Selena Gomez: Huwa nafuta App ya Mtandao wa Instagram kwenye simu yangu walau mara moja kila wiki

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Jan 29, 2021
577
2,595
51E07136-2F76-4BCB-9DFA-7C0AB35E7FCD.jpeg

Mwaka 2017, akihojiwa na baadhi ya vyombo vya habari kuhusu namna anavyoutumia mtandao huo, Selena alinukuliwa akisema “Huwa nafuta App ya mtandao huu walau mara moja kila wiki sababu Watu huandika maoni makali kama vile wanataka kukutoa roho”

Mwaka 2019 aliamua kusitisha matumizi ya mtandao wa Instagram ambapo pamoja na sababu zingine alidai ni kuwepo wa unyanyasaji mkubwa, hali iliyomfanya awe kwenye hatari ya kupatwa na sonona.

Baada ya kutokuwepo kwenye mtandao huo kwa zaidi ya miaka 4 huku akimuwaachia udhibiti wa Akaunti hiyo wasaidizi wake, January 13, 2023 alirejea tena kwa kupost picha iliyoambatana na maneno …”Wait, can you tell I’m back on Instagram?”

Selena Gomes ni mwanamuziki mwenye ushawishi mkubwa kwenye Mtandao wa Instagram. Anashikilia nafasi ya 5 ya kuwa mtu mwenye wafauasi wengi zaidi kwenye mtandao huo.

Umewahi kufuta mitandao ya kijamii baada ya kukutana na unyanyasaji wa aina yoyote ile?
 
Anakwama wap.si atumie followed wake awe anapata endorsed za matangazo.su angepiga hela.huyu gomez nae.nilivomuonaga miaka fulan anauza sura na yule dogo bieber nikajua hapa hamna kitu.bint kapevuka kiakil ila biber bado
Ohooo mkuu unadhani yeye kuacha kutumia Instagram inamaana ndio haitumiki kibiashara?

Alichofanya yeye ni kuwapa watu maalumu wa kuiendesha ili asiwe anasoma zile comments za maudhi na baadhi ya jumbe zinazotumwa DM

ila kwa upande wa kupiga mpunga kupitia Instagram sio haba, yupo miongoni mwa ma celebrity watano wanaolipwa pesa ndefu kwa post moja

Inakadiriwa anapata 3B kwa one post katika account yake ya Instagram, wakiongozwa na Ronaldo anaekula almost 7B kwa post moja
 
Ohooo mkuu unadhani yeye kuacha kutumia Instagram inamaana ndio haitumiki kibiashara?

Alichofanya yeye ni kuwapa watu maalumu wa kuiendesha ili asiwe anasoma zile comments za maudhi na baadhi ya jumbe zinazotumwa DM

ila kwa upande wa kupiga mpunga kupitia Instagram sio haba, yupo miongoni mwa ma celebrity watano wanaolipwa pesa ndefu kwa post moja

Inakadiriwa anapata 3B kwa one post katika account yake ya Instagram, wakiongozwa na Ronaldo anaekula almost 7B kwa post moja

Ronaldo anakula ela yote hiyo Daaah! Sasa kwanini hata kwa siku asiwe anapost hata post tatu au tano apige pesa ndefu zaidi
 
Ronaldo anakula ela yote hiyo Daaah! Sasa kwanini hata kwa siku asiwe anapost hata post tatu au tano apige pesa ndefu zaidi
Mfano, amepost picha binafsi na mtoto wake, au yule demu wake, hapo anapataje hela!?

Nadhani kwa post binafsi hapati hela, ila post za matangazo, mfano ile picha yake na Messi kipindi cha WC.

Kama kuna mjuzi tafadhali aje kutuelewesha!!
 
Mfano, amepost picha binafsi na mtoto wake, au yule demu wake, hapo anapataje hela!?

Nadhani kwa post binafsi hapati hela, ila post za matangazo, mfano ile picha yake na Messi kipindi cha WC.

Kama kuna mjuzi tafadhali aje kutuelewesha!!
Uko sawa sawa mkuu, hayo malipo ni kwa zile kampuni ambazo zinataka kutangaziwa bidhaa zao na sio kwamba anapopost tu picha zake yeye analipwa

Kwahiyo ukitaka kutangaziwa bidhaa zako katika page ya bwana CR7 ndio utahitaji kuwa na hizo 7B ila yeye picha zake anapost tu kila akijiskia
 
Ronaldo anakula ela yote hiyo Daaah! Sasa kwanini hata kwa siku asiwe anapost hata post tatu au tano apige pesa ndefu zaidi
mkuu analipwa pale anapo post bidhaa za watu wengine au kampuni zingine ila picha zake ye anapost tu kila akijiskia

ili apate hizo 7B ni hadi pale atakapotokea mteja na kuhitaji kujiuza kwenye page ya Ronaldo

Mfano wewe uwe una maji yako ya kunywa yanaitwa "Jaluo pure water" na unahitaji kuyatangaza itakubidi umlipe jamaa 7B lakini mbali na hiyo pesa anazingatia vigezo na masharti ambavyo yeye amejiwekea ili akubali kufanya kazi na wewe
 
Haya selena nimefika endeleeni kuongea,,for me nakapenda ni kazuri lakini kana sauti nzuri pia baada ya kuachana na Bieber kamejitahid kumove on
 
Back
Top Bottom