SoC04 Serikali iwe tayari kuzifuatilia mbegu za mazao Kwa majaribio ya kupanda sio Kwa majaribio ya upimaji kisasa bila kupanda

Tanzania Tuitakayo competition threads

hauleibrahim

Senior Member
May 17, 2024
171
111
Kilimo ni maisha na maisha yetu ni kilimo na chakula.ni serikali Sasa ifike mahali iache longolongo hasa linapokuja suala la kilimo chenye tija Kwa mkulima wa chini.

Kuna mambo machache serikali inapaswa kuyaboreaha Kwa vitendo ya majaribio sio matendo ya kisasa Kwa vifaa kila mwaka wa kilimo uanzapo.

1.Kuwe na ukaguzi wa mbegu zilizo sokoni na ubora wake katika upataji wake hasa hizi chotara:ni muhimu serikali ikawa na mashamba ambayo yatakuwa yanapandwa mbegu mbalimbali zinazo tarajiwa kuingizwa sokoni kumfikia mkulima kabla hazijafika Shamba ili kujiridhisha na ubora wa mbegu Kwa vitendo na sio bra bra ambazo mwishowe mbegu hizo zikija kumfikia mkulima baadhi ya mbegu za kampuni huwa hazina sifa shambani Kwa mkulima na kuongeza umaskini Kwa mnunuzi wa mbegu hizo za Gharama.

2.Tuzikague mbolea Kwa vitendo mashambani ili tuone mbolea zilizopo na zinazo tarajiwa kuingizwa sokoni zina sifa za kuboresha sekta ya ukuaji wa kilimo au zinakuja kuongeza umaskini Kwa mnunuzi wa mbolea na isiwe na tija shambani kwake pamoja na mazao.

Kuna mbegu chotara ni nzuri Kwa matangazo na mashamba darasa ya wauzaji mbegu ila sokoni mpka shambani Kwa mkulima mbegu na mbolea hizo huwa hazina sifa ni jukumu la serikali wakishirikiana na wadau kuzifungia na kizitaja hizo kampuni wazi wazi ili ziwajinishwe zinapo bainika kuwa na mbegu zisizo kidhi matakwa ya mkulima pia iwe hivyo hivyo kwenye mbolea ukaguzi uwe mara Kwa mara kwenye mbolea kbla ya msimu wa kulima kuanza kuepusha mbolea zisizo na sifa zilizo andikwa kumfikia mkulima na kumuongezea umaskini.

Mbolea za kisasa na mbegu za kisasa zinapaswa kufanyiwa majaribio mashambani Kwa vitendo ili kuona kama vinatija Kwa mkulima na sio kuingiza mbolea na mbegu ZeNye sifa za chini au zisizo na sifa alafu mkulima akaishia kupata hasara Kwa kupoteza fedha alizo nunua mbolea na kununua mbegu za kisasa.

Kuna wenzako walinunua mchicha walipo panda yakaota magugu Kuna wenzako walinunua mbolea baada ya mbolea kuchochea ukuaji wa mmea wenyewe ukachochea uharibifu shambani kwenye mazao ya mkulima.

Kuna mbegu mwaka huu zilizo kuwa hazija fanyiwa majaribio ya kutosha kuendana na hali zote zimeshindwa kuwa na tija hasa kwenye kilimo Cha mahindi hasa mbegu hizi ambazo hazihimili mvua nyingi kama za mwaka huu.

Hitimisho;mbegu zifanyiwe majaribio mashambani kabla ya msimu wa kilimo kuanza hivyo hivyo na mbolea ili kuondoa hasara Kwa mkulima kule kijijini kwetu
 
Back
Top Bottom