewe si bibi kizee”
Hao walikuwa ni Rafeli na Nifani wakiwa nyumbani kwa mtoto wao mkubwa Gladness.
*****
Masumbuko kama kawaida yake alikuwa kapiga zake nne hana habari huku pembeni akiwa na vijifuko vya Ice cream akiwa anakula na kilicho kuwa kikiangaliwa kwenye TV kilikuwa ni filamu za ngono , maana kila siku kwake alikuwa akiangalia kwa dozi
Alikuwa haamini kama kweli hana nguvu za kiume
“Aaa…. Masumbuko vipi tena na hizo video “ Aliongea Peter huku akionekana kushika kijibegi na muda huo alikuwa akionekana kabisa kuwa alikuwa akitoka safarini na ndio anarudi.
“ Zinanitia mzuka na mori mori” Aliongea masumbuko na kumfanya Peter atabasamu .
“Wewe si uneenda tu hapo nje na kumpa mwanamke kumbukumbu ,unamleta humu ndani unafanya yako , kama siku ile “
“Una maanisha kama kubaka vile , si ndio “
“ Nani kakwambia kubaka , pale haulazimishi mtu bhana “
“Yule mshikaji alikuja na akaniambia kuwa kitendo kile ni kubaka “
“Mshikaji gani huyo ambae una mzungumzia ?”
“ Yule wa siku ile , Sebastiani yule”
“ Kwa hio alikuaja hapa nyumbni na ukamfungulia?”
“Ndio alikuwa anagonga mlango kwa nguvu , ndio nikamchungulia na nilivyo muona ni yeye nikajiuliza nifungue au nisifungue ila ndio nikajikuta nishafungua mlango”
“Na alisemaje sasa?”
“Hana tu ndio alinisifia tu kuwa yule mwanamke nilimpa dozi kali ya kumbaka”
Peter ilibidi amuangalie tu Masumbuko na kisha kutabasamu maana aliona kichwa cha ndugu yake huyo wa hiari kilikuwa signal zinasoma na kupotea .
Basi Peter baada ya kuweka vitu vyake vizuri alikaa sebleni huku akionekana kuna jambo linamsumbua kwani aliionekana al kiwa kwenye mawazo , huku masumbuko yeye akiwa hana hata habari .
“Peter haya magorofa marefu ushawahi kuingia?”
“Aliuliza Masumbuko na kumshtua Peter alie kuwa kwenye mawazo .
“ Sikia Masumbuko , utaniuliza baadae sasa hihvi ngoja kuna sehemu naenda maramoja “ aliongea Peter na hapo hapo akatoka hadi nje na hakuchukua gari Zaidi ya kuchukua ufunguo wa honda yake .
“Ngoja na mimi nikazunguke zunguke huko mjini “ Aliongea Masumbuko huku akivaa nguo nyingine na kuchukua buku na kutoka . alitembea mpaka barabarani na kupanda daladala inayoelekea tegeta nyuki kwenda kariakoo “
“ Unaenda wapi?”
“Gari linapo simama “ Alijibu na kuingia ,muonekano wa masumbuko ulikuwa umebadilika kwa kiasi kikubwa kwani alianza kunenepa sio kama alivyo anza kuja, kwani alikuwa akionekana amekauka ngozi ,sasa alikuwa amejaa na kifua utadhaniaa alikuwa anapiga chuma bau kwenda gym
****
MAREKANI (USA)
Katika jiji la Calforinia Alionekana profesa Snart akiwa na mwanaume mmoja hivi mwenye muonekano kama wa kiarabu ndani ya hoteli ijulikanao kwa jina la The Royal iliopo katikati kabisa ya jiji hilo .
“Paco , lete habari za misituu ya amazon .“
“ Mkuu kwanza nafurahi sana kwa kunipa ofa ya kutembelea jiji hili , unajua kutokana na kazi yangu nakuaga sina hata muda wa kufika huku ,kwani hata hali yake ya hewa sio nzuri kama ya kule msituni “
“ Yeah paco upo ndani ya jiji lenye makazi ya watu wengi na shughuli nyingi lazima hali ya hewa iwe tofauti na ya msituni “
“ Yea ni kweli “
“Uliniambia una taarifa muhimu kuhusu Queen ya kuniambia?”
“ Ndio kwanza yuko wapi kwa sasa nataka kumuona kabla sijakueleza taarifa yenyewe “
“Paco , Paco , Queen wa sasa ni mtu maarufu sana na hata nikiuonesha saivi sijui kama utamtambua kama ulivyo kuwa unamuona kule msituni , sasa hivi ni Zaidi ya mrembo “
“ Una maanisha nini kusema hivyo?”
“ Sikia Queen ile ni siraha yangu , yule ni Zaidi ya bomu la nyuklia , kwanza ana akili , hana utu kabisa na pili hajui chochote kuhusu Mungu , na harufu inayo mfurahisha ni kuona damu ya mtu inamwagika muda wote , na pia hana hisia za mapenzi kabisa kama unavyofikiria ni kwamba hawezi kupenda mwanaume yeyote yule , kwani yule muundo wake sio kama wa binadamu wa kawaida , yule nimemtengeneza na nilipata hasara kubwa kwa ajili yake lakinni mpango wangu ulifeli”
“ Una maanisha nini ukisema umemtengeneza Sbart?”
“ Yule hajazaliwa kama wewe ulivyo zaliwa na wazazi wako na pia una ndugu, Queen yule hana ndugu wala wazazi , na kwangu Queen ni kama kifaa changu cha kazi , kwani ninapo agiza kinafanya , sasa nadhani hakuna haja ya kumfatilia sana Queen maana kazi yako ulishamaliza ya kumfundisha Queen , sasa wewe niambie hilo jambo ambalo unataka kuniambia “
“ Ni Kwamba Queen kunamuda nilikuwa kama simuelewi, ni kama anajua kumsoma mtu kila anacho kifikiria akimwangalia tu kwenye macho , kwani wakati nikichukua mazoezi nae alikuwa akinipiga mapigo ambayo hata siyaelewi ,kila pigo nililokuwa nikifikiria kumpiga nalo , ni kama tayarri alikuwa ashajua kile ninacho kifikiria na anakuwa tayari ashajua udhaifu wa pigo langu na anakuwa ananichakaza na kipigo kibaya sana”
“Una maanisha nini kusema hivyo bwana Paco?” Aliongea Snart kwani taarifa hio ilikuwa ni mpya kwake .
“ Mkuu Queen ni hatari sana , kwani ana uwezo ambao sio wa kawaida kama binadamu”
Aliongea bwana Paco ambae ndie alikuwa ni master(mkufunzi wa kimapigano) wa Queen wakati alivyo kuwa nchini brazili kwenye msitu wa amazon , ndie alie kuwa akimfundisha Queen kuua , kwani walikuwa wakienda na kukamata watu na kuwanyonga na kuwachinja bila hata huruma ,nakuwaua wanyama wakali sana kama Anaconda joka anae patikana kwenye msitu huo , Chui na Simba na mafunzo hayo Queen aliyaweza kwa muda mfupi tu.
“Nadhani misheni yangu haikufeli(it was not a failed mission) , Queen atakuwa anaficha uwezo wake inanibidi kufanya utafiti upya. “ Aliongea huku akivaa koti lake la kuingilia maabara yake ndani ya kasri lake ndani ya hapo Calfornia alikuwa akiwaza maneno alioongea Paco mara baada ya kukutana nae hotelini . .
****
Masumbuko alikuja kushushwa na gari katika kituo kimoja kilicho kuwa kina fahamika kama muhimbili na hio ni baada ya kuvutiwa na majengo yalio kuwepo katika eneo hilo ,ndio maana alimwambia konda kuwa keshafika anataka kushushwa.
Alianza kutembea huku akishangaa majengo hayo na muda huo ulikuwa ni saa kumi inaenda kama na robo hivi , alinyooshana kinjia flani kinapandisha kwenda juu kwani kulikuwa na kijimlima na kutokezea kwenye barabara mbele huko kwenye mtaa mmoja ujulikanao kwa jina la mindu, alinyoosha na bara bara hiio na kuja kufika sehemu moja kwa mbele yake kulikuwa kukinekana mwendokasi inazunguka na kuna kibao kikubwa kilicho andikwa ‘HOSPITALI YA MUHIMBILI’.
“Mama hivi ni vidude gani?” Aliongea Masumbuko baada ya kufika kwa mama mmoja alie kuwa akiuza koni , sasa Masumbuko aliona vile vya kuwekea koni ndivyo alivyo kuwa akiulizia.
“Ni koni hizi ni miatano tu moja “
“ Hii inatosha alitoa Masumbuko mia nne na kumuonesha yule mama , na hi ni hela alio rudishiwa chenchi kwenye ile buku (elfu moja)ya nauli maana gharama za usafiri ilikuwa ni mia sita na hapo alitoa yote na mama yule ampatia .
“ Kumbe tamu hivi nitakuwa nakutembelea mara kwa mara “
“ Sawa lakini siku nyingine nitakuuzia kwa miatano “
“ Sawa “
Aliongea huku akitemeba huku na huko akishangaa shangaa mpaka inatimia saa kumi na moja na nusu alijikuta amezunguka amezunguka na kurudi pale pale muhimbili , Alipanda gari bila ya kujiuliza ana nauli ,gari alio panda ilikuwa inaenda Masaki na ilikuwa imejaza kweli na Masumbuko aliwekwa mwisho kabisa ya gari kiasi kwamba kwa jiinsi watu walivyo kuwa wamejaa hata konda ingekuwa ni vigumu kwake kupita na kuomba nauli.
“ Hivi ule mtaa tunao kaa unaitwaje?”Alikuwa akijiuliza kwenye gari huku linaondoka maana hakujua ile sehemu jina.
“Ila nitapaona tu halafu nitashuka”
Sasa konda kwakuwa nafasi ilikuwa imebana sana , alikuwakichukua nauli kila unapo shuka.
“Macho ,Macho hio , kuna anaeshuka ?”Aliongea konda na hapo hapo Masumbuko akaropoka kwa sauti nimefika mpaka watu wakamwangalia.
“Njoo sasa umekaa huko nyuma halafu unajua unashukia hapa karibu”
Aliongea konda baada ya gari kusimama huku Masumbuko aliependeza akishuka , kwa jinsi alivyo kuwa amependeza usingedhania kuwa wakati huo hakuwa na kitu chochote mfukoni hata nauli .
“Toa hela , unapoteza muda bwana , unashangaa nini?” Masumbuko alimwangalia yule konda huku akiwaza afanye kama kawaida yake maana alijua nauli hana .
“Usijali nitamlipia” ilisikika sauti moja nyororo na kufanya hata wale walio kuwa kwenye daladala wamwangalie anaeongea , lakini ni kwamba tayari alikuwa ashachelewa maana Masimbuko ashachezesha jicho tayari na kumpachika masaa mawili ya kumbukumbu.
“Aaa.. aa hapana . ashalipa tayari mremboo hata usisumbuke ” Aliongea konda huku akigwaya gwaya na kufanya abiria waanze kucheka na hata dereva mwenyewe alijikuta akicheka na hapo ndipo ikawa gumzo kwenye daladala maana wengi walijua konda alichanganyikiwa na yule mrembo na ndio maana alikubali Masumbuko kashalipa, wengi walimhurumia pasina kujua uwezo Masumbuko. .
“Sema ni haki yake aisee , unajua yule mwanake ni mrembo sijapata ona .. na kwa ile sauti konda ni haki yake kuchanganyikiwa , ila kanifurahisha sana leo
.. hakuna mwanaume mjanja mbele ya utamu “ Aliongea jamaa mmoja lio kuwa amevaa kanzu kasimama kwenye daladala hio alikuwa na rafudhi ya kipemba .
“Nyie mnaongea nini nyie , mimi siwezi kuchanganywa na mwanamke, yule chalii kalipa kabisa nina uhakika.” Aliongea konda na hapo ndipo vicheko vilivyo zidi kabisaa
“Aisee nilikuwa na stress ila zishaisha daah .. aisee” Aliongea jamaa mmoja nae alieshikilia mfuko mdogo hivi uliokuwa na samaki akionekana kufurahishwa sana na hilo tukio.
****
Peter alisimamisha honda yake kwenye nyumba moja maeneo ya makongo juu na kisha akabonyeza kengele na hapo mlinzi alifungua
“Bwana Peter karibu sanaaa..” Aliongea mlinzi alionekana kumfahamu Peter
“Nimemkuta Steve?”
“Ndio yupo hajatoka leo “
Basi Peter alienda moja kwa moja mpaka ndani ya nyumba hio ilikuwa nzuri sana kwa jinsi ilivyojengwa.
“Mwanagu huyo , nona leo umekuja kutusalimia?”
“Ndio mama shikamoo “
Huku wakisalimiana kwa furaha na huyo mama aliononekana kuwa mkarimu kweli , alikuwa mnene kiasi mfupi alievalia dera lililoacha mabega wazi.
“Nimemfata Steve “ Aliongea Peter na kuambiwa kuwa yupo chumbni kwake aende tu.
“ Mzee mwenyewe naona usharudi karibu”
“Yeah mzee , nimerudi, nina mawazo nikona nije kabisa nisikusumbue kwa kukuita magetoni”
“Mawazo gani tena mzee si umetoka safarini?”
“Mambo ya kisasi mzee, naona kama kigumu vile kutekelezeka , unajua nilikuwa nachukulia simple sana ila sasa na uona ugumu wake”
“Ugumu gani sasa wewe si ulikuwa wajisifia kuwa unaswaga nyingi kibao , tantalila nyingii sasa umepigwa kibuti ndio unaona ugumu “
“Si hivyo ndugu yangu , simaanishi hvyo yaani bora hata ningepigwa hiko kibuti , lakini sasa hivi nishamla mke wa Samir tayari na mtoto wake kanambia ananipenda na anasubiria jjibu langu”
“ Unasema ushakula kitumbua cha lile limama tayari na lile lishepu “ Aliongea Steve kama haamini vile kwani aliona kama masihala vile , kwa maneno alio kuwa akizungumza . na wakati wanaongea ndio hapo , simu ya Peter ilitoa mlio kuwa ilikuwa inaita .
“ Oya huyu hapa anapiga kama huamini ngoja niweke loud speaker” Aliongea huku akipokea na kuweka loudspeaker .
SEHEMU YA 23
Peter aliweka simu ile kwenye loudspeaker baada tu ya kupokea na kuanza kuongea na Mama Rania.
“Vipi mpenzi mbona unachelewa kupokea simu?” Ilisikika sauti iliokuwa ikilalama na kumfanya Steve kutoa jicho kama kabanwa na mlango kwani hakuamini kabisa kile anacho kisikia , na sio kama jambo hilo ni geni kwake kuona kijana kufanywa kiben ten , lakini hadhi na heshima alio kuwa nayo mama huyo ni vitu ambavyo kwake aliona kama ajabu vile.
“Nilikuwa nipo chumbani simu niliacha living room (sebuleni) “ Aliongea uongo Peter.
“ Jamani mpenzi unajua nilivyo kumiss , natamani sana tukutane hata twende mzunguko mmoja “ Aliongea Mama Rania .
Laiti angejua kuwa amewekewa loudspeaker asingeongea hilo neno , Peter hakutaka Steve aendelee kusikiliza , alitoa loudspeaker na kulala kabisa kitandani na kuanza kuongea huku Steve yeye alikuwa amesimama kama mnara akimwangalia rafiki yake , na kuna kitu alikuwa ashakigundua kwa Peter alikuwa ameona dalili zote za rafiki yake kuonogewa , alikuwa mzoefu wa hayo mambo .
“Daah..! unajua ni hatari hio rafiki yangu”
“ Naelewa , ila Steve yaani kila nikiongea na huyu mwanamke dudu inasoma channeli hapo hapo na mawazo yangu yanabadilika”.
“Fanaleki ushanogewa wewe , na hivyo ni mwanamke wako wa kwanza kazi unayo , mimi naogopa tu mume wake akijua sijui atakufanyaje, naogopa sana ukiingia kwenye matatizo”
“Steve ndio maana nipo hapa unipe ushauri wewe ni rafiki yangu naamini utanipa ushauri mzuri”
“Sasa wewe unataka mimi ni kwambie nini na wakati wewe mwenyewe ulisema unaenda kwenye ile benki kwa ajili ya kisasi ,lakini saivi unaonekana umenogewa tayari , mimi nakushauri uache kabisa hio misheni yako , lakini kuhusu huyo Rania na mama yake , kaa chini fikiria , jiulize maamuzi utakayo fikiria na kuamua yatakuwa na madhara gani ukishalijua hilo basi mimi sitoingilia maamuzi yako ,lakini nakupa hint tu , kwamba unacho kifanya sio kizuri na ni hatari sana ,mke wa mtu sumu ndugu yangu”
“Poa mzee mimi nitafikiria cha kufanya , ila asante sana kwa maneno yako , ngoja nirudi home ni muwahi Masumbuko” Aliaga na Steve alimsindikiza mwenzie.
****
Nasma baada ya kukaa siku kama nne nyumbni kwao , hatimae aliamua kuondoka na kurejea sehemu alio kuwa akiishi , japo ya Rania kumbembeleza sana kuhusu kubaki kwani ana ichangamsha familia , lakini hakukubali na mama yake pia alijaribu kumshawishi lakini alisimamia msimamo wake .
Alipanda kwenye gari yake na siku hio alikuwa akiendesha yeye mwenyewe pasipo ya kuwa na Lucy mfanyakazi wake , aliendesha gari lake mpaka kufikia maeneo ya Macho , sasa wakati yuko kakodoa macho barabarani kionyesha umakini katika barabara hio ndipo daladala ilio kuwa ikija upande wake ilisimama mita chache mbele yake , hapo ndipo mapigo yake ya moyo na mshangao kwa ujumla vikamtawala, kwani mwanaume alie kuwa akimuota usiku na mchana alimuona kabisa mbele yake , kwanza aliona kama kamfananisha lakini kadri alivyo sogelea gari lile ndipo alipo kuja kugundua kuwa ni yeye.
Alipita daladala ile na kisha kasimamisha kwa mbele na kutoka haraka haraka huku akiwa kabisa amesahau kufunga hata mlango na kukimbilia sehemu ile , ndipo alipogundua kuwa mwanaume yule hana nauli na alikimbia na kisha kumwambia konda kuwa atamlipia , lakini kilichomshangaza kwa mara ya pili kwani mara ya kwanza jambo kama hilo lilikuwa likitokea tena ,pale konda alipomuambia kuwa ashalipa na wakati kwa masikio yake kabisa alisikia konda huo akimdai Masumbuko nauli , lakini kutokana na hamu yake kubwa ilikuwa ni kumuona Masumbuko aliachana na hilo swala na kisha kumsalimia .
“Mambo!” Alisalimia kwa shauku kubwa Nasma huku akimwangalia Masumbuko ambae wala hakuwa hata na time nae kwani alikuwa bado akishangaa hayo maeneo kana kwamba ataiona nyumba wanayoishi .
“Hivi sista naomba nikuulize , hivi unajua eneo ambalo lina magorofa magorofa machache halafu .. halafuu.. enhee .. kuna shule halafu na barabara .. halafu..nini tenaa.. kwa mbele kabisa kuna kanisa kubwa .. unaijua hio sehemu?”
Aliongea Masumbuko huku akionekana kabisa yuko seriasi na swali lake na kwa Nasma alikuwa akishangaa maana swali lenyewe hajalielewa .
.“Mambo kwanza” Aliendelea kusalimia Nasma kwani kwanza alikuwa ana aibu na hata hapo alikuwa hajui afanye , kwani ni kweli alikuwa akihitaji kuonana na Masumbuko lakini hakuwahi kufikiria siku akionana nae ataanza anza vipi kuongea nae na ndio maana aliendelea kusalimia lakini kwa masumbuko wala hakuwa na habari kichwa chake wakati huo kiliwaza nyumbani tu.
“Ila hapa sio penyewe hapa , sijui patakuwa ni upande gani ule . halafu .. , dada mbona haunijibu sasa “
“Sijakuelewa “
“ Ni kweli huwezi kuelewa maana nina maswali magumu” Huku akiondoka na kumfanya Nasma amwangalie Masumbuko akichapa raba hana hata habari kuwa mtu alie mfuata alikuwa akikesha usiku na mchana kumtafuta na kumuwazia alijikuta chozi likimdondoka bila hata ya kujua .. sasa wakati ameduaa akimwangalia Masumbuko ndipo alipo kuja kama kuzinduka na kuita
“Kaka , nisubiri” Masumbukoo alisimama na kumwangalia Nasma anae mkimbila .. na kwa jinsi alivyokuwa akimkimbilia kwa mapozi na uzuri wake na jinsi Masumbuko alivyo kuwa akumwangalia ilikuwa ina pendeza kama vile ni filamu za kihindi.
“Nimepajua hio sehemu ulio kuwa unasema”
“ Kweli … kuna kanisa .. kuna shule kwa nyuma na barabara katikati … si ndio ni hapo”
“Ndio “
Jibu hilo lilimfanya Masumbuko aachie tabasamu na kuufanya uhendsome wake uonekane na kumfanya Nasma amwangalie kama anamshangaa ..
“Twende kwenye gari .. nikupeleke “ Masumbuko hakuleta shida kwani hi ndio jambo ambalo lilikuwa likimpa shida kwa wakati huo na hivyo alimchukulia Nasma kama mtu ambae anaweza kumpatia msaada .
Basi aliingia kwenye gari na safari ikaanza na kwa Nasma kwakuwa alikuwa ana kichwa chepesi sana kuelewa ni kwamba aligundua kuwa Masumbuko yuko , kwenye hali ya wasiwasi na ndio maana hakuwa akimpa ushirikiano .
“Kwa hio kaka ulikuwa umepotea?”
“ Ndio mimi ni mgeni na haya maeneo “ Aliongea Masumbuko huku akiangalia nje ya gari na muda huo kajigiza kalikuwa kashaanza kuingia , na kuna wakati Nasma alikuwa akimwangalia Masumbuko kwenye kioo .. aliishia kutabasamu tu na alionekana moyo wake kuwa na Amani na furaha sana . Kwani aliamini mwanaume alie kuwa akimtafuta hatimae amempata .
“Hapo hapo nimepaona simamisha gari “ Aliongea Msumbuko kwa sauti na kumfanya Nasama asimamishe gari na masumbuko kuomba kufunguliwa mlango , na Nasma alipo mfungulia tu tayari alikuwa ameshatoka tayari kwenye gari .
“ Dada asante sana .. nimepafahamu ni hapa kabisa “ Aliongea Msumbuko na kwa wakati huo walikuwa washafika eneo la Mbezi Beach ilikuwa ni bahati kwa masumbuko kwani isingekuwa Nasma kuishi hayo maeneo asingeweza kurudi nyumbani. .
Masumbuko alindoka huku akisubiria kuvuka barabara na kumfanya Nasma na yeye kutoka kwenye gari na kumfuata Masumbuko kwa nyuma hakutaka kumpoteza tena , lakini kilichomshangaza Nasma ni kwamba nyumba alio ingia Masumbuko ni nyumba ya pili na ya kwake ilipo.
“Yaani kumbe huyu mkaka kumtafuta kote kule kumbe ni jirani yangu “ Aliongea Nasma huku akijikuta akitabasamu tu nakuona kuwa mageti muda mwingine yanakuwa hayasaidii maana yanafanya usijuane na majirani, alikaa kama dakika kama tano akiangalia nyumba hio ilioenda hewani kwa gorofa nne na kisha akatoka akafara gari yake na kwenda hapo mpaka kwenye nyumba yake na kuingia na kisha akampa mlinzi ufunguo akimwambia akachukue gari ameliacha kituoni , mlinzi alishangaa ila alichukua ufunguo kwani hakuruhusiwa kuuliza swali .
***
“Ulikuwa umeenda wapi umenifanya niwe kwenye wakti mgumu kiasi hicho “ Aliongea Peter huku akionekana kuwa na wasiwasi sana .
“ Nilienda kula bata kidogo ndio nimerudi “
“Nikajua umepotea huko njiani . inabidi kesho nikakununulie simu “
“Mimi siwezi kupotea ni mgeni lakini nayajua maeneo vizuri”Aliongea Masumbuko na kumfanya Peter atabasamu na alichogundua alijua kuwa Masumbuko alikuwa akipenda sana kujisifia .
“ Haya lakini usitoke toke tu utapotea au kugongwa na gari huko ndugu yangu , unafikiri nitaishije “
Aliongea na kuachana na Masumbuko kwani alijua pia ni mtu mzima hatakiwa kumlinda ila anatakiwa kumuonyesha mazingira na kumtembeza tembeza ili asipotee.
*****
Siku ilio fuata Peter hakwenda kazini na alibaki nyumbni kwani alikuwa amepewa siku mbili za kubaki nyumbani , kwenye muda wa saa kumi na moja ndio muda ambao Peter alipigiwa simu na Mama Rania kuwa wakutane barabarani kwenye kanisa la KKKT usharika wa Mbezi Beach .
Peter alivaa vizuri na kisha akatoka zake baada ya kumuaga Masumbuko ambae alikuwa akichezea simu ambayo amenunnuliwa asubuhi hio
“Peter aliingia kwenye gari yake , maana Mama Rania alimwambia kuwa aje na gari yake , baada ya kufika tu kweli alimuona Mama Rania aliekuwa amevalia gauni flani lenye mikanda huku akiwa ameshikilia pochi kubwa na alikuwa amependeza kweli ,kwa jjinsi alivyokuwa akionekana utadhani ni mwanmke ambae anaenda dating kwa mara ya kwanza , Peter alienda kufunga beki kwenye miguu ya mama huyo na kufungua kioo na kumfanya Mama Rania atabasamu na kuingia kwenye gari na kisha likaondoshwa na kwa maelekezo ya Mama Rania walikuja kukunja baada ya kufika eneo moja linaitwa jogoo na kuchukua upande wa kulia na gari ilitembea kwa dakika kadhaa na ikasimama nje ya geti kubwa na baada ya dakika kadhaa gari hio iliingizwa ndani ya jumba hilo , hapo ndipo Peter alipo patwa na mshangao kwani jumba hilo lilikuwa moja ya jumba kubwa sana na lilikuwa na mazingira mazuri kwani kulikuwa na swiming pool upande wa kushoto ukiingia ilio zungukwa na bustani na majani yalio chongwa kwa ustadi mkubwa sana , jengo hilo limepakwa rangi ya kuvutia nyeupe lakini ilio fifia na kupendeza sana .
“ Kwanini tuko hapa?” Aliuliza Peter maana alikuwa akiona mapicha picha tu .
“Hii ndio itakuwa nyumba yako mpenzi ‘ Aliongea Mama Rania .
“ Whaat.. usiniambie kuwa umeinunua hii”
“Sijainunua leo wala jana ilikuwa ni yangu ,japo hakuna mwanafamilia anae ijua na sasa nasema nyumba hii ni ya kwako mpenzi wangu na tutakuwa tunakutana hapa unipe vitu” Aliongea Mama Rania na kumfanya Peter moyo upige kwa nguvu kwani hakuamini kuwa jumba hilo ni la kwake alianza kuona faida za kutoka na majimama..
“Mimi bado hata sijasadiki kabisa “ Aliongea Peter na Mama Rania akaachia tabasamua na kumshika mkono Peter na kisha kumvuta na wakaingia ndani .
“Chukua hio bahasha mpenzi ‘ Aliongea Mama Rania na kumfanya Peter aisogelee hio bahasha na kuifungua na ilikuwa ni hati ya nyumba na jina lake ndilo lili kuwa ndani ya hio hati .
“Peter nayafanya haya yote kwaku nakupenda na sitotaka unisaliti , nitakupa chochote utakacho kitaka , ila nakuomba usinisaliti”
Peter hakujibu Zaidi ya kumsogelea mama huyo na kuanza kupigana naye mabusu na kisha wakaanza kazi na kitu alicho pewa Mama Rania siku hio alijikuta kama yuko kwenye dunia nyingine kabisa na hakuwa kwenye ulimwengu halisi .
Walidumu kwa masaa kadhaa na kisha wakarudia tena na tena na tena na kujikuta wakipitiwa na usingizi kabisa tena wakiwa sebleni .
****
Peter alianza kukolea kwenye penzi la Mama Rania au bosi wake , japo walikuwa wakifanya mambo yao kwa siri sana na hakuna mtu hata mmoja ambae aliweza kujua kuwa wawili hao walikuwa wapenzi, kwani walikuwa wakiwekeana heshima feki wakiwa kwenye kazi , lakini wakitoka nje ya kazi walikuwa wapenzi.
Huku kwa Rania nako mambo yalizidi kuwa magumu kwani , kwani alikufa na kuoza kwa Peter , alitamani sana kuwa karibu na Peter kila saa na hata wakati mwingine Mama Rania alianza kuogopa, kwani kwa macho ambayo mwanae alikuwa akimwangalia Peter hayakuwa yakawaida, zilipita kama wiki mbili hivi ndipo Peter na Rania wote waliacha kufika kazini kutokana na chuoni mitihani ilikuwa inakaribia na walitakiwa kujiandaa .
Sasa hapo ndipo ukaribu wa Peter na na Rania kuongezeka kwani walikuwa wakisoma wote chuo kimoja na ilikuwa Rania akitoka mapema kwenye kipindi na Peter akiwa bado hajatoka basi atamsubiri mpaka atoke na waongozane wote , kunywa chai ama kula.
Rania alizidi kumzoea Peter kiasi kwamba kila siku , kila saa na kila sekunde alitamani kumuona Peter tu , kwa upende wa Peter jinsi Rania alivyo kuwa akimuonyeshea mapenzi , basi alizidi kuwa na mawazo juu ya rania , yeye , kila alivyo kuwa karibu ya Rania alijikuta moyo wake kumpenda sana Rania.
Alitamani atamke neno nakupenda ili myo wake utulie lakini hakuweza hilo , kwani kila alipo kumbuka kuwa tayari ana mahusiano na mama yake basi hakutaka kabisa kumuumiza rania huko mbeleni pindi atakapoujua ukweli , kuna muda alikaa chini na kuyafikiria matendo yake aliona kabisa kile kisasi katika kichwa chake kinaanza kusahalulika kabisa , kwani mpango wake ulikuwa ni kumfanya Samir atoe machozi kwakitendo ambachoo alikwisha kumfanyia.
Siku moja wakati Peter anatoka chuo akitembea na rafiki yake Steve , ndipo Rania alipo kuja kumuita na kumwambia kuwa kuna jambo anataka kuongea nae na ni muhimu kwake , basi Peter japo aliogopa kile alicho kuwa anaenda kuambiwa na Rania ila alijikaza na kuondoka na Rania mpaka kwenye gari lake .
“Peter najua kama ujumbe wangu nilio kuandikia uliona?”
“Ndio niliuona Rania “ alijibu Peter huku moyo ukipiga kwa nguvu .
“Peter nataka kujua jibu kwani nimeshindwa tena kusubiria naomba nisikie jibu lako leo”
Aliongea Rania hapo nakumfanya Peter jasho limtoke kwani hapo alikuwa amebanwa sehemu yenyewe .
“Rania najua unanipenda sana na mimi sitaki kukuficha nakupenda sana ila kwasasa sitaki kuanzisha mahusiano maana akili yangu haipo sawa na sijajiandaa kisaikolojia kabisa , na wewe ni mwanamke wa kipekee naomba muda niweke mambo yanguu sawa halafu nitakuambia Rania please, sitaki kuja kukuumiza kwa kutokuwajibika maana mahusiano ni uwajibikaji baina ya wapenzi” Aliongea Peter kwa hisia na ukimtazama hutoamini kama ni yule ambae alikuwa anataka kulipiza kisasi , mapenzi yameyeyusha kila kitu na kilicho baki kwenye moyo wake ni hisia za uhitaji tu , japo alijitahidi sana kutokumpenda Rania lakini ni kwamba alikuwa akijidanganya kwani kadri alivyo kuwa akimfosi atoke kwenye moyo wake ndivyo alivyo kuwa akizidi kumpenda.
“Sawa Peter nitasubiri , ila jua wewe ndio mwanume wangu wa kwanza kukupenda kwa kiasi hiki , nakupenda Peter “ Aliongea Rania mpaka chozi linamtoka mtoto wa kike na kumfanya Peter moyo umuume sana , alijkuta akimkumbatia .
“ Nakupenda Sana Rania , nakupenda sana ila naomba univumilie sawa “ aliongea Peter huku akimwangalia usoni na Rania akakubali kwa kichwa kuwa amekubaliana nae , na Peter alitoka kwenye hilo gari baada ya simu yake kutoa mlio ikionyesha kabisa kuwa inaita na mpigaji alikuwa ni Mama rania. .
Shida moja alio kuwa nayo Peter ni kwamba kila anpo ongea na Mama Rania mwili wake ulikuwa ukimsisimka sana na kuhitaji kufanya ngono .
Peter aliongea na Mama Rania na waliahidiana kuwa wakutane bila kukosa siku hio wakapeane dudu , na Peter hakupindua alikubali , maana kwa wakati huo na yeye alikuwa akipenda sana kitumbua cha mama rania .
****
Upande wa Najma nae mambo yalikuwa mambo kwani kila siku alikua akimfikiria tu mwanaume anae mfahamu kwa sura , japo maswala yake ya kufungua kampuni yake ya urembo yalikuwa yakimfanya kuwa bize sana , ila hakumsahau Peter hata mara moja .
Alikuwa akiamini kuwa lazima atamuona tu , wanaume walimtongoza kila kukicha lakini hakuna aliepewa nafasi hata mmoja hata ya kumshika tu hakuna alie pewa nafasi hio , watu na pesa zao walimchombeza kwa hongo lakini mwandada hakuteteleka , alikuwa akimuwaza Peter .
Upande wa Nasma na yeye alikuwa ashajua Masumbuko anapo kaa lakini kilicho kuwa kikimsumbua ni kwamba alikuwa na aibu na pia hakutaka kujilasisha kwa Masumbuko .
Kuna kipindi alikuwa ni kama mtoto kwani alikuwa akienda mpaka katka geti la Masumbuko kwa ajili ya kugonga lakini aliishia kurudi tu kwani hakukua na sababu ya kumuona Masumbuko na alifikiria kuwa akimuona atamwambiaje kwani alikuwa na aibu sana .
Masumbuko yeye muda wote alikuwa akiwazia ni kwa jinsi gani atakuwa na uwezo wa mnara wake kusoma channel kwani , kwa jinsi alivyo kuwa akijua na uwezo wake wa kufikiria ulipooishia ni kuangalia filamu za ngono tu huku akijifaliji kuwa utaamka tu .
“Utasimama tu “Aliongea huku akiuchezea uume wake
******
“Boss nimegundua Madam anapo elekea “ Ilisikika saiti kwnye simu Samir akiwa ofisini
“ Endelea kumfatilia na kila kinacho endelea utaniambia “
“ Sawa boss “
Samir ni kama kibao kilikuwa kimemgeukia kwani alikuwa hamuelewi kabisa mke wake , kwani hakumsubiri tena kama zamani wakati yeye akichelewa , kwani kila alipo rudi alimkuta mke wake alishapotelea kwenye usingizi mzito na wala hakuwa na habari na hata akiamka , alikuwa haulizi chochote na kilicho kuwa kikimuuma sana Samir ni kwamba hata ile mke wake kuomba gemu aliacha kabisa , na pia mke wake hakuwa hata na mawazo kama mwanzoni na alionekana kuwa mwenye furaha.
Hapo ndipo Samir alipoanza kurudi nyumbni mapema kama zamani , na kurudisha mapenzi kwa mkewe , lakini ni kwamba Mama Rania alionesha hali ya kutokuwa kabisa na time na yeye na mara nyingi usiku alionekana akichat na simu huku akitabasamu jambo ambalo lilianza kumfanya kuwa na wivu na kuona kabisa kuwa mkewe kashapata mchepuko , kila akizifikiria hisia hizo alijikuta akipandwa na wivu mkali sana na kumchoma , alivumilia sana lakini kuna siku alijikuta akikosa uvumilivu na alitaka kujua kile kinacho endelea na aliapia kama atagundua kuna mwanaume anaetoka na mke wake kimapenzi ange muua , swala hilo lilimnyima usingizi kabisa
Siku aliojikuta roho kumuuma na kujihisi kuna ninja anakata kata vipande kwenye tumbo lake ni siku alio omba tendo kwa Mama Rania , kwani ile ana peleka mkono kumshikashika Mama Rania , mkono ulitolewa na Mama Rania akainua kichwa na kumwambia neno moja tu .
“ Naomba usinisumbue nimechoka nina mambo mengi ya kufikiria natakiwa kulala mapema “
Alijikuta akiipandwa ma hasira na kukosa hata hamu ya kulala hapo ndani kwake na alicho kifanya ni kutoka usiku huo huo na kwenda bar .
Na kuanzia siku hio alikuwa akimuinda sana Mama Rania ili apate kujua mwanaume anae toka na mke wake na kwa upande wa Mama Rania alikuwa akiwaza dudu ya kijana Peter tu masaa yote kwani kila akifikiria dudu ya kijana Peter inavyo muingia na utamu anao usikiaga basi mizuka ilikuwa ikimpanda hapo hapo na hata kazi hakuweza kufanya vizuri .
Basi siku ambayo Mama Rania alipanga kukutana na Peter muda wa saa tisa , ndio muda ambao kijana wa boss Samir alikuwa akimfatilia nyuma kwa siri sana .
SEHEMU YA 24
Mama rania wala hakuwa na wasiwasi wakufatiliwa kwani aliendesha gari yake kuelekea upande wa Tegeta ambako ndio kulikuwa na nyumba ambayo amemnunulia Peter kama zawaidi ya kupewa dudu.
Lakini pasipo kujua kuwa kuna mtu anamfatilia nyuma aliendesha gari yake na kwa wakati huo ndio alikuwa anapita mwenge huku kijana aliepewa kazi na Samir alihakikisha kuwa hampotezi kabisa mama huyo kwani alielewa nini maana ya kile kitakacho tokea kama tu atakuja kumpoteza kwene macho yake na ndio maana alikuwa akiendesha karibu kabisa na gari ya Mama Rania na hakutaka kuipita , kwani ilivyo kuwa ikipunguza mwendo na yeye alikuwa akipunguza mwendo na huyu alie kuwa akimfatilia alikuwa si mwingine ila ni Kadabra , kijana machachali kabisa kwenye kazi hio ya kufatilia watu , kwani hio ndio kazi yake kubwa ambayo ilikuwa ikimuweka mjini kazi ya Ubodigadi na kufatilia watu .
Mama rania alipita lugalo yote na kuingia Mbezi Beach huku Kadabra akiwa nyuma , lakini ilipo karibia karibu na kanisa la Mbezi Beach la kilutheri gari ya Mama Rania ilikata kulia na kuelekea upande kama unaelekea shule ya sekondari Mbezi Beach , upande ambao ulikuwa ndio maeneo ambayo Peter na Nasma walikuwa wakikaa, Mama Rania aliendesha gari na kuja kuingia kwenye nyumba ya Peter , na wakati gari ikiingia sehemu hio na Kadabra alikuwa akipita geti hilo kwa mwendo wa taratibu sana huku akikodolea geti hilo macho na kwenda kusimama mbele kabisa na kutoka huku akijifanya anaongea na simu , lakini hakukaa sana gari ya Mama Rania , ilitoka na taratibu na kisha ikachukua njia ya kulekea Tegeta na Kadabra hakutaka kupoteza muda alikimbilia gari yake na kisha kuingia harakaharaka na kuliwasha na kisha kuliungia gari la Mama Rania na uzuri ni kwamba aliliona kabisa na lilikuwa karibu yake , baada ya kufikia eneo la jogoo gari lilikunja kulia na kisha likatembea mita chche kutoka barabara kuu na hatimae likaja kusimama kwenye ile nyumba na Mama Rania na gari ,Kadabra aliishuhudia kabisa ikiingia na hapo ndipo alipo alipo toa simu yake na kumpigia Samir na lilisikika neno moja tu.
“ subiri hapo hapo nina kuja , nataka nikiua unisaidie kutoa hio mizoga”.
Samir alikuwa na hasira kweli na wivu ulikuwa umemkaba kooni ,yaani hata kuhema ilikuwa ni shida kwani kila alipo fikiria swala la mke wake kuwa na mchepuko kiasi cha yeye kudharauliwa ,kilimuuma sana tena Zaidi ya kuuma , kwani hata chakula kila siku alipo kuwa akila kilikuwa hata sio kitamu kwake.
Samir alijikuta akipandwa na hasira mara mbili baada ya kusikia mke wake kaingia kwenye nyumba ambayohaifahamu aliishia kutoa matusi ya nguoni na kisha akachukua bastola yake na kuiweka kiunoni na kisha kutoka hapo na alipishana na secretary wake alie shika mafaili alijaribu kumsimamisha lakini hata sijui alisikia kwa wakati huo kwani akili yake kwa muda huo ilikuwa ikiongozwa na hisia , alipanda gari na kulitoa ofisini hapo kwa spidi ya ajabau mpaka mlinzi akamshangaa bosss wake .
Samiri alitembea na gari isivyo kawaida , na aliishia kutukana tu madereva ambao walikuwa hawataki kumpisha , kuna mdada mmoja alikuwa akiendesha Spacio , yake na Samir alikuwa akimpigia honi kumpisha , lakini mdada huyo wala hakujali , sasa Samiri alipo pata nafasi upande mwingine ya kupita , alimwangalia mdada huyo na huku mdada huyo akimwangalia , na Samir aliishia kumnyooshea kidolea cha kati akimtusi na dada yule aaliishia kusikitika tu.
Baada ya kama dakika ishirini hivi Samir alikuwa ndio anaingia sehemu alio elekezwa na Kadabra
“Ndio Hapa” Aliuliza Samir kwa jazba huku akilisogelea geti ,lakini kadabra alimzuia
“ Boss utawashitua ,sisi tunataka tuone kinacho endelea” Aliongea Kadabra
“Sasa tunafanyaje”
“Ngoja nikuoneshe”
Kadabra aliilisogelea lile geti na kuliangalia na kisha kugonga mlango mdogo kwa stali ya chini kabisa ambayo haileti bughuza na hakutumia kengele , ila yeye aligonga geti hilo na ndani ya dakika moja ndipo walipo sikia komeo likifunguliwa na kajidirisha kadogo kakafunguliwa na akatokea mlinzi.
“Niwasaidie nini?” aliuliza na kumfanya kadabra aangalie upande wa kulia na kushoto na kungalia uwepo wa watu .
“Boss Wangu pale ana shida na wewe .. kuna vitu anataka akuulize” Aliongea Kadabra huku akitoa waleti yake na kumuonesha mlinzi kuwa kazi hio ina malipo .
Mlinzi alivyo ona pesa , hakuzubaa alifungua kageti haraharaka na kisha kutoka ,lakini ni kama kosa kwake kwani ile anafungua tayari Kadabra ashamsogelea kwa staili ya kupiga roba na kumkaba kwa nyuma yule mlinzi na kisha kuingia nae ndani ya geti na kwenda kumtuliza kwenye kibanda chake baada ya kupoteza fahamu na Kadabra , alimwita Samir kwa ishara na hapo Samir akingia na geti likafungwa kabisa na funguo .
Samir mapigo yake yalikuwa yanapiga kwa nguvu kwani katika maisha yake hajawahi kufumania , kwani alikuwa akizisikia tu hizo habari za watu kufumania wake zao lakini hajawahi kukutwa na msala kama huo wa yeye kumfumania mtu tena mke wake , alisogea huku akjihisi kama presha inapanda kwa kiasi kikubwa hasa alipo kuwa akisikia sauti za mahaba kutoka ndani na kwa namna moja alijua kabisa watu hao wako sebleni wanafanya yao .
“Aisiiiii…eeeh… mpenziii… nakupenda… agha…. Nakuja mpenzi ..,. usichomoe mwagia humo humoo .. mpenziii.. aaa…”
Alijikuta roho ikimuuma sana na hasira zikizidi kumjaa na kukosa uvumilivu kabisa , kwani sauti za mahaba alizo sikia tena akisikia kabisa mwagia humoo humo alijikuta presha na roho ya mauji vikimpanda na alikosa kabisa uvumilivu , aalisukuma mlango ambao ulikuwa haujafungwa vizuri na kuingia kama mwanajeshi na kuachia risasii.. akimlenga mwanaume aliekuwa akionekana uchi akishusha kiuno na kupandisha.
“Paa..” Ulikuwa ni mvumo wa risasi uliosikikakwa nguvu
****
Nasma alikuwa amekaa sebleni huku akionekana kuwa kuna jambo ambalo alikuwa akilifikiria na jambo hilo lilikuwa likimhusu Masumbuko , japo tokea waachane siku ile kwenye gari , pasipo kuongea jambo lolote lakini kuna jambo ambalo alikuwa akiliona kwa Masumbuko kama haliko sawa , na muda huo alikuwa akijaribu kuunganisha matukio na kuona kweli kuna kitu kipo kwa Masumbuko na kitu hicho alikuwa akitamani sana kukifahamu .
“Ila mimi ni mjinga sana yaani mtu yuko jirani yangu nasumbuka kichwa changu tu hapa” Aliongea Nasma na kumfanya Lucy aliekuwa kakaa kwenye sofa kwa kujiachia akiangalia tv amwangalie.
“Nini Nasma , unaongea na mimi ?”
“Hapana , kuna sehemu naenda hapo nje nakuja sasa hivi”
“Niagize mimi nitaenda kukuchukulia , hakuna haja ya wewe kwenda”
“Nimetaka kwenda mwenyewe Lucy wee kaa hapo nakuja” Aliongea Nasma na kisha akatoka na kutembea mpaka kwenye geti la nyumba ambayo anaishi Masumbuko , aligonga na kisha alikuja mlinzi na kufungua na kumuuliza maswali na kisha aliruhusiwa kuingia.
“Samahani naulizia floor ambayo anaishi mkaka fulani hivi mweusi rangi ya chocholate” Aliuliza baada ya kuingia ndani hapo na kuwakuta Anjeli na marafiki zake wakipiga stori .
“Mhmh , hapa kuna wengi , lakinii.. hebu nenda namba nne “ Aliongea Angeli huku wote wakimwangalia Nasma kwa uzuri alio kuwa nao.
“Jamani kuna wadada wazuri .. akii..Mungu ningekuwa mimi ningekuwa danga la jiji hili lote” Aliongea Angeli huku akiungwa mkono na marafiki zake
Masumbuko alikuwa amelala fofo kwenye sofa huku Steve ambae alikuja kumsalimia rafiki yake Peter akiwepo akiangalia muvi kwenye laptop yake , na ndio wakati huo ambao Nasma aligonga Mlango na Steve ndio aliesikia na kwenda kufungua,macho yalimtoka na kujikuta akifikicha macho.
“Mambo “ Alisalimia Nasma huku akiweka tabasamu lililomuacha hoi Steve na kujikuta akimwangalia usoni Nasma na mpaka Nasma mwenyewe akaona haya na kuangalia chini.
“ Aaa poa karibu “ Aliongea Steve huku akimwangalia Nasma na alikuwa amesimama tu hapo mlangoni na alijifikiria, ila akaona aingie tu .. alisogeea mpaka kwenye sofa moja refu , kwani hapo ndani kulikuwa na masofa manne na moja lilikuwa karibu na tv na hili lilikuwa ni dogo na dogo lingine lili kuwa upande wa kulia mbali kidogo na Tv na refu kakalia Steve , ila la karibu kabisa ambalo ndilo la kwanza ukiingia hapo ndani kalalia Masumbuko .
Nasma alisogea na alikuwa na wasiwasi sana kwani ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuingia katika vyumba ya wanaume tu , kwani hakuwahi kufanya hapo kabla , alisogea na ndipo alipo muona Masumbiuko aliejinyoosha kwenye sofa akiendesha jenereta kwani alikuwa amepitiwa na usingizi mzito sana .
Nasma alikaa pembeni ya kichwa cha masumbuko kwani alikuwa ameacha nafasi kidogo ambayo ilimuwezesha kukaa , ila wakti anakaa kichwa cha masumbuko kilimgusa kwani mtoto nae alikuwa amejaliwa chungu sio poa.
“Ngoja ni kuletee juisi” Aliongea Steve kwa kubabaika kwani alikuwa ni kama haamini ,kuna muda aliona labda mwanadada huyu alikuwa amepotea njia.
Masumbuko nae muda huo ndio usingizi unaisha na alikuwa akijifikicha macho huku Nasma alikuwa akimwangalia kwa macho yenye mahaba mazito , Masumbuko alianza kunusa kama mbwa maana alisikia harufu nzuri sana kwenye pua zake na wakati anafanya kitendo hicho alikuwa amefumba macho .
“Peter leo sijui kakaribisha jini” Aliongea Msumbuko huku akifungua macho akiangalia juu na hapo ndipo macho yake yakagongana na ya nasma alie kuwa akimwangalia huku akitabasamu na Masumbuko alipo fungua macho alijikuta akishangaa na kumfanya Nasma atoe kicheko.
Na kitendo hicho Steve alikuwa akikishuhudia na aliona kama anangalia sinema VR Gasses (hizi ni miwani ambazo unaweza ukaangalia muvi au kucheza gemu kwa mazingira ya 3D na kukupa hali ya kama unakiona kitu katika mazingira halisi ) ,maana jinsi Nasma alivyo inama na Masumbuko alie kuwa kalala na walivyo kuwa wanaangaliana ilikuwa ni kama sinema la kifilipino .
“Dada juisi hii hapa”
Aliongea Steve na kumfanya Nasma amwangalie na kuachia tabasamu na kisha kusema asante , na kumfanya Steve ahisi sauti hio ilikuwa ipo tumboni ,ikitekenya maini yake.
Masumbuko mara alishtuka maana sijui alifikiria nini na alinyanyuka haraka haraka na kumshika Nasma mkono na kumfanya Nasma amwangalie huku akitabasamu na Masumbuko alimnyanyua Nasma na kumpeleka karibu na mlango wa jikoni ambapo mtu wa sebleni hawezi kuona
“Usije ukasema siku ile tulikutana na nilipotea na wewe ndio ulio nileta maana niliwaambia nalijua sana jiji sasa usije ukaniumbua , yaani kimyaa shiiip” Aliongea akimnong`oneza Nasma na kumfanya Nasma atabasamu na kuhisi msisimko wa ajabu kwani alihisi pumzi ya Masumbuko .
“Hapa leo nadhani kwa mara yangu ya kwanza ndio naangalia tamthiliya la kifilipino laivu bila chenga aliongea Steve baada ya kumuona Masumbuko akimwambia jambo Nasma.
*****
Boss mkuu kapiga simu kuhusu ule mzigo wa Congo “ Aliongea jamaa mmoja mrefu mweusi aliekuwa na mwili ulio jazia na akiwa amevaa miwani .
“ Ramso nadhani wewe unajua nini cha kufanya hapa , na nimeona una majukumu mengi sana, lakini nataka nikupe jukumu lingine na hilo .
“Jukumu gani hilo boss?”
“Nataka kwanzia sasa uwe karibu na Rania kwa kila anacho kifanya kwani muda si mrefu nitakwenda kumuoa”
“Boss una amini atakubali?”
“ Ramso unafikiri ninasema jambo bila mpango , yeye akubali asikubali ila lazima nimuoe kwa namna yoyote ile kwani baba yake tayari yupo hapa kiganjani na hana pakwenda na mama yake na yeye nina udhaifu wake mkubwa sana na nikumuonesha huo tu hatokuwa na la kusema zaidi ya kunipa baraka zote.”
Aliongea Hemedi akiwa nyumbani kwake eneo la Mapinga Bagamoyo na ndani ya jumba hilo ilikuwa ni kama ikulu kwani walionekana mabodigadi wengi walio valia suti safi wakiwa wana hakikisha ulinzi na haikueleweka walikuwa ndio wanamlinda huyo Hemedi au kuna la ziada kwani kama tujuavyo Hemedi ni mfanya biashara wa mabasi .
“Sawa Boss nitalifatilia hilo”
“ Kingine hakikisha huyo panya (Peter ) hafanyi lolote kwa huyo mwanamke , kwani ndio roho yangu na nadhani nikishampata rania roho yangu iatulia na nitatulia nae ,huyu paka kama isingekuwa analindwa na Bosco ningekuwa nishampoteza muda mrefu sana”
“Boss unamaanisha wetu anamfahamu Peter”.
“Ndio ana mfahamu vizuri sana na namheshimu sana Bosco kwani kanifikisha hapa nilipo leo hii, ila asinenipa maelekezo ya kutomgusa Peter ningekuwa nishampoteza muda mwingi sana”
Aliongea Hemedi na kumfanya Ramso ashangae , kwani sio jambo la kawaida kwa tajiri mkubwa kama Bosco kumjua Peter , kwani Bosco alikuwa ni tajri mkubwa ndani ya Congo mwenye mtandao mkubwa wa madawa ya kulevya na alikuwa ni supplier(msambazaji) kwenye nchi nyingi sana ikiwemo Tanzania alikuwa akifahamika kwa jina la The Don.
*****
Ndani ya uwanja wa kimaaifa wa Julius kambarage nyerere (JNIA) , alionekana mrembo Najma akiwa na bodigadi wake akitoka eneo la ‘Arrival’ yaani wanofika, akiwa amependeza kwelikweli na alionekana kabisa alikuwa safarini na ndio anarudi .
“Rehema naomba usinipeleke nyumbni kwanza nataka nikakae Serena mpaka nitakapo kamilisha ufunguzi wa kampuni yangu” Aliongea huku akitembea kimadaha kabisa na kuingia kwenye gari.
Gari ilitembea mpaka kwenye hoteli ya Serena ikitumia masaa machache tu kuingia kwenye hoteli hio ya hadhi ya juu na kisha mrembo huyo akaingia . na kwenda moja kwa moja mpaka mapokezi na kuchukua chumba .
“Leo unaonekana kuwa nafuraha kuliko siku zote nilizo kuzoea”Aliongea Rehema huku akiingiza mizigo ya Najma ndani ya chumba hicho .
“Acha tu nitakwambia kila kitu ila kwa sasa kuna mambo makuu mawili nataka kuyatimiza ndani ya mwezi mmoja .
“Hongera yako ,kama kuna jambo ambalo unataka kulifanikisha pia ni mwanzo wa mafanikio na ni uthamani katika uso wa dunia kwani hauvuti hewa bure , hakuna jambo zuri kuwa na sababu ya kuishi”Aliongea rehema na kisha waliagana kwa ajili ya kukutana siku inayo fuata.
Najma alifungua begi lake nakutoa laptop na kisha akawasha mtandao wa Skype na kisha akabonyeza kwenye hio laptop na likaja jina la A2
“Hello A2 “ Aliongea Najma kwa mapozi . (A2 ni Artificial intelligence roboti ambayo ilitengenezwa na Profesa Gladness , roboti ambayo inafanana kwa kila kitu na binadamu wa kawaida unaweza ukamfahamu roboti A2 kutoka kwenye simulizi ya MY DREAM MY FAVOURITE)
“Hello Beuty Najma .”
“ Nimefurahi sana kuwasiliana na wewe A2 na niliongea na aunt(shangazi) na kaniambia nikuombe msaada unaweza kunisaidia kwenye tatizo langu .
“Ndio alinidokezea na ni kwamba tatizo lako linaweza kufanyiwa kazi kisayansi kutokana na kwamba sasa kuna teknolojia ya kuweza kufanya komputa kutoa picha yoyote ile unayohitaji kutoka katika mawazo yako”
“Naweza kufika lini ili swala langu uweze kulitatua?”
“Kesho asubuhi unaweza ukafika nitakusadia hakika “
Hili ni roboti A2 liliotengenezwa na profesa gladness, na lilikuwa lipo kwenye moja ya kitengo cha usalama wa nchi , kitengo ambacho kilibadilishwa jina kutoka kwenye jina la the Hollic Shadow na kwenda kuitwa jina la AFRICA MULTNATIONAL CYBER SECURITY (AMCS) na kiongozi wa kundi hili alikuwa hajulikani jina lake , kwani kitengo hichi kilikuwa kikifanya kazi zake kwa siri sana na hata wafanyakazi walikuwa hawafahamiki .
UNAWEZA PATA SOFTCOPY YA SIMULIZI HII YOTE.
SIMULZI ZANGU NYINGINE NI
-UMOJA NAMBA TISINI NA SABA
-NDOTO ZA KIKANUNI
-BOOK OF ALL NAMES (UMOJA NAMBA TISINI NA SABA )
-MY DREAM MY FAVOURITES)
KUHUSU UTARATIBU WA MALIPO
WASILIANA NAMI KWA KUGUSA HAPAA
mawasiliano 0687151346
Mtunzi wa huu Uzi ameingia vichakani haonekan tubamaliza karibu wiki Sasa hebu aseme neno tumsSEHEMU YA 18
“Boss mwenyewe unarudi kutoka kazini “ Aliongea Steve baada ya Peter kufika nyumbani na kumkuta rafiki yake .
“Yeah nishakuwa boss saivi nafanya kazi katika kampuni kubwa tena benki hela zinakokaa , lazima unite boss .”
“Yeah , ila unabahati sana , unajua washikaji kila ninae mwambia kuwa unafanya kzi kwenye ile benki hakuna hata mmoja ambae ana niamini “
“ Usiwalazimishe kuamini , vipi lakini mambo yako ya field ?“
“Field iko vyema nimepata kwenye kampuni moja ya Telecom kule Posta ndiko ninako fanyia “
“ Anhaa kumbe tuko upande mmoja “
“Yeah , mrembo Rania na kisasi chako umefikia wapi au ndo unambwela “
“Kisasi kinaenda kiurahisi sana tofauti na nilivyofikiria , yaani si tumii hata nguvu”
“Eii.... wewe jamaa muongo sana , yule Rania ni mgumu wewe utampataje kirahisi hivyo , hebu acha Kamba zako hizo “
“Shida yako husadiki , ila nataka nikirudi kutoka Tanga nikuonyeshe uone kama nadanganya au wewe ndio mwenye ugonjwa wa kuto kuniamini “
“Acha wee waenda tanga kufanyae tena? “
“Naenda kwa ajili ya kazi huko na boss “
“Mhmh! , kweli naona ushaanza kuaminika kiasi hicho mpaka unaenda na boss”
“Sio kuaminika ni kwamba mfumo mpya wa ulinzi bado haueleweki kwa IT wengi kwa hio natakiwa kuurekebisha mimi mwenyewe “
“Halafu yule boss wako ana lishepu hilo , yule nakubali ani bemende “
“Aaaa… mke wa mtu yule na ni kama mama yako yule”
“Ana umama gani , hivi unafikiri yule akikutega upo chumbani nae utachomoka kama wewe ni mwanaume rijali , lazima uingie ndo utajua huyo sio mama yako ni umri tu ila tuyaache hayo”
“ Sema huyu mshikaji wako una mpango gani nae au ndo umemfanya House boy“
“ Masumbuko nina malengo nae nataka nikirudi nimfundishe kusoma na kuhesabu halafu nimtafutie biashara ya kufanya”
“Peter wewe hata usijisumbue kuniletea mwalimu au kutaka kunifundisha kwani sitaelewa kitu” Aliongea masumbuko na kumfanya Peter amwangalie huku akisogea pale kwenye sofa alipo kaa .
“Sikia Masumbuko , sijui alie kuambia kuwa huna uwezo wa kusoma na kuelewa ,ila mimi nina fahamu kabisa kuwa wewe unaweza ukasoma na kuelewa ,sema haujapata mwalimu mzuri kwa hio kuanzia sasa jua wewe una akili na unaweza kusoma na ukaelewa umesikia? “
“Ndio nimekuelewa “ Alijibu Masumbuko kwa heshima kwani hakuwahi kumuona Peter akiwa kwene hali hio ya kuwa siriasi
“Naona mshakuwa ndugu kamili kwa sasa “
“ Yeah , yaani nafurahi sasa hivi nyumbanii kuna mtu ambae naweza kumuongelesha wakati wote , nimechoka kuishi mwenyewe , hivi wewe Steve unajisikiaje unatoka shule unarudi nyumbni huku ukijua kabisa hakuna mtu , na hata pale unapokuwa na tatizo huna mtu wa kusema huyu ni ndugu yangu naweza kumuita au kumpigia simu kumuomba msaada “
“Ndio ni maisha magumu sana kiufupi sipatii hata picha lakini cha kumshukuru Mungu ni kwamba bado kakuweka hai na kukupigania mpaka sasa”
“Ndio , nilikuwa nampenda sana mama yangu na nitaendelea kumpenda daima huko aliko , alinipigania yeye mwenyewe kanikuza kwenye mazingira magumu mpaka alipo patwa na umauti , ila naamini siku moja tu nitakuja kumpata alie husika na ajali ile”
“Peter rafiki yangu kwanini usisahau yote hayo ile ilikuwa ni ajali ya kawaida tu kama polisi walivyo sema , kwanini unataka kuweka visasi moyoni , mimi nikajua ulikwisha sahau”
“ Hapana Steve siwezi kusahau kabisa yaani , na hakuna mtu wa kunishawishi , nakaa kimya tu kutokana na kwamba sitaki kisasi kifute ndoto zangu kwani naamini hata mama hatofurahia kabisa akiniona naishi kwa ajili ya kulipiza kisasi”
“Kwa hio Peter kumbe mama yako alikufa kwa ajali”Aliuliza masumbuko
“ Ndio ni story ndefu Masumbuko sipendi kuikumbuka kabisa “
“Hata mimi mama yangu alikufa kwa ajali “ Aliongea Masumbuko na kumfanya Peter amwangalie kwa maswali .
“Alikufa kwa ajali gani ??”
****
“ Nakuona unavyo mfanya mtoto akolee rafiki yangu “
Aliongea Lea akiwa amejilaza pembeni kwenye viti vya kuegamia huku akiwa ameshikilia kikombe cha pombe (Solo cup) Pembeni yake kushoti akiwepo Sebastiani akiwa amekaa mkao kama wake wote alikuwa wamevaa mavazi ya kuogela huku wakimwangalia Stella alie kuwa katika Swimming pool akiogelea kwa ustadi mkubwa ,alikuwa akizama na kwenda kuibukia mbeleni , kiufupi alikuwa kama kivutio siku hio katika eneo hilo kwani uzuri alio kuwa nao wa maji ya kunde ulikuwa ukivutia sana na shepu ambayo mungu amembariki nayo ilizidi kufanya kuonekana mzuri na hata pale alipo kuwa akiingia na kuibuka kwenye maji alifanya kuonekana kama malaika
“Huyu mwanamke mzuri sana , nimeona wanawake wazuri ila huyu ni kiboko , yaani hata huyu bwana wako namuona fala kumuacha kimwana kama huyu”
“Aacha hizo ujue Sebastian kwani kuwa mzuri ndio kupendwa ,ingekuwa wanawake walio na sura mbaya hawaolewi sasa”.
“Acha wivu wewe.. kiufupi pale haumfikii hata kwa dawa , Stella mzuri na pia ana roho nzuri , na ndio maana anazidi kuwa mzuri , sio kama wewe”
“Sikia seba.. huo utani sitaki , yote nilio yafanya nimefanya kwakuwa nampenda sana James na ningemkosa ningekuwa mwehu , mimi ni tofauti na Stella huoni hata hali yake kwa sasa ni nzuri , mimi nisingeweza roho yangu nyepesi”
“Hahaha.. kwahio ulijuaje kama Stella ataweza .. hio ndio roho mbaya ninayo zungumzia sasa, kujijali mwenyewe pasipo kumjali mwingine”
“Sikia seba utaniudhi sasa hivi , jishaue tu na wakati mimi ndio nakufanya uwe na Stella , fikiria tu siku atakavyojua ulikuwa kwenye mpango wa kumuachanisha na boyfriend wake sijui atakufanya nini”
“Basi yaishe mrembo ee , nilikua natoa ya moyoni , lakini nina furaha maana sasa hivi ninae Stella nahisi Dunia yote yangu , japo hajanikubalia ila naamini atanikubalia tu”.
“Halafu seba hivi utakuwa mzito mpaka lini , wewe unavyo endelea kuamini , utajikuta mtoto sio wako , wewe humuoni alivyokuwa mzuri wewe haya tu zembea”
“Kwa hio wewe nataka nifanyaje , na wakati unaona Stella mwenyewe bado anaonekana ana majonzi sema anajikaza kuonekana yupo sawa”
“Ndio maana nakwambia jitahidi umsahaulishe mtoto huyo na jijengee mazingira akuone mwanaume wa tofauti na wengine , mfanye akuamini “
“Najitahidi sana ”
“Bado.. , sasa sikia Stella jambo ambalo lina muumiza kwa sasa ambalo ni kama udhaifu wake mkubwa ni kumfunga Masumbuko huyo rafiki yako , lakini kumbuka akimpata Masumbuko basi na wewe umekamatika na Stella hatokuamini tena na anaweza akakufunga na wewe, maana anaijua sana sheria na utakuwa umekosa kila kitu na mimi sipo tayari kwa hilo”
“Sasa nifanyaje mbona kama unanitisha , mimi akinikamata nakuunganisha”
“ Huo ndio utakuwa umama sasa , hautokuwa mwanaume wewe inabidi ufikiria namna ya kujitoa kwenye kesi ili hata Masumbuko siku atakayo kamatwa wewe hautahusika moja kwa moja, anza kutengeneza ushahidi wa lile tukio kuwa haukushusika na pia tafuta ushahidi au hata kwa kuutengeneza ili umfanye Masumbuko kuwa na hatia moja kwa moja”
“Seba nimefurahi kweli leo asante kwa kunileta hapa , unajua nilikuwa nasikia Sea breeze ila sikujua kuwa pako vizuri kama hivi” Aliongea Stella na kuwafanya Lea na sebastiani kukanyamaza.
“ Ni kweli Stella yaani pazuri ,tupigeni picha basi” Aliongea lea huku akimsogela Stella aliekuwa akijifuta maji na taulo .
“Seba kaa na Stella basi niwapige picha” Aliongea lea na kuwafanya Stella amwangalie Sebastian na Sebastian alimwangalia Stella na kisha wakatabasamu kwa pamoja na kwa ushawishi wa Lea basi walikubali na kupigwa picha na Stella”
“Nitawatumia hizi” Aliongea Lea huku akitabasamu sana maana zilitoka kama alivyokuwa anataka .
****
Huku nyumbaani kwa Mama Rania alionekana Najma akitoka kwenye chumba chake akipiga miayo akielekea chini kwenye sebule yao na muda huo ilikuwa ni muda wa saa saba mchana .
“Hi! dad good afternoon!” Alisalimia Najma baada ya kumuona baba yake wakati tu alipofika sebuleni wakati huo baba yake alikuwa akiingia na sijui alifata nini maana siku hioo alionekana kuwahi kurudi jambo ambal sio kawaida yake .
“Naona leo umewahi , maana nakuona ukirudi saa sita au saa saba usiku “
“Leo kuna kitu nimerudi kuchukua mara moja na nitarejea baada ya muda kidogo , wewe mbona haujatoka kwenda kwenye mandalizi ya ufunguzi wa kampuni yako”.
“Nimetoa tu maagizo kwa wafanyakazi wangu siku hizi sipendi hata kutoka”
“Unaonekana kuwa na jambo maana si kawaida yako my princess“
“Yeah dadie ni juu ya yule mkaka , I am head over heels for him, please help me to find him dadii please “ (Ninamuwaza yeye tu baba )Akijidekeza kwa baba yake .
“My daughter nafanya kila njia kuhakikisha nina mpata and very soon tu utasikia taarifa ya kufurahisha maana timu yangu ipo uraiani huko inamtafuta “
“Asante sana dad ndio maana nakupenda I real love you dad “ Aliongea Najma maana alikuwa na uzungu mwingi yaani alikuwa hamuogopi baba yake kabisa ,watoto wengi wa kiafrika kumwambia baba ya kuwa wapo kwenye mapenzi ni swala gumu sana na kwao linaonekana kama ni utomvu wa nidhamu , ila kwa maisha ya wenzetu uzunguni huko ni swala la kawaida , pia baadhi ya familia za kiafrika washaathirfika na tamaduni za kizungu .
“Vipi na dada yako , unataka kuolewa kabla yake?”
“Dada naye anaanza kuwa kama mimi tu “ Alingea Najma nakumfanya Samir kumwangalia kwa mshangao , huku wakikaa kwenye masofa ya hapo sebuleni .
“Unamaanisha nini kuwa anaanza kuwa kama wewe?”
“Siku hizi hata si muelewi kuna mkaka nadhani kaanza kazi kwenye benki yetu sasa kila saa dada anamzungumzia mara amsifie na hata wakati mwingine usiku anaota akiongea huku akilitaja jina lake”
“Sasa yeye anakuwaje kama wewe , wewe si mwanaume unaempenda ,wewe ni tofauti na Rania “
“ Hata kama Dady nataka niende hapo kazini kwao nikwamuone huyo mwanume anae mchanganya dada yangu yukoje koje huyo “ Alingea Najma na kumfanya baba yake mapigo kuongezeka maana alijua kama ataenda basi anaenda kukuutana na Peter mwanaume anae mtafuta .
“Sikia unaonaje tukienda wote,mimi na wewe ,ninataka kumuona huyo mwanume kama kweli anamfaa mwanangu Rania maana nawajua wanaume waongo sana “
“Sure dad , nitakuambia siku nikipanga kwenda kumuona ili twende wote “
“Hapana Najma mimi nina kazi nyingi so nitakuambia siku nzuri ya kwenda”
“Sawa dad , but I cant wait , better make it soon dady “
“Worry out my daughter , but promise we do this together right “(Usijali mwanangu lakini hii ni ahadi ua sisi kwenda pamoja )
“Yess dady “
Samir alijikuta akitoka hapo huku akijifuta jasho maana anaona kazi inazidi kuwa ngumu watoto wake wanamchanganya vibaya .
“Nisipo fanya kitu hawa wapuuzi watakutana na inaweza kuleta matatizo kwa wote , inabidi nifanye kitu mapema kabla jambo baya halijatokea ,sina jinsi inabidi Rania aolewe na Hemedi , halafu anisaidie kumwangamiza Peter ili hawa mapacha wanaojifanya wanajua kupenda , nawaletea habari ya kifo tu”Alijiwazia huku akiingia chumbani kwake kwa ajili ya kuchukua kitu kilichomrudisha nyumbani .
SEHEMU YA 19
Samiri alikuwa kweli amedhamiria kumfanya Rania aolewe , aliamini njia ya kumuepusha na Peter ni ndoa .
Hivyo hakuwa na jinsi zaidi kumkubali rafiki yake awe mkwe, sababu hakuwa na cha kupoteza Ramia aolewapo na Hemedi , pia mali zake zingekuwa salama kuliko watoto wake kuwa na mahusiano na kijana Peter .
Alishangaa wakati mwingine ni kwanini alikuwa akimchukia sana Peter na kujithamini wapi chuki hio imetokea mpaka kuwa na nguvu ya kutomtaka kijana huyo kuingia katika maisha ya wanae , lakini hisia zake zilimwambia Peter hakuwa mtu sahihi kwa wanae zaidi ya maslahi na pia hakuamini kama kijana huyo alikuwa na mapenzi ya dhati kwa wanae , lakini pia aliona hatari ilioko kwa kijana huyo kupendwa na familia yake yote .
Siku hio wakati akiwa nyumbani alijihisi kuboreka kubakia hpo kwa muda mrefu ,lakini pia hata ile muwashawasha wa kwenda kutembea uliongezeka mara baada ya kuona meseji ya mchepuko wake Amanda , aliingia bafuni na kujiswafi .
Na kisha akaanza kujiandaa lakini wakati anachukua ufunguo ndio Mama Rannia alikuwa akiingia kutokea kazini.
Mwana mama huyu japo mume wake alikuwa akimnunia ila hakuacha kuonyesha heshima kwa mume .
“Haa ! Mume leo naona umewahi kurudi kazini”
“Ndio kuna kitu nilifuata ila ninaondoka na nitachelewa kurudi”
“Sawa mimi kesho nasafiri kikazi , unaonaje leo ukiwahi kurudi nyumbni mume wangu nimekumisi sana mpaka najisikia vibaya jamani”
Samiri wala hakujibu neno lolote zaidi ya kufungua mlango lakini kutokomea lakini sekunde mbili mlango ulifunguliwa tena na alikuwa ni Samiri , Mama Rania alimwangalia.
“Nimesahau kukutakia safari njema”
Aliongea na kisha alifunga mlango ,mwanamama huyu chozi lilimtoka na kujawa na hudhuni ,hakuamini kabisa mabadiliko ya mumewe kiasi cha kutomjali.
Alikaa kwenye kitanda akifikiria kosa gani amelifanya mpaka hali ya ndoa yake kufikia hatua hio , kuna muda alitamani hata kumfukuza Peter kazini ili hali ya ndoa yake irudi kama awali , lakini akikumbuka kuwa Peter alikuwa tegemezi katika kuimarisha ulinzi wa benki ,wazo alilitupilia mbali , ni zaidi ya mwezi yeye na mume wake kuishi kama dada na kaka
****
Ndani ya hoteli ya Coral Beach alionekana Lea siku hio ndani ya chumba kikubwa cha hadhi ya juu akiwa ameshikiliwa kiuno na James huku akiingiza mwiko wake ndani na kutoa huku kimwana huyo akitoa miliio ya kimahaba ,alionekana dozi anayopewa na james haikuwa ya kawaida .
James alikuwa akimkunja kama kambale na alionekana kubobea kweli kwenye mambo ya sita kwa sira kwani alionekana shughuli kuimudu vizuri takribani dakika kumi na tano walikuwa washamaliza na wote kufika ukingoni.
“Asante sana Hubby “ Aliongea Lea huku akimwangali James usoni aliekuwa akihema kama mbwa alie kimbia maili nyingi “
“Hauna haja ya kushukuru mpenzi wangu mimi hii ndo kazi yangu ya kuhakikisha kwamba nakuridhisha ili usije ukanitoroka ukaenda kwa wengine kwani nitaumia sana mpenzi , nimeumizwa na Stella sitaki kuumizwa na wewe tena”
“Usiwe na wasiwasi mpenzi kwa ninavyokupenda haitokuja itokee eti nakusaliti mpenzi wangu , mimi niwako tu peke yako , unavyo niacha ndivyo unavyo nikuta “
“Hata mimi nakupenda sana Lea na sipo tayari kuuona huu uso wako unatoa machozi kisa mimi kukusaliti , kwanza nataka ukimaliza tu chuo nakuoa”
“Kweli mpenzi , uko siriasi “
“Ndio kwani wewe hautaki kuolewa ,
“Nataka mpenzi ila unajua mapenzi yetu hayana uhuru kwani lazima kila siku tukifanya yetu tujifiche ili Stella asione , natamani kutembea na wewe kila mahali kuonyesha ulimwengu mzima kama napendwa na wewe james mwanume wa maisha yangu ”
Aliongea Lea kwa hisia kubwa na walianza akuchokozana tena, na kwa mara nyingine wakaingia kwenye tendo hilo la kuzini na walidumu kwa dakika kama ishirini , na kati yao hakuna hata mmoja alie kuwa akikumbuka kondomu walionekana kuaminiana.
“Vipi mpenzi lini tena warudi Kenya?”
“Kesho narudi ,nitakuwa huko kwa mwezi mmoja , halafu haujaniambia Stella anaendelaje kwa sasa , si rafiki yako?” Aliuliza James na lea kumuona bado anawasiwasi na hali ya Stella.
“Anaendelea vizuri tu wala hakuwazii , ngoja nikuoneshe maana saivi ana mpenzi mpya na hana habari na wewe “ Aliongea huku akimuonyesha baadhi ya picha ambazo zilimuonesha Stella akiwa kwenye kivazi cha kuogelea ,James alisisimka baada ya kuona umbile la Stella
Lea alikuwa akifanya kumuonesha James ,alimjunesha za Stella na Sebastian wakiwa kwenye pozi mbele ya Swimming pool
“Huyu ndio mpenzi wake mpya ?”
“Ndio huoni walivyo pendeza “
“ Hongera yake , nilijua tu kama hanipendi huyu mwanamke nilikuwa namwamini sana kumbe mchafu namna hii , sitokuja kumsamehe “
“ Usimchukie sana mpenzi , kwanza upo na mimi mwanamke ninaye kupenda , haina haja ya kumuwazia Stella tena” Aliongea Lea huku Stella akielekea bafuni akimwacha James.
James alishika simu yake na kuwasha data na kuangalia message za Watsapp, alijikuta akitabasamu baada ya kuona jumbe kutoka kwa jina la Business partner ,jumbe ya sauti (voice notes) , aliweka ‘Earphone’ masikioni na kusikiliza huku tabasamu pana likiwa limeupamba uso wake , inaonekana jumbe hio ilimfurahisha mno , pale alipomuona Lea anatoka bafuni ndio akajikausha na kuweka simu pembeni baada ya kufuta ule ujumbe .
****
Ilikuwa ni siku nyingine siku ambayo Mama Rania na kijana Peter walikuwa kwenye gari moja aina ya Range Rover Spot huku dereva akiwa Peter akiwa makini na usukani , pembeni yake alikuwa ni Mama rania alieonekana kusinzia, hakuwa na habari kabisa kwa alivyojiachia kwani sketi aliovaa ilikuwa imepanda mpaka kwenye mapaja ,ukizingatia pia kigauni alicho vaa kilikuwa chepesi sana , mwanamama huyu hayo ndio maisha yake ,alikuwa na uzungu mwingi hata kazini kwake.
Gari ilizidi kuyoyoma na ndani ya masaa manne gari ilikuwa ikipita sehemu moja inayoitwa Soni hapa ndio Mama rania alishtuka kutoka usingizini .
“Nimelala sana?”
“Yeah ndio tuko eneo moja linaitwa Soni na muda si mrefu tunafika lushoto mjini “
“ Aisee nimelala”
“Unaonekana kuchoka sana”
“Yeah nimechoka sana jana sikulala kabisa mpaka kuna kucha “
“Tatizo lilikuwa ni nini sasa ?”Aliuliza Peter huku akiwa makini zaidi na barabara kwani makona yalikuwa mengi .
“Mambo ya kawaida tu , halafu kuna baridi huku” Aliongea Mama Rania baada ya kupandisha kioo.
“Ndio huku ni juu milimani , milima ya Usambara , ni kuzuri kweli nishawahi kufika mara nyingi nyingi kuna baridi ,ila kuna maeneo mazuri ya kutembelea”
“Kumbe nipo na mwenyejii, basi inabidi unipeleke peleke hayo maeneo ya vivutio nikaone na mimi”
“Hilo hata usijali Boss”
Walitumia masaa machache sana kufika Soni, na moja kwa moja waliingia Lushoto mjini na kwakuwa ailikuwa mapema sana , waliingia kunywa chai kwenye mgahawa na baada ya hapo wakaanza ukaguzi ndani ya jengo hilo la benki , na Peter yeye akiwa na kazi ya kuweka mfumo mpya kwenye tarakishi pamoja na vimashine flani vya mtandao .
Kazi ilifanyika kwa masaa manne mpaka kuisha na iliisha mapema kabla hata ya muda ambao walipanga kuutumia , baada ya kazi zote hatimae waliondoka huku wote wakiingia kwenye gari na kuelekea kwenye hoteli moja maarufu sana ndani ya Lushoto ilio kuwa ikijulikana kama “IRENTE VIEW “ hii ni hoteli moja nzuri sana ilio kuwa ikimilikiwa na marehemu raisi mstaafu Benjamini mkapa , ilikuwa juu ya mlima na ukiangalia kwa chini unaona maeneno ya tambarare , kama nji za kwenda Moshi , Mazinde na baadhi ya maeneo mengine ni eneo zuri kweli kwa hoteli hio kuwepo .
:Jamani kuzuri huku , kuna mazingira safi hadi raha na hewa safi kabisa “ Aliongea Mama Rania wakati wakitoka kwenye gari baada ya kuingia ndani ya hoteli hio.
****
Tajiri Samir hakurudi nyumbani siku ambayo mke wake alikuwa amemuambia kuwa kesho yake atasafiri kikazi na wala hakujua kabisa mke wake alikuwa amesafiri kuelekea wapi Zaidi ya kujua yupo safari kikazi .
Usiku wa siku hio Mama Rania alimsubiri sana , alikuwa akitamani kupata haki yake ya ndoa na alikuwa kwenye hali mbaya sana , lakini Samir hakurudi kabisa kwani mchepuko ulikuwa umemshikilia sana siku hio .
“Umeamkaje mpenzi?” Aliuliza Amanda ,alikuwa amekaa kwenye Dressing table akijipodoa ,ilikuwa ni muda wa asubuhi na Samir ndio kwanza alikuwa akitoka usingizini .
“Jana umeniweza kweli yaani nimesahau kabisa kurudi nyumbani “
“Nipo hapa kwa ajili ya kukusahaulisha kuhusu mkeo maana najua upo kwenye wakati mgumu sana wewe ni familia yako “
“Ni kweli , ila yataisha tu ,”
“Vipi mke wako leo si atakuwa na presha huko”
“Kweli na anavyonipenda sidhani kama jana alilala, maana kila siku namkuta yupo macho ananisubiria , halafu aliniambia kuwa anasafiri kikazi”
“Masikini saivi atakuwa na mawazo safari nzima”Aliongea Amanda pasipo kujali kuwa anaye mfanyia hivyo ni mwanamke mwenzake na anaiharibu nda ya mwanamke mwenzie.
****
Sebastiani alikuwa ndio kwanza kutoka chuoni , aliingia ndani kwake na kisha akajirusha kwenye sofa lilipo ndani ya chumba chake .
“Stella unaninyima usingizi , ila nitakupata tu kwa namna yoyote ile upo ndani ya mawazo yangu sana , nakufikiria kila wakati” Alijiwazia sebastiani huku akiangalia feni inavyozunguka .
“Inabidi nikusaidie katika swala lako na Masumbuko na naamini kupitia hili lazima unipende mwenyewe”
Alinyanyuka na kuweka begi lake lilibeba tarakishi mpakato kwenye meza na kisha, alivua nguo zake na kuingia bafuni ,chumba chake kilikuwa ni self container , alimaliza kuoga na kuanza kujifuta maji , kuna wazo lilimjia ambalo lilimfanya atabasamu .
“Aliifuata simu yake na kisha akamtafuta Steve na kumuuliza yuko wapi na alijibiwa kuwa yupo kazini bado , aliuliza na kuhusu Masumbuko na kupewa jibu kuwa yupo nyumbani na Peter alikuwa mkoani kikazi . majibu hayo yalimfanya atabasamu na kuvaa nguo zake na kujiandaa haraka haraka .
“Hapa naenda kwa masumbuko kuchukua ushahidi au kuutengeneza na hivyo hana akili atajaa tu” Alijiongelesha huku akitabasamu kinafiki.
SEHEMU YA 20
Sebastian alipanda daladala na moja kwa moja alielekea Mbezi Beach nyumbani kwa Peter na Masumbuko , kutokana na muda huo kutokuwa na foleni kubwa , alitumia dakika arobaini na tano hivi kufika Mbezi Beach , alikuwa akipahafamu sehemu ambayo alikuwa akiishi Peter , alivuka barabara na kunyoosha juu kabisa mpaka nyumbani wanapoishi .
Masumbuko wala hakuwa na habari kwani muda huo alikuwa akiangalia muvi kama kawaida yake maana alikuwa akipenda sana TV.
Alisikia mlango unagongwa na akanyanyuka na kusogelea na kuchungulia kwanza ni nani anaye gonga na alivyo muona ni Sebastian kwanza aliogopa na kuanza kujishauri kufungua ama asifungue , lakini mlango ulizidi kugongwa ndipo alipo kata shauri na kufungua mlango .
“ Wewe fala nagonga hata haufungui , ulikuwa umelala nini?”
“Hamna nilikua najishauri nifungue au nisifungue “
“ Ulijua anaye gonga alikuwa mimi au? “
“ Ndio nilichungulia kabla ya kufungua”
“Sasa kwanini ulikuwa unajishauri kufungua , au ulikuwa unaogopa yale ya siku ile , yale yalipita na sina time nayo chukulia poa tu “
“ Unasema kweli ?”
“Ndio namaanisha , mimi siwezi kukosana na mwanaume mwenzangu kisa demu”
“ Asante sana , mimi hata siku ile sijui nilifikiria nini maana nilijikuta tu nimefanya vile “
“Vipi umefanya” Aliuliza huku akikaa kwenye sofa
“Si kukufanya uwe muhudumu”
“Hahaha... sema ulichonifanyia wewe boya ,ndio hivyo nimekusamehe maana Peter ni rafiki yangu na wewe pia umekuwa rafiki yangu kuanzia leo na kuendelea”
“Asante Sana”
“Peter yuko wapi?”
“Kasafiri “ Alijibu Masumbuko huku akikaa na yeye maana muda wote alikuwa amesimama . wakati huo Sebastian na yeye alikaa vizuri nakutoa simu yake akatachi akapangusa pangusa na kugusa ,ilikuwa simu janja ,kisha akamwangalia Masumbuko .
“ Masumbuko halafu unajua ile siku ulinishangaza sana hivi ulimla yule mwanamke ?”
“Ndio nilimpiga kitu safi mpaka akazimia nikaachana nae maana pale nilimpa kumbukumbu za masaa mawili”
“ Haha .. kwahio ni kama ulimpiga changa la macho na ukala kitumbua si ndio?”
“Yeah nilimbadilisha mawazo sijampiga changa la macho “
“Sasa kwani kuna utoafauti gani kati ya changa la macho na kumbadilisha mtu mawazo?”
“Mimi Sijui jibu wewe”
“Namaanisha si kama umembaka vile?”
“ Kwani kumbaka mtu inakuwaje kuwaje?”
“ Si kama kumfanya bila ya kujua anacho fanyiwa, hapo utakuwa umebaka mtu kwa sababu alikuwa hajui “
“Ndio nimembaka basi”
Basi Sebastian aliaga huku akimwambia Masumbuko kuwa amekuja kwa jili ya kuonana na Peter ila kwa sababu hakuwepo alisema atakuja siku nyingine .
Sebastian alifika geto kwake huku akitabasamu na kutoa simu yake na kuanza kuplay na hapo hapo ikaanza kusikika sauti ya Masumbuko .
”Ahahaha.. nimembaka basi , masumbuko wewe huna akili na utaenda jela bila ya kupenda fala wewe”Aliongea Sebastian huku akitoa ile memory kadi na kuweka kwenye kijiboksi hapo ndani . .
*****
Tajiri Samir alikuwa amedhamiria kwa silimia mia kuwa lazima afanye maamuzi mapema , kwani kila alipo fikiria kuwa Rania ashaanza kuwa na hisia na Peter alipata wasiwasi hali hio aliiona kama bomu linalotaka kulipuka na ni yeye tu ambae anaweza kulitengua .
Wakati akiwa ofisini kwake alitoa simu yake na kumpigia rafiki yake Hemedi na kumwambia kuwa jioni wakutane maeneo yao ya kukutania kwani ana jambo la kumwambia .
Basi baada yakufanya kazi na kumaliza tayari ilikuwa ni mida ya jioni ambayo alipanga kukutana na tajiri Hemedi katika hoteli ya Kilimanjaro kwani hapo ndipo makazi ya Hemedi akitaka kujivinjari na mwanamke yeyote yule .
Samiri alifika nakuegesha gari yake na kwakuwa aliambiwa na bwana Hemedi kuwa wakutane kwenye chumba alichokuwa anapendelea kuchukua hotelini hapo , basi Samir alipandisha juu kabisa mpaka kwenye chumba hicho.
Alifungua mlango na kuingia ,alimkuta Hemedi akiwa na mwanamke mmoja alie valia chupi tu , Hemedi baada ya kumuona rafiki yake alimruhusu yule mwanadada aondoke huku akimminya kalio .
Kitendo kile alikishuhudia Samir na kujikuta akipandwa na hasira hasa alipo fikiria kuwa huyo ndio mwanume ambaye anapaswa kumpa Rania kwa ajili ya kumuoa .
“ Niambie Samir , umefikiria juu ya ombi langu?” Aliongea huku akimimina pombe kwenye glass na kumpa Samir , huku Samir wakati huo alikuwa na hasira kila akifikiria vitendo vichafu vya Hemedi alijiona kabisa huyo hafai kabisa kumuoa mwanae.
“ Ndio nimefikiria”
“ Haya niambie baba mkwe”
“ Sikia Hemedi nimegundua wewe sio rafiki yangu umnafiki , unatumia nafasi ya matatizo yangu ili kumpata mwanangu , sasa mimi kama baba yake sipo tayari kwa hilo.”
“ Samir wewe ni rafiki yangu sana na tumesaidiana katika mengi na unanijua vizuri , kwani kuna shida gani ya mimi kumuoa mwanao?: na kwanza wewe unakuwa kwenye nafasi nzuri kwani Rania utampa mali zako na mimi sina shida na mali zake atazitunza na kumpa mwanae atakae mzaa na hakutakuwa na mgogoro wa mali zangu na watoto wangu wakubwa sasa hiko unacho kichukia ni kipi, mbona kuna watu wengi tu wazima wana oa mabinti “
“Sikia Hemedi wewe ni mnafiki sana na nia yako nishaijua wewe kwa kupenda kwako ngono najua unamtaka na mtoto wangu kwa ajili ya kumchezea , hivi na hio tabia yako kweli naweza nikakupa kweli mtoto wangu mimi si nina mchimbia kaburi mwenyewe “
“ Sikia Samir ni kweli unajua tabia yangu ila ni kuhakikishie kuwa nipo tayari kubadilika kwa ajili ya Rania kwasababu sijampenda Rania jana wala leo , ni muda mrefu sana na nilikuwa nikiogopa sana kukuambia hilo lisije lika leta athari kwenye urafiki wetu”
“ Kwa hio ulisubiri mpaka sasa ambapo nina matatizo ndio kuniambia kwakuwa unajua kabisa sitokuwa na jinsi?”
“ Sio hivyo rafiki yangu , ni kwamba sipo tayari kumuona Rania anampenda mtu mwingine na wakati mimi nipo hai , na isitoshe pia sitaki na familia yako kusambaratika na kuingia kwenye migogoro kisa mwanaume , tena mwanaume ambae hana mbele wala nyuma”
“ Hio sio sababu ya kutosha ya mimi kukupa mtoto wangu”
“Sababu kubwa ni hii hapa” Alivuta bahasha moja na kutoa picha na kuzimwaga mezani na hapo ndipo Samir aliona kama akili yake haifanyi kazi vizuri kwani aliona picha zikimuonesha Rania akibusiwa kwenye paji la uso na Peter”
“ Nadhani umeona sasa, hio nayo ni sababu kwani inanikasirisha sana kumuona mwanmke ninae mpenda akibusiwa hivyo na hio ni kwenye paji la uso kesho na kesho kutwa atabusiwa kwenye lipsi na kumpa kabisa kitumbua , nadhani kwa kiburi ambacho watoto wako wamerithi kutoka kwako sijui utamwambia nini akuelewe kuwa umemtafutia mchumba wa kumuoa”
Samir alijikuta akikaa chini na kunywa glass yote ya bia na kuisikilizia inavyo choma koo na kisha akatulia na kuanza kufikiria huku akiziangalia picha zilizo kuwepo hapo mezani , alipeleka mawazo yake kwa Rania na kufikiria ubishi wake na msimamo wake pale anapohitaji kitu , akamfikiria Nasma
ujeuri aliokuwa nao , akamfikiria Peter na yeye na kuanza kumpima sifa zake kama anafaa kuwa na mwanae hata mmoja aliona hafai.
“ Unajua Samiri wewe hata kuua mtu najua hauwezi , ila mimi nitakusadia kumpoteza kijana Peter kwajili ya kuwaokoa wanao “ Aliongea Hemedi na kumfanya Samir aliekuwa kwenye mawazo amwangalie na kujiuliza hitaji lake kuu ni nini , alijibu kuwa kujiambia kuwa hitaji lake kuu ni Peter kupotea katika uso wa Dunia ili kuiokoa familia yake.
“ Una uhakika juu ya hilo la kumpoteza Peter “
“ Ndio hilo naweza sana na lipo ndani ya uwezo wangu ,ni wewe tu kunipa baraka nimuoe mwanao na wewe utumie ubaba kumfosi mwanao nimuoe na mimi najua jinsi ya kumpata Rania kama ndio jambo ambalo lina kuumiza kichwa .
Samir alimwangalia rafiki yake huyo ambae dakika chache za nyuma alikuwa akimwamini sana katika kumwambia shida zake , kwake aliona mazungumzo hayo yalikuwa ni kama ya kibiashara.
“ Daah..! “ Aliongea Samiri na kukatishwa na simu ilokuwa ikitoa mlio wa sauti ikioonesha kuwa kuna mpigaji , alitoa na kuona ni namba ngeni .
“ Boss za siku nyingi!”
“ Salama nani mwenzangu?”
“ Ni mimi Krispine kutoka kampuni ya POPOTE TUNAFIKA , ulinipa kazi nifuatilie taarifa za yule mwanamke ,nimepata taarifa yake na mwanae”
“Uko wapi?”
“Nipo Ubungo”
“ Nakuja “
“Hili tutaongea siku nyingine Hemedi” Aliongea Samir na kisha kuondoka .
****
Tukiingia ndani ya mji wa Lushoto , alionekanna Mama Rania akiwa kwenye chumba chake ndani ya hoteli , baada ya kila mtu kuchukua chumba .
Chumba cha Peter kikiwa kipo mkabala na chumba cha Mama Rania , hoteli ilikuwa na mazingira ya kuvutia sana kwani chumba kilionekana kuwa kizuri mno .
Mama Rania alikuwa amekaa kwenye kitanda chake akionekana kuwa na mawazo , akiwa ameshikilia simu yake , ni kama alikuwa akisubiria mtu amtafute . na nikweli alikuwa akisubiria ujumbe ama simu kutoka kwa mume wake , kwani tokea alivyo ondoka jana yake nyumbani hakurejea kabisa , na mbaya Zaidi ni kwamba na yeye ameondoka bila ya kuonana nae , japo alikuwa akijua kuwa mume wake alikuwa akichepuka lakini hakuacha kumpenda mume wake na alitaka tu kujua hali ya mme wake kuwa anandeleaje .
Wakati akiwa kwenye mawazo akiwa amekaa kwenye sofa , jina la ‘My favourite Naa’ lilisomeka kwenye kioo cha simu yake janja ukiambatana na mlio wa sauti wa wimbo wa ‘Alan walker –Faded’, alikuwa ni mwanadada Nasma ,alitabasamu huku akiipokea na kuweka sikioni na kuanza kuongea na mwanae . alionekana kuna jambo la kufurahisha ambalo alikuwa akiongea na mwanae huyo maana hali yake ilibadilika na kuonekana kutabasamu .
Mama Rania alijikuta akitamani kupiga soga na Peter mara baada ya kumaliza kuongea na simu , kwani alikuwa amemzoea sana Peter na hususani akiwa kwenye hali ya mawazo mara nyingi mtu ambae amekuwa tabibu wake wa kumrudisha katika hali sawa alikua ni Peter , alinyanyuka kivivu na kuchukua kitenge chake na kujifunga huku akiwa amevalia kijisketi chake chepesi kwa ndani alitoka na kwenda mpaka kwenye chumba cha Peter , aligonga na kusubiria na baada ya muda Peter alifungua mlango hukua akiwa amevalia singlend na bukta lake .
“ Vipi naweza kuingia? “ Aliongea Mama Rania huku akimwangalia Peter usoni aliejifikiria kwa sekunde na kisha alimruhusu mama huyo na kuingia
“ Najihisi upweke kukaa mwenyewe nimeona nije unichangamshe
changamshe maana naona kama mawazo yananiandama”Aliongea Mama Rania
na Peter kwa akili yake ya haraka alijua kabisa mama huyo alikuwa akisumbuliwa na mawazo kwani kule njiani alikumbuka alimwambia kuwa hakulala kabisa usiku wa jana mpaka kunakucha .
“ Basi stori zilianza , na kama kawaida Peter kwakuwa alikuwa haishiwi na stori za uongo na kweli Mama Rania hali yake ya furaha hatimae ilikuwa imerudi kwa kiasi fulani , uzuri wa kile chumba ni kwamba kilikuwa na sehemu ya kukaa yaani kulikuwa na masofa(master suite room) ambayo yamepangwa na yalikuwa yakiruhusu watu kama watatu kukaa .
Baada ya kupiga stori kwa muda mrefu , huku hali ya hewa ya Lushoto ikizidi kuwapa kajiubaridi na kumfanya Mama Rania atoe ile khanga alio jifunga na kujifunika mabegani na wakati huo walikuwa wamehamia kwenye kungalia onyesho fulani la wanamuziki kutoka Marekani wakionyesha uwezo wa kwenye kuimba(Stage perfomance ) , sasa Peter alidhania mama Rania anapenda kile alichokuwa akiangalia kumbe mwenzake alikuwa ashalala muda na saa ilikuwa ikisoma saa nne usiku muda huo , Peter muda wote alikuwa akijua kuwa na mwenzake yupo makini kwenye kuangalia maana alikuwa akiona vijiaibu flani hivi vya kugeuka na kumwangalia Mama Rania usoni. Na hakujua kwa nini alikuwa na hali hio .
Baada ya dakika kadhaa alijikuta akigeuka na kumwangalia Mama Rania , hapo ndipo alipo gundua kumbe mwenzake ashapotelea usingizini muda mrefu huku akijiegamiza vibaya kwenye lile sofa ,Peter alimwangalia na kuona kweli boss wake kachoka , aliamua kunyanyuka lakini mara Mama Rania kwa jinsi alivyo kuwa ameegamia lile sofa alijikuta akielekea chini na Peter kwa uharaka wake alijikuta akichuchumaa na kumdaka na hapo Mama Rania ndipo alipo kuja kushituka akiwa kwenye kifua cha mwanaume na uso umekaribiana na wa Peter huku akihisi pumzi ya joto ya kijana , kwakuwa kijisketi alicho vaa kilikuwa kifupi kwani hizo ndio nguo zake , basi mapaja yote yalikuwa yamegusana na miguu ya Peter kwani alikuwa amevalia bukta .
Mama Rania alijikuta akihisi joto Fulani na pumzi ya Peter ilio kuwa ikimpumulia na kujikuta hisia za mapenzi zikimpanda na kwa upande wa Peter kama mwanaume rijali alikuwa akihisi joto la ajabu sana kutoka kwenye mwili wa Mama Rania na kujikuta dunguso yake kusimama wima na kugusa mapaja ya Mama Rania.
Mama Rania alijikuta akishusha mdomo wake taratibu kwa Peter , kisha lips zikagusana na kwakuwa Peter alikuwa mgeni alikuwa haelewi haelewi chakufanya alikuwa kama mtu aliepigwa shoto na kuhitaji kunasuliwa , Mama Rania alicharuka kwani hisia zilikuwa zimempanda kiasi kwamba kwa hali alio kuwa nayo shetani asingeweza kujizuia , na ukizingatia hajakutana na mwanaume kwa muda mrefu hali ilikuwa mbaya kwake alijisemea liwalo na liwe .
Mama Rania alimshika Peter mkono na kuushikisha kwenye mapaja yake karibu kabisa na kitumbua na kumfanya Peter ahisi msisimko wa ajabu sana na uliongezeka pale Mama Rania alipogusa dunguso ya Peter.
Peter alishindwa kabisa kujizuia kwani hisia zilikuwa zipo juu na ukizingatia kuwa hakuwahi kufanya kitendo hicho tokea azaliwe, basi kujikontrol ilikuwa ni ngumu sana kwa kijana kama Peter kwani alianza kabisa kutoa ushirikiano , Mama Rania alinyanyuka na kumuinua Peter huku wakipeana juisi ya mdomoni na mwanzoni Peter alikuwa hajui hatua ila muda ulivyo zidi kwenda alijikuta akianza kuwa fundi , Mama Rania alishusha nguo yake ya ndani pasipo kuvua ile sketi na kisha akatoa na sidiria na kijiblazia alichovaa, alichukua mkono wa Peter na kushikisha kwenye hazina yake na Peter alielewa somo na kutumbukiza kidole na kuanza kazi ya kusugua na kumfanya Mama Rania atoe miguno huku akijinyonga nyonga , Mama Rania aliona kama anacheleweshwa kwani wakati huo hata haikueleweka Peter alivua saa ngapi lile libukta ,wakati huo msumali ulikuwa dede na umetuna ,Mama Rania aliinama na kupandisha kile kijisketi juu kabisa na kumwachia Peter kazi na Peter mwenyewe hakuzubaa maana akili yake hapo ilikuwa haifanyi kazi vizuri , aliingiza mtwangio wake na kumfanya mama wa watu apanue mdomo na kukugugumia kwa utamu kama wote.
Baada ya nusu saa mbele Peter alionekana fahamu kumrudia huku Mama Rania akiwa hana nguo hata moja na Peter nae alivaa bukta lake haraka haraka na kuangalia pembeni kwani alianza kujutia kwa kile alichofnya , kwani aliona kabisa ashakwisha lala na mke wa mtu.
Kwa Mama Rania wala hakuwa hata na wasiwasi , tena tabasamu lilionekana likipamba uso wake , kwake kufika kileleni lilikuwa ni historia ya muda mrefu na histora hio ndio imejirudia siku hio akiwa na kijana mdogo Peter , alitambua wasiwasi aliokuwa nao Peter hivyo aliamua kumsogelea na kisha alimkumbatia huku akimwagia sifa kedekede .
Naam ! Liwalo na liwe .
****
Samiri aliendesha gari lake kwa haraka kubwa ili kuwahi sehemu ambayo amepanga kuonana na bwana Krispine ambae ni mfanya kazi wa kampuni ya kutafuta watu ijulikanayo kwa jina la “POPOTE TUNAFIKA” , alitumia muda wa saa limoja tu kutoka mjini Posta mpaka Ubungo Landmark Hotel , sehemu ambayo ndio alipo panga kukutana na bwana huyo .
“Za Siku Nyingi Boss” Alisalimia kijana mdogo kabisa alie valia suti yake safi kwa heshima kabisa , huku akiweka mkoba wake pembeni .
“ Salama kabisa namshukuru mwenyezi Mungu kwa kila hali”
“Nimechelewa kidogo kulikamilisha zoezi hili, kutokana na kwamba sikua na muongozo wowote katika kumtafuta ila nashukuru nimefanikiwa kumpata .
“Niambie anapatikana wapi?” Aliuliza Samir kwa shauku kubwa ya kutaka kujua sehemu ambayo anapatikana
“Kwa majina anaitwa Irene mshana ni mwenyeji wa mji wa Arusha sehemiu alipozaliwa:”Alipozi kidogo huku akifungua makaratasi yalio kuwa kwenye begi lake hilo .
“Alihamia jijini Dar kwa ajili ya kutafuta maisha baada ya mama yake kufariki kwa ugonjwa wa maralia , kuhusu taarifa za baba yake na ndugu kwa ujumla sijazipata .
Hapa jijini alikuwa akiishi maeneo ya Sinza mpaka alipo jifungua mtoto wa kiume ndipo alipo hama , na taarifa kwa sehemu alipo hamia hazijafahamika kwa undani Zaidi ,lakini nimefahamu kuwa alijifungua mtoto wa kiume lakini jambo la kusikitisha ni kwamba kwa utafutaji wa kampuni tumeweza kugundua kuwa mwanamama huyu alipoteza maisha yeye pamoja na mwanae.”
Samir alijikuta kwenye mshangao mkubwa sana na maumivu makali baada ya kusikia kuwa wote wawili walipoteza maisha hapo hapo .
“ Samir alijikuta akinyong`onyea baada ya taarifa hio kwani ilikuwa ni taarifa ambayo ilisikitisha mno mbali na mategemeo yake , hasa alipo sikia kuwa mwamke yule alijifungua mtoto wa kiume ambae anamtafuta usiku na mchana ili kuja kumrithisha mali zake kwani hakuwa na uhakika na maamuzi ya mali zake kuzirithisha kwa wanae wa kike .
“Ni hayo tu mheshimiwa na kama kuna jipya nitakalo libaini basi nitakuambia mapema iwezekenzvyo “ Aliongea bwana yule na kisha akapeana mkono na Samir na kisha kuondoka .
Alikaa chini na kujifikiria kwa muda huku akihuzunika kwa uzembe wake ,lakini mwishowe alikubaliana na hali halisi kwa kuona kwamba hayo yote yalikuwa mapenzi ya Allah.
Alijkuta akitoa simu yake na kumpigia tajiri Hemedi rafiki yake
“Una baraka zangu zote, nipo tayari kukupa mtoto wangu umuoe ila kwa masharti makuu mawili la kwanza ubadili tabia yako , kwani sipo tayri kumuona mwanangu akilia kwa kuumizwa na tabia yako ,na pili najua wewe ni mtu mwenye mtandao mkubwa sana kwa hio naomba umpoteze kijana Peter kwenye uso wa hii Tanzania maana sitaki kumuona akihusika na familia yangu “ Alisema maneno hayo Samir na kisha akaagiza chupa ya bia na kuanza kunywa hapo hapo hotelini na alipanga siku hio alewe chakari kutoa mawazo.
Wahenga wanasema”Majuto ni mjukuu” na “usiloijua ni kama usiku wa kiza kinene .
SEHEMU YA 21
Peter aliekuwa amegeuka upande wa dirishani alikuwa akiona hata aibu ya kumwangalia mama huyo , kwani kitendo walicho kifanya muda mfupi ulio pita kilikkuwa ni kitendo ambacho alikiona kama ushetani au dhambi kubwa sana japo hakuwa na dini , ila aliamini kuwepo kwa Mungu mhukumu wa watu wenye dhambi na yeye aliona kuwa amefanya dhambi kulaa na mke wa mtu, ilishangaza kwa yeye kujutia kwani moja ya malengo yake katika kisasi chake ni kutembea na familia nzima ya Samiri .
Peter aliitoa mikono ya Mama Rania na kisha kumgeukia na hapo ndipo alipo kosea kwani ile anageuka tu Mama Rania alikuwa tayari ashapeleka mdomo wake na kuanza kumyonya midomo , Peter aliannza kuleta ugumu lakini aliposhikwa dunguso yake na mikono milaini ya mama huyo alijikuta akinywea kama maji kwenye mtungi na kumuacha afanye kile anacho taka , mchezo uliendelea kwani walisogea mpaka kitandani na Peter kusukummwa kitandani na boss wake Shani au Mama Rania na kisha akamvua bukta na kutupa kwenye kona ,Mama huyu alishika kirungu na kuanza kuchezea jambo ambalo lilimfanya Peter awehuke kwani kitu anacho fanyiwa kilikuwa ni cha levo ya ktabu cha ‘Super Erotic Romance’ mama alikuwa akijua mambo kwani yeye alikuwa tayari ameolewa ukiachana na historia ya nyuma ya maisha yake kabla ya ndoa ,alijua mbinu jinsi ya kumpoteza mwanaume yeyote yule kwenye dunia ya mapenzi, Peter hakufurukuta kwani alikuwa kwenye sayari nyingine kabisa , sayari ambayo hakuna mtaalamu yoyote wa mambo ya anga amefanikiwa kuiona kwa Darubini .
“Liwalo na liwe” Aliongea Peter na kumshika Shani na kumgeuza hata Shani mwenyewe alishangaa kitendo hicho cha Peter kumgeuza kwanguvu kama mbogo . alimkunja kama kambale na kuingiza mtwagio wake maana ulikuwa mkubwa wa haja na kwakuwa Mama Rania katika kujifungua kwake kote ilikuwa ni kwa njia ya upasuaji basi eneo lake lilikuwa kama la binti mdogo .
Peter alimpelekea moto mama huyu Rwanda magere anaziiita Bakora za kimkakati , haikujulikana hata ujuzi alikuwa ameutolea (hivi vitu tunazaliwa navyo ni asili ) ,Mama Rania au ukipenda muite Shani alikunjwa na kukunjuliwa na kunyoooshwa na kupinduliwa , akafika kitonga akashuka akapanda tena akashuka akapanda tena na kushuka tena na kujikuta akiweka historia ya kuukwea na kuupanda mlima kitonga kwa mara kibao.
“Asante sana mpenzi , yaani hata siamini nikajua unajuwa kuchezesha vidole kwenye komputa tu kumbe hata kwenye mwili wa mtu uko vizuri ,umenifanyia kitu ambacho sitakaa chini na kuukosa uhondo huu “ Alijidekeza kabisa huku akitoa sifa zote kwa Peter huku akisahau kabisa mkononi ana pete ya ndoa .
Basi ukawa mwanzo na mwendelezo wa kupanda vilima na kushuka , siku tatu zote walizo kuwa katika jiji hilo la Lushoto kwaminajiri ya kufungua benki katika wilaya hilo uliambatana na ufunguzi wa mapenzi yao yasio na kibali mbele za Mwenyezi Mungu, walitembea kwenye vivutio vyote vya utalii vilivyopo ndani ya wilaya hio , huku kila siku wakirudi kupeana dudu , hata chumba alicho chukua Peter ilibidi akirudishe tu kwani alikuwa hakitumii tena, ilikuwa ni mwendo wa kupeana dudu tu , kiufupi sio Mama Rania sio Peter wote walinogewa , Peter alinogewa na vitu alivyo kuwa akipewa na mama huyo na Mama Rania na yeye alijikuta hata akimdharau mume wake kabisa na kuona sasa wako droo.
“Peter mpenzi wangu nakupenda sana , yaani natamani ungekuwa wewe ndio mume wangu “ Aliongea huyu kwa mapozi kabisa ukidhania ni binti wa miaka therathini au ishirini na hajawahi kuzaa kumbe ana mitoto tena mikubwa na mizuri kabisa ambayo ipo kwenye lika la kuolewa na kuwa na familia kama kijana Peter. .
“Nakupenda pia mpenzi , siku zote sikujua kumbe hii sehemu inanoga kiasi hiki” Huku akimshika na wakati huo walikuwa kwenye gari kuelekea hotelini wakitokea eneo moja linaitwa Mkuzi huko kwenye vivutio vya utalii , na mama Rania hakuwa hata na wasiwasi yaani alikuwa akijiona dunia nyingine kabisa na alitamani kabisa kutorudi nyumbni ,wakae tu huko hata mwezi mzima , na kwa Peter alikuwa amenogewa na yeye alitamani alekitumbua tu kwani utamu aliokuwa akihisi wakati akichovya kibuyu hicho cha asali haukuwa wakawaida laiti angejua kuwa mwanamke ambae ana mkunja kila siku na kumkunjua na kuonesha ubabe wake ni mwanamke alie husika na mauaji ya mama yake sijui angefanya nini na kwa Mama Rania na yeye laiti angejua kuwa mwanaume huyo alio kuwepo hapo ndio mtoto aliotoa maagizo kwa ajili ya kuuliwa na pia ni mtoto wa mume wake na kaka wa wanae sijui ingekuwaje .
“Vipi nikununulie ndizi naona zimeiva na zinavutia “ Aliongea Peter baada ya kufika eneo moja liitwalo Magamba .
“Ndio nunua “ Alijibu Mama Rania huku akijilaza kwenye kiti.
“Peter alitoa wallet yake kutoa hela kwa ajili ya kulipa , lakini ile anachomoa hela kulidondoka kitu kutoka kwenye waleti yake alinunua kwanza zile ndizi na kisha na kuziweka mbele na kisha aliinama na kuokota , alijikuta macho yakimtoka na hapo hapo akakumbuka siku ambayo Rania alimletea waleti yake .
****
Rania tokea Peter aondoke alijikuta kwenye wakati mgumu sana , kwani kila akikumbka tukiio la Peter kumbusu kwenye paji la uso mwili wote ulikuwa ukimsisimka , kila saa alikuwa akiangalia kidani cha holder ya funguo alicho pewa na Peter , huku akikumbuka maneno yake kuwa huo ni kama ushahidi wa wao kuwa marafiki, alijikuta akitabasamu usiku huo , huku akijiviringisha kwenye kitanda .
“Lakini yupo kimya sijui ujumbe wangu hakuupata?? “ Alijiongesha mwenyewe huku akionekana kabisa kuna ujumbe alimtumia Peter haikujulikana kamtumia kwa njia gani ila alionekan kabisa kuna ujumbe ambao alikuwa amemtumia Peter na alikuwa akisubiria majibu.
“Sis....” Ilisikika sauti ikiit na kumfnya Rania alie lala kugeuka na kuangalia mlangoni.
“Waoh!, Nasma.. karibu sana, leo umekuja kutusalimia jamani nimekumisije mdogo wangu” Kumbe alikuwa ni Nasma.
“Nimekumiss pia mrembo , leo nimekuja kabisa kulala na ndio maana unaniona usiku”
“That is great , karibu sana mdogo wangu yaani ungejua nilivyo kumiss wewe acha tu , sema majukumu ndio yananibana nimeshindwa kuja kukusalimia huko nyumbni kwako”
“Mewe muongo , ila nafurahi nimekuona , unazidi kuwa mzuri tu dada yangu”
“Ahahaha jamanii.. wakati wewe ndio mzuri katika familia yetu kuliko wote”
“Ahaha.. sio kweli wote tunalingana” Aliongea Nasma huku wakionekana kufurahia kuonana, kwani japo walikuwa wakiishi kwenye jiji moja lakini ni mara achache sana kwa wao kuonana ,Nasma yeye alikuwa kiishi sehemu yake , kutokana na kwamba yeye haelewani kabisa na baba,Nasma hakupenda ukoloni wa baba yake.
“Jamani chakula atayari , dada Najma anawasubiri”Aliongea mfanya kazi wa ndani akiwakaribisha kwenda kula achakula cha usiku.
“Najma mambo!” Alisalimia Nasma baada ya kumkuta pacha wake kwenye meza akiwasubiri maana ndio ulikuwa utaratibu lazima kuwasubiri watu wote wafike kwenye meza ndipo uanze kujipakulia na kama sio sheria hio Najma angekuwa ashajipakulia mapema mno..
“Safi nakuona karibu” Aliongea Najma kwa kujilazimisha .
“Hata mimi nakuona tokea miaka mingi tulipo achana tokea uende masomoni umebadilika na umezizi kuwa mzuri “
“Ndio ila najua si kushidi wewe” Aliongea najma huku akijipakulia chakula
“Halafu jamani baba siku hizi anachelwa “
“Nani anachelewa ?: , mimi hapa nimerudi “ Ilisikika sauti kutoka mlangoni na Samir alionekana akiingia huku amelewa chakali huku akiyumba yumba na kuwasogelea wanae .
“Watoto wangu warembooo.. naonaaa… leo mmekusanyika kunijadili .. mimi baba yenu , ..hiki kikao chenu tukipe jina gani vilee.. eti Nasma mtukutu ... aa... mimi nakiita kikao cha masimango”Aliongea Samir kilevi na kumfanya najma aamke na kumkalisha baba yake kwenye kiti .
“Dadii.. mbona uko hivi leo jamanii “.
“Nilikuwa nasherehekea”Aliongea
“Ulikuwa unasherehekea nini ?”
“Najma msaidieni baba aende chumbni kwake acha kumuuliza maswali”Aliongea Rania
“Nilikuwa nasherehekea kupatikana kwa mchumba wa Rania “Aliongea kilevi na kumfanya Rania ashituke na kumwangali baba yake huku Nasma na Najma wakimsadia baba yao apande ngazi kueekea juu chumbani
“Hii tabia ya baba kulewa kaanza lini Najma?”Aliuliza Nasma
“Mimi hata najua sasa , ila kaanza wiki ya tatu hii na leo kawahi “
Nasma ndio alikuwa kulwa na Najma alikuwa doto.
Basi walirudi na kuanza kupiga stori , huku Rania akiwahadithia kuwa yupo mbioni kupata mchumba jambo aambalo wadogo zake walishangaa huku wakitabasamu .
“Anaitwa nani huyo ?”
“Anaitwa Peter”Alijibu bila hata ya wasiwasi
“ Jamanii ..natamani kumuona , kwa hio mshaanza kuwa na mahusiano au ni mapenzi ya mtu mmoja “ Aliuliza Nasma
“ Bado ila naamini ana nipenda maana ashanipa zawadi na kasema yeye ni tofauti na wanaume waliopita , kasema hayuko tayari kuniacha”
“wow ! jamanii.., am so so happy for you sis..”Aliongea Nasma
“Na wewe Nasma vipi ?”
“ Yes , yes .. me too” Alijibu huku akijifumba uso kwa mikono na kumfanya Rania acheke na Najma kumwangalia huku akilazimisha tabasamu .
“Haha what ! ,So all of us we are in love , how if we arrange a day kukutanishana sisi wote na wapenzi wetu au mnaonaje? Aliongea Rania
“Kwa hio hata Najma ana mpezi tayari ?”
Hapo ndipo alipo haribu kwani Najma aliondoka bila ya kusema kitu na kukimbilia ndani kwake , alifika na kujikuta akianza kulia kilio cha kwikwi.
“Uko wapi , mbona sikuoni , mbon aunaufanya mtima wangu kuwa katika maumivu kwa kiasi hiki , nakupenda njoo unitoe kwenye haya haya mawingu ya sintofahamu” Aliongea Najma kwa hisia huku akitoa machozi laiti angejua mwanaume anae mlilia ni kaka yake angeacha mara moja, lakini ndo hivyo kosa si lake kupenda kosa linaanzia kwa baba kumtelekeza mwanamke huku ilihali akijua ni damu yake , sasa watoto wanakuja kumpenda mwanaume huyo huyo ,huku mama nae akinogewa na mwaname huyo huyo
“Wanaume wajibikeni na matendo yenu madhara yake yanakuja kuwa makubwa sana na ni kama haya yanayo onekana kwa familia hi ” Maneno ya mwandishi yanywe au yateme
“Halafu mbona na wewe umenuna ghafla “ Aliuliza Rania .
“Sijakutana na mpenzi wangu bado , kwani tumekutana mara moja tu na jina simjui” Aliongea Nasma nakumfanya na yeye kushangaa
“Mhmh! basi wewe na Najma mko sawa “
“Una maanisha nini dada ?”
“ Namaanisha na yeye amependa mwanaume ambae hamjui”
Nasma na yeye alishangaa huku akimuelewa pacha wake ni maumivu kiasi gani aliokuwa akipitia kwani alikuwa akijua ni jinsi gani inauma kumpenda mtu ambae bado haujamfahamu vizuri na huna namna ya kuonana huku ukisubiria bahati ya Mungu kuwakutanisha tena ..
****
Peter alijikuta akichukua ile picha na kuigeuza nyuma na kuona maneno yameandikwa , Mama Rania alikuwa akimuangalia hivyo aliamua kuweka ile picha kwenye waleti na kisha akaendela na safari .
walifika ndani na kisha waliagiza chakula na kuanza kula na kumaliza na kisha wakaanza kuangaliia movie huku wakiwa wamekaa kwenye pozi la kimahaba kabisa , hakuna hata mmoja alie kuwa na wasiwasi.
“Nikifika nataka kukununulia nyumba kubwa mpenzi”
“Unasema kweli?”
“Ndio natamani hata ya kuishi na wewe , ila nina mume nitakununulia nyumba na nitakuwa nakuja mara kwa mara kufurahia penzi letu”
“Asante mpenzi nakupenda sana”Huku wakianza kunyonyana na hata ile muvi ikaachwa kuangaliwa na kuanza kunyanduana na kijana huyu ambae kusudi la kwendca kufanya kazi kwenye benki anayosimamia mwanamama huyu ni kwa sabababu alitaka kulipiza kisasi kwa Samiri kwa kitendo cha kumdharau , na katka kisasi chake hicho alikuwa amedhamiria kulala na wanae wote ,lakini sasa anamkula mama mtu huku watoto wa mama huyu wakiliwazia penzi la Peter yaani kisasi kinajilipa chenyewe .
Kwa yaliokuwa yanafanywa na wawili hawa pamoja na historia zao ilikuwa ni jambo la kutisha kweli kweli ,Mama Rania hakumuona tena Peter kama mtoto , tena mtu ambae alikuwa anapaswa kutembea na mwanae Rania , alimuona kama mwanaume Tena mwanaume wa kukidhi haja zake zote .
Baada ya kumaliza kufanya waliokuwa wanafanya mambo ambayo \mnele za Mungu hayakuwa na kibali , Mama Rania alipotelea usingizini , na Peter alitumia wasaa huo kuangalia kile alichokuwa na hamu ya kuona muda wote
Ilikuwa ni picha ya mrembo Rania picha ambayo ilikuwa imekatwa kipande na kufanywa kama passport , huku ikimuonesha kimwana huyo kupendeza kweli kwa tabasamu lililopamba uso wake ,Aliangalia kwa sekunde kadhaa picha hio na kisha aliigeuza nyuma na kusoma vimaandishi vidogo vilivyoandikwa . “Najua ni kipindi kifupi nimekufahamu ila umekuwa na mchango mkubwa sana kwenye furaha yangu na umenitoa kwenye kiza kinene sana juu ya mtazamo wangu kuhusu wanaume nimegundua kuwa wewe ni mwanaume wa kipekee sana , na mwanume ambae ninaweza kuishi nae , nimetokea kukupenda sana Peter nipo tayari kuwa mpenzi wako naomba unikubalie na usinione mimi kama maaya ni hisia zangu juu yako nitasubiri jibu lako ni mimi rania nakupenda sana peter naomba unifikire na unipe jibu linalotoka ndani ya moyo wako sitaki kuumia tena”
Peter alijikuta jasho likimtoka huku akiwa haamini kwa kile anacho kisoma , kwa upande wake ilikuwa ni jambo ambalo angeshangilia kwani ni kitu alicho kuwa akikitaka kwa mrembo huyo kutoa bikra tu na kuondoka zake kwani aaatakuwa kashalipa kisasi , ila maneno yale yalimfanya apatwe kutokana na kwamba japo maandihi yale yalikuwa machache lakini aligundua kuwa yalikuwa yamebeba hisiaa nzito mno .
SEHEMU YA 22
“Nadhani ni wakati wa kutafuta mrithi wangu sasa nishachoka kuongoza kampuni nataka nibakie kwenye bodi tu ya kampuni” Aliongea Profesa Gladness.
“Sasa profesa utamwachia nani kampuni , wakati hakuna mtu ambae anafikia hata nusu yako”
“Mary ukiona natamka haya maneno jua nishapata mtu wa kukalia kiti changu”
“Ni yule mtu anae husishwa na viumbe kutoka sayari nyingine au kuna mwingine?”
“Kuhusu hilo nitaliweka wazi hivi karibuni haina haja ya kuwahi kuwaambia” Aliongea profesa Gladness bila ya kumtajia jina Mary kwani alikuwa ni shushu na hapo alikuwa yupo kiuchunguzi Zaidi kwa kile kilicho kuwa kinaendelea .Na uzuri wa profesa Gladness hakuwa akimuani mtu , na hio ndio slogani yake..
“Boss kuna wageni wako wamekuja kukutembelea “ Aliongea Mary na kumruhusu awaingize.
“ Haa…!! Mom .., dadii” Aliongea Gladness na kuwakumbatia wazazi wake ambao alikuwa ni Rafaeli na Nifani
“Mmerudi lini nchini ?”
“Ndio tumeingia leo hii nchini ,tumepitia KIA”
Gladness alifurahi sana kukutana na familia yake hio , kwani ni kipindi kirefu kidogo tokea wasafiri , kwani walikuwa wakila bata tu , na kutembelea nchi mbali mbali .
Basi familia hio walitoka na kwenda nyumbani kwa gladness sehemu ilo kuwa ikijulikana kama kijiji cha maroboti au Village G.
“UNAITWA RAFAELI MSWAKI UNAMIAKA 65 ,UFANYAJI KAZI WA TEZI YA MAFUTA MWILINI IMEPUNGUA KUFIKIA NUSU YA UZALISHAJI WAKE , PRESHA YAKO NI 137/88mmhg …, NGOZI ISHAANZA KUKUNJAMANA , UWEZO WA KUFANYA MAPENZI UMEPUNGUA KUFIKIA ROBO TATU,KWA MAKADIRIO UMEBAKISHA MIAKA SI CHINI YA KUMI KAMILI UTAKUWA USHAKUFA”
Ni baada ya kuingia tu ndani ya nyumba ya profesa Gladness na roboti lifahamikalo kwa jina la Nimrod lilimscan(skani) Rafeali na kutoa hayo maneno.
“ Nimrod tulia “ Aliongea Gladness na roboti hilo likiondoka zake huku lishaharibu hali ya hewa kwa kiherehera cha kumchunguza kila mgeni anaeingia nyumbani kwa Profesa Gladness.
“Daaa! Wewe mtoto maroboti yako yashaanza kunipa stress” Aliongea Rafeli kwani alikuwa hajui kuwa kabakisha miaka kumi mpaka kufariki kutokana na maneno na uchunguzi wa Nimrodi.
“Hapanna baba kuna muda mwingine yanakosea” Alijitetea gladness huku akimwangalia Rafaeli ambae alionekana kweli ashaanza kuwa mzee kibabu .
“Umesikia mke wangu huko ,nimebakisha miaka kumi tu kufa “
“Mume wangu bwana hayo ni maroboti “
“Kama ni maroboti basi ngja niliiite likuchunguze na wewe na wewe”
“ Hapana .. hapana .. mimi sitaki kujua nitakufa lini”
“Ahaha .. wewe si umesema hayo ni maroboti .. mbona unaogopa sasa”
“Ahahaha..mume wangu wewe anza kukaa na watoto wako vizuri na tumia muda mwingi kuwa nao “
“Ila limenidhalilisha lilivyo sema , siiwezi kazi ya chumbani vizuri .. hii dunia inavyo endelea hivi hatutaweza tunza siri kweli”
“Hahaha .. mume wangu ushakuwa babu tayari bhana “
“Na wewe si bibi kizee”
Hao walikuwa ni Rafeli na Nifani wakiwa nyumbani kwa mtoto wao mkubwa Gladness.
*****
Masumbuko kama kawaida yake alikuwa kapiga zake nne hana habari huku pembeni akiwa na vijifuko vya Ice cream akiwa anakula na kilicho kuwa kikiangaliwa kwenye TV kilikuwa ni filamu za ngono , maana kila siku kwake alikuwa akiangalia kwa dozi
Alikuwa haamini kama kweli hana nguvu za kiume
“Aaa…. Masumbuko vipi tena na hizo video “ Aliongea Peter huku akionekana kushika kijibegi na muda huo alikuwa akionekana kabisa kuwa alikuwa akitoka safarini na ndio anarudi.
“ Zinanitia mzuka na mori mori” Aliongea masumbuko na kumfanya Peter atabasamu .
“Wewe si uneenda tu hapo nje na kumpa mwanamke kumbukumbu ,unamleta humu ndani unafanya yako , kama siku ile “
“Una maanisha kama kubaka vile , si ndio “
“ Nani kakwambia kubaka , pale haulazimishi mtu bhana “
“Yule mshikaji alikuja na akaniambia kuwa kitendo kile ni kubaka “
“Mshikaji gani huyo ambae una mzungumzia ?”
“ Yule wa siku ile , Sebastiani yule”
“ Kwa hio alikuaja hapa nyumbni na ukamfungulia?”
“Ndio alikuwa anagonga mlango kwa nguvu , ndio nikamchungulia na nilivyo muona ni yeye nikajiuliza nifungue au nisifungue ila ndio nikajikuta nishafungua mlango”
“Na alisemaje sasa?”
“Hana tu ndio alinisifia tu kuwa yule mwanamke nilimpa dozi kali ya kumbaka”
Peter ilibidi amuangalie tu Masumbuko na kisha kutabasamu maana aliona kichwa cha ndugu yake huyo wa hiari kilikuwa signal zinasoma na kupotea .
Basi Peter baada ya kuweka vitu vyake vizuri alikaa sebleni huku akionekana kuna jambo linamsumbua kwani aliionekana al kiwa kwenye mawazo , huku masumbuko yeye akiwa hana hata habari .
“Peter haya magorofa marefu ushawahi kuingia?”
“Aliuliza Masumbuko na kumshtua Peter alie kuwa kwenye mawazo .
“ Sikia Masumbuko , utaniuliza baadae sasa hihvi ngoja kuna sehemu naenda maramoja “ aliongea Peter na hapo hapo akatoka hadi nje na hakuchukua gari Zaidi ya kuchukua ufunguo wa honda yake .
“Ngoja na mimi nikazunguke zunguke huko mjini “ Aliongea Masumbuko huku akivaa nguo nyingine na kuchukua buku na kutoka . alitembea mpaka barabarani na kupanda daladala inayoelekea tegeta nyuki kwenda kariakoo “
“ Unaenda wapi?”
“Gari linapo simama “ Alijibu na kuingia ,muonekano wa masumbuko ulikuwa umebadilika kwa kiasi kikubwa kwani alianza kunenepa sio kama alivyo anza kuja, kwani alikuwa akionekana amekauka ngozi ,sasa alikuwa amejaa na kifua utadhaniaa alikuwa anapiga chuma bau kwenda gym
****
MAREKANI (USA)
Katika jiji la Calforinia Alionekana profesa Snart akiwa na mwanaume mmoja hivi mwenye muonekano kama wa kiarabu ndani ya hoteli ijulikanao kwa jina la The Royal iliopo katikati kabisa ya jiji hilo .
“Paco , lete habari za misituu ya amazon .“
“ Mkuu kwanza nafurahi sana kwa kunipa ofa ya kutembelea jiji hili , unajua kutokana na kazi yangu nakuaga sina hata muda wa kufika huku ,kwani hata hali yake ya hewa sio nzuri kama ya kule msituni “
“ Yeah paco upo ndani ya jiji lenye makazi ya watu wengi na shughuli nyingi lazima hali ya hewa iwe tofauti na ya msituni “
“ Yea ni kweli “
“Uliniambia una taarifa muhimu kuhusu Queen ya kuniambia?”
“ Ndio kwanza yuko wapi kwa sasa nataka kumuona kabla sijakueleza taarifa yenyewe “
“Paco , Paco , Queen wa sasa ni mtu maarufu sana na hata nikiuonesha saivi sijui kama utamtambua kama ulivyo kuwa unamuona kule msituni , sasa hivi ni Zaidi ya mrembo “
“ Una maanisha nini kusema hivyo?”
“ Sikia Queen ile ni siraha yangu , yule ni Zaidi ya bomu la nyuklia , kwanza ana akili , hana utu kabisa na pili hajui chochote kuhusu Mungu , na harufu inayo mfurahisha ni kuona damu ya mtu inamwagika muda wote , na pia hana hisia za mapenzi kabisa kama unavyofikiria ni kwamba hawezi kupenda mwanaume yeyote yule , kwani yule muundo wake sio kama wa binadamu wa kawaida , yule nimemtengeneza na nilipata hasara kubwa kwa ajili yake lakinni mpango wangu ulifeli”
“ Una maanisha nini ukisema umemtengeneza Sbart?”
“ Yule hajazaliwa kama wewe ulivyo zaliwa na wazazi wako na pia una ndugu, Queen yule hana ndugu wala wazazi , na kwangu Queen ni kama kifaa changu cha kazi , kwani ninapo agiza kinafanya , sasa nadhani hakuna haja ya kumfatilia sana Queen maana kazi yako ulishamaliza ya kumfundisha Queen , sasa wewe niambie hilo jambo ambalo unataka kuniambia “
“ Ni Kwamba Queen kunamuda nilikuwa kama simuelewi, ni kama anajua kumsoma mtu kila anacho kifikiria akimwangalia tu kwenye macho , kwani wakati nikichukua mazoezi nae alikuwa akinipiga mapigo ambayo hata siyaelewi ,kila pigo nililokuwa nikifikiria kumpiga nalo , ni kama tayarri alikuwa ashajua kile ninacho kifikiria na anakuwa tayari ashajua udhaifu wa pigo langu na anakuwa ananichakaza na kipigo kibaya sana”
“Una maanisha nini kusema hivyo bwana Paco?” Aliongea Snart kwani taarifa hio ilikuwa ni mpya kwake .
“ Mkuu Queen ni hatari sana , kwani ana uwezo ambao sio wa kawaida kama binadamu”
Aliongea bwana Paco ambae ndie alikuwa ni master(mkufunzi wa kimapigano) wa Queen wakati alivyo kuwa nchini brazili kwenye msitu wa amazon , ndie alie kuwa akimfundisha Queen kuua , kwani walikuwa wakienda na kukamata watu na kuwanyonga na kuwachinja bila hata huruma ,nakuwaua wanyama wakali sana kama Anaconda joka anae patikana kwenye msitu huo , Chui na Simba na mafunzo hayo Queen aliyaweza kwa muda mfupi tu.
“Nadhani misheni yangu haikufeli(it was not a failed mission) , Queen atakuwa anaficha uwezo wake inanibidi kufanya utafiti upya. “ Aliongea huku akivaa koti lake la kuingilia maabara yake ndani ya kasri lake ndani ya hapo Calfornia alikuwa akiwaza maneno alioongea Paco mara baada ya kukutana nae hotelini . .
****
Masumbuko alikuja kushushwa na gari katika kituo kimoja kilicho kuwa kina fahamika kama muhimbili na hio ni baada ya kuvutiwa na majengo yalio kuwepo katika eneo hilo ,ndio maana alimwambia konda kuwa keshafika anataka kushushwa.
Alianza kutembea huku akishangaa majengo hayo na muda huo ulikuwa ni saa kumi inaenda kama na robo hivi , alinyooshana kinjia flani kinapandisha kwenda juu kwani kulikuwa na kijimlima na kutokezea kwenye barabara mbele huko kwenye mtaa mmoja ujulikanao kwa jina la mindu, alinyoosha na bara bara hiio na kuja kufika sehemu moja kwa mbele yake kulikuwa kukinekana mwendokasi inazunguka na kuna kibao kikubwa kilicho andikwa ‘HOSPITALI YA MUHIMBILI’.
“Mama hivi ni vidude gani?” Aliongea Masumbuko baada ya kufika kwa mama mmoja alie kuwa akiuza koni , sasa Masumbuko aliona vile vya kuwekea koni ndivyo alivyo kuwa akiulizia.
“Ni koni hizi ni miatano tu moja “
“ Hii inatosha alitoa Masumbuko mia nne na kumuonesha yule mama , na hi ni hela alio rudishiwa chenchi kwenye ile buku (elfu moja)ya nauli maana gharama za usafiri ilikuwa ni mia sita na hapo alitoa yote na mama yule ampatia .
“ Kumbe tamu hivi nitakuwa nakutembelea mara kwa mara “
“ Sawa lakini siku nyingine nitakuuzia kwa miatano “
“ Sawa “
Aliongea huku akitemeba huku na huko akishangaa shangaa mpaka inatimia saa kumi na moja na nusu alijikuta amezunguka amezunguka na kurudi pale pale muhimbili , Alipanda gari bila ya kujiuliza ana nauli ,gari alio panda ilikuwa inaenda Masaki na ilikuwa imejaza kweli na Masumbuko aliwekwa mwisho kabisa ya gari kiasi kwamba kwa jiinsi watu walivyo kuwa wamejaa hata konda ingekuwa ni vigumu kwake kupita na kuomba nauli.
“ Hivi ule mtaa tunao kaa unaitwaje?”Alikuwa akijiuliza kwenye gari huku linaondoka maana hakujua ile sehemu jina.
“Ila nitapaona tu halafu nitashuka”
Sasa konda kwakuwa nafasi ilikuwa imebana sana , alikuwakichukua nauli kila unapo shuka.
“Macho ,Macho hio , kuna anaeshuka ?”Aliongea konda na hapo hapo Masumbuko akaropoka kwa sauti nimefika mpaka watu wakamwangalia.
“Njoo sasa umekaa huko nyuma halafu unajua unashukia hapa karibu”
Aliongea konda baada ya gari kusimama huku Masumbuko aliependeza akishuka , kwa jinsi alivyo kuwa amependeza usingedhania kuwa wakati huo hakuwa na kitu chochote mfukoni hata nauli .
“Toa hela , unapoteza muda bwana , unashangaa nini?” Masumbuko alimwangalia yule konda huku akiwaza afanye kama kawaida yake maana alijua nauli hana .
“Usijali nitamlipia” ilisikika sauti moja nyororo na kufanya hata wale walio kuwa kwenye daladala wamwangalie anaeongea , lakini ni kwamba tayari alikuwa ashachelewa maana Masimbuko ashachezesha jicho tayari na kumpachika masaa mawili ya kumbukumbu.
“Aaa.. aa hapana . ashalipa tayari mremboo hata usisumbuke ” Aliongea konda huku akigwaya gwaya na kufanya abiria waanze kucheka na hata dereva mwenyewe alijikuta akicheka na hapo ndipo ikawa gumzo kwenye daladala maana wengi walijua konda alichanganyikiwa na yule mrembo na ndio maana alikubali Masumbuko kashalipa, wengi walimhurumia pasina kujua uwezo Masumbuko. .
“Sema ni haki yake aisee , unajua yule mwanake ni mrembo sijapata ona .. na kwa ile sauti konda ni haki yake kuchanganyikiwa , ila kanifurahisha sana leo
.. hakuna mwanaume mjanja mbele ya utamu “ Aliongea jamaa mmoja lio kuwa amevaa kanzu kasimama kwenye daladala hio alikuwa na rafudhi ya kipemba .
“Nyie mnaongea nini nyie , mimi siwezi kuchanganywa na mwanamke, yule chalii kalipa kabisa nina uhakika.” Aliongea konda na hapo ndipo vicheko vilivyo zidi kabisaa
“Aisee nilikuwa na stress ila zishaisha daah .. aisee” Aliongea jamaa mmoja nae alieshikilia mfuko mdogo hivi uliokuwa na samaki akionekana kufurahishwa sana na hilo tukio.
****
Peter alisimamisha honda yake kwenye nyumba moja maeneo ya makongo juu na kisha akabonyeza kengele na hapo mlinzi alifungua
“Bwana Peter karibu sanaaa..” Aliongea mlinzi alionekana kumfahamu Peter
“Nimemkuta Steve?”
“Ndio yupo hajatoka leo “
Basi Peter alienda moja kwa moja mpaka ndani ya nyumba hio ilikuwa nzuri sana kwa jinsi ilivyojengwa.
“Mwanagu huyo , nona leo umekuja kutusalimia?”
“Ndio mama shikamoo “
Huku wakisalimiana kwa furaha na huyo mama aliononekana kuwa mkarimu kweli , alikuwa mnene kiasi mfupi alievalia dera lililoacha mabega wazi.
“Nimemfata Steve “ Aliongea Peter na kuambiwa kuwa yupo chumbni kwake aende tu.
“ Mzee mwenyewe naona usharudi karibu”
“Yeah mzee , nimerudi, nina mawazo nikona nije kabisa nisikusumbue kwa kukuita magetoni”
“Mawazo gani tena mzee si umetoka safarini?”
“Mambo ya kisasi mzee, naona kama kigumu vile kutekelezeka , unajua nilikuwa nachukulia simple sana ila sasa na uona ugumu wake”
“Ugumu gani sasa wewe si ulikuwa wajisifia kuwa unaswaga nyingi kibao , tantalila nyingii sasa umepigwa kibuti ndio unaona ugumu “
“Si hivyo ndugu yangu , simaanishi hvyo yaani bora hata ningepigwa hiko kibuti , lakini sasa hivi nishamla mke wa Samir tayari na mtoto wake kanambia ananipenda na anasubiria jjibu langu”
“ Unasema ushakula kitumbua cha lile limama tayari na lile lishepu “ Aliongea Steve kama haamini vile kwani aliona kama masihala vile , kwa maneno alio kuwa akizungumza . na wakati wanaongea ndio hapo , simu ya Peter ilitoa mlio kuwa ilikuwa inaita .
“ Oya huyu hapa anapiga kama huamini ngoja niweke loud speaker” Aliongea huku akipokea na kuweka loudspeaker .
SEHEMU YA 23
Peter aliweka simu ile kwenye loudspeaker baada tu ya kupokea na kuanza kuongea na Mama Rania.
“Vipi mpenzi mbona unachelewa kupokea simu?” Ilisikika sauti iliokuwa ikilalama na kumfanya Steve kutoa jicho kama kabanwa na mlango kwani hakuamini kabisa kile anacho kisikia , na sio kama jambo hilo ni geni kwake kuona kijana kufanywa kiben ten , lakini hadhi na heshima alio kuwa nayo mama huyo ni vitu ambavyo kwake aliona kama ajabu vile.
“Nilikuwa nipo chumbani simu niliacha living room (sebuleni) “ Aliongea uongo Peter.
“ Jamani mpenzi unajua nilivyo kumiss , natamani sana tukutane hata twende mzunguko mmoja “ Aliongea Mama Rania .
Laiti angejua kuwa amewekewa loudspeaker asingeongea hilo neno , Peter hakutaka Steve aendelee kusikiliza , alitoa loudspeaker na kulala kabisa kitandani na kuanza kuongea huku Steve yeye alikuwa amesimama kama mnara akimwangalia rafiki yake , na kuna kitu alikuwa ashakigundua kwa Peter alikuwa ameona dalili zote za rafiki yake kuonogewa , alikuwa mzoefu wa hayo mambo .
“Daah..! unajua ni hatari hio rafiki yangu”
“ Naelewa , ila Steve yaani kila nikiongea na huyu mwanamke dudu inasoma channeli hapo hapo na mawazo yangu yanabadilika”.
“Fanaleki ushanogewa wewe , na hivyo ni mwanamke wako wa kwanza kazi unayo , mimi naogopa tu mume wake akijua sijui atakufanyaje, naogopa sana ukiingia kwenye matatizo”
“Steve ndio maana nipo hapa unipe ushauri wewe ni rafiki yangu naamini utanipa ushauri mzuri”
“Sasa wewe unataka mimi ni kwambie nini na wakati wewe mwenyewe ulisema unaenda kwenye ile benki kwa ajili ya kisasi ,lakini saivi unaonekana umenogewa tayari , mimi nakushauri uache kabisa hio misheni yako , lakini kuhusu huyo Rania na mama yake , kaa chini fikiria , jiulize maamuzi utakayo fikiria na kuamua yatakuwa na madhara gani ukishalijua hilo basi mimi sitoingilia maamuzi yako ,lakini nakupa hint tu , kwamba unacho kifanya sio kizuri na ni hatari sana ,mke wa mtu sumu ndugu yangu”
“Poa mzee mimi nitafikiria cha kufanya , ila asante sana kwa maneno yako , ngoja nirudi home ni muwahi Masumbuko” Aliaga na Steve alimsindikiza mwenzie.
****
Nasma baada ya kukaa siku kama nne nyumbni kwao , hatimae aliamua kuondoka na kurejea sehemu alio kuwa akiishi , japo ya Rania kumbembeleza sana kuhusu kubaki kwani ana ichangamsha familia , lakini hakukubali na mama yake pia alijaribu kumshawishi lakini alisimamia msimamo wake .
Alipanda kwenye gari yake na siku hio alikuwa akiendesha yeye mwenyewe pasipo ya kuwa na Lucy mfanyakazi wake , aliendesha gari lake mpaka kufikia maeneo ya Macho , sasa wakati yuko kakodoa macho barabarani kionyesha umakini katika barabara hio ndipo daladala ilio kuwa ikija upande wake ilisimama mita chache mbele yake , hapo ndipo mapigo yake ya moyo na mshangao kwa ujumla vikamtawala, kwani mwanaume alie kuwa akimuota usiku na mchana alimuona kabisa mbele yake , kwanza aliona kama kamfananisha lakini kadri alivyo sogelea gari lile ndipo alipo kuja kugundua kuwa ni yeye.
Alipita daladala ile na kisha kasimamisha kwa mbele na kutoka haraka haraka huku akiwa kabisa amesahau kufunga hata mlango na kukimbilia sehemu ile , ndipo alipogundua kuwa mwanaume yule hana nauli na alikimbia na kisha kumwambia konda kuwa atamlipia , lakini kilichomshangaza kwa mara ya pili kwani mara ya kwanza jambo kama hilo lilikuwa likitokea tena ,pale konda alipomuambia kuwa ashalipa na wakati kwa masikio yake kabisa alisikia konda huo akimdai Masumbuko nauli , lakini kutokana na hamu yake kubwa ilikuwa ni kumuona Masumbuko aliachana na hilo swala na kisha kumsalimia .
“Mambo!” Alisalimia kwa shauku kubwa Nasma huku akimwangalia Masumbuko ambae wala hakuwa hata na time nae kwani alikuwa bado akishangaa hayo maeneo kana kwamba ataiona nyumba wanayoishi .
“Hivi sista naomba nikuulize , hivi unajua eneo ambalo lina magorofa magorofa machache halafu .. halafuu.. enhee .. kuna shule halafu na barabara .. halafu..nini tenaa.. kwa mbele kabisa kuna kanisa kubwa .. unaijua hio sehemu?”
Aliongea Masumbuko huku akionekana kabisa yuko seriasi na swali lake na kwa Nasma alikuwa akishangaa maana swali lenyewe hajalielewa .
.“Mambo kwanza” Aliendelea kusalimia Nasma kwani kwanza alikuwa ana aibu na hata hapo alikuwa hajui afanye , kwani ni kweli alikuwa akihitaji kuonana na Masumbuko lakini hakuwahi kufikiria siku akionana nae ataanza anza vipi kuongea nae na ndio maana aliendelea kusalimia lakini kwa masumbuko wala hakuwa na habari kichwa chake wakati huo kiliwaza nyumbani tu.
“Ila hapa sio penyewe hapa , sijui patakuwa ni upande gani ule . halafu .. , dada mbona haunijibu sasa “
“Sijakuelewa “
“ Ni kweli huwezi kuelewa maana nina maswali magumu” Huku akiondoka na kumfanya Nasma amwangalie Masumbuko akichapa raba hana hata habari kuwa mtu alie mfuata alikuwa akikesha usiku na mchana kumtafuta na kumuwazia alijikuta chozi likimdondoka bila hata ya kujua .. sasa wakati ameduaa akimwangalia Masumbuko ndipo alipo kuja kama kuzinduka na kuita
“Kaka , nisubiri” Masumbukoo alisimama na kumwangalia Nasma anae mkimbila .. na kwa jinsi alivyokuwa akimkimbilia kwa mapozi na uzuri wake na jinsi Masumbuko alivyo kuwa akumwangalia ilikuwa ina pendeza kama vile ni filamu za kihindi.
“Nimepajua hio sehemu ulio kuwa unasema”
“ Kweli … kuna kanisa .. kuna shule kwa nyuma na barabara katikati … si ndio ni hapo”
“Ndio “
Jibu hilo lilimfanya Masumbuko aachie tabasamu na kuufanya uhendsome wake uonekane na kumfanya Nasma amwangalie kama anamshangaa ..
“Twende kwenye gari .. nikupeleke “ Masumbuko hakuleta shida kwani hi ndio jambo ambalo lilikuwa likimpa shida kwa wakati huo na hivyo alimchukulia Nasma kama mtu ambae anaweza kumpatia msaada .
Basi aliingia kwenye gari na safari ikaanza na kwa Nasma kwakuwa alikuwa ana kichwa chepesi sana kuelewa ni kwamba aligundua kuwa Masumbuko yuko , kwenye hali ya wasiwasi na ndio maana hakuwa akimpa ushirikiano .
“Kwa hio kaka ulikuwa umepotea?”
“ Ndio mimi ni mgeni na haya maeneo “ Aliongea Masumbuko huku akiangalia nje ya gari na muda huo kajigiza kalikuwa kashaanza kuingia , na kuna wakati Nasma alikuwa akimwangalia Masumbuko kwenye kioo .. aliishia kutabasamu tu na alionekana moyo wake kuwa na Amani na furaha sana . Kwani aliamini mwanaume alie kuwa akimtafuta hatimae amempata .
“Hapo hapo nimepaona simamisha gari “ Aliongea Msumbuko kwa sauti na kumfanya Nasama asimamishe gari na masumbuko kuomba kufunguliwa mlango , na Nasma alipo mfungulia tu tayari alikuwa ameshatoka tayari kwenye gari .
“ Dada asante sana .. nimepafahamu ni hapa kabisa “ Aliongea Msumbuko na kwa wakati huo walikuwa washafika eneo la Mbezi Beach ilikuwa ni bahati kwa masumbuko kwani isingekuwa Nasma kuishi hayo maeneo asingeweza kurudi nyumbani. .
Masumbuko alindoka huku akisubiria kuvuka barabara na kumfanya Nasma na yeye kutoka kwenye gari na kumfuata Masumbuko kwa nyuma hakutaka kumpoteza tena , lakini kilichomshangaza Nasma ni kwamba nyumba alio ingia Masumbuko ni nyumba ya pili na ya kwake ilipo.
“Yaani kumbe huyu mkaka kumtafuta kote kule kumbe ni jirani yangu “ Aliongea Nasma huku akijikuta akitabasamu tu nakuona kuwa mageti muda mwingine yanakuwa hayasaidii maana yanafanya usijuane na majirani, alikaa kama dakika kama tano akiangalia nyumba hio ilioenda hewani kwa gorofa nne na kisha akatoka akafara gari yake na kwenda hapo mpaka kwenye nyumba yake na kuingia na kisha akampa mlinzi ufunguo akimwambia akachukue gari ameliacha kituoni , mlinzi alishangaa ila alichukua ufunguo kwani hakuruhusiwa kuuliza swali .
***
“Ulikuwa umeenda wapi umenifanya niwe kwenye wakti mgumu kiasi hicho “ Aliongea Peter huku akionekana kuwa na wasiwasi sana .
“ Nilienda kula bata kidogo ndio nimerudi “
“Nikajua umepotea huko njiani . inabidi kesho nikakununulie simu “
“Mimi siwezi kupotea ni mgeni lakini nayajua maeneo vizuri”Aliongea Masumbuko na kumfanya Peter atabasamu na alichogundua alijua kuwa Masumbuko alikuwa akipenda sana kujisifia .
“ Haya lakini usitoke toke tu utapotea au kugongwa na gari huko ndugu yangu , unafikiri nitaishije “
Aliongea na kuachana na Masumbuko kwani alijua pia ni mtu mzima hatakiwa kumlinda ila anatakiwa kumuonyesha mazingira na kumtembeza tembeza ili asipotee.
*****
Siku ilio fuata Peter hakwenda kazini na alibaki nyumbni kwani alikuwa amepewa siku mbili za kubaki nyumbani , kwenye muda wa saa kumi na moja ndio muda ambao Peter alipigiwa simu na Mama Rania kuwa wakutane barabarani kwenye kanisa la KKKT usharika wa Mbezi Beach .
Peter alivaa vizuri na kisha akatoka zake baada ya kumuaga Masumbuko ambae alikuwa akichezea simu ambayo amenunnuliwa asubuhi hio
“Peter aliingia kwenye gari yake , maana Mama Rania alimwambia kuwa aje na gari yake , baada ya kufika tu kweli alimuona Mama Rania aliekuwa amevalia gauni flani lenye mikanda huku akiwa ameshikilia pochi kubwa na alikuwa amependeza kweli ,kwa jjinsi alivyokuwa akionekana utadhani ni mwanmke ambae anaenda dating kwa mara ya kwanza , Peter alienda kufunga beki kwenye miguu ya mama huyo na kufungua kioo na kumfanya Mama Rania atabasamu na kuingia kwenye gari na kisha likaondoshwa na kwa maelekezo ya Mama Rania walikuja kukunja baada ya kufika eneo moja linaitwa jogoo na kuchukua upande wa kulia na gari ilitembea kwa dakika kadhaa na ikasimama nje ya geti kubwa na baada ya dakika kadhaa gari hio iliingizwa ndani ya jumba hilo , hapo ndipo Peter alipo patwa na mshangao kwani jumba hilo lilikuwa moja ya jumba kubwa sana na lilikuwa na mazingira mazuri kwani kulikuwa na swiming pool upande wa kushoto ukiingia ilio zungukwa na bustani na majani yalio chongwa kwa ustadi mkubwa sana , jengo hilo limepakwa rangi ya kuvutia nyeupe lakini ilio fifia na kupendeza sana .
“ Kwanini tuko hapa?” Aliuliza Peter maana alikuwa akiona mapicha picha tu .
“Hii ndio itakuwa nyumba yako mpenzi ‘ Aliongea Mama Rania .
“ Whaat.. usiniambie kuwa umeinunua hii”
“Sijainunua leo wala jana ilikuwa ni yangu ,japo hakuna mwanafamilia anae ijua na sasa nasema nyumba hii ni ya kwako mpenzi wangu na tutakuwa tunakutana hapa unipe vitu” Aliongea Mama Rania na kumfanya Peter moyo upige kwa nguvu kwani hakuamini kuwa jumba hilo ni la kwake alianza kuona faida za kutoka na majimama..
“Mimi bado hata sijasadiki kabisa “ Aliongea Peter na Mama Rania akaachia tabasamua na kumshika mkono Peter na kisha kumvuta na wakaingia ndani .
“Chukua hio bahasha mpenzi ‘ Aliongea Mama Rania na kumfanya Peter aisogelee hio bahasha na kuifungua na ilikuwa ni hati ya nyumba na jina lake ndilo lili kuwa ndani ya hio hati .
“Peter nayafanya haya yote kwaku nakupenda na sitotaka unisaliti , nitakupa chochote utakacho kitaka , ila nakuomba usinisaliti”
Peter hakujibu Zaidi ya kumsogelea mama huyo na kuanza kupigana naye mabusu na kisha wakaanza kazi na kitu alicho pewa Mama Rania siku hio alijikuta kama yuko kwenye dunia nyingine kabisa na hakuwa kwenye ulimwengu halisi .
Walidumu kwa masaa kadhaa na kisha wakarudia tena na tena na tena na kujikuta wakipitiwa na usingizi kabisa tena wakiwa sebleni .
****
Peter alianza kukolea kwenye penzi la Mama Rania au bosi wake , japo walikuwa wakifanya mambo yao kwa siri sana na hakuna mtu hata mmoja ambae aliweza kujua kuwa wawili hao walikuwa wapenzi, kwani walikuwa wakiwekeana heshima feki wakiwa kwenye kazi , lakini wakitoka nje ya kazi walikuwa wapenzi.
Huku kwa Rania nako mambo yalizidi kuwa magumu kwani , kwani alikufa na kuoza kwa Peter , alitamani sana kuwa karibu na Peter kila saa na hata wakati mwingine Mama Rania alianza kuogopa, kwani kwa macho ambayo mwanae alikuwa akimwangalia Peter hayakuwa yakawaida, zilipita kama wiki mbili hivi ndipo Peter na Rania wote waliacha kufika kazini kutokana na chuoni mitihani ilikuwa inakaribia na walitakiwa kujiandaa .
Sasa hapo ndipo ukaribu wa Peter na na Rania kuongezeka kwani walikuwa wakisoma wote chuo kimoja na ilikuwa Rania akitoka mapema kwenye kipindi na Peter akiwa bado hajatoka basi atamsubiri mpaka atoke na waongozane wote , kunywa chai ama kula.
Rania alizidi kumzoea Peter kiasi kwamba kila siku , kila saa na kila sekunde alitamani kumuona Peter tu , kwa upende wa Peter jinsi Rania alivyo kuwa akimuonyeshea mapenzi , basi alizidi kuwa na mawazo juu ya rania , yeye , kila alivyo kuwa karibu ya Rania alijikuta moyo wake kumpenda sana Rania.
Alitamani atamke neno nakupenda ili myo wake utulie lakini hakuweza hilo , kwani kila alipo kumbuka kuwa tayari ana mahusiano na mama yake basi hakutaka kabisa kumuumiza rania huko mbeleni pindi atakapoujua ukweli , kuna muda alikaa chini na kuyafikiria matendo yake aliona kabisa kile kisasi katika kichwa chake kinaanza kusahalulika kabisa , kwani mpango wake ulikuwa ni kumfanya Samir atoe machozi kwakitendo ambachoo alikwisha kumfanyia.
Siku moja wakati Peter anatoka chuo akitembea na rafiki yake Steve , ndipo Rania alipo kuja kumuita na kumwambia kuwa kuna jambo anataka kuongea nae na ni muhimu kwake , basi Peter japo aliogopa kile alicho kuwa anaenda kuambiwa na Rania ila alijikaza na kuondoka na Rania mpaka kwenye gari lake .
“Peter najua kama ujumbe wangu nilio kuandikia uliona?”
“Ndio niliuona Rania “ alijibu Peter huku moyo ukipiga kwa nguvu .
“Peter nataka kujua jibu kwani nimeshindwa tena kusubiria naomba nisikie jibu lako leo”
Aliongea Rania hapo nakumfanya Peter jasho limtoke kwani hapo alikuwa amebanwa sehemu yenyewe .
“Rania najua unanipenda sana na mimi sitaki kukuficha nakupenda sana ila kwasasa sitaki kuanzisha mahusiano maana akili yangu haipo sawa na sijajiandaa kisaikolojia kabisa , na wewe ni mwanamke wa kipekee naomba muda niweke mambo yanguu sawa halafu nitakuambia Rania please, sitaki kuja kukuumiza kwa kutokuwajibika maana mahusiano ni uwajibikaji baina ya wapenzi” Aliongea Peter kwa hisia na ukimtazama hutoamini kama ni yule ambae alikuwa anataka kulipiza kisasi , mapenzi yameyeyusha kila kitu na kilicho baki kwenye moyo wake ni hisia za uhitaji tu , japo alijitahidi sana kutokumpenda Rania lakini ni kwamba alikuwa akijidanganya kwani kadri alivyo kuwa akimfosi atoke kwenye moyo wake ndivyo alivyo kuwa akizidi kumpenda.
“Sawa Peter nitasubiri , ila jua wewe ndio mwanume wangu wa kwanza kukupenda kwa kiasi hiki , nakupenda Peter “ Aliongea Rania mpaka chozi linamtoka mtoto wa kike na kumfanya Peter moyo umuume sana , alijkuta akimkumbatia .
“ Nakupenda Sana Rania , nakupenda sana ila naomba univumilie sawa “ aliongea Peter huku akimwangalia usoni na Rania akakubali kwa kichwa kuwa amekubaliana nae , na Peter alitoka kwenye hilo gari baada ya simu yake kutoa mlio ikionyesha kabisa kuwa inaita na mpigaji alikuwa ni Mama rania. .
Shida moja alio kuwa nayo Peter ni kwamba kila anpo ongea na Mama Rania mwili wake ulikuwa ukimsisimka sana na kuhitaji kufanya ngono .
Peter aliongea na Mama Rania na waliahidiana kuwa wakutane bila kukosa siku hio wakapeane dudu , na Peter hakupindua alikubali , maana kwa wakati huo na yeye alikuwa akipenda sana kitumbua cha mama rania .
****
Upande wa Najma nae mambo yalikuwa mambo kwani kila siku alikua akimfikiria tu mwanaume anae mfahamu kwa sura , japo maswala yake ya kufungua kampuni yake ya urembo yalikuwa yakimfanya kuwa bize sana , ila hakumsahau Peter hata mara moja .
Alikuwa akiamini kuwa lazima atamuona tu , wanaume walimtongoza kila kukicha lakini hakuna aliepewa nafasi hata mmoja hata ya kumshika tu hakuna alie pewa nafasi hio , watu na pesa zao walimchombeza kwa hongo lakini mwandada hakuteteleka , alikuwa akimuwaza Peter .
Upande wa Nasma na yeye alikuwa ashajua Masumbuko anapo kaa lakini kilicho kuwa kikimsumbua ni kwamba alikuwa na aibu na pia hakutaka kujilasisha kwa Masumbuko .
Kuna kipindi alikuwa ni kama mtoto kwani alikuwa akienda mpaka katka geti la Masumbuko kwa ajili ya kugonga lakini aliishia kurudi tu kwani hakukua na sababu ya kumuona Masumbuko na alifikiria kuwa akimuona atamwambiaje kwani alikuwa na aibu sana .
Masumbuko yeye muda wote alikuwa akiwazia ni kwa jinsi gani atakuwa na uwezo wa mnara wake kusoma channel kwani , kwa jinsi alivyo kuwa akijua na uwezo wake wa kufikiria ulipooishia ni kuangalia filamu za ngono tu huku akijifaliji kuwa utaamka tu .
“Utasimama tu “Aliongea huku akiuchezea uume wake
******
“Boss nimegundua Madam anapo elekea “ Ilisikika saiti kwnye simu Samir akiwa ofisini
“ Endelea kumfatilia na kila kinacho endelea utaniambia “
“ Sawa boss “
Samir ni kama kibao kilikuwa kimemgeukia kwani alikuwa hamuelewi kabisa mke wake , kwani hakumsubiri tena kama zamani wakati yeye akichelewa , kwani kila alipo rudi alimkuta mke wake alishapotelea kwenye usingizi mzito na wala hakuwa na habari na hata akiamka , alikuwa haulizi chochote na kilicho kuwa kikimuuma sana Samir ni kwamba hata ile mke wake kuomba gemu aliacha kabisa , na pia mke wake hakuwa hata na mawazo kama mwanzoni na alionekana kuwa mwenye furaha.
Hapo ndipo Samir alipoanza kurudi nyumbni mapema kama zamani , na kurudisha mapenzi kwa mkewe , lakini ni kwamba Mama Rania alionesha hali ya kutokuwa kabisa na time na yeye na mara nyingi usiku alionekana akichat na simu huku akitabasamu jambo ambalo lilianza kumfanya kuwa na wivu na kuona kabisa kuwa mkewe kashapata mchepuko , kila akizifikiria hisia hizo alijikuta akipandwa na wivu mkali sana na kumchoma , alivumilia sana lakini kuna siku alijikuta akikosa uvumilivu na alitaka kujua kile kinacho endelea na aliapia kama atagundua kuna mwanaume anaetoka na mke wake kimapenzi ange muua , swala hilo lilimnyima usingizi kabisa
Siku aliojikuta roho kumuuma na kujihisi kuna ninja anakata kata vipande kwenye tumbo lake ni siku alio omba tendo kwa Mama Rania , kwani ile ana peleka mkono kumshikashika Mama Rania , mkono ulitolewa na Mama Rania akainua kichwa na kumwambia neno moja tu .
“ Naomba usinisumbue nimechoka nina mambo mengi ya kufikiria natakiwa kulala mapema “
Alijikuta akiipandwa ma hasira na kukosa hata hamu ya kulala hapo ndani kwake na alicho kifanya ni kutoka usiku huo huo na kwenda bar .
Na kuanzia siku hio alikuwa akimuinda sana Mama Rania ili apate kujua mwanaume anae toka na mke wake na kwa upande wa Mama Rania alikuwa akiwaza dudu ya kijana Peter tu masaa yote kwani kila akifikiria dudu ya kijana Peter inavyo muingia na utamu anao usikiaga basi mizuka ilikuwa ikimpanda hapo hapo na hata kazi hakuweza kufanya vizuri .
Basi siku ambayo Mama Rania alipanga kukutana na Peter muda wa saa tisa , ndio muda ambao kijana wa boss Samir alikuwa akimfatilia nyuma kwa siri sana .
SEHEMU YA 24
Mama rania wala hakuwa na wasiwasi wakufatiliwa kwani aliendesha gari yake kuelekea upande wa Tegeta ambako ndio kulikuwa na nyumba ambayo amemnunulia Peter kama zawaidi ya kupewa dudu.
Lakini pasipo kujua kuwa kuna mtu anamfatilia nyuma aliendesha gari yake na kwa wakati huo ndio alikuwa anapita mwenge huku kijana aliepewa kazi na Samir alihakikisha kuwa hampotezi kabisa mama huyo kwani alielewa nini maana ya kile kitakacho tokea kama tu atakuja kumpoteza kwene macho yake na ndio maana alikuwa akiendesha karibu kabisa na gari ya Mama Rania na hakutaka kuipita , kwani ilivyo kuwa ikipunguza mwendo na yeye alikuwa akipunguza mwendo na huyu alie kuwa akimfatilia alikuwa si mwingine ila ni Kadabra , kijana machachali kabisa kwenye kazi hio ya kufatilia watu , kwani hio ndio kazi yake kubwa ambayo ilikuwa ikimuweka mjini kazi ya Ubodigadi na kufatilia watu .
Mama rania alipita lugalo yote na kuingia Mbezi Beach huku Kadabra akiwa nyuma , lakini ilipo karibia karibu na kanisa la Mbezi Beach la kilutheri gari ya Mama Rania ilikata kulia na kuelekea upande kama unaelekea shule ya sekondari Mbezi Beach , upande ambao ulikuwa ndio maeneo ambayo Peter na Nasma walikuwa wakikaa, Mama Rania aliendesha gari na kuja kuingia kwenye nyumba ya Peter , na wakati gari ikiingia sehemu hio na Kadabra alikuwa akipita geti hilo kwa mwendo wa taratibu sana huku akikodolea geti hilo macho na kwenda kusimama mbele kabisa na kutoka huku akijifanya anaongea na simu , lakini hakukaa sana gari ya Mama Rania , ilitoka na taratibu na kisha ikachukua njia ya kulekea Tegeta na Kadabra hakutaka kupoteza muda alikimbilia gari yake na kisha kuingia harakaharaka na kuliwasha na kisha kuliungia gari la Mama Rania na uzuri ni kwamba aliliona kabisa na lilikuwa karibu yake , baada ya kufikia eneo la jogoo gari lilikunja kulia na kisha likatembea mita chche kutoka barabara kuu na hatimae likaja kusimama kwenye ile nyumba na Mama Rania na gari ,Kadabra aliishuhudia kabisa ikiingia na hapo ndipo alipo alipo toa simu yake na kumpigia Samir na lilisikika neno moja tu.
“ subiri hapo hapo nina kuja , nataka nikiua unisaidie kutoa hio mizoga”.
Samir alikuwa na hasira kweli na wivu ulikuwa umemkaba kooni ,yaani hata kuhema ilikuwa ni shida kwani kila alipo fikiria swala la mke wake kuwa na mchepuko kiasi cha yeye kudharauliwa ,kilimuuma sana tena Zaidi ya kuuma , kwani hata chakula kila siku alipo kuwa akila kilikuwa hata sio kitamu kwake.
Samir alijikuta akipandwa na hasira mara mbili baada ya kusikia mke wake kaingia kwenye nyumba ambayohaifahamu aliishia kutoa matusi ya nguoni na kisha akachukua bastola yake na kuiweka kiunoni na kisha kutoka hapo na alipishana na secretary wake alie shika mafaili alijaribu kumsimamisha lakini hata sijui alisikia kwa wakati huo kwani akili yake kwa muda huo ilikuwa ikiongozwa na hisia , alipanda gari na kulitoa ofisini hapo kwa spidi ya ajabau mpaka mlinzi akamshangaa bosss wake .
Samiri alitembea na gari isivyo kawaida , na aliishia kutukana tu madereva ambao walikuwa hawataki kumpisha , kuna mdada mmoja alikuwa akiendesha Spacio , yake na Samir alikuwa akimpigia honi kumpisha , lakini mdada huyo wala hakujali , sasa Samiri alipo pata nafasi upande mwingine ya kupita , alimwangalia mdada huyo na huku mdada huyo akimwangalia , na Samir aliishia kumnyooshea kidolea cha kati akimtusi na dada yule aaliishia kusikitika tu.
Baada ya kama dakika ishirini hivi Samir alikuwa ndio anaingia sehemu alio elekezwa na Kadabra
“Ndio Hapa” Aliuliza Samir kwa jazba huku akilisogelea geti ,lakini kadabra alimzuia
“ Boss utawashitua ,sisi tunataka tuone kinacho endelea” Aliongea Kadabra
“Sasa tunafanyaje”
“Ngoja nikuoneshe”
Kadabra aliilisogelea lile geti na kuliangalia na kisha kugonga mlango mdogo kwa stali ya chini kabisa ambayo haileti bughuza na hakutumia kengele , ila yeye aligonga geti hilo na ndani ya dakika moja ndipo walipo sikia komeo likifunguliwa na kajidirisha kadogo kakafunguliwa na akatokea mlinzi.
“Niwasaidie nini?” aliuliza na kumfanya kadabra aangalie upande wa kulia na kushoto na kungalia uwepo wa watu .
“Boss Wangu pale ana shida na wewe .. kuna vitu anataka akuulize” Aliongea Kadabra huku akitoa waleti yake na kumuonesha mlinzi kuwa kazi hio ina malipo .
Mlinzi alivyo ona pesa , hakuzubaa alifungua kageti haraharaka na kisha kutoka ,lakini ni kama kosa kwake kwani ile anafungua tayari Kadabra ashamsogelea kwa staili ya kupiga roba na kumkaba kwa nyuma yule mlinzi na kisha kuingia nae ndani ya geti na kwenda kumtuliza kwenye kibanda chake baada ya kupoteza fahamu na Kadabra , alimwita Samir kwa ishara na hapo Samir akingia na geti likafungwa kabisa na funguo .
Samir mapigo yake yalikuwa yanapiga kwa nguvu kwani katika maisha yake hajawahi kufumania , kwani alikuwa akizisikia tu hizo habari za watu kufumania wake zao lakini hajawahi kukutwa na msala kama huo wa yeye kumfumania mtu tena mke wake , alisogea huku akjihisi kama presha inapanda kwa kiasi kikubwa hasa alipo kuwa akisikia sauti za mahaba kutoka ndani na kwa namna moja alijua kabisa watu hao wako sebleni wanafanya yao .
“Aisiiiii…eeeh… mpenziii… nakupenda… agha…. Nakuja mpenzi ..,. usichomoe mwagia humo humoo .. mpenziii.. aaa…”
Alijikuta roho ikimuuma sana na hasira zikizidi kumjaa na kukosa uvumilivu kabisa , kwani sauti za mahaba alizo sikia tena akisikia kabisa mwagia humoo humo alijikuta presha na roho ya mauji vikimpanda na alikosa kabisa uvumilivu , aalisukuma mlango ambao ulikuwa haujafungwa vizuri na kuingia kama mwanajeshi na kuachia risasii.. akimlenga mwanaume aliekuwa akionekana uchi akishusha kiuno na kupandisha.
“Paa..” Ulikuwa ni mvumo wa risasi uliosikikakwa nguvu
****
Nasma alikuwa amekaa sebleni huku akionekana kuwa kuna jambo ambalo alikuwa akilifikiria na jambo hilo lilikuwa likimhusu Masumbuko , japo tokea waachane siku ile kwenye gari , pasipo kuongea jambo lolote lakini kuna jambo ambalo alikuwa akiliona kwa Masumbuko kama haliko sawa , na muda huo alikuwa akijaribu kuunganisha matukio na kuona kweli kuna kitu kipo kwa Masumbuko na kitu hicho alikuwa akitamani sana kukifahamu .
“Ila mimi ni mjinga sana yaani mtu yuko jirani yangu nasumbuka kichwa changu tu hapa” Aliongea Nasma na kumfanya Lucy aliekuwa kakaa kwenye sofa kwa kujiachia akiangalia tv amwangalie.
“Nini Nasma , unaongea na mimi ?”
“Hapana , kuna sehemu naenda hapo nje nakuja sasa hivi”
“Niagize mimi nitaenda kukuchukulia , hakuna haja ya wewe kwenda”
“Nimetaka kwenda mwenyewe Lucy wee kaa hapo nakuja” Aliongea Nasma na kisha akatoka na kutembea mpaka kwenye geti la nyumba ambayo anaishi Masumbuko , aligonga na kisha alikuja mlinzi na kufungua na kumuuliza maswali na kisha aliruhusiwa kuingia.
“Samahani naulizia floor ambayo anaishi mkaka fulani hivi mweusi rangi ya chocholate” Aliuliza baada ya kuingia ndani hapo na kuwakuta Anjeli na marafiki zake wakipiga stori .
“Mhmh , hapa kuna wengi , lakinii.. hebu nenda namba nne “ Aliongea Angeli huku wote wakimwangalia Nasma kwa uzuri alio kuwa nao.
“Jamani kuna wadada wazuri .. akii..Mungu ningekuwa mimi ningekuwa danga la jiji hili lote” Aliongea Angeli huku akiungwa mkono na marafiki zake
Masumbuko alikuwa amelala fofo kwenye sofa huku Steve ambae alikuja kumsalimia rafiki yake Peter akiwepo akiangalia muvi kwenye laptop yake , na ndio wakati huo ambao Nasma aligonga Mlango na Steve ndio aliesikia na kwenda kufungua,macho yalimtoka na kujikuta akifikicha macho.
“Mambo “ Alisalimia Nasma huku akiweka tabasamu lililomuacha hoi Steve na kujikuta akimwangalia usoni Nasma na mpaka Nasma mwenyewe akaona haya na kuangalia chini.
“ Aaa poa karibu “ Aliongea Steve huku akimwangalia Nasma na alikuwa amesimama tu hapo mlangoni na alijifikiria, ila akaona aingie tu .. alisogeea mpaka kwenye sofa moja refu , kwani hapo ndani kulikuwa na masofa manne na moja lilikuwa karibu na tv na hili lilikuwa ni dogo na dogo lingine lili kuwa upande wa kulia mbali kidogo na Tv na refu kakalia Steve , ila la karibu kabisa ambalo ndilo la kwanza ukiingia hapo ndani kalalia Masumbuko .
Nasma alisogea na alikuwa na wasiwasi sana kwani ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuingia katika vyumba ya wanaume tu , kwani hakuwahi kufanya hapo kabla , alisogea na ndipo alipo muona Masumbiuko aliejinyoosha kwenye sofa akiendesha jenereta kwani alikuwa amepitiwa na usingizi mzito sana .
Nasma alikaa pembeni ya kichwa cha masumbuko kwani alikuwa ameacha nafasi kidogo ambayo ilimuwezesha kukaa , ila wakti anakaa kichwa cha masumbuko kilimgusa kwani mtoto nae alikuwa amejaliwa chungu sio poa.
“Ngoja ni kuletee juisi” Aliongea Steve kwa kubabaika kwani alikuwa ni kama haamini ,kuna muda aliona labda mwanadada huyu alikuwa amepotea njia.
Masumbuko nae muda huo ndio usingizi unaisha na alikuwa akijifikicha macho huku Nasma alikuwa akimwangalia kwa macho yenye mahaba mazito , Masumbuko alianza kunusa kama mbwa maana alisikia harufu nzuri sana kwenye pua zake na wakati anafanya kitendo hicho alikuwa amefumba macho .
“Peter leo sijui kakaribisha jini” Aliongea Msumbuko huku akifungua macho akiangalia juu na hapo ndipo macho yake yakagongana na ya nasma alie kuwa akimwangalia huku akitabasamu na Masumbuko alipo fungua macho alijikuta akishangaa na kumfanya Nasma atoe kicheko.
Na kitendo hicho Steve alikuwa akikishuhudia na aliona kama anangalia sinema VR Gasses (hizi ni miwani ambazo unaweza ukaangalia muvi au kucheza gemu kwa mazingira ya 3D na kukupa hali ya kama unakiona kitu katika mazingira halisi ) ,maana jinsi Nasma alivyo inama na Masumbuko alie kuwa kalala na walivyo kuwa wanaangaliana ilikuwa ni kama sinema la kifilipino .
“Dada juisi hii hapa”
Aliongea Steve na kumfanya Nasma amwangalie na kuachia tabasamu na kisha kusema asante , na kumfanya Steve ahisi sauti hio ilikuwa ipo tumboni ,ikitekenya maini yake.
Masumbuko mara alishtuka maana sijui alifikiria nini na alinyanyuka haraka haraka na kumshika Nasma mkono na kumfanya Nasma amwangalie huku akitabasamu na Masumbuko alimnyanyua Nasma na kumpeleka karibu na mlango wa jikoni ambapo mtu wa sebleni hawezi kuona
“Usije ukasema siku ile tulikutana na nilipotea na wewe ndio ulio nileta maana niliwaambia nalijua sana jiji sasa usije ukaniumbua , yaani kimyaa shiiip” Aliongea akimnong`oneza Nasma na kumfanya Nasma atabasamu na kuhisi msisimko wa ajabu kwani alihisi pumzi ya Masumbuko .
“Hapa leo nadhani kwa mara yangu ya kwanza ndio naangalia tamthiliya la kifilipino laivu bila chenga aliongea Steve baada ya kumuona Masumbuko akimwambia jambo Nasma.
*****
Boss mkuu kapiga simu kuhusu ule mzigo wa Congo “ Aliongea jamaa mmoja mrefu mweusi aliekuwa na mwili ulio jazia na akiwa amevaa miwani .
“ Ramso nadhani wewe unajua nini cha kufanya hapa , na nimeona una majukumu mengi sana, lakini nataka nikupe jukumu lingine na hilo .
“Jukumu gani hilo boss?”
“Nataka kwanzia sasa uwe karibu na Rania kwa kila anacho kifanya kwani muda si mrefu nitakwenda kumuoa”
“Boss una amini atakubali?”
“ Ramso unafikiri ninasema jambo bila mpango , yeye akubali asikubali ila lazima nimuoe kwa namna yoyote ile kwani baba yake tayari yupo hapa kiganjani na hana pakwenda na mama yake na yeye nina udhaifu wake mkubwa sana na nikumuonesha huo tu hatokuwa na la kusema zaidi ya kunipa baraka zote.”
Aliongea Hemedi akiwa nyumbani kwake eneo la Mapinga Bagamoyo na ndani ya jumba hilo ilikuwa ni kama ikulu kwani walionekana mabodigadi wengi walio valia suti safi wakiwa wana hakikisha ulinzi na haikueleweka walikuwa ndio wanamlinda huyo Hemedi au kuna la ziada kwani kama tujuavyo Hemedi ni mfanya biashara wa mabasi .
“Sawa Boss nitalifatilia hilo”
“ Kingine hakikisha huyo panya (Peter ) hafanyi lolote kwa huyo mwanamke , kwani ndio roho yangu na nadhani nikishampata rania roho yangu iatulia na nitatulia nae ,huyu paka kama isingekuwa analindwa na Bosco ningekuwa nishampoteza muda mrefu sana”
“Boss unamaanisha wetu anamfahamu Peter”.
“Ndio ana mfahamu vizuri sana na namheshimu sana Bosco kwani kanifikisha hapa nilipo leo hii, ila asinenipa maelekezo ya kutomgusa Peter ningekuwa nishampoteza muda mwingi sana”
Aliongea Hemedi na kumfanya Ramso ashangae , kwani sio jambo la kawaida kwa tajiri mkubwa kama Bosco kumjua Peter , kwani Bosco alikuwa ni tajri mkubwa ndani ya Congo mwenye mtandao mkubwa wa madawa ya kulevya na alikuwa ni supplier(msambazaji) kwenye nchi nyingi sana ikiwemo Tanzania alikuwa akifahamika kwa jina la The Don.
*****
Ndani ya uwanja wa kimaaifa wa Julius kambarage nyerere (JNIA) , alionekana mrembo Najma akiwa na bodigadi wake akitoka eneo la ‘Arrival’ yaani wanofika, akiwa amependeza kwelikweli na alionekana kabisa alikuwa safarini na ndio anarudi .
“Rehema naomba usinipeleke nyumbni kwanza nataka nikakae Serena mpaka nitakapo kamilisha ufunguzi wa kampuni yangu” Aliongea huku akitembea kimadaha kabisa na kuingia kwenye gari.
Gari ilitembea mpaka kwenye hoteli ya Serena ikitumia masaa machache tu kuingia kwenye hoteli hio ya hadhi ya juu na kisha mrembo huyo akaingia . na kwenda moja kwa moja mpaka mapokezi na kuchukua chumba .
“Leo unaonekana kuwa nafuraha kuliko siku zote nilizo kuzoea”Aliongea Rehema huku akiingiza mizigo ya Najma ndani ya chumba hicho .
“Acha tu nitakwambia kila kitu ila kwa sasa kuna mambo makuu mawili nataka kuyatimiza ndani ya mwezi mmoja .
“Hongera yako ,kama kuna jambo ambalo unataka kulifanikisha pia ni mwanzo wa mafanikio na ni uthamani katika uso wa dunia kwani hauvuti hewa bure , hakuna jambo zuri kuwa na sababu ya kuishi”Aliongea rehema na kisha waliagana kwa ajili ya kukutana siku inayo fuata.
Najma alifungua begi lake nakutoa laptop na kisha akawasha mtandao wa Skype na kisha akabonyeza kwenye hio laptop na likaja jina la A2
“Hello A2 “ Aliongea Najma kwa mapozi . (A2 ni Artificial intelligence roboti ambayo ilitengenezwa na Profesa Gladness , roboti ambayo inafanana kwa kila kitu na binadamu wa kawaida unaweza ukamfahamu roboti A2 kutoka kwenye simulizi ya MY DREAM MY FAVOURITE)
“Hello Beuty Najma .”
“ Nimefurahi sana kuwasiliana na wewe A2 na niliongea na aunt(shangazi) na kaniambia nikuombe msaada unaweza kunisaidia kwenye tatizo langu .
“Ndio alinidokezea na ni kwamba tatizo lako linaweza kufanyiwa kazi kisayansi kutokana na kwamba sasa kuna teknolojia ya kuweza kufanya komputa kutoa picha yoyote ile unayohitaji kutoka katika mawazo yako”
“Naweza kufika lini ili swala langu uweze kulitatua?”
“Kesho asubuhi unaweza ukafika nitakusadia hakika “
Hili ni roboti A2 liliotengenezwa na profesa gladness, na lilikuwa lipo kwenye moja ya kitengo cha usalama wa nchi , kitengo ambacho kilibadilishwa jina kutoka kwenye jina la the Hollic Shadow na kwenda kuitwa jina la AFRICA MULTNATIONAL CYBER SECURITY (AMCS) na kiongozi wa kundi hili alikuwa hajulikani jina lake , kwani kitengo hichi kilikuwa kikifanya kazi zake kwa siri sana na hata wafanyakazi walikuwa hawafahamiki .
UNAWEZA PATA SOFTCOPY YA SIMULIZI HII YOTE.
SIMULZI ZANGU NYINGINE NI
-UMOJA NAMBA TISINI NA SABA
-NDOTO ZA KIKANUNI
-BOOK OF ALL NAMES (UMOJA NAMBA TISINI NA SABA )
-MY DREAM MY FAVOURITES)
KUHUSU UTARATIBU WA MALIPO
WASILIANA NAMI KWA KUGUSA HAPAA
mawasiliano 0687151346
Singano jr Tubeless vigongo weekend hii tutaisahau Sasa huu UziSEHEMU YA 18
“Boss mwenyewe unarudi kutoka kazini “ Aliongea Steve baada ya Peter kufika nyumbani na kumkuta rafiki yake .
“Yeah nishakuwa boss saivi nafanya kazi katika kampuni kubwa tena benki hela zinakokaa , lazima unite boss .”
“Yeah , ila unabahati sana , unajua washikaji kila ninae mwambia kuwa unafanya kzi kwenye ile benki hakuna hata mmoja ambae ana niamini “
“ Usiwalazimishe kuamini , vipi lakini mambo yako ya field ?“
“Field iko vyema nimepata kwenye kampuni moja ya Telecom kule Posta ndiko ninako fanyia “
“ Anhaa kumbe tuko upande mmoja “
“Yeah , mrembo Rania na kisasi chako umefikia wapi au ndo unambwela “
“Kisasi kinaenda kiurahisi sana tofauti na nilivyofikiria , yaani si tumii hata nguvu”
“Eii.... wewe jamaa muongo sana , yule Rania ni mgumu wewe utampataje kirahisi hivyo , hebu acha Kamba zako hizo “
“Shida yako husadiki , ila nataka nikirudi kutoka Tanga nikuonyeshe uone kama nadanganya au wewe ndio mwenye ugonjwa wa kuto kuniamini “
“Acha wee waenda tanga kufanyae tena? “
“Naenda kwa ajili ya kazi huko na boss “
“Mhmh! , kweli naona ushaanza kuaminika kiasi hicho mpaka unaenda na boss”
“Sio kuaminika ni kwamba mfumo mpya wa ulinzi bado haueleweki kwa IT wengi kwa hio natakiwa kuurekebisha mimi mwenyewe “
“Halafu yule boss wako ana lishepu hilo , yule nakubali ani bemende “
“Aaaa… mke wa mtu yule na ni kama mama yako yule”
“Ana umama gani , hivi unafikiri yule akikutega upo chumbani nae utachomoka kama wewe ni mwanaume rijali , lazima uingie ndo utajua huyo sio mama yako ni umri tu ila tuyaache hayo”
“ Sema huyu mshikaji wako una mpango gani nae au ndo umemfanya House boy“
“ Masumbuko nina malengo nae nataka nikirudi nimfundishe kusoma na kuhesabu halafu nimtafutie biashara ya kufanya”
“Peter wewe hata usijisumbue kuniletea mwalimu au kutaka kunifundisha kwani sitaelewa kitu” Aliongea masumbuko na kumfanya Peter amwangalie huku akisogea pale kwenye sofa alipo kaa .
“Sikia Masumbuko , sijui alie kuambia kuwa huna uwezo wa kusoma na kuelewa ,ila mimi nina fahamu kabisa kuwa wewe unaweza ukasoma na kuelewa ,sema haujapata mwalimu mzuri kwa hio kuanzia sasa jua wewe una akili na unaweza kusoma na ukaelewa umesikia? “
“Ndio nimekuelewa “ Alijibu Masumbuko kwa heshima kwani hakuwahi kumuona Peter akiwa kwene hali hio ya kuwa siriasi
“Naona mshakuwa ndugu kamili kwa sasa “
“ Yeah , yaani nafurahi sasa hivi nyumbanii kuna mtu ambae naweza kumuongelesha wakati wote , nimechoka kuishi mwenyewe , hivi wewe Steve unajisikiaje unatoka shule unarudi nyumbni huku ukijua kabisa hakuna mtu , na hata pale unapokuwa na tatizo huna mtu wa kusema huyu ni ndugu yangu naweza kumuita au kumpigia simu kumuomba msaada “
“Ndio ni maisha magumu sana kiufupi sipatii hata picha lakini cha kumshukuru Mungu ni kwamba bado kakuweka hai na kukupigania mpaka sasa”
“Ndio , nilikuwa nampenda sana mama yangu na nitaendelea kumpenda daima huko aliko , alinipigania yeye mwenyewe kanikuza kwenye mazingira magumu mpaka alipo patwa na umauti , ila naamini siku moja tu nitakuja kumpata alie husika na ajali ile”
“Peter rafiki yangu kwanini usisahau yote hayo ile ilikuwa ni ajali ya kawaida tu kama polisi walivyo sema , kwanini unataka kuweka visasi moyoni , mimi nikajua ulikwisha sahau”
“ Hapana Steve siwezi kusahau kabisa yaani , na hakuna mtu wa kunishawishi , nakaa kimya tu kutokana na kwamba sitaki kisasi kifute ndoto zangu kwani naamini hata mama hatofurahia kabisa akiniona naishi kwa ajili ya kulipiza kisasi”
“Kwa hio Peter kumbe mama yako alikufa kwa ajali”Aliuliza masumbuko
“ Ndio ni story ndefu Masumbuko sipendi kuikumbuka kabisa “
“Hata mimi mama yangu alikufa kwa ajali “ Aliongea Masumbuko na kumfanya Peter amwangalie kwa maswali .
“Alikufa kwa ajali gani ??”
****
“ Nakuona unavyo mfanya mtoto akolee rafiki yangu “
Aliongea Lea akiwa amejilaza pembeni kwenye viti vya kuegamia huku akiwa ameshikilia kikombe cha pombe (Solo cup) Pembeni yake kushoti akiwepo Sebastiani akiwa amekaa mkao kama wake wote alikuwa wamevaa mavazi ya kuogela huku wakimwangalia Stella alie kuwa katika Swimming pool akiogelea kwa ustadi mkubwa ,alikuwa akizama na kwenda kuibukia mbeleni , kiufupi alikuwa kama kivutio siku hio katika eneo hilo kwani uzuri alio kuwa nao wa maji ya kunde ulikuwa ukivutia sana na shepu ambayo mungu amembariki nayo ilizidi kufanya kuonekana mzuri na hata pale alipo kuwa akiingia na kuibuka kwenye maji alifanya kuonekana kama malaika
“Huyu mwanamke mzuri sana , nimeona wanawake wazuri ila huyu ni kiboko , yaani hata huyu bwana wako namuona fala kumuacha kimwana kama huyu”
“Aacha hizo ujue Sebastian kwani kuwa mzuri ndio kupendwa ,ingekuwa wanawake walio na sura mbaya hawaolewi sasa”.
“Acha wivu wewe.. kiufupi pale haumfikii hata kwa dawa , Stella mzuri na pia ana roho nzuri , na ndio maana anazidi kuwa mzuri , sio kama wewe”
“Sikia seba.. huo utani sitaki , yote nilio yafanya nimefanya kwakuwa nampenda sana James na ningemkosa ningekuwa mwehu , mimi ni tofauti na Stella huoni hata hali yake kwa sasa ni nzuri , mimi nisingeweza roho yangu nyepesi”
“Hahaha.. kwahio ulijuaje kama Stella ataweza .. hio ndio roho mbaya ninayo zungumzia sasa, kujijali mwenyewe pasipo kumjali mwingine”
“Sikia seba utaniudhi sasa hivi , jishaue tu na wakati mimi ndio nakufanya uwe na Stella , fikiria tu siku atakavyojua ulikuwa kwenye mpango wa kumuachanisha na boyfriend wake sijui atakufanya nini”
“Basi yaishe mrembo ee , nilikua natoa ya moyoni , lakini nina furaha maana sasa hivi ninae Stella nahisi Dunia yote yangu , japo hajanikubalia ila naamini atanikubalia tu”.
“Halafu seba hivi utakuwa mzito mpaka lini , wewe unavyo endelea kuamini , utajikuta mtoto sio wako , wewe humuoni alivyokuwa mzuri wewe haya tu zembea”
“Kwa hio wewe nataka nifanyaje , na wakati unaona Stella mwenyewe bado anaonekana ana majonzi sema anajikaza kuonekana yupo sawa”
“Ndio maana nakwambia jitahidi umsahaulishe mtoto huyo na jijengee mazingira akuone mwanaume wa tofauti na wengine , mfanye akuamini “
“Najitahidi sana ”
“Bado.. , sasa sikia Stella jambo ambalo lina muumiza kwa sasa ambalo ni kama udhaifu wake mkubwa ni kumfunga Masumbuko huyo rafiki yako , lakini kumbuka akimpata Masumbuko basi na wewe umekamatika na Stella hatokuamini tena na anaweza akakufunga na wewe, maana anaijua sana sheria na utakuwa umekosa kila kitu na mimi sipo tayari kwa hilo”
“Sasa nifanyaje mbona kama unanitisha , mimi akinikamata nakuunganisha”
“ Huo ndio utakuwa umama sasa , hautokuwa mwanaume wewe inabidi ufikiria namna ya kujitoa kwenye kesi ili hata Masumbuko siku atakayo kamatwa wewe hautahusika moja kwa moja, anza kutengeneza ushahidi wa lile tukio kuwa haukushusika na pia tafuta ushahidi au hata kwa kuutengeneza ili umfanye Masumbuko kuwa na hatia moja kwa moja”
“Seba nimefurahi kweli leo asante kwa kunileta hapa , unajua nilikuwa nasikia Sea breeze ila sikujua kuwa pako vizuri kama hivi” Aliongea Stella na kuwafanya Lea na sebastiani kukanyamaza.
“ Ni kweli Stella yaani pazuri ,tupigeni picha basi” Aliongea lea huku akimsogela Stella aliekuwa akijifuta maji na taulo .
“Seba kaa na Stella basi niwapige picha” Aliongea lea na kuwafanya Stella amwangalie Sebastian na Sebastian alimwangalia Stella na kisha wakatabasamu kwa pamoja na kwa ushawishi wa Lea basi walikubali na kupigwa picha na Stella”
“Nitawatumia hizi” Aliongea Lea huku akitabasamu sana maana zilitoka kama alivyokuwa anataka .
****
Huku nyumbaani kwa Mama Rania alionekana Najma akitoka kwenye chumba chake akipiga miayo akielekea chini kwenye sebule yao na muda huo ilikuwa ni muda wa saa saba mchana .
“Hi! dad good afternoon!” Alisalimia Najma baada ya kumuona baba yake wakati tu alipofika sebuleni wakati huo baba yake alikuwa akiingia na sijui alifata nini maana siku hioo alionekana kuwahi kurudi jambo ambal sio kawaida yake .
“Naona leo umewahi , maana nakuona ukirudi saa sita au saa saba usiku “
“Leo kuna kitu nimerudi kuchukua mara moja na nitarejea baada ya muda kidogo , wewe mbona haujatoka kwenda kwenye mandalizi ya ufunguzi wa kampuni yako”.
“Nimetoa tu maagizo kwa wafanyakazi wangu siku hizi sipendi hata kutoka”
“Unaonekana kuwa na jambo maana si kawaida yako my princess“
“Yeah dadie ni juu ya yule mkaka , I am head over heels for him, please help me to find him dadii please “ (Ninamuwaza yeye tu baba )Akijidekeza kwa baba yake .
“My daughter nafanya kila njia kuhakikisha nina mpata and very soon tu utasikia taarifa ya kufurahisha maana timu yangu ipo uraiani huko inamtafuta “
“Asante sana dad ndio maana nakupenda I real love you dad “ Aliongea Najma maana alikuwa na uzungu mwingi yaani alikuwa hamuogopi baba yake kabisa ,watoto wengi wa kiafrika kumwambia baba ya kuwa wapo kwenye mapenzi ni swala gumu sana na kwao linaonekana kama ni utomvu wa nidhamu , ila kwa maisha ya wenzetu uzunguni huko ni swala la kawaida , pia baadhi ya familia za kiafrika washaathirfika na tamaduni za kizungu .
“Vipi na dada yako , unataka kuolewa kabla yake?”
“Dada naye anaanza kuwa kama mimi tu “ Alingea Najma nakumfanya Samir kumwangalia kwa mshangao , huku wakikaa kwenye masofa ya hapo sebuleni .
“Unamaanisha nini kuwa anaanza kuwa kama wewe?”
“Siku hizi hata si muelewi kuna mkaka nadhani kaanza kazi kwenye benki yetu sasa kila saa dada anamzungumzia mara amsifie na hata wakati mwingine usiku anaota akiongea huku akilitaja jina lake”
“Sasa yeye anakuwaje kama wewe , wewe si mwanaume unaempenda ,wewe ni tofauti na Rania “
“ Hata kama Dady nataka niende hapo kazini kwao nikwamuone huyo mwanume anae mchanganya dada yangu yukoje koje huyo “ Alingea Najma na kumfanya baba yake mapigo kuongezeka maana alijua kama ataenda basi anaenda kukuutana na Peter mwanaume anae mtafuta .
“Sikia unaonaje tukienda wote,mimi na wewe ,ninataka kumuona huyo mwanume kama kweli anamfaa mwanangu Rania maana nawajua wanaume waongo sana “
“Sure dad , nitakuambia siku nikipanga kwenda kumuona ili twende wote “
“Hapana Najma mimi nina kazi nyingi so nitakuambia siku nzuri ya kwenda”
“Sawa dad , but I cant wait , better make it soon dady “
“Worry out my daughter , but promise we do this together right “(Usijali mwanangu lakini hii ni ahadi ua sisi kwenda pamoja )
“Yess dady “
Samir alijikuta akitoka hapo huku akijifuta jasho maana anaona kazi inazidi kuwa ngumu watoto wake wanamchanganya vibaya .
“Nisipo fanya kitu hawa wapuuzi watakutana na inaweza kuleta matatizo kwa wote , inabidi nifanye kitu mapema kabla jambo baya halijatokea ,sina jinsi inabidi Rania aolewe na Hemedi , halafu anisaidie kumwangamiza Peter ili hawa mapacha wanaojifanya wanajua kupenda , nawaletea habari ya kifo tu”Alijiwazia huku akiingia chumbani kwake kwa ajili ya kuchukua kitu kilichomrudisha nyumbani .
SEHEMU YA 19
Samiri alikuwa kweli amedhamiria kumfanya Rania aolewe , aliamini njia ya kumuepusha na Peter ni ndoa .
Hivyo hakuwa na jinsi zaidi kumkubali rafiki yake awe mkwe, sababu hakuwa na cha kupoteza Ramia aolewapo na Hemedi , pia mali zake zingekuwa salama kuliko watoto wake kuwa na mahusiano na kijana Peter .
Alishangaa wakati mwingine ni kwanini alikuwa akimchukia sana Peter na kujithamini wapi chuki hio imetokea mpaka kuwa na nguvu ya kutomtaka kijana huyo kuingia katika maisha ya wanae , lakini hisia zake zilimwambia Peter hakuwa mtu sahihi kwa wanae zaidi ya maslahi na pia hakuamini kama kijana huyo alikuwa na mapenzi ya dhati kwa wanae , lakini pia aliona hatari ilioko kwa kijana huyo kupendwa na familia yake yote .
Siku hio wakati akiwa nyumbani alijihisi kuboreka kubakia hpo kwa muda mrefu ,lakini pia hata ile muwashawasha wa kwenda kutembea uliongezeka mara baada ya kuona meseji ya mchepuko wake Amanda , aliingia bafuni na kujiswafi .
Na kisha akaanza kujiandaa lakini wakati anachukua ufunguo ndio Mama Rannia alikuwa akiingia kutokea kazini.
Mwana mama huyu japo mume wake alikuwa akimnunia ila hakuacha kuonyesha heshima kwa mume .
“Haa ! Mume leo naona umewahi kurudi kazini”
“Ndio kuna kitu nilifuata ila ninaondoka na nitachelewa kurudi”
“Sawa mimi kesho nasafiri kikazi , unaonaje leo ukiwahi kurudi nyumbni mume wangu nimekumisi sana mpaka najisikia vibaya jamani”
Samiri wala hakujibu neno lolote zaidi ya kufungua mlango lakini kutokomea lakini sekunde mbili mlango ulifunguliwa tena na alikuwa ni Samiri , Mama Rania alimwangalia.
“Nimesahau kukutakia safari njema”
Aliongea na kisha alifunga mlango ,mwanamama huyu chozi lilimtoka na kujawa na hudhuni ,hakuamini kabisa mabadiliko ya mumewe kiasi cha kutomjali.
Alikaa kwenye kitanda akifikiria kosa gani amelifanya mpaka hali ya ndoa yake kufikia hatua hio , kuna muda alitamani hata kumfukuza Peter kazini ili hali ya ndoa yake irudi kama awali , lakini akikumbuka kuwa Peter alikuwa tegemezi katika kuimarisha ulinzi wa benki ,wazo alilitupilia mbali , ni zaidi ya mwezi yeye na mume wake kuishi kama dada na kaka
****
Ndani ya hoteli ya Coral Beach alionekana Lea siku hio ndani ya chumba kikubwa cha hadhi ya juu akiwa ameshikiliwa kiuno na James huku akiingiza mwiko wake ndani na kutoa huku kimwana huyo akitoa miliio ya kimahaba ,alionekana dozi anayopewa na james haikuwa ya kawaida .
James alikuwa akimkunja kama kambale na alionekana kubobea kweli kwenye mambo ya sita kwa sira kwani alionekana shughuli kuimudu vizuri takribani dakika kumi na tano walikuwa washamaliza na wote kufika ukingoni.
“Asante sana Hubby “ Aliongea Lea huku akimwangali James usoni aliekuwa akihema kama mbwa alie kimbia maili nyingi “
“Hauna haja ya kushukuru mpenzi wangu mimi hii ndo kazi yangu ya kuhakikisha kwamba nakuridhisha ili usije ukanitoroka ukaenda kwa wengine kwani nitaumia sana mpenzi , nimeumizwa na Stella sitaki kuumizwa na wewe tena”
“Usiwe na wasiwasi mpenzi kwa ninavyokupenda haitokuja itokee eti nakusaliti mpenzi wangu , mimi niwako tu peke yako , unavyo niacha ndivyo unavyo nikuta “
“Hata mimi nakupenda sana Lea na sipo tayari kuuona huu uso wako unatoa machozi kisa mimi kukusaliti , kwanza nataka ukimaliza tu chuo nakuoa”
“Kweli mpenzi , uko siriasi “
“Ndio kwani wewe hautaki kuolewa ,
“Nataka mpenzi ila unajua mapenzi yetu hayana uhuru kwani lazima kila siku tukifanya yetu tujifiche ili Stella asione , natamani kutembea na wewe kila mahali kuonyesha ulimwengu mzima kama napendwa na wewe james mwanume wa maisha yangu ”
Aliongea Lea kwa hisia kubwa na walianza akuchokozana tena, na kwa mara nyingine wakaingia kwenye tendo hilo la kuzini na walidumu kwa dakika kama ishirini , na kati yao hakuna hata mmoja alie kuwa akikumbuka kondomu walionekana kuaminiana.
“Vipi mpenzi lini tena warudi Kenya?”
“Kesho narudi ,nitakuwa huko kwa mwezi mmoja , halafu haujaniambia Stella anaendelaje kwa sasa , si rafiki yako?” Aliuliza James na lea kumuona bado anawasiwasi na hali ya Stella.
“Anaendelea vizuri tu wala hakuwazii , ngoja nikuoneshe maana saivi ana mpenzi mpya na hana habari na wewe “ Aliongea huku akimuonyesha baadhi ya picha ambazo zilimuonesha Stella akiwa kwenye kivazi cha kuogelea ,James alisisimka baada ya kuona umbile la Stella
Lea alikuwa akifanya kumuonesha James ,alimjunesha za Stella na Sebastian wakiwa kwenye pozi mbele ya Swimming pool
“Huyu ndio mpenzi wake mpya ?”
“Ndio huoni walivyo pendeza “
“ Hongera yake , nilijua tu kama hanipendi huyu mwanamke nilikuwa namwamini sana kumbe mchafu namna hii , sitokuja kumsamehe “
“ Usimchukie sana mpenzi , kwanza upo na mimi mwanamke ninaye kupenda , haina haja ya kumuwazia Stella tena” Aliongea Lea huku Stella akielekea bafuni akimwacha James.
James alishika simu yake na kuwasha data na kuangalia message za Watsapp, alijikuta akitabasamu baada ya kuona jumbe kutoka kwa jina la Business partner ,jumbe ya sauti (voice notes) , aliweka ‘Earphone’ masikioni na kusikiliza huku tabasamu pana likiwa limeupamba uso wake , inaonekana jumbe hio ilimfurahisha mno , pale alipomuona Lea anatoka bafuni ndio akajikausha na kuweka simu pembeni baada ya kufuta ule ujumbe .
****
Ilikuwa ni siku nyingine siku ambayo Mama Rania na kijana Peter walikuwa kwenye gari moja aina ya Range Rover Spot huku dereva akiwa Peter akiwa makini na usukani , pembeni yake alikuwa ni Mama rania alieonekana kusinzia, hakuwa na habari kabisa kwa alivyojiachia kwani sketi aliovaa ilikuwa imepanda mpaka kwenye mapaja ,ukizingatia pia kigauni alicho vaa kilikuwa chepesi sana , mwanamama huyu hayo ndio maisha yake ,alikuwa na uzungu mwingi hata kazini kwake.
Gari ilizidi kuyoyoma na ndani ya masaa manne gari ilikuwa ikipita sehemu moja inayoitwa Soni hapa ndio Mama rania alishtuka kutoka usingizini .
“Nimelala sana?”
“Yeah ndio tuko eneo moja linaitwa Soni na muda si mrefu tunafika lushoto mjini “
“ Aisee nimelala”
“Unaonekana kuchoka sana”
“Yeah nimechoka sana jana sikulala kabisa mpaka kuna kucha “
“Tatizo lilikuwa ni nini sasa ?”Aliuliza Peter huku akiwa makini zaidi na barabara kwani makona yalikuwa mengi .
“Mambo ya kawaida tu , halafu kuna baridi huku” Aliongea Mama Rania baada ya kupandisha kioo.
“Ndio huku ni juu milimani , milima ya Usambara , ni kuzuri kweli nishawahi kufika mara nyingi nyingi kuna baridi ,ila kuna maeneo mazuri ya kutembelea”
“Kumbe nipo na mwenyejii, basi inabidi unipeleke peleke hayo maeneo ya vivutio nikaone na mimi”
“Hilo hata usijali Boss”
Walitumia masaa machache sana kufika Soni, na moja kwa moja waliingia Lushoto mjini na kwakuwa ailikuwa mapema sana , waliingia kunywa chai kwenye mgahawa na baada ya hapo wakaanza ukaguzi ndani ya jengo hilo la benki , na Peter yeye akiwa na kazi ya kuweka mfumo mpya kwenye tarakishi pamoja na vimashine flani vya mtandao .
Kazi ilifanyika kwa masaa manne mpaka kuisha na iliisha mapema kabla hata ya muda ambao walipanga kuutumia , baada ya kazi zote hatimae waliondoka huku wote wakiingia kwenye gari na kuelekea kwenye hoteli moja maarufu sana ndani ya Lushoto ilio kuwa ikijulikana kama “IRENTE VIEW “ hii ni hoteli moja nzuri sana ilio kuwa ikimilikiwa na marehemu raisi mstaafu Benjamini mkapa , ilikuwa juu ya mlima na ukiangalia kwa chini unaona maeneno ya tambarare , kama nji za kwenda Moshi , Mazinde na baadhi ya maeneo mengine ni eneo zuri kweli kwa hoteli hio kuwepo .
:Jamani kuzuri huku , kuna mazingira safi hadi raha na hewa safi kabisa “ Aliongea Mama Rania wakati wakitoka kwenye gari baada ya kuingia ndani ya hoteli hio.
****
Tajiri Samir hakurudi nyumbani siku ambayo mke wake alikuwa amemuambia kuwa kesho yake atasafiri kikazi na wala hakujua kabisa mke wake alikuwa amesafiri kuelekea wapi Zaidi ya kujua yupo safari kikazi .
Usiku wa siku hio Mama Rania alimsubiri sana , alikuwa akitamani kupata haki yake ya ndoa na alikuwa kwenye hali mbaya sana , lakini Samir hakurudi kabisa kwani mchepuko ulikuwa umemshikilia sana siku hio .
“Umeamkaje mpenzi?” Aliuliza Amanda ,alikuwa amekaa kwenye Dressing table akijipodoa ,ilikuwa ni muda wa asubuhi na Samir ndio kwanza alikuwa akitoka usingizini .
“Jana umeniweza kweli yaani nimesahau kabisa kurudi nyumbani “
“Nipo hapa kwa ajili ya kukusahaulisha kuhusu mkeo maana najua upo kwenye wakati mgumu sana wewe ni familia yako “
“Ni kweli , ila yataisha tu ,”
“Vipi mke wako leo si atakuwa na presha huko”
“Kweli na anavyonipenda sidhani kama jana alilala, maana kila siku namkuta yupo macho ananisubiria , halafu aliniambia kuwa anasafiri kikazi”
“Masikini saivi atakuwa na mawazo safari nzima”Aliongea Amanda pasipo kujali kuwa anaye mfanyia hivyo ni mwanamke mwenzake na anaiharibu nda ya mwanamke mwenzie.
****
Sebastiani alikuwa ndio kwanza kutoka chuoni , aliingia ndani kwake na kisha akajirusha kwenye sofa lilipo ndani ya chumba chake .
“Stella unaninyima usingizi , ila nitakupata tu kwa namna yoyote ile upo ndani ya mawazo yangu sana , nakufikiria kila wakati” Alijiwazia sebastiani huku akiangalia feni inavyozunguka .
“Inabidi nikusaidie katika swala lako na Masumbuko na naamini kupitia hili lazima unipende mwenyewe”
Alinyanyuka na kuweka begi lake lilibeba tarakishi mpakato kwenye meza na kisha, alivua nguo zake na kuingia bafuni ,chumba chake kilikuwa ni self container , alimaliza kuoga na kuanza kujifuta maji , kuna wazo lilimjia ambalo lilimfanya atabasamu .
“Aliifuata simu yake na kisha akamtafuta Steve na kumuuliza yuko wapi na alijibiwa kuwa yupo kazini bado , aliuliza na kuhusu Masumbuko na kupewa jibu kuwa yupo nyumbani na Peter alikuwa mkoani kikazi . majibu hayo yalimfanya atabasamu na kuvaa nguo zake na kujiandaa haraka haraka .
“Hapa naenda kwa masumbuko kuchukua ushahidi au kuutengeneza na hivyo hana akili atajaa tu” Alijiongelesha huku akitabasamu kinafiki.
SEHEMU YA 20
Sebastian alipanda daladala na moja kwa moja alielekea Mbezi Beach nyumbani kwa Peter na Masumbuko , kutokana na muda huo kutokuwa na foleni kubwa , alitumia dakika arobaini na tano hivi kufika Mbezi Beach , alikuwa akipahafamu sehemu ambayo alikuwa akiishi Peter , alivuka barabara na kunyoosha juu kabisa mpaka nyumbani wanapoishi .
Masumbuko wala hakuwa na habari kwani muda huo alikuwa akiangalia muvi kama kawaida yake maana alikuwa akipenda sana TV.
Alisikia mlango unagongwa na akanyanyuka na kusogelea na kuchungulia kwanza ni nani anaye gonga na alivyo muona ni Sebastian kwanza aliogopa na kuanza kujishauri kufungua ama asifungue , lakini mlango ulizidi kugongwa ndipo alipo kata shauri na kufungua mlango .
“ Wewe fala nagonga hata haufungui , ulikuwa umelala nini?”
“Hamna nilikua najishauri nifungue au nisifungue “
“ Ulijua anaye gonga alikuwa mimi au? “
“ Ndio nilichungulia kabla ya kufungua”
“Sasa kwanini ulikuwa unajishauri kufungua , au ulikuwa unaogopa yale ya siku ile , yale yalipita na sina time nayo chukulia poa tu “
“ Unasema kweli ?”
“Ndio namaanisha , mimi siwezi kukosana na mwanaume mwenzangu kisa demu”
“ Asante sana , mimi hata siku ile sijui nilifikiria nini maana nilijikuta tu nimefanya vile “
“Vipi umefanya” Aliuliza huku akikaa kwenye sofa
“Si kukufanya uwe muhudumu”
“Hahaha... sema ulichonifanyia wewe boya ,ndio hivyo nimekusamehe maana Peter ni rafiki yangu na wewe pia umekuwa rafiki yangu kuanzia leo na kuendelea”
“Asante Sana”
“Peter yuko wapi?”
“Kasafiri “ Alijibu Masumbuko huku akikaa na yeye maana muda wote alikuwa amesimama . wakati huo Sebastian na yeye alikaa vizuri nakutoa simu yake akatachi akapangusa pangusa na kugusa ,ilikuwa simu janja ,kisha akamwangalia Masumbuko .
“ Masumbuko halafu unajua ile siku ulinishangaza sana hivi ulimla yule mwanamke ?”
“Ndio nilimpiga kitu safi mpaka akazimia nikaachana nae maana pale nilimpa kumbukumbu za masaa mawili”
“ Haha .. kwahio ni kama ulimpiga changa la macho na ukala kitumbua si ndio?”
“Yeah nilimbadilisha mawazo sijampiga changa la macho “
“Sasa kwani kuna utoafauti gani kati ya changa la macho na kumbadilisha mtu mawazo?”
“Mimi Sijui jibu wewe”
“Namaanisha si kama umembaka vile?”
“ Kwani kumbaka mtu inakuwaje kuwaje?”
“ Si kama kumfanya bila ya kujua anacho fanyiwa, hapo utakuwa umebaka mtu kwa sababu alikuwa hajui “
“Ndio nimembaka basi”
Basi Sebastian aliaga huku akimwambia Masumbuko kuwa amekuja kwa jili ya kuonana na Peter ila kwa sababu hakuwepo alisema atakuja siku nyingine .
Sebastian alifika geto kwake huku akitabasamu na kutoa simu yake na kuanza kuplay na hapo hapo ikaanza kusikika sauti ya Masumbuko .
”Ahahaha.. nimembaka basi , masumbuko wewe huna akili na utaenda jela bila ya kupenda fala wewe”Aliongea Sebastian huku akitoa ile memory kadi na kuweka kwenye kijiboksi hapo ndani . .
*****
Tajiri Samir alikuwa amedhamiria kwa silimia mia kuwa lazima afanye maamuzi mapema , kwani kila alipo fikiria kuwa Rania ashaanza kuwa na hisia na Peter alipata wasiwasi hali hio aliiona kama bomu linalotaka kulipuka na ni yeye tu ambae anaweza kulitengua .
Wakati akiwa ofisini kwake alitoa simu yake na kumpigia rafiki yake Hemedi na kumwambia kuwa jioni wakutane maeneo yao ya kukutania kwani ana jambo la kumwambia .
Basi baada yakufanya kazi na kumaliza tayari ilikuwa ni mida ya jioni ambayo alipanga kukutana na tajiri Hemedi katika hoteli ya Kilimanjaro kwani hapo ndipo makazi ya Hemedi akitaka kujivinjari na mwanamke yeyote yule .
Samiri alifika nakuegesha gari yake na kwakuwa aliambiwa na bwana Hemedi kuwa wakutane kwenye chumba alichokuwa anapendelea kuchukua hotelini hapo , basi Samir alipandisha juu kabisa mpaka kwenye chumba hicho.
Alifungua mlango na kuingia ,alimkuta Hemedi akiwa na mwanamke mmoja alie valia chupi tu , Hemedi baada ya kumuona rafiki yake alimruhusu yule mwanadada aondoke huku akimminya kalio .
Kitendo kile alikishuhudia Samir na kujikuta akipandwa na hasira hasa alipo fikiria kuwa huyo ndio mwanume ambaye anapaswa kumpa Rania kwa ajili ya kumuoa .
“ Niambie Samir , umefikiria juu ya ombi langu?” Aliongea huku akimimina pombe kwenye glass na kumpa Samir , huku Samir wakati huo alikuwa na hasira kila akifikiria vitendo vichafu vya Hemedi alijiona kabisa huyo hafai kabisa kumuoa mwanae.
“ Ndio nimefikiria”
“ Haya niambie baba mkwe”
“ Sikia Hemedi nimegundua wewe sio rafiki yangu umnafiki , unatumia nafasi ya matatizo yangu ili kumpata mwanangu , sasa mimi kama baba yake sipo tayari kwa hilo.”
“ Samir wewe ni rafiki yangu sana na tumesaidiana katika mengi na unanijua vizuri , kwani kuna shida gani ya mimi kumuoa mwanao?: na kwanza wewe unakuwa kwenye nafasi nzuri kwani Rania utampa mali zako na mimi sina shida na mali zake atazitunza na kumpa mwanae atakae mzaa na hakutakuwa na mgogoro wa mali zangu na watoto wangu wakubwa sasa hiko unacho kichukia ni kipi, mbona kuna watu wengi tu wazima wana oa mabinti “
“Sikia Hemedi wewe ni mnafiki sana na nia yako nishaijua wewe kwa kupenda kwako ngono najua unamtaka na mtoto wangu kwa ajili ya kumchezea , hivi na hio tabia yako kweli naweza nikakupa kweli mtoto wangu mimi si nina mchimbia kaburi mwenyewe “
“ Sikia Samir ni kweli unajua tabia yangu ila ni kuhakikishie kuwa nipo tayari kubadilika kwa ajili ya Rania kwasababu sijampenda Rania jana wala leo , ni muda mrefu sana na nilikuwa nikiogopa sana kukuambia hilo lisije lika leta athari kwenye urafiki wetu”
“ Kwa hio ulisubiri mpaka sasa ambapo nina matatizo ndio kuniambia kwakuwa unajua kabisa sitokuwa na jinsi?”
“ Sio hivyo rafiki yangu , ni kwamba sipo tayari kumuona Rania anampenda mtu mwingine na wakati mimi nipo hai , na isitoshe pia sitaki na familia yako kusambaratika na kuingia kwenye migogoro kisa mwanaume , tena mwanaume ambae hana mbele wala nyuma”
“ Hio sio sababu ya kutosha ya mimi kukupa mtoto wangu”
“Sababu kubwa ni hii hapa” Alivuta bahasha moja na kutoa picha na kuzimwaga mezani na hapo ndipo Samir aliona kama akili yake haifanyi kazi vizuri kwani aliona picha zikimuonesha Rania akibusiwa kwenye paji la uso na Peter”
“ Nadhani umeona sasa, hio nayo ni sababu kwani inanikasirisha sana kumuona mwanmke ninae mpenda akibusiwa hivyo na hio ni kwenye paji la uso kesho na kesho kutwa atabusiwa kwenye lipsi na kumpa kabisa kitumbua , nadhani kwa kiburi ambacho watoto wako wamerithi kutoka kwako sijui utamwambia nini akuelewe kuwa umemtafutia mchumba wa kumuoa”
Samir alijikuta akikaa chini na kunywa glass yote ya bia na kuisikilizia inavyo choma koo na kisha akatulia na kuanza kufikiria huku akiziangalia picha zilizo kuwepo hapo mezani , alipeleka mawazo yake kwa Rania na kufikiria ubishi wake na msimamo wake pale anapohitaji kitu , akamfikiria Nasma
ujeuri aliokuwa nao , akamfikiria Peter na yeye na kuanza kumpima sifa zake kama anafaa kuwa na mwanae hata mmoja aliona hafai.
“ Unajua Samiri wewe hata kuua mtu najua hauwezi , ila mimi nitakusadia kumpoteza kijana Peter kwajili ya kuwaokoa wanao “ Aliongea Hemedi na kumfanya Samir aliekuwa kwenye mawazo amwangalie na kujiuliza hitaji lake kuu ni nini , alijibu kuwa kujiambia kuwa hitaji lake kuu ni Peter kupotea katika uso wa Dunia ili kuiokoa familia yake.
“ Una uhakika juu ya hilo la kumpoteza Peter “
“ Ndio hilo naweza sana na lipo ndani ya uwezo wangu ,ni wewe tu kunipa baraka nimuoe mwanao na wewe utumie ubaba kumfosi mwanao nimuoe na mimi najua jinsi ya kumpata Rania kama ndio jambo ambalo lina kuumiza kichwa .
Samir alimwangalia rafiki yake huyo ambae dakika chache za nyuma alikuwa akimwamini sana katika kumwambia shida zake , kwake aliona mazungumzo hayo yalikuwa ni kama ya kibiashara.
“ Daah..! “ Aliongea Samiri na kukatishwa na simu ilokuwa ikitoa mlio wa sauti ikioonesha kuwa kuna mpigaji , alitoa na kuona ni namba ngeni .
“ Boss za siku nyingi!”
“ Salama nani mwenzangu?”
“ Ni mimi Krispine kutoka kampuni ya POPOTE TUNAFIKA , ulinipa kazi nifuatilie taarifa za yule mwanamke ,nimepata taarifa yake na mwanae”
“Uko wapi?”
“Nipo Ubungo”
“ Nakuja “
“Hili tutaongea siku nyingine Hemedi” Aliongea Samir na kisha kuondoka .
****
Tukiingia ndani ya mji wa Lushoto , alionekanna Mama Rania akiwa kwenye chumba chake ndani ya hoteli , baada ya kila mtu kuchukua chumba .
Chumba cha Peter kikiwa kipo mkabala na chumba cha Mama Rania , hoteli ilikuwa na mazingira ya kuvutia sana kwani chumba kilionekana kuwa kizuri mno .
Mama Rania alikuwa amekaa kwenye kitanda chake akionekana kuwa na mawazo , akiwa ameshikilia simu yake , ni kama alikuwa akisubiria mtu amtafute . na nikweli alikuwa akisubiria ujumbe ama simu kutoka kwa mume wake , kwani tokea alivyo ondoka jana yake nyumbani hakurejea kabisa , na mbaya Zaidi ni kwamba na yeye ameondoka bila ya kuonana nae , japo alikuwa akijua kuwa mume wake alikuwa akichepuka lakini hakuacha kumpenda mume wake na alitaka tu kujua hali ya mme wake kuwa anandeleaje .
Wakati akiwa kwenye mawazo akiwa amekaa kwenye sofa , jina la ‘My favourite Naa’ lilisomeka kwenye kioo cha simu yake janja ukiambatana na mlio wa sauti wa wimbo wa ‘Alan walker –Faded’, alikuwa ni mwanadada Nasma ,alitabasamu huku akiipokea na kuweka sikioni na kuanza kuongea na mwanae . alionekana kuna jambo la kufurahisha ambalo alikuwa akiongea na mwanae huyo maana hali yake ilibadilika na kuonekana kutabasamu .
Mama Rania alijikuta akitamani kupiga soga na Peter mara baada ya kumaliza kuongea na simu , kwani alikuwa amemzoea sana Peter na hususani akiwa kwenye hali ya mawazo mara nyingi mtu ambae amekuwa tabibu wake wa kumrudisha katika hali sawa alikua ni Peter , alinyanyuka kivivu na kuchukua kitenge chake na kujifunga huku akiwa amevalia kijisketi chake chepesi kwa ndani alitoka na kwenda mpaka kwenye chumba cha Peter , aligonga na kusubiria na baada ya muda Peter alifungua mlango hukua akiwa amevalia singlend na bukta lake .
“ Vipi naweza kuingia? “ Aliongea Mama Rania huku akimwangalia Peter usoni aliejifikiria kwa sekunde na kisha alimruhusu mama huyo na kuingia
“ Najihisi upweke kukaa mwenyewe nimeona nije unichangamshe
changamshe maana naona kama mawazo yananiandama”Aliongea Mama Rania
na Peter kwa akili yake ya haraka alijua kabisa mama huyo alikuwa akisumbuliwa na mawazo kwani kule njiani alikumbuka alimwambia kuwa hakulala kabisa usiku wa jana mpaka kunakucha .
“ Basi stori zilianza , na kama kawaida Peter kwakuwa alikuwa haishiwi na stori za uongo na kweli Mama Rania hali yake ya furaha hatimae ilikuwa imerudi kwa kiasi fulani , uzuri wa kile chumba ni kwamba kilikuwa na sehemu ya kukaa yaani kulikuwa na masofa(master suite room) ambayo yamepangwa na yalikuwa yakiruhusu watu kama watatu kukaa .
Baada ya kupiga stori kwa muda mrefu , huku hali ya hewa ya Lushoto ikizidi kuwapa kajiubaridi na kumfanya Mama Rania atoe ile khanga alio jifunga na kujifunika mabegani na wakati huo walikuwa wamehamia kwenye kungalia onyesho fulani la wanamuziki kutoka Marekani wakionyesha uwezo wa kwenye kuimba(Stage perfomance ) , sasa Peter alidhania mama Rania anapenda kile alichokuwa akiangalia kumbe mwenzake alikuwa ashalala muda na saa ilikuwa ikisoma saa nne usiku muda huo , Peter muda wote alikuwa akijua kuwa na mwenzake yupo makini kwenye kuangalia maana alikuwa akiona vijiaibu flani hivi vya kugeuka na kumwangalia Mama Rania usoni. Na hakujua kwa nini alikuwa na hali hio .
Baada ya dakika kadhaa alijikuta akigeuka na kumwangalia Mama Rania , hapo ndipo alipo gundua kumbe mwenzake ashapotelea usingizini muda mrefu huku akijiegamiza vibaya kwenye lile sofa ,Peter alimwangalia na kuona kweli boss wake kachoka , aliamua kunyanyuka lakini mara Mama Rania kwa jinsi alivyo kuwa ameegamia lile sofa alijikuta akielekea chini na Peter kwa uharaka wake alijikuta akichuchumaa na kumdaka na hapo Mama Rania ndipo alipo kuja kushituka akiwa kwenye kifua cha mwanaume na uso umekaribiana na wa Peter huku akihisi pumzi ya joto ya kijana , kwakuwa kijisketi alicho vaa kilikuwa kifupi kwani hizo ndio nguo zake , basi mapaja yote yalikuwa yamegusana na miguu ya Peter kwani alikuwa amevalia bukta .
Mama Rania alijikuta akihisi joto Fulani na pumzi ya Peter ilio kuwa ikimpumulia na kujikuta hisia za mapenzi zikimpanda na kwa upande wa Peter kama mwanaume rijali alikuwa akihisi joto la ajabu sana kutoka kwenye mwili wa Mama Rania na kujikuta dunguso yake kusimama wima na kugusa mapaja ya Mama Rania.
Mama Rania alijikuta akishusha mdomo wake taratibu kwa Peter , kisha lips zikagusana na kwakuwa Peter alikuwa mgeni alikuwa haelewi haelewi chakufanya alikuwa kama mtu aliepigwa shoto na kuhitaji kunasuliwa , Mama Rania alicharuka kwani hisia zilikuwa zimempanda kiasi kwamba kwa hali alio kuwa nayo shetani asingeweza kujizuia , na ukizingatia hajakutana na mwanaume kwa muda mrefu hali ilikuwa mbaya kwake alijisemea liwalo na liwe .
Mama Rania alimshika Peter mkono na kuushikisha kwenye mapaja yake karibu kabisa na kitumbua na kumfanya Peter ahisi msisimko wa ajabu sana na uliongezeka pale Mama Rania alipogusa dunguso ya Peter.
Peter alishindwa kabisa kujizuia kwani hisia zilikuwa zipo juu na ukizingatia kuwa hakuwahi kufanya kitendo hicho tokea azaliwe, basi kujikontrol ilikuwa ni ngumu sana kwa kijana kama Peter kwani alianza kabisa kutoa ushirikiano , Mama Rania alinyanyuka na kumuinua Peter huku wakipeana juisi ya mdomoni na mwanzoni Peter alikuwa hajui hatua ila muda ulivyo zidi kwenda alijikuta akianza kuwa fundi , Mama Rania alishusha nguo yake ya ndani pasipo kuvua ile sketi na kisha akatoa na sidiria na kijiblazia alichovaa, alichukua mkono wa Peter na kushikisha kwenye hazina yake na Peter alielewa somo na kutumbukiza kidole na kuanza kazi ya kusugua na kumfanya Mama Rania atoe miguno huku akijinyonga nyonga , Mama Rania aliona kama anacheleweshwa kwani wakati huo hata haikueleweka Peter alivua saa ngapi lile libukta ,wakati huo msumali ulikuwa dede na umetuna ,Mama Rania aliinama na kupandisha kile kijisketi juu kabisa na kumwachia Peter kazi na Peter mwenyewe hakuzubaa maana akili yake hapo ilikuwa haifanyi kazi vizuri , aliingiza mtwangio wake na kumfanya mama wa watu apanue mdomo na kukugugumia kwa utamu kama wote.
Baada ya nusu saa mbele Peter alionekana fahamu kumrudia huku Mama Rania akiwa hana nguo hata moja na Peter nae alivaa bukta lake haraka haraka na kuangalia pembeni kwani alianza kujutia kwa kile alichofnya , kwani aliona kabisa ashakwisha lala na mke wa mtu.
Kwa Mama Rania wala hakuwa hata na wasiwasi , tena tabasamu lilionekana likipamba uso wake , kwake kufika kileleni lilikuwa ni historia ya muda mrefu na histora hio ndio imejirudia siku hio akiwa na kijana mdogo Peter , alitambua wasiwasi aliokuwa nao Peter hivyo aliamua kumsogelea na kisha alimkumbatia huku akimwagia sifa kedekede .
Naam ! Liwalo na liwe .
****
Samiri aliendesha gari lake kwa haraka kubwa ili kuwahi sehemu ambayo amepanga kuonana na bwana Krispine ambae ni mfanya kazi wa kampuni ya kutafuta watu ijulikanayo kwa jina la “POPOTE TUNAFIKA” , alitumia muda wa saa limoja tu kutoka mjini Posta mpaka Ubungo Landmark Hotel , sehemu ambayo ndio alipo panga kukutana na bwana huyo .
“Za Siku Nyingi Boss” Alisalimia kijana mdogo kabisa alie valia suti yake safi kwa heshima kabisa , huku akiweka mkoba wake pembeni .
“ Salama kabisa namshukuru mwenyezi Mungu kwa kila hali”
“Nimechelewa kidogo kulikamilisha zoezi hili, kutokana na kwamba sikua na muongozo wowote katika kumtafuta ila nashukuru nimefanikiwa kumpata .
“Niambie anapatikana wapi?” Aliuliza Samir kwa shauku kubwa ya kutaka kujua sehemu ambayo anapatikana
“Kwa majina anaitwa Irene mshana ni mwenyeji wa mji wa Arusha sehemiu alipozaliwa:”Alipozi kidogo huku akifungua makaratasi yalio kuwa kwenye begi lake hilo .
“Alihamia jijini Dar kwa ajili ya kutafuta maisha baada ya mama yake kufariki kwa ugonjwa wa maralia , kuhusu taarifa za baba yake na ndugu kwa ujumla sijazipata .
Hapa jijini alikuwa akiishi maeneo ya Sinza mpaka alipo jifungua mtoto wa kiume ndipo alipo hama , na taarifa kwa sehemu alipo hamia hazijafahamika kwa undani Zaidi ,lakini nimefahamu kuwa alijifungua mtoto wa kiume lakini jambo la kusikitisha ni kwamba kwa utafutaji wa kampuni tumeweza kugundua kuwa mwanamama huyu alipoteza maisha yeye pamoja na mwanae.”
Samir alijikuta kwenye mshangao mkubwa sana na maumivu makali baada ya kusikia kuwa wote wawili walipoteza maisha hapo hapo .
“ Samir alijikuta akinyong`onyea baada ya taarifa hio kwani ilikuwa ni taarifa ambayo ilisikitisha mno mbali na mategemeo yake , hasa alipo sikia kuwa mwamke yule alijifungua mtoto wa kiume ambae anamtafuta usiku na mchana ili kuja kumrithisha mali zake kwani hakuwa na uhakika na maamuzi ya mali zake kuzirithisha kwa wanae wa kike .
“Ni hayo tu mheshimiwa na kama kuna jipya nitakalo libaini basi nitakuambia mapema iwezekenzvyo “ Aliongea bwana yule na kisha akapeana mkono na Samir na kisha kuondoka .
Alikaa chini na kujifikiria kwa muda huku akihuzunika kwa uzembe wake ,lakini mwishowe alikubaliana na hali halisi kwa kuona kwamba hayo yote yalikuwa mapenzi ya Allah.
Alijkuta akitoa simu yake na kumpigia tajiri Hemedi rafiki yake
“Una baraka zangu zote, nipo tayari kukupa mtoto wangu umuoe ila kwa masharti makuu mawili la kwanza ubadili tabia yako , kwani sipo tayri kumuona mwanangu akilia kwa kuumizwa na tabia yako ,na pili najua wewe ni mtu mwenye mtandao mkubwa sana kwa hio naomba umpoteze kijana Peter kwenye uso wa hii Tanzania maana sitaki kumuona akihusika na familia yangu “ Alisema maneno hayo Samir na kisha akaagiza chupa ya bia na kuanza kunywa hapo hapo hotelini na alipanga siku hio alewe chakari kutoa mawazo.
Wahenga wanasema”Majuto ni mjukuu” na “usiloijua ni kama usiku wa kiza kinene .
SEHEMU YA 21
Peter aliekuwa amegeuka upande wa dirishani alikuwa akiona hata aibu ya kumwangalia mama huyo , kwani kitendo walicho kifanya muda mfupi ulio pita kilikkuwa ni kitendo ambacho alikiona kama ushetani au dhambi kubwa sana japo hakuwa na dini , ila aliamini kuwepo kwa Mungu mhukumu wa watu wenye dhambi na yeye aliona kuwa amefanya dhambi kulaa na mke wa mtu, ilishangaza kwa yeye kujutia kwani moja ya malengo yake katika kisasi chake ni kutembea na familia nzima ya Samiri .
Peter aliitoa mikono ya Mama Rania na kisha kumgeukia na hapo ndipo alipo kosea kwani ile anageuka tu Mama Rania alikuwa tayari ashapeleka mdomo wake na kuanza kumyonya midomo , Peter aliannza kuleta ugumu lakini aliposhikwa dunguso yake na mikono milaini ya mama huyo alijikuta akinywea kama maji kwenye mtungi na kumuacha afanye kile anacho taka , mchezo uliendelea kwani walisogea mpaka kitandani na Peter kusukummwa kitandani na boss wake Shani au Mama Rania na kisha akamvua bukta na kutupa kwenye kona ,Mama huyu alishika kirungu na kuanza kuchezea jambo ambalo lilimfanya Peter awehuke kwani kitu anacho fanyiwa kilikuwa ni cha levo ya ktabu cha ‘Super Erotic Romance’ mama alikuwa akijua mambo kwani yeye alikuwa tayari ameolewa ukiachana na historia ya nyuma ya maisha yake kabla ya ndoa ,alijua mbinu jinsi ya kumpoteza mwanaume yeyote yule kwenye dunia ya mapenzi, Peter hakufurukuta kwani alikuwa kwenye sayari nyingine kabisa , sayari ambayo hakuna mtaalamu yoyote wa mambo ya anga amefanikiwa kuiona kwa Darubini .
“Liwalo na liwe” Aliongea Peter na kumshika Shani na kumgeuza hata Shani mwenyewe alishangaa kitendo hicho cha Peter kumgeuza kwanguvu kama mbogo . alimkunja kama kambale na kuingiza mtwagio wake maana ulikuwa mkubwa wa haja na kwakuwa Mama Rania katika kujifungua kwake kote ilikuwa ni kwa njia ya upasuaji basi eneo lake lilikuwa kama la binti mdogo .
Peter alimpelekea moto mama huyu Rwanda magere anaziiita Bakora za kimkakati , haikujulikana hata ujuzi alikuwa ameutolea (hivi vitu tunazaliwa navyo ni asili ) ,Mama Rania au ukipenda muite Shani alikunjwa na kukunjuliwa na kunyoooshwa na kupinduliwa , akafika kitonga akashuka akapanda tena akashuka akapanda tena na kushuka tena na kujikuta akiweka historia ya kuukwea na kuupanda mlima kitonga kwa mara kibao.
“Asante sana mpenzi , yaani hata siamini nikajua unajuwa kuchezesha vidole kwenye komputa tu kumbe hata kwenye mwili wa mtu uko vizuri ,umenifanyia kitu ambacho sitakaa chini na kuukosa uhondo huu “ Alijidekeza kabisa huku akitoa sifa zote kwa Peter huku akisahau kabisa mkononi ana pete ya ndoa .
Basi ukawa mwanzo na mwendelezo wa kupanda vilima na kushuka , siku tatu zote walizo kuwa katika jiji hilo la Lushoto kwaminajiri ya kufungua benki katika wilaya hilo uliambatana na ufunguzi wa mapenzi yao yasio na kibali mbele za Mwenyezi Mungu, walitembea kwenye vivutio vyote vya utalii vilivyopo ndani ya wilaya hio , huku kila siku wakirudi kupeana dudu , hata chumba alicho chukua Peter ilibidi akirudishe tu kwani alikuwa hakitumii tena, ilikuwa ni mwendo wa kupeana dudu tu , kiufupi sio Mama Rania sio Peter wote walinogewa , Peter alinogewa na vitu alivyo kuwa akipewa na mama huyo na Mama Rania na yeye alijikuta hata akimdharau mume wake kabisa na kuona sasa wako droo.
“Peter mpenzi wangu nakupenda sana , yaani natamani ungekuwa wewe ndio mume wangu “ Aliongea huyu kwa mapozi kabisa ukidhania ni binti wa miaka therathini au ishirini na hajawahi kuzaa kumbe ana mitoto tena mikubwa na mizuri kabisa ambayo ipo kwenye lika la kuolewa na kuwa na familia kama kijana Peter. .
“Nakupenda pia mpenzi , siku zote sikujua kumbe hii sehemu inanoga kiasi hiki” Huku akimshika na wakati huo walikuwa kwenye gari kuelekea hotelini wakitokea eneo moja linaitwa Mkuzi huko kwenye vivutio vya utalii , na mama Rania hakuwa hata na wasiwasi yaani alikuwa akijiona dunia nyingine kabisa na alitamani kabisa kutorudi nyumbni ,wakae tu huko hata mwezi mzima , na kwa Peter alikuwa amenogewa na yeye alitamani alekitumbua tu kwani utamu aliokuwa akihisi wakati akichovya kibuyu hicho cha asali haukuwa wakawaida laiti angejua kuwa mwanamke ambae ana mkunja kila siku na kumkunjua na kuonesha ubabe wake ni mwanamke alie husika na mauaji ya mama yake sijui angefanya nini na kwa Mama Rania na yeye laiti angejua kuwa mwanaume huyo alio kuwepo hapo ndio mtoto aliotoa maagizo kwa ajili ya kuuliwa na pia ni mtoto wa mume wake na kaka wa wanae sijui ingekuwaje .
“Vipi nikununulie ndizi naona zimeiva na zinavutia “ Aliongea Peter baada ya kufika eneo moja liitwalo Magamba .
“Ndio nunua “ Alijibu Mama Rania huku akijilaza kwenye kiti.
“Peter alitoa wallet yake kutoa hela kwa ajili ya kulipa , lakini ile anachomoa hela kulidondoka kitu kutoka kwenye waleti yake alinunua kwanza zile ndizi na kisha na kuziweka mbele na kisha aliinama na kuokota , alijikuta macho yakimtoka na hapo hapo akakumbuka siku ambayo Rania alimletea waleti yake .
****
Rania tokea Peter aondoke alijikuta kwenye wakati mgumu sana , kwani kila akikumbka tukiio la Peter kumbusu kwenye paji la uso mwili wote ulikuwa ukimsisimka , kila saa alikuwa akiangalia kidani cha holder ya funguo alicho pewa na Peter , huku akikumbuka maneno yake kuwa huo ni kama ushahidi wa wao kuwa marafiki, alijikuta akitabasamu usiku huo , huku akijiviringisha kwenye kitanda .
“Lakini yupo kimya sijui ujumbe wangu hakuupata?? “ Alijiongesha mwenyewe huku akionekana kabisa kuna ujumbe alimtumia Peter haikujulikana kamtumia kwa njia gani ila alionekan kabisa kuna ujumbe ambao alikuwa amemtumia Peter na alikuwa akisubiria majibu.
“Sis....” Ilisikika sauti ikiit na kumfnya Rania alie lala kugeuka na kuangalia mlangoni.
“Waoh!, Nasma.. karibu sana, leo umekuja kutusalimia jamani nimekumisije mdogo wangu” Kumbe alikuwa ni Nasma.
“Nimekumiss pia mrembo , leo nimekuja kabisa kulala na ndio maana unaniona usiku”
“That is great , karibu sana mdogo wangu yaani ungejua nilivyo kumiss wewe acha tu , sema majukumu ndio yananibana nimeshindwa kuja kukusalimia huko nyumbni kwako”
“Mewe muongo , ila nafurahi nimekuona , unazidi kuwa mzuri tu dada yangu”
“Ahahaha jamanii.. wakati wewe ndio mzuri katika familia yetu kuliko wote”
“Ahaha.. sio kweli wote tunalingana” Aliongea Nasma huku wakionekana kufurahia kuonana, kwani japo walikuwa wakiishi kwenye jiji moja lakini ni mara achache sana kwa wao kuonana ,Nasma yeye alikuwa kiishi sehemu yake , kutokana na kwamba yeye haelewani kabisa na baba,Nasma hakupenda ukoloni wa baba yake.
“Jamani chakula atayari , dada Najma anawasubiri”Aliongea mfanya kazi wa ndani akiwakaribisha kwenda kula achakula cha usiku.
“Najma mambo!” Alisalimia Nasma baada ya kumkuta pacha wake kwenye meza akiwasubiri maana ndio ulikuwa utaratibu lazima kuwasubiri watu wote wafike kwenye meza ndipo uanze kujipakulia na kama sio sheria hio Najma angekuwa ashajipakulia mapema mno..
“Safi nakuona karibu” Aliongea Najma kwa kujilazimisha .
“Hata mimi nakuona tokea miaka mingi tulipo achana tokea uende masomoni umebadilika na umezizi kuwa mzuri “
“Ndio ila najua si kushidi wewe” Aliongea najma huku akijipakulia chakula
“Halafu jamani baba siku hizi anachelwa “
“Nani anachelewa ?: , mimi hapa nimerudi “ Ilisikika sauti kutoka mlangoni na Samir alionekana akiingia huku amelewa chakali huku akiyumba yumba na kuwasogelea wanae .
“Watoto wangu warembooo.. naonaaa… leo mmekusanyika kunijadili .. mimi baba yenu , ..hiki kikao chenu tukipe jina gani vilee.. eti Nasma mtukutu ... aa... mimi nakiita kikao cha masimango”Aliongea Samir kilevi na kumfanya najma aamke na kumkalisha baba yake kwenye kiti .
“Dadii.. mbona uko hivi leo jamanii “.
“Nilikuwa nasherehekea”Aliongea
“Ulikuwa unasherehekea nini ?”
“Najma msaidieni baba aende chumbni kwake acha kumuuliza maswali”Aliongea Rania
“Nilikuwa nasherehekea kupatikana kwa mchumba wa Rania “Aliongea kilevi na kumfanya Rania ashituke na kumwangali baba yake huku Nasma na Najma wakimsadia baba yao apande ngazi kueekea juu chumbani
“Hii tabia ya baba kulewa kaanza lini Najma?”Aliuliza Nasma
“Mimi hata najua sasa , ila kaanza wiki ya tatu hii na leo kawahi “
Nasma ndio alikuwa kulwa na Najma alikuwa doto.
Basi walirudi na kuanza kupiga stori , huku Rania akiwahadithia kuwa yupo mbioni kupata mchumba jambo aambalo wadogo zake walishangaa huku wakitabasamu .
“Anaitwa nani huyo ?”
“Anaitwa Peter”Alijibu bila hata ya wasiwasi
“ Jamanii ..natamani kumuona , kwa hio mshaanza kuwa na mahusiano au ni mapenzi ya mtu mmoja “ Aliuliza Nasma
“ Bado ila naamini ana nipenda maana ashanipa zawadi na kasema yeye ni tofauti na wanaume waliopita , kasema hayuko tayari kuniacha”
“wow ! jamanii.., am so so happy for you sis..”Aliongea Nasma
“Na wewe Nasma vipi ?”
“ Yes , yes .. me too” Alijibu huku akijifumba uso kwa mikono na kumfanya Rania acheke na Najma kumwangalia huku akilazimisha tabasamu .
“Haha what ! ,So all of us we are in love , how if we arrange a day kukutanishana sisi wote na wapenzi wetu au mnaonaje? Aliongea Rania
“Kwa hio hata Najma ana mpezi tayari ?”
Hapo ndipo alipo haribu kwani Najma aliondoka bila ya kusema kitu na kukimbilia ndani kwake , alifika na kujikuta akianza kulia kilio cha kwikwi.
“Uko wapi , mbona sikuoni , mbon aunaufanya mtima wangu kuwa katika maumivu kwa kiasi hiki , nakupenda njoo unitoe kwenye haya haya mawingu ya sintofahamu” Aliongea Najma kwa hisia huku akitoa machozi laiti angejua mwanaume anae mlilia ni kaka yake angeacha mara moja, lakini ndo hivyo kosa si lake kupenda kosa linaanzia kwa baba kumtelekeza mwanamke huku ilihali akijua ni damu yake , sasa watoto wanakuja kumpenda mwanaume huyo huyo ,huku mama nae akinogewa na mwaname huyo huyo
“Wanaume wajibikeni na matendo yenu madhara yake yanakuja kuwa makubwa sana na ni kama haya yanayo onekana kwa familia hi ” Maneno ya mwandishi yanywe au yateme
“Halafu mbona na wewe umenuna ghafla “ Aliuliza Rania .
“Sijakutana na mpenzi wangu bado , kwani tumekutana mara moja tu na jina simjui” Aliongea Nasma nakumfanya na yeye kushangaa
“Mhmh! basi wewe na Najma mko sawa “
“Una maanisha nini dada ?”
“ Namaanisha na yeye amependa mwanaume ambae hamjui”
Nasma na yeye alishangaa huku akimuelewa pacha wake ni maumivu kiasi gani aliokuwa akipitia kwani alikuwa akijua ni jinsi gani inauma kumpenda mtu ambae bado haujamfahamu vizuri na huna namna ya kuonana huku ukisubiria bahati ya Mungu kuwakutanisha tena ..
****
Peter alijikuta akichukua ile picha na kuigeuza nyuma na kuona maneno yameandikwa , Mama Rania alikuwa akimuangalia hivyo aliamua kuweka ile picha kwenye waleti na kisha akaendela na safari .
walifika ndani na kisha waliagiza chakula na kuanza kula na kumaliza na kisha wakaanza kuangaliia movie huku wakiwa wamekaa kwenye pozi la kimahaba kabisa , hakuna hata mmoja alie kuwa na wasiwasi.
“Nikifika nataka kukununulia nyumba kubwa mpenzi”
“Unasema kweli?”
“Ndio natamani hata ya kuishi na wewe , ila nina mume nitakununulia nyumba na nitakuwa nakuja mara kwa mara kufurahia penzi letu”
“Asante mpenzi nakupenda sana”Huku wakianza kunyonyana na hata ile muvi ikaachwa kuangaliwa na kuanza kunyanduana na kijana huyu ambae kusudi la kwendca kufanya kazi kwenye benki anayosimamia mwanamama huyu ni kwa sabababu alitaka kulipiza kisasi kwa Samiri kwa kitendo cha kumdharau , na katka kisasi chake hicho alikuwa amedhamiria kulala na wanae wote ,lakini sasa anamkula mama mtu huku watoto wa mama huyu wakiliwazia penzi la Peter yaani kisasi kinajilipa chenyewe .
Kwa yaliokuwa yanafanywa na wawili hawa pamoja na historia zao ilikuwa ni jambo la kutisha kweli kweli ,Mama Rania hakumuona tena Peter kama mtoto , tena mtu ambae alikuwa anapaswa kutembea na mwanae Rania , alimuona kama mwanaume Tena mwanaume wa kukidhi haja zake zote .
Baada ya kumaliza kufanya waliokuwa wanafanya mambo ambayo \mnele za Mungu hayakuwa na kibali , Mama Rania alipotelea usingizini , na Peter alitumia wasaa huo kuangalia kile alichokuwa na hamu ya kuona muda wote
Ilikuwa ni picha ya mrembo Rania picha ambayo ilikuwa imekatwa kipande na kufanywa kama passport , huku ikimuonesha kimwana huyo kupendeza kweli kwa tabasamu lililopamba uso wake ,Aliangalia kwa sekunde kadhaa picha hio na kisha aliigeuza nyuma na kusoma vimaandishi vidogo vilivyoandikwa . “Najua ni kipindi kifupi nimekufahamu ila umekuwa na mchango mkubwa sana kwenye furaha yangu na umenitoa kwenye kiza kinene sana juu ya mtazamo wangu kuhusu wanaume nimegundua kuwa wewe ni mwanaume wa kipekee sana , na mwanume ambae ninaweza kuishi nae , nimetokea kukupenda sana Peter nipo tayari kuwa mpenzi wako naomba unikubalie na usinione mimi kama maaya ni hisia zangu juu yako nitasubiri jibu lako ni mimi rania nakupenda sana peter naomba unifikire na unipe jibu linalotoka ndani ya moyo wako sitaki kuumia tena”
Peter alijikuta jasho likimtoka huku akiwa haamini kwa kile anacho kisoma , kwa upande wake ilikuwa ni jambo ambalo angeshangilia kwani ni kitu alicho kuwa akikitaka kwa mrembo huyo kutoa bikra tu na kuondoka zake kwani aaatakuwa kashalipa kisasi , ila maneno yale yalimfanya apatwe kutokana na kwamba japo maandihi yale yalikuwa machache lakini aligundua kuwa yalikuwa yamebeba hisiaa nzito mno .
SEHEMU YA 22
“Nadhani ni wakati wa kutafuta mrithi wangu sasa nishachoka kuongoza kampuni nataka nibakie kwenye bodi tu ya kampuni” Aliongea Profesa Gladness.
“Sasa profesa utamwachia nani kampuni , wakati hakuna mtu ambae anafikia hata nusu yako”
“Mary ukiona natamka haya maneno jua nishapata mtu wa kukalia kiti changu”
“Ni yule mtu anae husishwa na viumbe kutoka sayari nyingine au kuna mwingine?”
“Kuhusu hilo nitaliweka wazi hivi karibuni haina haja ya kuwahi kuwaambia” Aliongea profesa Gladness bila ya kumtajia jina Mary kwani alikuwa ni shushu na hapo alikuwa yupo kiuchunguzi Zaidi kwa kile kilicho kuwa kinaendelea .Na uzuri wa profesa Gladness hakuwa akimuani mtu , na hio ndio slogani yake..
“Boss kuna wageni wako wamekuja kukutembelea “ Aliongea Mary na kumruhusu awaingize.
“ Haa…!! Mom .., dadii” Aliongea Gladness na kuwakumbatia wazazi wake ambao alikuwa ni Rafaeli na Nifani
“Mmerudi lini nchini ?”
“Ndio tumeingia leo hii nchini ,tumepitia KIA”
Gladness alifurahi sana kukutana na familia yake hio , kwani ni kipindi kirefu kidogo tokea wasafiri , kwani walikuwa wakila bata tu , na kutembelea nchi mbali mbali .
Basi familia hio walitoka na kwenda nyumbani kwa gladness sehemu ilo kuwa ikijulikana kama kijiji cha maroboti au Village G.
“UNAITWA RAFAELI MSWAKI UNAMIAKA 65 ,UFANYAJI KAZI WA TEZI YA MAFUTA MWILINI IMEPUNGUA KUFIKIA NUSU YA UZALISHAJI WAKE , PRESHA YAKO NI 137/88mmhg …, NGOZI ISHAANZA KUKUNJAMANA , UWEZO WA KUFANYA MAPENZI UMEPUNGUA KUFIKIA ROBO TATU,KWA MAKADIRIO UMEBAKISHA MIAKA SI CHINI YA KUMI KAMILI UTAKUWA USHAKUFA”
Ni baada ya kuingia tu ndani ya nyumba ya profesa Gladness na roboti lifahamikalo kwa jina la Nimrod lilimscan(skani) Rafeali na kutoa hayo maneno.
“ Nimrod tulia “ Aliongea Gladness na roboti hilo likiondoka zake huku lishaharibu hali ya hewa kwa kiherehera cha kumchunguza kila mgeni anaeingia nyumbani kwa Profesa Gladness.
“Daaa! Wewe mtoto maroboti yako yashaanza kunipa stress” Aliongea Rafeli kwani alikuwa hajui kuwa kabakisha miaka kumi mpaka kufariki kutokana na maneno na uchunguzi wa Nimrodi.
“Hapanna baba kuna muda mwingine yanakosea” Alijitetea gladness huku akimwangalia Rafaeli ambae alionekana kweli ashaanza kuwa mzee kibabu .
“Umesikia mke wangu huko ,nimebakisha miaka kumi tu kufa “
“Mume wangu bwana hayo ni maroboti “
“Kama ni maroboti basi ngja niliiite likuchunguze na wewe na wewe”
“ Hapana .. hapana .. mimi sitaki kujua nitakufa lini”
“Ahaha .. wewe si umesema hayo ni maroboti .. mbona unaogopa sasa”
“Ahahaha..mume wangu wewe anza kukaa na watoto wako vizuri na tumia muda mwingi kuwa nao “
“Ila limenidhalilisha lilivyo sema , siiwezi kazi ya chumbani vizuri .. hii dunia inavyo endelea hivi hatutaweza tunza siri kweli”
“Hahaha .. mume wangu ushakuwa babu tayari bhana “
“Na wewe si bibi kizee”
Hao walikuwa ni Rafeli na Nifani wakiwa nyumbani kwa mtoto wao mkubwa Gladness.
*****
Masumbuko kama kawaida yake alikuwa kapiga zake nne hana habari huku pembeni akiwa na vijifuko vya Ice cream akiwa anakula na kilicho kuwa kikiangaliwa kwenye TV kilikuwa ni filamu za ngono , maana kila siku kwake alikuwa akiangalia kwa dozi
Alikuwa haamini kama kweli hana nguvu za kiume
“Aaa…. Masumbuko vipi tena na hizo video “ Aliongea Peter huku akionekana kushika kijibegi na muda huo alikuwa akionekana kabisa kuwa alikuwa akitoka safarini na ndio anarudi.
“ Zinanitia mzuka na mori mori” Aliongea masumbuko na kumfanya Peter atabasamu .
“Wewe si uneenda tu hapo nje na kumpa mwanamke kumbukumbu ,unamleta humu ndani unafanya yako , kama siku ile “
“Una maanisha kama kubaka vile , si ndio “
“ Nani kakwambia kubaka , pale haulazimishi mtu bhana “
“Yule mshikaji alikuja na akaniambia kuwa kitendo kile ni kubaka “
“Mshikaji gani huyo ambae una mzungumzia ?”
“ Yule wa siku ile , Sebastiani yule”
“ Kwa hio alikuaja hapa nyumbni na ukamfungulia?”
“Ndio alikuwa anagonga mlango kwa nguvu , ndio nikamchungulia na nilivyo muona ni yeye nikajiuliza nifungue au nisifungue ila ndio nikajikuta nishafungua mlango”
“Na alisemaje sasa?”
“Hana tu ndio alinisifia tu kuwa yule mwanamke nilimpa dozi kali ya kumbaka”
Peter ilibidi amuangalie tu Masumbuko na kisha kutabasamu maana aliona kichwa cha ndugu yake huyo wa hiari kilikuwa signal zinasoma na kupotea .
Basi Peter baada ya kuweka vitu vyake vizuri alikaa sebleni huku akionekana kuna jambo linamsumbua kwani aliionekana al kiwa kwenye mawazo , huku masumbuko yeye akiwa hana hata habari .
“Peter haya magorofa marefu ushawahi kuingia?”
“Aliuliza Masumbuko na kumshtua Peter alie kuwa kwenye mawazo .
“ Sikia Masumbuko , utaniuliza baadae sasa hihvi ngoja kuna sehemu naenda maramoja “ aliongea Peter na hapo hapo akatoka hadi nje na hakuchukua gari Zaidi ya kuchukua ufunguo wa honda yake .
“Ngoja na mimi nikazunguke zunguke huko mjini “ Aliongea Masumbuko huku akivaa nguo nyingine na kuchukua buku na kutoka . alitembea mpaka barabarani na kupanda daladala inayoelekea tegeta nyuki kwenda kariakoo “
“ Unaenda wapi?”
“Gari linapo simama “ Alijibu na kuingia ,muonekano wa masumbuko ulikuwa umebadilika kwa kiasi kikubwa kwani alianza kunenepa sio kama alivyo anza kuja, kwani alikuwa akionekana amekauka ngozi ,sasa alikuwa amejaa na kifua utadhaniaa alikuwa anapiga chuma bau kwenda gym
****
MAREKANI (USA)
Katika jiji la Calforinia Alionekana profesa Snart akiwa na mwanaume mmoja hivi mwenye muonekano kama wa kiarabu ndani ya hoteli ijulikanao kwa jina la The Royal iliopo katikati kabisa ya jiji hilo .
“Paco , lete habari za misituu ya amazon .“
“ Mkuu kwanza nafurahi sana kwa kunipa ofa ya kutembelea jiji hili , unajua kutokana na kazi yangu nakuaga sina hata muda wa kufika huku ,kwani hata hali yake ya hewa sio nzuri kama ya kule msituni “
“ Yeah paco upo ndani ya jiji lenye makazi ya watu wengi na shughuli nyingi lazima hali ya hewa iwe tofauti na ya msituni “
“ Yea ni kweli “
“Uliniambia una taarifa muhimu kuhusu Queen ya kuniambia?”
“ Ndio kwanza yuko wapi kwa sasa nataka kumuona kabla sijakueleza taarifa yenyewe “
“Paco , Paco , Queen wa sasa ni mtu maarufu sana na hata nikiuonesha saivi sijui kama utamtambua kama ulivyo kuwa unamuona kule msituni , sasa hivi ni Zaidi ya mrembo “
“ Una maanisha nini kusema hivyo?”
“ Sikia Queen ile ni siraha yangu , yule ni Zaidi ya bomu la nyuklia , kwanza ana akili , hana utu kabisa na pili hajui chochote kuhusu Mungu , na harufu inayo mfurahisha ni kuona damu ya mtu inamwagika muda wote , na pia hana hisia za mapenzi kabisa kama unavyofikiria ni kwamba hawezi kupenda mwanaume yeyote yule , kwani yule muundo wake sio kama wa binadamu wa kawaida , yule nimemtengeneza na nilipata hasara kubwa kwa ajili yake lakinni mpango wangu ulifeli”
“ Una maanisha nini ukisema umemtengeneza Sbart?”
“ Yule hajazaliwa kama wewe ulivyo zaliwa na wazazi wako na pia una ndugu, Queen yule hana ndugu wala wazazi , na kwangu Queen ni kama kifaa changu cha kazi , kwani ninapo agiza kinafanya , sasa nadhani hakuna haja ya kumfatilia sana Queen maana kazi yako ulishamaliza ya kumfundisha Queen , sasa wewe niambie hilo jambo ambalo unataka kuniambia “
“ Ni Kwamba Queen kunamuda nilikuwa kama simuelewi, ni kama anajua kumsoma mtu kila anacho kifikiria akimwangalia tu kwenye macho , kwani wakati nikichukua mazoezi nae alikuwa akinipiga mapigo ambayo hata siyaelewi ,kila pigo nililokuwa nikifikiria kumpiga nalo , ni kama tayarri alikuwa ashajua kile ninacho kifikiria na anakuwa tayari ashajua udhaifu wa pigo langu na anakuwa ananichakaza na kipigo kibaya sana”
“Una maanisha nini kusema hivyo bwana Paco?” Aliongea Snart kwani taarifa hio ilikuwa ni mpya kwake .
“ Mkuu Queen ni hatari sana , kwani ana uwezo ambao sio wa kawaida kama binadamu”
Aliongea bwana Paco ambae ndie alikuwa ni master(mkufunzi wa kimapigano) wa Queen wakati alivyo kuwa nchini brazili kwenye msitu wa amazon , ndie alie kuwa akimfundisha Queen kuua , kwani walikuwa wakienda na kukamata watu na kuwanyonga na kuwachinja bila hata huruma ,nakuwaua wanyama wakali sana kama Anaconda joka anae patikana kwenye msitu huo , Chui na Simba na mafunzo hayo Queen aliyaweza kwa muda mfupi tu.
“Nadhani misheni yangu haikufeli(it was not a failed mission) , Queen atakuwa anaficha uwezo wake inanibidi kufanya utafiti upya. “ Aliongea huku akivaa koti lake la kuingilia maabara yake ndani ya kasri lake ndani ya hapo Calfornia alikuwa akiwaza maneno alioongea Paco mara baada ya kukutana nae hotelini . .
****
Masumbuko alikuja kushushwa na gari katika kituo kimoja kilicho kuwa kina fahamika kama muhimbili na hio ni baada ya kuvutiwa na majengo yalio kuwepo katika eneo hilo ,ndio maana alimwambia konda kuwa keshafika anataka kushushwa.
Alianza kutembea huku akishangaa majengo hayo na muda huo ulikuwa ni saa kumi inaenda kama na robo hivi , alinyooshana kinjia flani kinapandisha kwenda juu kwani kulikuwa na kijimlima na kutokezea kwenye barabara mbele huko kwenye mtaa mmoja ujulikanao kwa jina la mindu, alinyoosha na bara bara hiio na kuja kufika sehemu moja kwa mbele yake kulikuwa kukinekana mwendokasi inazunguka na kuna kibao kikubwa kilicho andikwa ‘HOSPITALI YA MUHIMBILI’.
“Mama hivi ni vidude gani?” Aliongea Masumbuko baada ya kufika kwa mama mmoja alie kuwa akiuza koni , sasa Masumbuko aliona vile vya kuwekea koni ndivyo alivyo kuwa akiulizia.
“Ni koni hizi ni miatano tu moja “
“ Hii inatosha alitoa Masumbuko mia nne na kumuonesha yule mama , na hi ni hela alio rudishiwa chenchi kwenye ile buku (elfu moja)ya nauli maana gharama za usafiri ilikuwa ni mia sita na hapo alitoa yote na mama yule ampatia .
“ Kumbe tamu hivi nitakuwa nakutembelea mara kwa mara “
“ Sawa lakini siku nyingine nitakuuzia kwa miatano “
“ Sawa “
Aliongea huku akitemeba huku na huko akishangaa shangaa mpaka inatimia saa kumi na moja na nusu alijikuta amezunguka amezunguka na kurudi pale pale muhimbili , Alipanda gari bila ya kujiuliza ana nauli ,gari alio panda ilikuwa inaenda Masaki na ilikuwa imejaza kweli na Masumbuko aliwekwa mwisho kabisa ya gari kiasi kwamba kwa jiinsi watu walivyo kuwa wamejaa hata konda ingekuwa ni vigumu kwake kupita na kuomba nauli.
“ Hivi ule mtaa tunao kaa unaitwaje?”Alikuwa akijiuliza kwenye gari huku linaondoka maana hakujua ile sehemu jina.
“Ila nitapaona tu halafu nitashuka”
Sasa konda kwakuwa nafasi ilikuwa imebana sana , alikuwakichukua nauli kila unapo shuka.
“Macho ,Macho hio , kuna anaeshuka ?”Aliongea konda na hapo hapo Masumbuko akaropoka kwa sauti nimefika mpaka watu wakamwangalia.
“Njoo sasa umekaa huko nyuma halafu unajua unashukia hapa karibu”
Aliongea konda baada ya gari kusimama huku Masumbuko aliependeza akishuka , kwa jinsi alivyo kuwa amependeza usingedhania kuwa wakati huo hakuwa na kitu chochote mfukoni hata nauli .
“Toa hela , unapoteza muda bwana , unashangaa nini?” Masumbuko alimwangalia yule konda huku akiwaza afanye kama kawaida yake maana alijua nauli hana .
“Usijali nitamlipia” ilisikika sauti moja nyororo na kufanya hata wale walio kuwa kwenye daladala wamwangalie anaeongea , lakini ni kwamba tayari alikuwa ashachelewa maana Masimbuko ashachezesha jicho tayari na kumpachika masaa mawili ya kumbukumbu.
“Aaa.. aa hapana . ashalipa tayari mremboo hata usisumbuke ” Aliongea konda huku akigwaya gwaya na kufanya abiria waanze kucheka na hata dereva mwenyewe alijikuta akicheka na hapo ndipo ikawa gumzo kwenye daladala maana wengi walijua konda alichanganyikiwa na yule mrembo na ndio maana alikubali Masumbuko kashalipa, wengi walimhurumia pasina kujua uwezo Masumbuko. .
“Sema ni haki yake aisee , unajua yule mwanake ni mrembo sijapata ona .. na kwa ile sauti konda ni haki yake kuchanganyikiwa , ila kanifurahisha sana leo
.. hakuna mwanaume mjanja mbele ya utamu “ Aliongea jamaa mmoja lio kuwa amevaa kanzu kasimama kwenye daladala hio alikuwa na rafudhi ya kipemba .
“Nyie mnaongea nini nyie , mimi siwezi kuchanganywa na mwanamke, yule chalii kalipa kabisa nina uhakika.” Aliongea konda na hapo ndipo vicheko vilivyo zidi kabisaa
“Aisee nilikuwa na stress ila zishaisha daah .. aisee” Aliongea jamaa mmoja nae alieshikilia mfuko mdogo hivi uliokuwa na samaki akionekana kufurahishwa sana na hilo tukio.
****
Peter alisimamisha honda yake kwenye nyumba moja maeneo ya makongo juu na kisha akabonyeza kengele na hapo mlinzi alifungua
“Bwana Peter karibu sanaaa..” Aliongea mlinzi alionekana kumfahamu Peter
“Nimemkuta Steve?”
“Ndio yupo hajatoka leo “
Basi Peter alienda moja kwa moja mpaka ndani ya nyumba hio ilikuwa nzuri sana kwa jinsi ilivyojengwa.
“Mwanagu huyo , nona leo umekuja kutusalimia?”
“Ndio mama shikamoo “
Huku wakisalimiana kwa furaha na huyo mama aliononekana kuwa mkarimu kweli , alikuwa mnene kiasi mfupi alievalia dera lililoacha mabega wazi.
“Nimemfata Steve “ Aliongea Peter na kuambiwa kuwa yupo chumbni kwake aende tu.
“ Mzee mwenyewe naona usharudi karibu”
“Yeah mzee , nimerudi, nina mawazo nikona nije kabisa nisikusumbue kwa kukuita magetoni”
“Mawazo gani tena mzee si umetoka safarini?”
“Mambo ya kisasi mzee, naona kama kigumu vile kutekelezeka , unajua nilikuwa nachukulia simple sana ila sasa na uona ugumu wake”
“Ugumu gani sasa wewe si ulikuwa wajisifia kuwa unaswaga nyingi kibao , tantalila nyingii sasa umepigwa kibuti ndio unaona ugumu “
“Si hivyo ndugu yangu , simaanishi hvyo yaani bora hata ningepigwa hiko kibuti , lakini sasa hivi nishamla mke wa Samir tayari na mtoto wake kanambia ananipenda na anasubiria jjibu langu”
“ Unasema ushakula kitumbua cha lile limama tayari na lile lishepu “ Aliongea Steve kama haamini vile kwani aliona kama masihala vile , kwa maneno alio kuwa akizungumza . na wakati wanaongea ndio hapo , simu ya Peter ilitoa mlio kuwa ilikuwa inaita .
“ Oya huyu hapa anapiga kama huamini ngoja niweke loud speaker” Aliongea huku akipokea na kuweka loudspeaker .
SEHEMU YA 23
Peter aliweka simu ile kwenye loudspeaker baada tu ya kupokea na kuanza kuongea na Mama Rania.
“Vipi mpenzi mbona unachelewa kupokea simu?” Ilisikika sauti iliokuwa ikilalama na kumfanya Steve kutoa jicho kama kabanwa na mlango kwani hakuamini kabisa kile anacho kisikia , na sio kama jambo hilo ni geni kwake kuona kijana kufanywa kiben ten , lakini hadhi na heshima alio kuwa nayo mama huyo ni vitu ambavyo kwake aliona kama ajabu vile.
“Nilikuwa nipo chumbani simu niliacha living room (sebuleni) “ Aliongea uongo Peter.
“ Jamani mpenzi unajua nilivyo kumiss , natamani sana tukutane hata twende mzunguko mmoja “ Aliongea Mama Rania .
Laiti angejua kuwa amewekewa loudspeaker asingeongea hilo neno , Peter hakutaka Steve aendelee kusikiliza , alitoa loudspeaker na kulala kabisa kitandani na kuanza kuongea huku Steve yeye alikuwa amesimama kama mnara akimwangalia rafiki yake , na kuna kitu alikuwa ashakigundua kwa Peter alikuwa ameona dalili zote za rafiki yake kuonogewa , alikuwa mzoefu wa hayo mambo .
“Daah..! unajua ni hatari hio rafiki yangu”
“ Naelewa , ila Steve yaani kila nikiongea na huyu mwanamke dudu inasoma channeli hapo hapo na mawazo yangu yanabadilika”.
“Fanaleki ushanogewa wewe , na hivyo ni mwanamke wako wa kwanza kazi unayo , mimi naogopa tu mume wake akijua sijui atakufanyaje, naogopa sana ukiingia kwenye matatizo”
“Steve ndio maana nipo hapa unipe ushauri wewe ni rafiki yangu naamini utanipa ushauri mzuri”
“Sasa wewe unataka mimi ni kwambie nini na wakati wewe mwenyewe ulisema unaenda kwenye ile benki kwa ajili ya kisasi ,lakini saivi unaonekana umenogewa tayari , mimi nakushauri uache kabisa hio misheni yako , lakini kuhusu huyo Rania na mama yake , kaa chini fikiria , jiulize maamuzi utakayo fikiria na kuamua yatakuwa na madhara gani ukishalijua hilo basi mimi sitoingilia maamuzi yako ,lakini nakupa hint tu , kwamba unacho kifanya sio kizuri na ni hatari sana ,mke wa mtu sumu ndugu yangu”
“Poa mzee mimi nitafikiria cha kufanya , ila asante sana kwa maneno yako , ngoja nirudi home ni muwahi Masumbuko” Aliaga na Steve alimsindikiza mwenzie.
****
Nasma baada ya kukaa siku kama nne nyumbni kwao , hatimae aliamua kuondoka na kurejea sehemu alio kuwa akiishi , japo ya Rania kumbembeleza sana kuhusu kubaki kwani ana ichangamsha familia , lakini hakukubali na mama yake pia alijaribu kumshawishi lakini alisimamia msimamo wake .
Alipanda kwenye gari yake na siku hio alikuwa akiendesha yeye mwenyewe pasipo ya kuwa na Lucy mfanyakazi wake , aliendesha gari lake mpaka kufikia maeneo ya Macho , sasa wakati yuko kakodoa macho barabarani kionyesha umakini katika barabara hio ndipo daladala ilio kuwa ikija upande wake ilisimama mita chache mbele yake , hapo ndipo mapigo yake ya moyo na mshangao kwa ujumla vikamtawala, kwani mwanaume alie kuwa akimuota usiku na mchana alimuona kabisa mbele yake , kwanza aliona kama kamfananisha lakini kadri alivyo sogelea gari lile ndipo alipo kuja kugundua kuwa ni yeye.
Alipita daladala ile na kisha kasimamisha kwa mbele na kutoka haraka haraka huku akiwa kabisa amesahau kufunga hata mlango na kukimbilia sehemu ile , ndipo alipogundua kuwa mwanaume yule hana nauli na alikimbia na kisha kumwambia konda kuwa atamlipia , lakini kilichomshangaza kwa mara ya pili kwani mara ya kwanza jambo kama hilo lilikuwa likitokea tena ,pale konda alipomuambia kuwa ashalipa na wakati kwa masikio yake kabisa alisikia konda huo akimdai Masumbuko nauli , lakini kutokana na hamu yake kubwa ilikuwa ni kumuona Masumbuko aliachana na hilo swala na kisha kumsalimia .
“Mambo!” Alisalimia kwa shauku kubwa Nasma huku akimwangalia Masumbuko ambae wala hakuwa hata na time nae kwani alikuwa bado akishangaa hayo maeneo kana kwamba ataiona nyumba wanayoishi .
“Hivi sista naomba nikuulize , hivi unajua eneo ambalo lina magorofa magorofa machache halafu .. halafuu.. enhee .. kuna shule halafu na barabara .. halafu..nini tenaa.. kwa mbele kabisa kuna kanisa kubwa .. unaijua hio sehemu?”
Aliongea Masumbuko huku akionekana kabisa yuko seriasi na swali lake na kwa Nasma alikuwa akishangaa maana swali lenyewe hajalielewa .
.“Mambo kwanza” Aliendelea kusalimia Nasma kwani kwanza alikuwa ana aibu na hata hapo alikuwa hajui afanye , kwani ni kweli alikuwa akihitaji kuonana na Masumbuko lakini hakuwahi kufikiria siku akionana nae ataanza anza vipi kuongea nae na ndio maana aliendelea kusalimia lakini kwa masumbuko wala hakuwa na habari kichwa chake wakati huo kiliwaza nyumbani tu.
“Ila hapa sio penyewe hapa , sijui patakuwa ni upande gani ule . halafu .. , dada mbona haunijibu sasa “
“Sijakuelewa “
“ Ni kweli huwezi kuelewa maana nina maswali magumu” Huku akiondoka na kumfanya Nasma amwangalie Masumbuko akichapa raba hana hata habari kuwa mtu alie mfuata alikuwa akikesha usiku na mchana kumtafuta na kumuwazia alijikuta chozi likimdondoka bila hata ya kujua .. sasa wakati ameduaa akimwangalia Masumbuko ndipo alipo kuja kama kuzinduka na kuita
“Kaka , nisubiri” Masumbukoo alisimama na kumwangalia Nasma anae mkimbila .. na kwa jinsi alivyokuwa akimkimbilia kwa mapozi na uzuri wake na jinsi Masumbuko alivyo kuwa akumwangalia ilikuwa ina pendeza kama vile ni filamu za kihindi.
“Nimepajua hio sehemu ulio kuwa unasema”
“ Kweli … kuna kanisa .. kuna shule kwa nyuma na barabara katikati … si ndio ni hapo”
“Ndio “
Jibu hilo lilimfanya Masumbuko aachie tabasamu na kuufanya uhendsome wake uonekane na kumfanya Nasma amwangalie kama anamshangaa ..
“Twende kwenye gari .. nikupeleke “ Masumbuko hakuleta shida kwani hi ndio jambo ambalo lilikuwa likimpa shida kwa wakati huo na hivyo alimchukulia Nasma kama mtu ambae anaweza kumpatia msaada .
Basi aliingia kwenye gari na safari ikaanza na kwa Nasma kwakuwa alikuwa ana kichwa chepesi sana kuelewa ni kwamba aligundua kuwa Masumbuko yuko , kwenye hali ya wasiwasi na ndio maana hakuwa akimpa ushirikiano .
“Kwa hio kaka ulikuwa umepotea?”
“ Ndio mimi ni mgeni na haya maeneo “ Aliongea Masumbuko huku akiangalia nje ya gari na muda huo kajigiza kalikuwa kashaanza kuingia , na kuna wakati Nasma alikuwa akimwangalia Masumbuko kwenye kioo .. aliishia kutabasamu tu na alionekana moyo wake kuwa na Amani na furaha sana . Kwani aliamini mwanaume alie kuwa akimtafuta hatimae amempata .
“Hapo hapo nimepaona simamisha gari “ Aliongea Msumbuko kwa sauti na kumfanya Nasama asimamishe gari na masumbuko kuomba kufunguliwa mlango , na Nasma alipo mfungulia tu tayari alikuwa ameshatoka tayari kwenye gari .
“ Dada asante sana .. nimepafahamu ni hapa kabisa “ Aliongea Msumbuko na kwa wakati huo walikuwa washafika eneo la Mbezi Beach ilikuwa ni bahati kwa masumbuko kwani isingekuwa Nasma kuishi hayo maeneo asingeweza kurudi nyumbani. .
Masumbuko alindoka huku akisubiria kuvuka barabara na kumfanya Nasma na yeye kutoka kwenye gari na kumfuata Masumbuko kwa nyuma hakutaka kumpoteza tena , lakini kilichomshangaza Nasma ni kwamba nyumba alio ingia Masumbuko ni nyumba ya pili na ya kwake ilipo.
“Yaani kumbe huyu mkaka kumtafuta kote kule kumbe ni jirani yangu “ Aliongea Nasma huku akijikuta akitabasamu tu nakuona kuwa mageti muda mwingine yanakuwa hayasaidii maana yanafanya usijuane na majirani, alikaa kama dakika kama tano akiangalia nyumba hio ilioenda hewani kwa gorofa nne na kisha akatoka akafara gari yake na kwenda hapo mpaka kwenye nyumba yake na kuingia na kisha akampa mlinzi ufunguo akimwambia akachukue gari ameliacha kituoni , mlinzi alishangaa ila alichukua ufunguo kwani hakuruhusiwa kuuliza swali .
***
“Ulikuwa umeenda wapi umenifanya niwe kwenye wakti mgumu kiasi hicho “ Aliongea Peter huku akionekana kuwa na wasiwasi sana .
“ Nilienda kula bata kidogo ndio nimerudi “
“Nikajua umepotea huko njiani . inabidi kesho nikakununulie simu “
“Mimi siwezi kupotea ni mgeni lakini nayajua maeneo vizuri”Aliongea Masumbuko na kumfanya Peter atabasamu na alichogundua alijua kuwa Masumbuko alikuwa akipenda sana kujisifia .
“ Haya lakini usitoke toke tu utapotea au kugongwa na gari huko ndugu yangu , unafikiri nitaishije “
Aliongea na kuachana na Masumbuko kwani alijua pia ni mtu mzima hatakiwa kumlinda ila anatakiwa kumuonyesha mazingira na kumtembeza tembeza ili asipotee.
*****
Siku ilio fuata Peter hakwenda kazini na alibaki nyumbni kwani alikuwa amepewa siku mbili za kubaki nyumbani , kwenye muda wa saa kumi na moja ndio muda ambao Peter alipigiwa simu na Mama Rania kuwa wakutane barabarani kwenye kanisa la KKKT usharika wa Mbezi Beach .
Peter alivaa vizuri na kisha akatoka zake baada ya kumuaga Masumbuko ambae alikuwa akichezea simu ambayo amenunnuliwa asubuhi hio
“Peter aliingia kwenye gari yake , maana Mama Rania alimwambia kuwa aje na gari yake , baada ya kufika tu kweli alimuona Mama Rania aliekuwa amevalia gauni flani lenye mikanda huku akiwa ameshikilia pochi kubwa na alikuwa amependeza kweli ,kwa jjinsi alivyokuwa akionekana utadhani ni mwanmke ambae anaenda dating kwa mara ya kwanza , Peter alienda kufunga beki kwenye miguu ya mama huyo na kufungua kioo na kumfanya Mama Rania atabasamu na kuingia kwenye gari na kisha likaondoshwa na kwa maelekezo ya Mama Rania walikuja kukunja baada ya kufika eneo moja linaitwa jogoo na kuchukua upande wa kulia na gari ilitembea kwa dakika kadhaa na ikasimama nje ya geti kubwa na baada ya dakika kadhaa gari hio iliingizwa ndani ya jumba hilo , hapo ndipo Peter alipo patwa na mshangao kwani jumba hilo lilikuwa moja ya jumba kubwa sana na lilikuwa na mazingira mazuri kwani kulikuwa na swiming pool upande wa kushoto ukiingia ilio zungukwa na bustani na majani yalio chongwa kwa ustadi mkubwa sana , jengo hilo limepakwa rangi ya kuvutia nyeupe lakini ilio fifia na kupendeza sana .
“ Kwanini tuko hapa?” Aliuliza Peter maana alikuwa akiona mapicha picha tu .
“Hii ndio itakuwa nyumba yako mpenzi ‘ Aliongea Mama Rania .
“ Whaat.. usiniambie kuwa umeinunua hii”
“Sijainunua leo wala jana ilikuwa ni yangu ,japo hakuna mwanafamilia anae ijua na sasa nasema nyumba hii ni ya kwako mpenzi wangu na tutakuwa tunakutana hapa unipe vitu” Aliongea Mama Rania na kumfanya Peter moyo upige kwa nguvu kwani hakuamini kuwa jumba hilo ni la kwake alianza kuona faida za kutoka na majimama..
“Mimi bado hata sijasadiki kabisa “ Aliongea Peter na Mama Rania akaachia tabasamua na kumshika mkono Peter na kisha kumvuta na wakaingia ndani .
“Chukua hio bahasha mpenzi ‘ Aliongea Mama Rania na kumfanya Peter aisogelee hio bahasha na kuifungua na ilikuwa ni hati ya nyumba na jina lake ndilo lili kuwa ndani ya hio hati .
“Peter nayafanya haya yote kwaku nakupenda na sitotaka unisaliti , nitakupa chochote utakacho kitaka , ila nakuomba usinisaliti”
Peter hakujibu Zaidi ya kumsogelea mama huyo na kuanza kupigana naye mabusu na kisha wakaanza kazi na kitu alicho pewa Mama Rania siku hio alijikuta kama yuko kwenye dunia nyingine kabisa na hakuwa kwenye ulimwengu halisi .
Walidumu kwa masaa kadhaa na kisha wakarudia tena na tena na tena na kujikuta wakipitiwa na usingizi kabisa tena wakiwa sebleni .
****
Peter alianza kukolea kwenye penzi la Mama Rania au bosi wake , japo walikuwa wakifanya mambo yao kwa siri sana na hakuna mtu hata mmoja ambae aliweza kujua kuwa wawili hao walikuwa wapenzi, kwani walikuwa wakiwekeana heshima feki wakiwa kwenye kazi , lakini wakitoka nje ya kazi walikuwa wapenzi.
Huku kwa Rania nako mambo yalizidi kuwa magumu kwani , kwani alikufa na kuoza kwa Peter , alitamani sana kuwa karibu na Peter kila saa na hata wakati mwingine Mama Rania alianza kuogopa, kwani kwa macho ambayo mwanae alikuwa akimwangalia Peter hayakuwa yakawaida, zilipita kama wiki mbili hivi ndipo Peter na Rania wote waliacha kufika kazini kutokana na chuoni mitihani ilikuwa inakaribia na walitakiwa kujiandaa .
Sasa hapo ndipo ukaribu wa Peter na na Rania kuongezeka kwani walikuwa wakisoma wote chuo kimoja na ilikuwa Rania akitoka mapema kwenye kipindi na Peter akiwa bado hajatoka basi atamsubiri mpaka atoke na waongozane wote , kunywa chai ama kula.
Rania alizidi kumzoea Peter kiasi kwamba kila siku , kila saa na kila sekunde alitamani kumuona Peter tu , kwa upende wa Peter jinsi Rania alivyo kuwa akimuonyeshea mapenzi , basi alizidi kuwa na mawazo juu ya rania , yeye , kila alivyo kuwa karibu ya Rania alijikuta moyo wake kumpenda sana Rania.
Alitamani atamke neno nakupenda ili myo wake utulie lakini hakuweza hilo , kwani kila alipo kumbuka kuwa tayari ana mahusiano na mama yake basi hakutaka kabisa kumuumiza rania huko mbeleni pindi atakapoujua ukweli , kuna muda alikaa chini na kuyafikiria matendo yake aliona kabisa kile kisasi katika kichwa chake kinaanza kusahalulika kabisa , kwani mpango wake ulikuwa ni kumfanya Samir atoe machozi kwakitendo ambachoo alikwisha kumfanyia.
Siku moja wakati Peter anatoka chuo akitembea na rafiki yake Steve , ndipo Rania alipo kuja kumuita na kumwambia kuwa kuna jambo anataka kuongea nae na ni muhimu kwake , basi Peter japo aliogopa kile alicho kuwa anaenda kuambiwa na Rania ila alijikaza na kuondoka na Rania mpaka kwenye gari lake .
“Peter najua kama ujumbe wangu nilio kuandikia uliona?”
“Ndio niliuona Rania “ alijibu Peter huku moyo ukipiga kwa nguvu .
“Peter nataka kujua jibu kwani nimeshindwa tena kusubiria naomba nisikie jibu lako leo”
Aliongea Rania hapo nakumfanya Peter jasho limtoke kwani hapo alikuwa amebanwa sehemu yenyewe .
“Rania najua unanipenda sana na mimi sitaki kukuficha nakupenda sana ila kwasasa sitaki kuanzisha mahusiano maana akili yangu haipo sawa na sijajiandaa kisaikolojia kabisa , na wewe ni mwanamke wa kipekee naomba muda niweke mambo yanguu sawa halafu nitakuambia Rania please, sitaki kuja kukuumiza kwa kutokuwajibika maana mahusiano ni uwajibikaji baina ya wapenzi” Aliongea Peter kwa hisia na ukimtazama hutoamini kama ni yule ambae alikuwa anataka kulipiza kisasi , mapenzi yameyeyusha kila kitu na kilicho baki kwenye moyo wake ni hisia za uhitaji tu , japo alijitahidi sana kutokumpenda Rania lakini ni kwamba alikuwa akijidanganya kwani kadri alivyo kuwa akimfosi atoke kwenye moyo wake ndivyo alivyo kuwa akizidi kumpenda.
“Sawa Peter nitasubiri , ila jua wewe ndio mwanume wangu wa kwanza kukupenda kwa kiasi hiki , nakupenda Peter “ Aliongea Rania mpaka chozi linamtoka mtoto wa kike na kumfanya Peter moyo umuume sana , alijkuta akimkumbatia .
“ Nakupenda Sana Rania , nakupenda sana ila naomba univumilie sawa “ aliongea Peter huku akimwangalia usoni na Rania akakubali kwa kichwa kuwa amekubaliana nae , na Peter alitoka kwenye hilo gari baada ya simu yake kutoa mlio ikionyesha kabisa kuwa inaita na mpigaji alikuwa ni Mama rania. .
Shida moja alio kuwa nayo Peter ni kwamba kila anpo ongea na Mama Rania mwili wake ulikuwa ukimsisimka sana na kuhitaji kufanya ngono .
Peter aliongea na Mama Rania na waliahidiana kuwa wakutane bila kukosa siku hio wakapeane dudu , na Peter hakupindua alikubali , maana kwa wakati huo na yeye alikuwa akipenda sana kitumbua cha mama rania .
****
Upande wa Najma nae mambo yalikuwa mambo kwani kila siku alikua akimfikiria tu mwanaume anae mfahamu kwa sura , japo maswala yake ya kufungua kampuni yake ya urembo yalikuwa yakimfanya kuwa bize sana , ila hakumsahau Peter hata mara moja .
Alikuwa akiamini kuwa lazima atamuona tu , wanaume walimtongoza kila kukicha lakini hakuna aliepewa nafasi hata mmoja hata ya kumshika tu hakuna alie pewa nafasi hio , watu na pesa zao walimchombeza kwa hongo lakini mwandada hakuteteleka , alikuwa akimuwaza Peter .
Upande wa Nasma na yeye alikuwa ashajua Masumbuko anapo kaa lakini kilicho kuwa kikimsumbua ni kwamba alikuwa na aibu na pia hakutaka kujilasisha kwa Masumbuko .
Kuna kipindi alikuwa ni kama mtoto kwani alikuwa akienda mpaka katka geti la Masumbuko kwa ajili ya kugonga lakini aliishia kurudi tu kwani hakukua na sababu ya kumuona Masumbuko na alifikiria kuwa akimuona atamwambiaje kwani alikuwa na aibu sana .
Masumbuko yeye muda wote alikuwa akiwazia ni kwa jinsi gani atakuwa na uwezo wa mnara wake kusoma channel kwani , kwa jinsi alivyo kuwa akijua na uwezo wake wa kufikiria ulipooishia ni kuangalia filamu za ngono tu huku akijifaliji kuwa utaamka tu .
“Utasimama tu “Aliongea huku akiuchezea uume wake
******
“Boss nimegundua Madam anapo elekea “ Ilisikika saiti kwnye simu Samir akiwa ofisini
“ Endelea kumfatilia na kila kinacho endelea utaniambia “
“ Sawa boss “
Samir ni kama kibao kilikuwa kimemgeukia kwani alikuwa hamuelewi kabisa mke wake , kwani hakumsubiri tena kama zamani wakati yeye akichelewa , kwani kila alipo rudi alimkuta mke wake alishapotelea kwenye usingizi mzito na wala hakuwa na habari na hata akiamka , alikuwa haulizi chochote na kilicho kuwa kikimuuma sana Samir ni kwamba hata ile mke wake kuomba gemu aliacha kabisa , na pia mke wake hakuwa hata na mawazo kama mwanzoni na alionekana kuwa mwenye furaha.
Hapo ndipo Samir alipoanza kurudi nyumbni mapema kama zamani , na kurudisha mapenzi kwa mkewe , lakini ni kwamba Mama Rania alionesha hali ya kutokuwa kabisa na time na yeye na mara nyingi usiku alionekana akichat na simu huku akitabasamu jambo ambalo lilianza kumfanya kuwa na wivu na kuona kabisa kuwa mkewe kashapata mchepuko , kila akizifikiria hisia hizo alijikuta akipandwa na wivu mkali sana na kumchoma , alivumilia sana lakini kuna siku alijikuta akikosa uvumilivu na alitaka kujua kile kinacho endelea na aliapia kama atagundua kuna mwanaume anaetoka na mke wake kimapenzi ange muua , swala hilo lilimnyima usingizi kabisa
Siku aliojikuta roho kumuuma na kujihisi kuna ninja anakata kata vipande kwenye tumbo lake ni siku alio omba tendo kwa Mama Rania , kwani ile ana peleka mkono kumshikashika Mama Rania , mkono ulitolewa na Mama Rania akainua kichwa na kumwambia neno moja tu .
“ Naomba usinisumbue nimechoka nina mambo mengi ya kufikiria natakiwa kulala mapema “
Alijikuta akiipandwa ma hasira na kukosa hata hamu ya kulala hapo ndani kwake na alicho kifanya ni kutoka usiku huo huo na kwenda bar .
Na kuanzia siku hio alikuwa akimuinda sana Mama Rania ili apate kujua mwanaume anae toka na mke wake na kwa upande wa Mama Rania alikuwa akiwaza dudu ya kijana Peter tu masaa yote kwani kila akifikiria dudu ya kijana Peter inavyo muingia na utamu anao usikiaga basi mizuka ilikuwa ikimpanda hapo hapo na hata kazi hakuweza kufanya vizuri .
Basi siku ambayo Mama Rania alipanga kukutana na Peter muda wa saa tisa , ndio muda ambao kijana wa boss Samir alikuwa akimfatilia nyuma kwa siri sana .
SEHEMU YA 24
Mama rania wala hakuwa na wasiwasi wakufatiliwa kwani aliendesha gari yake kuelekea upande wa Tegeta ambako ndio kulikuwa na nyumba ambayo amemnunulia Peter kama zawaidi ya kupewa dudu.
Lakini pasipo kujua kuwa kuna mtu anamfatilia nyuma aliendesha gari yake na kwa wakati huo ndio alikuwa anapita mwenge huku kijana aliepewa kazi na Samir alihakikisha kuwa hampotezi kabisa mama huyo kwani alielewa nini maana ya kile kitakacho tokea kama tu atakuja kumpoteza kwene macho yake na ndio maana alikuwa akiendesha karibu kabisa na gari ya Mama Rania na hakutaka kuipita , kwani ilivyo kuwa ikipunguza mwendo na yeye alikuwa akipunguza mwendo na huyu alie kuwa akimfatilia alikuwa si mwingine ila ni Kadabra , kijana machachali kabisa kwenye kazi hio ya kufatilia watu , kwani hio ndio kazi yake kubwa ambayo ilikuwa ikimuweka mjini kazi ya Ubodigadi na kufatilia watu .
Mama rania alipita lugalo yote na kuingia Mbezi Beach huku Kadabra akiwa nyuma , lakini ilipo karibia karibu na kanisa la Mbezi Beach la kilutheri gari ya Mama Rania ilikata kulia na kuelekea upande kama unaelekea shule ya sekondari Mbezi Beach , upande ambao ulikuwa ndio maeneo ambayo Peter na Nasma walikuwa wakikaa, Mama Rania aliendesha gari na kuja kuingia kwenye nyumba ya Peter , na wakati gari ikiingia sehemu hio na Kadabra alikuwa akipita geti hilo kwa mwendo wa taratibu sana huku akikodolea geti hilo macho na kwenda kusimama mbele kabisa na kutoka huku akijifanya anaongea na simu , lakini hakukaa sana gari ya Mama Rania , ilitoka na taratibu na kisha ikachukua njia ya kulekea Tegeta na Kadabra hakutaka kupoteza muda alikimbilia gari yake na kisha kuingia harakaharaka na kuliwasha na kisha kuliungia gari la Mama Rania na uzuri ni kwamba aliliona kabisa na lilikuwa karibu yake , baada ya kufikia eneo la jogoo gari lilikunja kulia na kisha likatembea mita chche kutoka barabara kuu na hatimae likaja kusimama kwenye ile nyumba na Mama Rania na gari ,Kadabra aliishuhudia kabisa ikiingia na hapo ndipo alipo alipo toa simu yake na kumpigia Samir na lilisikika neno moja tu.
“ subiri hapo hapo nina kuja , nataka nikiua unisaidie kutoa hio mizoga”.
Samir alikuwa na hasira kweli na wivu ulikuwa umemkaba kooni ,yaani hata kuhema ilikuwa ni shida kwani kila alipo fikiria swala la mke wake kuwa na mchepuko kiasi cha yeye kudharauliwa ,kilimuuma sana tena Zaidi ya kuuma , kwani hata chakula kila siku alipo kuwa akila kilikuwa hata sio kitamu kwake.
Samir alijikuta akipandwa na hasira mara mbili baada ya kusikia mke wake kaingia kwenye nyumba ambayohaifahamu aliishia kutoa matusi ya nguoni na kisha akachukua bastola yake na kuiweka kiunoni na kisha kutoka hapo na alipishana na secretary wake alie shika mafaili alijaribu kumsimamisha lakini hata sijui alisikia kwa wakati huo kwani akili yake kwa muda huo ilikuwa ikiongozwa na hisia , alipanda gari na kulitoa ofisini hapo kwa spidi ya ajabau mpaka mlinzi akamshangaa bosss wake .
Samiri alitembea na gari isivyo kawaida , na aliishia kutukana tu madereva ambao walikuwa hawataki kumpisha , kuna mdada mmoja alikuwa akiendesha Spacio , yake na Samir alikuwa akimpigia honi kumpisha , lakini mdada huyo wala hakujali , sasa Samiri alipo pata nafasi upande mwingine ya kupita , alimwangalia mdada huyo na huku mdada huyo akimwangalia , na Samir aliishia kumnyooshea kidolea cha kati akimtusi na dada yule aaliishia kusikitika tu.
Baada ya kama dakika ishirini hivi Samir alikuwa ndio anaingia sehemu alio elekezwa na Kadabra
“Ndio Hapa” Aliuliza Samir kwa jazba huku akilisogelea geti ,lakini kadabra alimzuia
“ Boss utawashitua ,sisi tunataka tuone kinacho endelea” Aliongea Kadabra
“Sasa tunafanyaje”
“Ngoja nikuoneshe”
Kadabra aliilisogelea lile geti na kuliangalia na kisha kugonga mlango mdogo kwa stali ya chini kabisa ambayo haileti bughuza na hakutumia kengele , ila yeye aligonga geti hilo na ndani ya dakika moja ndipo walipo sikia komeo likifunguliwa na kajidirisha kadogo kakafunguliwa na akatokea mlinzi.
“Niwasaidie nini?” aliuliza na kumfanya kadabra aangalie upande wa kulia na kushoto na kungalia uwepo wa watu .
“Boss Wangu pale ana shida na wewe .. kuna vitu anataka akuulize” Aliongea Kadabra huku akitoa waleti yake na kumuonesha mlinzi kuwa kazi hio ina malipo .
Mlinzi alivyo ona pesa , hakuzubaa alifungua kageti haraharaka na kisha kutoka ,lakini ni kama kosa kwake kwani ile anafungua tayari Kadabra ashamsogelea kwa staili ya kupiga roba na kumkaba kwa nyuma yule mlinzi na kisha kuingia nae ndani ya geti na kwenda kumtuliza kwenye kibanda chake baada ya kupoteza fahamu na Kadabra , alimwita Samir kwa ishara na hapo Samir akingia na geti likafungwa kabisa na funguo .
Samir mapigo yake yalikuwa yanapiga kwa nguvu kwani katika maisha yake hajawahi kufumania , kwani alikuwa akizisikia tu hizo habari za watu kufumania wake zao lakini hajawahi kukutwa na msala kama huo wa yeye kumfumania mtu tena mke wake , alisogea huku akjihisi kama presha inapanda kwa kiasi kikubwa hasa alipo kuwa akisikia sauti za mahaba kutoka ndani na kwa namna moja alijua kabisa watu hao wako sebleni wanafanya yao .
“Aisiiiii…eeeh… mpenziii… nakupenda… agha…. Nakuja mpenzi ..,. usichomoe mwagia humo humoo .. mpenziii.. aaa…”
Alijikuta roho ikimuuma sana na hasira zikizidi kumjaa na kukosa uvumilivu kabisa , kwani sauti za mahaba alizo sikia tena akisikia kabisa mwagia humoo humo alijikuta presha na roho ya mauji vikimpanda na alikosa kabisa uvumilivu , aalisukuma mlango ambao ulikuwa haujafungwa vizuri na kuingia kama mwanajeshi na kuachia risasii.. akimlenga mwanaume aliekuwa akionekana uchi akishusha kiuno na kupandisha.
“Paa..” Ulikuwa ni mvumo wa risasi uliosikikakwa nguvu
****
Nasma alikuwa amekaa sebleni huku akionekana kuwa kuna jambo ambalo alikuwa akilifikiria na jambo hilo lilikuwa likimhusu Masumbuko , japo tokea waachane siku ile kwenye gari , pasipo kuongea jambo lolote lakini kuna jambo ambalo alikuwa akiliona kwa Masumbuko kama haliko sawa , na muda huo alikuwa akijaribu kuunganisha matukio na kuona kweli kuna kitu kipo kwa Masumbuko na kitu hicho alikuwa akitamani sana kukifahamu .
“Ila mimi ni mjinga sana yaani mtu yuko jirani yangu nasumbuka kichwa changu tu hapa” Aliongea Nasma na kumfanya Lucy aliekuwa kakaa kwenye sofa kwa kujiachia akiangalia tv amwangalie.
“Nini Nasma , unaongea na mimi ?”
“Hapana , kuna sehemu naenda hapo nje nakuja sasa hivi”
“Niagize mimi nitaenda kukuchukulia , hakuna haja ya wewe kwenda”
“Nimetaka kwenda mwenyewe Lucy wee kaa hapo nakuja” Aliongea Nasma na kisha akatoka na kutembea mpaka kwenye geti la nyumba ambayo anaishi Masumbuko , aligonga na kisha alikuja mlinzi na kufungua na kumuuliza maswali na kisha aliruhusiwa kuingia.
“Samahani naulizia floor ambayo anaishi mkaka fulani hivi mweusi rangi ya chocholate” Aliuliza baada ya kuingia ndani hapo na kuwakuta Anjeli na marafiki zake wakipiga stori .
“Mhmh , hapa kuna wengi , lakinii.. hebu nenda namba nne “ Aliongea Angeli huku wote wakimwangalia Nasma kwa uzuri alio kuwa nao.
“Jamani kuna wadada wazuri .. akii..Mungu ningekuwa mimi ningekuwa danga la jiji hili lote” Aliongea Angeli huku akiungwa mkono na marafiki zake
Masumbuko alikuwa amelala fofo kwenye sofa huku Steve ambae alikuja kumsalimia rafiki yake Peter akiwepo akiangalia muvi kwenye laptop yake , na ndio wakati huo ambao Nasma aligonga Mlango na Steve ndio aliesikia na kwenda kufungua,macho yalimtoka na kujikuta akifikicha macho.
“Mambo “ Alisalimia Nasma huku akiweka tabasamu lililomuacha hoi Steve na kujikuta akimwangalia usoni Nasma na mpaka Nasma mwenyewe akaona haya na kuangalia chini.
“ Aaa poa karibu “ Aliongea Steve huku akimwangalia Nasma na alikuwa amesimama tu hapo mlangoni na alijifikiria, ila akaona aingie tu .. alisogeea mpaka kwenye sofa moja refu , kwani hapo ndani kulikuwa na masofa manne na moja lilikuwa karibu na tv na hili lilikuwa ni dogo na dogo lingine lili kuwa upande wa kulia mbali kidogo na Tv na refu kakalia Steve , ila la karibu kabisa ambalo ndilo la kwanza ukiingia hapo ndani kalalia Masumbuko .
Nasma alisogea na alikuwa na wasiwasi sana kwani ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuingia katika vyumba ya wanaume tu , kwani hakuwahi kufanya hapo kabla , alisogea na ndipo alipo muona Masumbiuko aliejinyoosha kwenye sofa akiendesha jenereta kwani alikuwa amepitiwa na usingizi mzito sana .
Nasma alikaa pembeni ya kichwa cha masumbuko kwani alikuwa ameacha nafasi kidogo ambayo ilimuwezesha kukaa , ila wakti anakaa kichwa cha masumbuko kilimgusa kwani mtoto nae alikuwa amejaliwa chungu sio poa.
“Ngoja ni kuletee juisi” Aliongea Steve kwa kubabaika kwani alikuwa ni kama haamini ,kuna muda aliona labda mwanadada huyu alikuwa amepotea njia.
Masumbuko nae muda huo ndio usingizi unaisha na alikuwa akijifikicha macho huku Nasma alikuwa akimwangalia kwa macho yenye mahaba mazito , Masumbuko alianza kunusa kama mbwa maana alisikia harufu nzuri sana kwenye pua zake na wakati anafanya kitendo hicho alikuwa amefumba macho .
“Peter leo sijui kakaribisha jini” Aliongea Msumbuko huku akifungua macho akiangalia juu na hapo ndipo macho yake yakagongana na ya nasma alie kuwa akimwangalia huku akitabasamu na Masumbuko alipo fungua macho alijikuta akishangaa na kumfanya Nasma atoe kicheko.
Na kitendo hicho Steve alikuwa akikishuhudia na aliona kama anangalia sinema VR Gasses (hizi ni miwani ambazo unaweza ukaangalia muvi au kucheza gemu kwa mazingira ya 3D na kukupa hali ya kama unakiona kitu katika mazingira halisi ) ,maana jinsi Nasma alivyo inama na Masumbuko alie kuwa kalala na walivyo kuwa wanaangaliana ilikuwa ni kama sinema la kifilipino .
“Dada juisi hii hapa”
Aliongea Steve na kumfanya Nasma amwangalie na kuachia tabasamu na kisha kusema asante , na kumfanya Steve ahisi sauti hio ilikuwa ipo tumboni ,ikitekenya maini yake.
Masumbuko mara alishtuka maana sijui alifikiria nini na alinyanyuka haraka haraka na kumshika Nasma mkono na kumfanya Nasma amwangalie huku akitabasamu na Masumbuko alimnyanyua Nasma na kumpeleka karibu na mlango wa jikoni ambapo mtu wa sebleni hawezi kuona
“Usije ukasema siku ile tulikutana na nilipotea na wewe ndio ulio nileta maana niliwaambia nalijua sana jiji sasa usije ukaniumbua , yaani kimyaa shiiip” Aliongea akimnong`oneza Nasma na kumfanya Nasma atabasamu na kuhisi msisimko wa ajabu kwani alihisi pumzi ya Masumbuko .
“Hapa leo nadhani kwa mara yangu ya kwanza ndio naangalia tamthiliya la kifilipino laivu bila chenga aliongea Steve baada ya kumuona Masumbuko akimwambia jambo Nasma.
*****
Boss mkuu kapiga simu kuhusu ule mzigo wa Congo “ Aliongea jamaa mmoja mrefu mweusi aliekuwa na mwili ulio jazia na akiwa amevaa miwani .
“ Ramso nadhani wewe unajua nini cha kufanya hapa , na nimeona una majukumu mengi sana, lakini nataka nikupe jukumu lingine na hilo .
“Jukumu gani hilo boss?”
“Nataka kwanzia sasa uwe karibu na Rania kwa kila anacho kifanya kwani muda si mrefu nitakwenda kumuoa”
“Boss una amini atakubali?”
“ Ramso unafikiri ninasema jambo bila mpango , yeye akubali asikubali ila lazima nimuoe kwa namna yoyote ile kwani baba yake tayari yupo hapa kiganjani na hana pakwenda na mama yake na yeye nina udhaifu wake mkubwa sana na nikumuonesha huo tu hatokuwa na la kusema zaidi ya kunipa baraka zote.”
Aliongea Hemedi akiwa nyumbani kwake eneo la Mapinga Bagamoyo na ndani ya jumba hilo ilikuwa ni kama ikulu kwani walionekana mabodigadi wengi walio valia suti safi wakiwa wana hakikisha ulinzi na haikueleweka walikuwa ndio wanamlinda huyo Hemedi au kuna la ziada kwani kama tujuavyo Hemedi ni mfanya biashara wa mabasi .
“Sawa Boss nitalifatilia hilo”
“ Kingine hakikisha huyo panya (Peter ) hafanyi lolote kwa huyo mwanamke , kwani ndio roho yangu na nadhani nikishampata rania roho yangu iatulia na nitatulia nae ,huyu paka kama isingekuwa analindwa na Bosco ningekuwa nishampoteza muda mrefu sana”
“Boss unamaanisha wetu anamfahamu Peter”.
“Ndio ana mfahamu vizuri sana na namheshimu sana Bosco kwani kanifikisha hapa nilipo leo hii, ila asinenipa maelekezo ya kutomgusa Peter ningekuwa nishampoteza muda mwingi sana”
Aliongea Hemedi na kumfanya Ramso ashangae , kwani sio jambo la kawaida kwa tajiri mkubwa kama Bosco kumjua Peter , kwani Bosco alikuwa ni tajri mkubwa ndani ya Congo mwenye mtandao mkubwa wa madawa ya kulevya na alikuwa ni supplier(msambazaji) kwenye nchi nyingi sana ikiwemo Tanzania alikuwa akifahamika kwa jina la The Don.
*****
Ndani ya uwanja wa kimaaifa wa Julius kambarage nyerere (JNIA) , alionekana mrembo Najma akiwa na bodigadi wake akitoka eneo la ‘Arrival’ yaani wanofika, akiwa amependeza kwelikweli na alionekana kabisa alikuwa safarini na ndio anarudi .
“Rehema naomba usinipeleke nyumbni kwanza nataka nikakae Serena mpaka nitakapo kamilisha ufunguzi wa kampuni yangu” Aliongea huku akitembea kimadaha kabisa na kuingia kwenye gari.
Gari ilitembea mpaka kwenye hoteli ya Serena ikitumia masaa machache tu kuingia kwenye hoteli hio ya hadhi ya juu na kisha mrembo huyo akaingia . na kwenda moja kwa moja mpaka mapokezi na kuchukua chumba .
“Leo unaonekana kuwa nafuraha kuliko siku zote nilizo kuzoea”Aliongea Rehema huku akiingiza mizigo ya Najma ndani ya chumba hicho .
“Acha tu nitakwambia kila kitu ila kwa sasa kuna mambo makuu mawili nataka kuyatimiza ndani ya mwezi mmoja .
“Hongera yako ,kama kuna jambo ambalo unataka kulifanikisha pia ni mwanzo wa mafanikio na ni uthamani katika uso wa dunia kwani hauvuti hewa bure , hakuna jambo zuri kuwa na sababu ya kuishi”Aliongea rehema na kisha waliagana kwa ajili ya kukutana siku inayo fuata.
Najma alifungua begi lake nakutoa laptop na kisha akawasha mtandao wa Skype na kisha akabonyeza kwenye hio laptop na likaja jina la A2
“Hello A2 “ Aliongea Najma kwa mapozi . (A2 ni Artificial intelligence roboti ambayo ilitengenezwa na Profesa Gladness , roboti ambayo inafanana kwa kila kitu na binadamu wa kawaida unaweza ukamfahamu roboti A2 kutoka kwenye simulizi ya MY DREAM MY FAVOURITE)
“Hello Beuty Najma .”
“ Nimefurahi sana kuwasiliana na wewe A2 na niliongea na aunt(shangazi) na kaniambia nikuombe msaada unaweza kunisaidia kwenye tatizo langu .
“Ndio alinidokezea na ni kwamba tatizo lako linaweza kufanyiwa kazi kisayansi kutokana na kwamba sasa kuna teknolojia ya kuweza kufanya komputa kutoa picha yoyote ile unayohitaji kutoka katika mawazo yako”
“Naweza kufika lini ili swala langu uweze kulitatua?”
“Kesho asubuhi unaweza ukafika nitakusadia hakika “
Hili ni roboti A2 liliotengenezwa na profesa gladness, na lilikuwa lipo kwenye moja ya kitengo cha usalama wa nchi , kitengo ambacho kilibadilishwa jina kutoka kwenye jina la the Hollic Shadow na kwenda kuitwa jina la AFRICA MULTNATIONAL CYBER SECURITY (AMCS) na kiongozi wa kundi hili alikuwa hajulikani jina lake , kwani kitengo hichi kilikuwa kikifanya kazi zake kwa siri sana na hata wafanyakazi walikuwa hawafahamiki .
UNAWEZA PATA SOFTCOPY YA SIMULIZI HII YOTE.
SIMULZI ZANGU NYINGINE NI
-UMOJA NAMBA TISINI NA SABA
-NDOTO ZA KIKANUNI
-BOOK OF ALL NAMES (UMOJA NAMBA TISINI NA SABA )
-MY DREAM MY FAVOURITES)
KUHUSU UTARATIBU WA MALIPO
WASILIANA NAMI KWA KUGUSA HAPAA
mawasiliano 0687151346
Dah hii mesadoni inabidi iwe na tembe 5 za maanaKesho jioni naeleta mwendelezo stay tuned