Simba haikufanya mazoezi uwanja wa Jamhuri Morogoro ikapoteza mechi muhimu

SAYVILLE

JF-Expert Member
Mar 25, 2010
8,537
13,847
Kuna watu wanachukulia poa utaratibu na haki iliyopewa timu ngeni kufanya mazoezi katika uwanja utakaochezewa mechi siku moja kabla ya mechi.

Wachezaji wanapokuwa wamefanya mazoezi katika uwanja wa vita watakaoenda kuutumia, hili ni suala la kiufundi na linasaidia kuandaa wachezaji kimwili na kisaikolojia. Lengo kuu ni kuweka mizania sawa kati ya timu zote mbili kuelekea mchezo husika. Kumbuka football inaendeshwa na dhana nzima ya "fair play" na kanuni nyingi zimetengenezwa kulinda dhana hii.

Nakumbuka misimu miwili iliyopita Simba ilifanya kosa moja kubwa sana lililoigharimu timu na kufifisha harakati zake za ubingwa.

Simba ilihamishia mechi yake dhidi ya Prisons katika uwanja wa Jamhuri, Morogoro na kupoteza mchezo ule kwa goli 1-2. Sikumbuki sababu hasa ilikuwa nini ila pamoja na kwamba ilikuwa ndiyo mwenyeji wa mchezo, Simba haikufanya mazoezi katika uwanja ule wa Jamhuri kabla ya mchezo husika. Nakumbuka kulaumu kuwa moja ya sababu ya Simba kupoteza mchezo ule hii inaweza kuwa ilichangia pakubwa sana.

SOMA HAPA:
Simba imeenda kuutumia uwanja wa Jamhuri bila kuujaribu

Utagundua issue siyo kuwa mwenyeji bali kuwa na familiarity na uwanja husika na kuutumia muda mfupi kabla ya mechi ni jambo muhimu kwa wachezaji wa timu zote mbili.

Kwa kulipanua zaidi hili suala na kuongeza uelewa, ndiyo maana mara nyingi utaona Simba huwa inaenda kufanya mazoezi Uwanja wa Mkapa walau siku moja kabla ya mechi za kimataifa na pia huwa inafanya hivyo pia katika uwanja wa KMC kabla ya mechi ya ligi. Hili ni suala la kiufundi zaidi na usipokuwa mtu wa mpira hauwezi kulielewa.

NYONGEZA: Hapa sijaongelea ukweli kuwa kuizuia timu iliyo na haki ya kutumia uwanja siku moja kabla ya mechi ni kuvuruga ratiba yake ya maandalizi ya mechi husika na inaua dhana nzima ya fair play. Ukiizuia timu kama ilivyotokea kwa Simba, itatakiwa kwenda katika mechi bila kuwa imefanya mazoezi kwa masaa 48. Hapo utimamu wa kimwili wa wachezaji utakuwaje?
 
Simba ndo alitumia uwanja wa Taifa dhidi ya Azam week hii, unasema hayupo familiar na uwanja wa Taifa kivipi?

Bodi ya ligi inasema Simba hawakutoa taarifa za mamlaka ya uwanja kuhusu ujio wao.
Walitaka wafanye vip mazoezi usiku bila kuwajulisha wenye mamlaka ili wawake mazingira rafiki ikiwa pamoja na mwanga au walitaka watumie tochi za simu?

Simba waliandaa mangenge Yao ili kutafuta sababu ya kukimbia mechi

Simba wamefanya uhuni hapa laZima kanuni zisimame
 
Simba ndo alitumia uwanja wa Taifa dhidi ya Azam week hii, unasema hayupo familiar na uwanja wa Taifa kivipi?

Bodi ya ligi inasema Simba hawakutoa taarifa za mamlaka ya uwanja kuhusu ujio wao.
Walitaka wafanye vip mazoezi usiku bila kuwajulisha wenye mamlaka ili wawake mazingira rafiki ikiwa pamoja na mwanga au walitaka watumie tochi za simu?

Simba waliandaa mangenge Yao ili kutafuta sababu ya kukimbia mechi

Simba wamefanya uhuni hapa laZima kanuni zisimame
Mechi ya Simba na Azam imechezwa siku 12 zilizopita. Wataalamu wangekuwa na akili kisoda kama zako wangesema haki itolewe kwa kwanza kuangalia ni lini mara ya mwisho timu ilitumia uwanja husika. Badala yake kanuni ipo wazi na clear na kanuni lazima ziheshimiwe maana hazijatungwa kujaza tu makaratasi.
 
Kuna watu wanachukulia poa utaratibu na haki iliyopewa timu ngeni kufanya mazoezi katika uwanja utakaochezewa mechi siku moja kabla ya mechi.

Wachezaji wanapokuwa wamefanya mazoezi katika uwanja wa vita watakaoenda kuutumia, hili ni suala la kiufundi na linasaidia kuandaa wachezaji kimwili na kisaikolojia. Lengo kuu ni kuweka mizania sawa kati ya timu zote mbili kuelekea mchezo husika. Kumbuka football inaendeshwa na dhana nzima ya "fair play" na kanuni nyingi zimetengenezwa kulinda dhana hii.

Nakumbuka misimu miwili iliyopita Simba ilifanya kosa moja kubwa sana lililoigharimu timu na kufifisha harakati zake za ubingwa.

Simba ilihamishia mechi yake dhidi ya Prisons katika uwanja wa Jamhuri, Morogoro na kupoteza mchezo ule kwa goli 1-2. Sikumbuki sababu hasa ilikuwa nini ila pamoja na kwamba ilikuwa ndiyo mwenyeji wa mchezo, Simba haikufanya mazoezi katika uwanja ule wa Jamhuri kabla ya mchezo husika. Nakumbuka kulaumu kuwa moja ya sababu ya Simba kupoteza mchezo ule hii inaweza kuwa ilichangia pakubwa sana.

Utagundua issue siyo kuwa mwenyeji bali kuwa na familiarity na uwanja husika na kuutumia muda mfupi kabla ya mechi ni jambo muhimu kwa wachezaji wa timu zote mbili.

Kwa kulipanua zaidi hili suala na kuongeza uelewa, ndiyo maana mara nyingi utaona Simba huwa inaenda kufanya mazoezi Uwanja wa Mkapa walau siku moja kabla ya mechi za kimataifa na pia huwa inafanya hivyo pia katika uwanja wa KMC kabla ya mechi ya ligi. Hili ni suala la kiufundi zaidi na usipokuwa mtu wa mpira hauwezi kulielewa.

NYONGEZA: Hapa sijaongelea ukweli kuwa kuizuia timu iliyo na haki ya kutumia uwanja siku moja kabla ya mechi ni kuvuruga ratiba yake ya maandalizi ya mechi husika na inaua dhana nzima ya fair play. Ukiizuia timu kama ilivyotokea kwa Simba, itatakiwa kwenda katika mechi bila kuwa imefanya mazoezi kwa masaa 48. Hapo utimamu wa kimwili wa wachezaji utakuwaje?
Sasa kama mwenyewe unakili Simba haikufanya mazoezi ambalo ni takwa la msingi na nyinyi ni watu wa kufata kanuni kwanini hamkugoma kucheza mchezo huo na prisons?

Au hilo takwa la kimsingi la kufanya mazoezi siku moja kabla ya mechi lipo na Yanga tu na prisons halipo?

Halafu huwezi kusema Simba hayuko familiar na uwanja wa taifa(kwa mkapa).

Huku ndio kule mna Kauli mbiu yenu ya kwa mkapa hatoki mtu huo ugeni na uwanja mmeupata lini?

Kubalini tu mmeiogopa Yanga na kuamua kukimbia kwa sababu za kitoto kabisa.
 
Mechi ya Simba na Azam imechezwa siku 12 zilizopita. Wataalamu wangekuwa na akili kisoda kama zako wangesema haki itolewe kwa kwanza kuangalia ni lini mara ya mwisho timu ilitumia uwanja husika. Badala yake kanuni ipo wazi na clear na kanuni lazima ziheshimiwe maana hazijatungwa kujaza tu makaratasi.
Haya wewe una siku 12, Yanga amecheza mara ya mwisho hapo Taifa lini?

Kwanini ukimbie mechi na kanuni hazitaki hivo na kanuni timu yako ilishiriki kuzitunga na kuzipitisha kwanini ugomee mchezo
 
Sasa kama mwenyewe unakili Simba haikufanya mazoezi ambalo ni takwa la msingi na nyinyi ni watu wa kufata kanuni kwanini hamkugoma kucheza mchezo huo na prisons?

Au hilo takwa la kimsingi la kufanya mazoezi siku moja kabla ya mechi lipo na Yanga tu na prisons halipo?

Kubalini tu mmeiogopa Yanga na kuamua kukimbia kwa sababu za kitoto kabisa.
Simba hawana hoja ya msingi
 
Sasa kama mwenyewe unakili Simba haikufanya mazoezi ambalo ni takwa la msingi na nyinyi ni watu wa kufata kanuni kwanini hamkugoma kucheza mchezo huo na prisons?

Au hilo takwa la kimsingi la kufanya mazoezi siku moja kabla ya mechi lipo na Yanga tu na prisons halipo?

Kubalini tu mmeiogopa Yanga na kuamua kukimbia kwa sababu za kitoto kabisa.

Sasa kama mwenyewe unakili Simba haikufanya mazoezi ambalo ni takwa la msingi na nyinyi ni watu wa kufata kanuni kwanini hamkugoma kucheza mchezo huo na prisons?

Au hilo takwa la kimsingi la kufanya mazoezi siku moja kabla ya mechi lipo na Yanga tu na prisons halipo?

Kubalini tu mmeiogopa Yanga na kuamua kukimbia kwa sababu za kitoto kabisa.
Ile ilikuwa game ya simba vs prison ambapo simba alikuwa mwenyeji hivyo kuto kufanya mazoezi ilikuwa ni usembe wake mwenyewe kwasababu hakuzuiwa tofauti na game ya yanga vs simba ambapo yanga ni mwenyeji.
 
Ile ilikuwa game ya simba vs prison ambapo simba alikuwa mwenyeji hivyo kuto kufanya mazoezi ilikuwa ni usembe wake mwenyewe kwasababu hakuzuiwa tofauti na game ya yanga vs simba ambapo yanga ni mwenyeji.
Sahihi kabisa. Utaona jinsi wanavyojibu kwa kukurupuka wakati kila kitu nimeweka wazi.
 
Kwenye hili bwana, tuseme tu ukweli bila kumung'unya maneno, simba tumeaibisha yaani mazoezi ya dk 30 ndio yafanye tususie mechi? hii mechi kila mtu alijiandaa kuanzia kwa mashabiki mpaka kwa wachezaji iweje sababu ya et kukataliwa kufanya mazoezi siku moja kabla ya mechi iwe nongwa ilihali tulikuwa tumejiandaa?
 
Haya wewe una siku 12, Yanga amecheza mara ya mwisho hapo Taifa lini?

Kwanini ukimbie mechi na kanuni hazitaki hivo na kanuni timu yako ilishiriki kuzitunga na kuzipitisha kwanini ugomee mchezo
Mnavunja kanuni mkijua adhabu zake mnazimudu, sasa msala mnao.
 
Ile ilikuwa game ya simba vs prison ambapo simba alikuwa mwenyeji hivyo kuto kufanya mazoezi ilikuwa ni usembe wake mwenyewe kwasababu hakuzuiwa tofauti na game ya yanga vs simba ambapo yanga ni mwenyeji.
Simba hawakutoa taarifa Kwa wenye mamlaka ya uwanja, na mazoezi walitaka wafanye usiku Sasa ww ulitaka wafanyeje bila kuandaliwa mazingira rafiki ya mazoezi ikiwa ni pamoja na mwanga na vifaa vingine
 
Ile ilikuwa game ya simba vs prison ambapo simba alikuwa mwenyeji hivyo kuto kufanya mazoezi ilikuwa ni usembe wake mwenyewe kwasababu hakuzuiwa tofauti na game ya yanga vs simba ambapo yanga ni mwenyeji
Ivi ile BM coach ilikuwa inaenda wapi? na ilikuwa imembeba nani?
 
Kwenye hili bwana, tuseme tu ukweli bila kumung'unya maneno, simba tumeaibisha yaani mazoezi ya dk 30 ndio yafanye tususie mechi? hii mechi kila mtu alijiandaa kuanzia kwa mashabiki mpaka kwa wachezaji iweje sababu ya et kukataliwa kufanya mazoezi siku moja kabla ya mechi iwe nongwa ilihali tulikuwa tumejiandaa?
Ukijua kusimama kwenye principles na umuhimu wa kulinda heshima ya taasisi wala hauwezi kushangaa. Sheria na kanuni hazijawekwa ili kumfurahisha mtu kiasi kwamba mtu anaweza kuamka na bangi zake anaenda tu kuzivunja. Maisha hayaendi hivyo.
 
Ukijua kusimama kwenye principles na umuhimu wa kulinda heshima ya taasisi wala hauwezi kushangaa. Sheria na kanuni hazijawekwa ili kumfurahisha mtu kiasi kwamba mtu anaweza kuamka na bangi zake anaenda tu kuzivunja. Maisha hayaendi hivyo.
Hakuna haki isiyoambatana na wajibu
Haki ya kufanya mazoezi kabla ya mechi walikuwa nayo sawa
Kwanini hawakutimiza wajibu wa kuwapa taarifa kamshina wa mchezo, wamiliki wa uwanja na mwenyeji wa mchezo kuwa timu utafika muda fulani Kwa ajili ya mazoezi ili wawapokee na kuwaandalia mazingira rafiki kwanini walivizia
 
Ukijua kusimama kwenye principles na umuhimu wa kulinda heshima ya taasisi wala hauwezi kushangaa. Sheria na kanuni hazijawekwa ili kumfurahisha mtu kiasi kwamba mtu anaweza kuamka na bangi zake anaenda tu kuzivunja. Maisha hayaendi hivyo.
Kama tungekuwa tunafuata principle kweli, tungetoa taarifa kwa wahusika, taarifa ya bod inasema simba hatukutoa taarifa
 
Ivi ile BM coach ilikuwa inaenda wapi? na ilikuwa imembeba nani?
Ilibeba watu wanaohusika na timu. Kama mnahisia mambo ya kishirikina mngeacha waingie wafanye, mrekodi kumbukumbu then tff na bodi ya ligi wangechukua hatua zinazostahili kuliko nyie kufanya majukumu yasiyo wahusu
 
Hakuna haki isiyoambatana na wajibu
Haki ya kufanya mazoezi kabla ya mechi walikuwa nayo sawa
Kwanini hawakutimiza wajibu wa kuwapa taarifa kamshina wa mchezo, wamiliki wa uwanja na mwenyeji wa mchezo kuwa timu utafika muda fulani Kwa ajili ya mazoezi ili wawapokee na kuwaandalia mazingira rafiki kwanini walivizia

Kama tungekuwa tunafuata principle kweli, tungetoa taarifa kwa wahusika, taarifa ya bod inasema simba hatukutoa taarifa
Simba inacheza kila siku mechi za ndani na nje ya nchi na imekuwa inatumia hiyo hiyo kanuni bila shida kwa kufanya mazoezi katika uwanja siku moja kabla ya mechi. Leo ndiyo ionekane haijui taratibu za kutumia kanuni hiyo?
 
Ivi ile BM coach ilikuwa inaenda wapi? na ilikuwa imembeba nani?
Kwani basi la BM lina shida gani? Mbona timu za nje zikija zinatumia mabasi hayo kupeleka wachezaji uwanjani bila shida?

Yanga derby ngapi wanakwenda uwanjani na basi la timu likiwa tupu na wachezaji wakiwa kwenye vicoaster? Ukiambiwa basi la Simba lilikuwa tupu na wachezaji walikuwa kwenye hilo BM utajibu nini?
 
Simba inacheza kila siku mechi za ndani na nje ya nchi na imekuwa inatumia hiyo hiyo kanuni bila shida kwa kufanya mazoezi katika uwanja siku moja kabla ya mechi. Leo ndiyo ionekane haijui taratibu za kutumia kanuni hiyo?
Hiyo kanuni kazuiliwa na nani kunitumia
Wamiliki wa uwanja wanasema hawakuwa na taarifa za ujio wao.

Yanga ni mwenyeji wa mchezo kiitafaki tu
Lakini hatunzi funguo za magetinya uwanja
Yanga hana mafundi wa umeme wa uwanja kuwapa Simba mwanga kwenye mazoezi ya usiku
 
Back
Top Bottom