Harvey Specter
Member
- Jun 26, 2024
- 23
- 27
Kufuatia kuongezeka kwa miamala ya fedha za kigeni katika manunuzi ya bidhaa na huduma mbalimbali nchini, Wizara ya Fedha kupitia Sheria ya Benki Kuu, Sura ya 197 imetangaza Kanuni za Matumizi ya Fedha za Kigeni za mwaka 2025. Kanuni hizi zimeanza kutumika rasmi Machi 28, 2025.
Kanuni namba 2 ya Kanuni hizi, inaelekeza kwamba bei zote za bidhaa na huduma nchini zitangazwe kwa shilingi ya Tanzania.
Aidha Kanuni zinaelekeza kwamba mtu yeyote atakayefanya yafuatayo atakua anatenda kosa;
(a) atalazimisha, atashiriki, atasaidia au kuwezesha upangaji bei ya bidhaa au huduma yoyote nchini kwa kutumia fedha ya kigeni;
(b) atanukuu, atatangaza, atabainisha au kuchapisha bei ya bidhaa au huduma yoyote nchini kwa kutumia fedha ya kigeni;
(c) atalazimisha au kuwezesha malipo ya bidhaa au huduma yoyote nchini kufanyika kwa kutumia fedha ya kigeni;
(d) atakataa bidhaa au huduma yoyote nchini kulipiwa kwa kutumia shilingi ya Tanzania; au
(e) atapokea malipo ya bidhaa au huduma ndani ya nchi kwa kutumia fedha ya kigeni.
Pia Kanuni zinakataza mtu yeyote kuingia katika mkataba wa bidhaa au huduma kwa malipo ya fedha ya kigeni ndani ya nchi isipokua kwa mikataba kadhaa.
Kufuatia hilo, Kanuni zimetoa muda wa mwaka mmoja kwa watu na makampuni kurekebisha mikataba yote ya utoaji wa bidhaa au huduma iliyosainiwa kabla ya Kanuni hizi kuanza kutumika ambayo imeelekeza malipo kwa fedha za kigeni. Endapo haitafanyiwa marekebisho ndani ya mwaka mmoja tangu tarehe 28, machi 2025, mikataba hiyo itakuwa batili.
Ikumbukwe kwamba bidhaa na huduma hizo ni pamoja na kuuza au kupangisha nyumba, viwanja na ofisi, ada za shule, pamoja na malipo na ushauri.
Miamala inayoruhusiwa kutozwa kwa fedha za kigeni ni kama ifuatayo;
Kanuni namba 2 ya Kanuni hizi, inaelekeza kwamba bei zote za bidhaa na huduma nchini zitangazwe kwa shilingi ya Tanzania.
Aidha Kanuni zinaelekeza kwamba mtu yeyote atakayefanya yafuatayo atakua anatenda kosa;
(a) atalazimisha, atashiriki, atasaidia au kuwezesha upangaji bei ya bidhaa au huduma yoyote nchini kwa kutumia fedha ya kigeni;
(b) atanukuu, atatangaza, atabainisha au kuchapisha bei ya bidhaa au huduma yoyote nchini kwa kutumia fedha ya kigeni;
(c) atalazimisha au kuwezesha malipo ya bidhaa au huduma yoyote nchini kufanyika kwa kutumia fedha ya kigeni;
(d) atakataa bidhaa au huduma yoyote nchini kulipiwa kwa kutumia shilingi ya Tanzania; au
(e) atapokea malipo ya bidhaa au huduma ndani ya nchi kwa kutumia fedha ya kigeni.
Pia Kanuni zinakataza mtu yeyote kuingia katika mkataba wa bidhaa au huduma kwa malipo ya fedha ya kigeni ndani ya nchi isipokua kwa mikataba kadhaa.
Kufuatia hilo, Kanuni zimetoa muda wa mwaka mmoja kwa watu na makampuni kurekebisha mikataba yote ya utoaji wa bidhaa au huduma iliyosainiwa kabla ya Kanuni hizi kuanza kutumika ambayo imeelekeza malipo kwa fedha za kigeni. Endapo haitafanyiwa marekebisho ndani ya mwaka mmoja tangu tarehe 28, machi 2025, mikataba hiyo itakuwa batili.
Ikumbukwe kwamba bidhaa na huduma hizo ni pamoja na kuuza au kupangisha nyumba, viwanja na ofisi, ada za shule, pamoja na malipo na ushauri.
Miamala inayoruhusiwa kutozwa kwa fedha za kigeni ni kama ifuatayo;
- Michango ya uanachama inayolipwa na Serikali kwa taasisi za kikanda zilizopo nchini
- Miamala inahusisha Balozi na mashirika ya kimataifa yaliyopo nchini
- Mikopo ya fedha za kigeni inayotolewa na benki za biashara na taasisi za fedha zilizopo nchini
- Malipo ya bidhaa katika maduka yasiyotoza ushuru