Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
2,005
5,297

Hatimaye kijana Shadrack Yusuph Chaula (24) mkazi wa kijiji cha Ntokela kata ya Ndanto Tukuyu wilayani Rungwe, ameachiwa huru kutoka mikononi mwa jeshi la magereza baada ya kufanikiwa kulipa faini ya shilingi million tano kutokana na hatia aliyokutwa nayo ya udanganyifu juma lililopita.

Kijana Shadrack Chaula amelipa fedha hizo baada ya kuchangwa na wanaharakati na wananchi kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Chaula alihukumiwa na mahakama ya wilaya ya Rungwe kwenda jela miaka miwili au kulipa faini ya shilingi million tano baada ya kukiri kosa la kudanganya.

Baada ya hukumu hiyo juma lililopita, kijana huyo alienda gerezani kuanza kutumikia kifungo cha miaka miwili jela ndipo baadaye wanaharakati akiwemo Godlisten Malisa wakaanzisha mchango ili kupata fedha za kumtoa gerezani na kufanikiwa kupata zaidi ya shilingi million sita.

PIA SOMA
- Kuelekea 2025 - Mbeya: RC Homera aagiza kukamatwa kwa kijana aliyemkashifu Rais Samia na kuichoma picha yake

- Aliyekamatwa kwa kuchoma picha ya Rais Samia ahukumiwa faini Tsh. Milioni 5 au miaka miwili jela

- Baada ya alichechoma picha ya Rais Samia kuhukumiwa Miaka miwili Jela, Wakili asema wanafikiria kukata rufaa

- Mvutano wa kisheria, tuhuma ya msanii aliyechoma picha ya Rais

- Baada ya alichechoma picha ya Rais Samia kuhukumiwa Miaka miwili Jela, Wakili asema wanafikiria kukata rufaa
 
Hatimaye kijana Shadrack Yusuph Chaula (24) mkazi wa kijiji cha Ntokela kata ya Ndanto Tukuyu wilayani Rungwe, ameachiwa huru kutoka mikononi mwa jeshi la magereza baada ya kufanikiwa kulipa faini ya shilingi million tano kutokana na hatia aliyokutwa nayo ya udanganyifu juma lililopita.

Kijana Shadrack Chaula amelipa fedha hizo baada ya kuchangwa na wanaharakati na wananchi kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Chaula alihukumiwa na mahakama ya wilaya ya Rungwe kwenda jela miaka miwili au kulipa faini ya shilingi million tano baada ya kukiri kosa la kudanganya.

Baada ya hukumu hiyo juma lililopita, kijana huyo alienda gerezani kuanza kutumikia kifungo cha miaka miwili jela ndipo baadaye wanaharakati akiwemo Godlisten Malisa wakaanzisha mchango ili kupata fedha za kumtoa gerezani na kufanikiwa kupata zaidi ya shilingi million sita.

PIA SOMA
- Kuelekea 2025 - Mbeya: RC Homera aagiza kukamatwa kwa kijana aliyemkashifu Rais Samia na kuichoma picha yake

- Aliyekamatwa kwa kuchoma picha ya Rais Samia ahukumiwa faini Tsh. Milioni 5 au miaka miwili jela

- Baada ya alichechoma picha ya Rais Samia kuhukumiwa Miaka miwili Jela, Wakili asema wanafikiria kukata rufaa

- Mvutano wa kisheria, tuhuma ya msanii aliyechoma picha ya Rais
mlindeni uyo kijana, naamini bado watakuwa na hasira. tafadhali.
 
Shadrack Chaula (24) ameachiwa huru leo Julai 8, 2024 baada ya kulipa faini ya Tsh. Milioni 5 ikiwa ni siku chache tangu alipohukumiwa kifungo cha Miaka Miwili jela au kulipa Faini hiyo kwa kosa la kutoa taarifa za uongo Mtandaoni.

Pia soma:
Aliyekamatwa kwa kuchoma picha ya Rais Samia ahukumiwa faini Tsh. Milioni 5 au miaka miwili jela

Chaula ambaye ni Msanii wa Sanaa ya Uchoraji, Julai 2, 2024 alionekana kupitia kipande cha video akichoma moto picha ya Rais Samia Suluhu Hassan, alihukumiwa na Mahakama ya Wilaya ya Rungwe Mkoa wa Mbeya, alishindwa kulipa faini na kwenda jela, Wadau mbalimbali walianza kumchangia fedha kupitia Mtandao kwa nia ya kumlipia faini.

Wakili Michael Lugina amesema “Sisi Mawakili tumekuja kusimamia zoezi la kumlipia faini iliyochangwa na Wadau wa Mtandaoni, tayari ametoka na tumekamilisha mchakato lakini tunafanya taratibu nyingine za kukata rufaa kwa maana ya kupinga mwenendo wote wa kesi.”

Wakili Peter Kibatala, ameandika haya.

Snapinsta.app_450387592_18445660651017157_7113877887012309739_n_1080.jpg
Ladies and Gentlemen;

As can be evidenced by the photo; Mr. Shradrack Yusuph Chaula is free.

You paid for his freedom; and for freedom of speech in this country.

My boys: Adv. Mike Michael Mwangasa, Thank You. You treated Me as Your elder Brother;and Your names shall live forever. I love both of You;so much.

Dear country:We kept out solemn vows to Mzee Chaula. We promised that by Wednesday 10th July 2024 we should have his Son released. Here we are:ready to be showered in all his blessings.


====

Msanii wa picha nchini Tanzania aliyetuhumiwa kuchoma moto picha ya Rais Samia Suluhu Hassan amechangiwa Sh.6.5 milioni kulipa faini ya Chaula ili aachiliwe kutoka jela.

Watanzania kupitia mitandao ya kijami ya X (zamani ikiitwa Twitter) na Instagram walijitokeza kumchangia Shadrack Chaula mwenye umri wa miaka 24, ili aweze kulipa faini.

Chaula alihukumiwa kifungo cha miaka miwili jela au faini ya takriban dola $2,500 baada ya kupatikana na hatia ya uhalifu wa mtandaoni.

Alikamatwa kwa madai ya kurekodi video ya mtandaoni, iliomuonyesha akiichoma picha ya Rais Suluhu huku akimtukana kwa maneno.

Pia soma:
Mbeya: RC Homera aagiza kukamatwa kwa kijana aliyemkashifu Rais Samia na kuichoma picha yake

Mchoraji huyo mwenye umri wa miaka 24 alikiri kutenda uhalifu huo na kushindwa kutetea hatua yake mahakamani.

Kukamatwa kwake kulizua utata wa kisheria, huku baadhi ya mawakili wakisema kuwa hakuna sheria iliyovunjwa katika kuchoma picha hiyo.
 
Hatimaye kijana Shadrack Yusuph Chaula (24) mkazi wa kijiji cha Ntokela kata ya Ndanto Tukuyu wilayani Rungwe, ameachiwa huru kutoka mikononi mwa jeshi la magereza baada ya kufanikiwa kulipa faini ya shilingi million tano kutokana na hatia aliyokutwa nayo ya udanganyifu juma lililopita.

Kijana Shadrack Chaula amelipa fedha hizo baada ya kuchangwa na wanaharakati na wananchi kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Chaula alihukumiwa na mahakama ya wilaya ya Rungwe kwenda jela miaka miwili au kulipa faini ya shilingi million tano baada ya kukiri kosa la kudanganya.

Baada ya hukumu hiyo juma lililopita, kijana huyo alienda gerezani kuanza kutumikia kifungo cha miaka miwili jela ndipo baadaye wanaharakati akiwemo Godlisten Malisa wakaanzisha mchango ili kupata fedha za kumtoa gerezani na kufanikiwa kupata zaidi ya shilingi million sita.

PIA SOMA
- Kuelekea 2025 - Mbeya: RC Homera aagiza kukamatwa kwa kijana aliyemkashifu Rais Samia na kuichoma picha yake

- Aliyekamatwa kwa kuchoma picha ya Rais Samia ahukumiwa faini Tsh. Milioni 5 au miaka miwili jela

- Baada ya alichechoma picha ya Rais Samia kuhukumiwa Miaka miwili Jela, Wakili asema wanafikiria kukata rufaa

- Mvutano wa kisheria, tuhuma ya msanii aliyechoma picha ya Rais
Apewe milioni tano nyingine ya kuzungusha
 
Back
Top Bottom