Sambusa za nyama na juice ya matunda

Mwachiluwi

JF-Expert Member
Mar 10, 2022
24,993
48,019
Leo tujifunze hii kitu sambusa za nyama

MAHITAJI
Unga wa ngano
Nyama
Hoho
Karoti
Chumvi
Mafuta

Kwanza chemsha nyama yako kisha isage vizuri
Then chukua ngano weka mafuta na chumvi anza kukanda mimi natengeneza za kula mwenyewe so nilitumia unga nusu
1739448296802.jpeg


Baada ya hapo ngano yako ulio kanda ipumue kidogo kisha kata na utengeneze madonge kama ya chapati
1739448403411.jpeg

Baada ya hapo anza kusukuma moja moja iwe kama chapati hakikisha isiwe nzito
1739448471016.jpeg

Baada ya hapo andaa sahani pembeni weka unga kwenye sahani kisha weka chapati yako kwenye sahani
1739448558470.jpeg

Na ukiwa unaweka unazibebanisha juu yake unapaka mafut kama ivyo ili ukija babua inakuwa ni vyepesi kuzitoa
1739448632761.jpeg

Ukimaliza hapo chukua kidogo mimi nilichukua kama chapati tatu zikiwa zimebebana nikazisukuma tena
1739448705564.jpeg

Baada ya hapo unakata kwa njia ya msalaba kama hivi
1739448750155.jpeg

Baada ya hapo unaenda kubabua
1739448789081.jpeg

Weka pole pole ukimaliza kubabua njoo uziachanishe kama hivi
Baada ya hapo nikachukua nyama nilio isaga na kuikaanga nilichanganya pilipili karot na hoho
1739449167500.jpeg

Baada ya hapo chukua sasa vipande vyako na ulivyo achanisha kunja kama hivi
1739449327183.jpeg
na uweke nyama kidogo tu usijaze mpaka juu
1739449368575.jpeg

Na kunja vizur hakikisha hakuna pembe ya sambusa inayo weza fanya mafuta yaingie ndani
1739449479883.jpeg

Kisha zikaange kwenye mafuta yalio chemka ili zisinyonye mafuta na ziwe za kawahawia
1739449538494.jpeg

Zilikuwa mzuri sana
1739449565269.jpeg

Juice mnajua kusaga nitawapa mahitaji tu
Embe moja
Nanasi moja
Passion matatu

1739449669927.jpeg
 

Attachments

  • RPReplay_Final1739448856.mov
    4.5 MB

Similar Discussions

Back
Top Bottom