Sakata la Mafao: Wanakati Tunaangalika na hii Nusu Shari ya Sasa tusisahau Shari Kamili inayokuja

Logikos

JF-Expert Member
Feb 26, 2014
12,789
19,958
Ni kweli mafao ya wastaafu hayatoshi (si wao tu asilimia kubwa ya wabangaizaji Tanzania either hakuna wanachopata na wakipata hakitoshi)...; Lakini wakati tunachemsha Bongo jinsi ya kuwarekebishia hawa kidogo kiwe kikubwa kidogo, ni vema tukaangalia ni vipi hatari inayokuja kesho ya wazee wa kesho ambao watakuwa hata hicho kidogo hawana....


Mafao / Pensheni moja ya sababu yake kubwa ni pale huyu mchumia juani nguvu zake zitakapomtupa aweze kupata hata mahitaji yake muhimu na asiwe omba omba wala kusumbua jamii inayomzunguka..., lakini kinachotokea sasa, sababu wengi wa vijana hawana sehemu ya kuchumia uzee wao watakuwa sio tu kwamba hawana nguvu hata kile kidogo cha kuwawezesha kitakuwa hakipo....

Na hapo ndio tutakuwa na Taifa la Wazee wengi omba omba na hii itakuwa sio Haki kwa vijana wa wakati huo au Taifa kuzungukwa na omba omba (Taifa linaloshindwa kuangalia wazee wao)
1713599707733.png
 
@Mods, Active
Msaada kwenye Heading Wakati Tunahangaika na sio Wanakati Tunaangalika
 
Tatizo haliko huko, tatizo ni kwamba serikali imewekeza zaidi kwenye upigaji, kama serikali ingebana matumizi na kuimbarisha maslahi ya watumishi wake, hiyo misukosuko yote isingekuwepo, sioni sababu kununua magari ya mil 600 kwa mamia ya viongozi huku barabara zikiwa hoi, gharama za matengennezo ni kubwa huku watumishi wakiwa hoi na ufanisi ukiwa chini ya 10%
 
Tatizo haliko huko, tatizo ni kwamba serikali imewekeza zaidi kwenye upigaji, kama serikali ingebana matumizi na kuimbarisha maslahi ya watumishi wake, hiyo misukosuko yote isingekuwepo, sioni sababu kununua magari ya mil 600 kwa mamia ya viongozi huku barabara zikiwa hoi, gharama za matengennezo ni kubwa huku watumishi wakiwa hoi na ufanisi ukiwa chini ya 10%
Hivi kweli mwanasiasa tena wa kiafrika anaweza kuwa na huruma na watu wasiojitambua?? Usione wazungu wamefikia hapo ni kutokana na kujitambua kwao!! Hata kama ni weee kwenye deal zako unapokutana na jitu jinga unafanyaje??
 
Hivi kweli mwanasiasa tena wa kiafrika anaweza kuwa na huruma na watu wasiojitambua?? Usione wazungu wamefikia hapo ni kutokana na kujitambua kwao!! Hata kama ni weee kwenye deal zako unapokutana na jitu jinga unafanyaje??
Hilo jinga siku likiuchoka ujinga ndiyo utalielewa
 
Tatizo haliko huko, tatizo ni kwamba serikali imewekeza zaidi kwenye upigaji, kama serikali ingebana matumizi na kuimbarisha maslahi ya watumishi wake, hiyo misukosuko yote isingekuwepo, sioni sababu kununua magari ya mil 600 kwa mamia ya viongozi huku barabara zikiwa hoi, gharama za matengennezo ni kubwa huku watumishi wakiwa hoi na ufanisi ukiwa chini ya 10%
Hapo unaongelea Nusu Shari...; waliopo wanapata kisichotosha..., Vipi kuhusu Shari / Hatari kamili.., wabangaizaji / machinga wa sasa ambao kazi zao ni (hand to mouth) kesho yao itakuwaje ? Sababu sio Pensionable na hawana asset yoyote zaidi ya mtaji wa nguvu ambazo hazihitajiki sababu hakuna ajira zenye ujira....Hao kesho yao itakuwaje.... ?

Kurekebisha mafao ya waliopo ni rahisi sana lakini ku-detonate hii time Bomb itakayokuja hapo kesho inahitaji deep thinking na jitihada za jumla na sio kuangalia mambo kwa mafungu... Na sio kwamba wanasiasa hawajui, lakini wanaona bora wafanye mambo rahisi rahisi lakini hili Bomu wanalotega leo siku litakapoleta madhara watakuwa walisha-retire wanakula pensheni (wanasahau mchuma janga hula na wakwao)
 
Hapo unaongelea Nusu Shari...; waliopo wanapata kisichotosha..., Vipi kuhusu Shari / Hatari kamili.., wabangaizaji / machinga wa sasa ambao kazi zao ni (hand to mouth) kesho yao itakuwaje ? Sababu sio Pensionable na hawana asset yoyote zaidi ya mtaji wa nguvu ambazo hazihitajiki sababu hakuna ajira zenye ujira....Hao kesho yao itakuwaje.... ?
Labda sijaelewa faida za mfumo uliopo na namna gani machinga wananufaika nao
 
Labda sijaelewa faida za mfumo uliopo na namna gani machinga wananufaika nao
Kwa majority kukosa ajira leo ni kwamba kesho yao watakuwa hawana hata hicho kidogo..., Ungeweza kusema wajiwekee wenyewe ila sababu ni hand to mouth hawana hata pesa ya kutumia leo let alone ya kutunza...

Kwa muajiriwa afadhali anakatwa kwenye mshahara wake na kuongezewa na muajiri anakuwekea ili uzeeni apate insurance / wasio na ajira hawana hio insurance ya kupata kila mwezi...

Na mifumo ya Pensheni naweza kusema ni National Insurance kuwa-protect hawa ambao leo wana nguvu za kuweza kuhangaika ili kesho wakichoka wapate chochote...; Sasa kama Taifa tumeshindwa kuwatumia kama nguvu kazi wakati wana-weza kuchangia nguvu wakizeeka pia itakuwa mzigo kwa Taifa kwa kuwa na omba omba wazee....
 
Sasa kama Taifa tumeshindwa kuwatumia kama nguvu kazi wakati wana-weza kuchangia nguvu wakizeeka pia itakuwa mzigo kwa Taifa kwa kuwa na omba omba wazee....
Nimekuelewa, upo sahihi
 
Tatizo wataàlam hawakazii mañeno yaobtukawaelewa.FÀO LA KUJITOA sio sahihi ila ndio kimbilio la vijana wengi na wakizeeka(kuishiwa nguvu) sijui itàkuaje.
 
Tatizo wataàlam hawakazii mañeno yaobtukawaelewa.FÀO LA KUJITOA sio sahihi ila ndio kimbilio la vijana wengi na wakizeeka(kuishiwa nguvu) sijui itàkuaje.
Naam wanaleta Siasa....; badala ya kuhakikisha vijana hawa wakiwa na nguvu zao wanaweza kuzalisha na kuendesha maisha wanakimbilia kwenye cheap politics kwamba sababu ni cha kwao tuwape wasepe...., Okay wakisepa alafu wakala zikaisha wakizeeka wakiwa ombaomba ni hasara ya nani kama sio Taifa zima..

Pili bora hata hao wanaweza kujitoa (ni kwamba walipata ka-ajira fulani) Je mbangaizaji mtaani / mkimbiza mwenge ambaye hajawai hata kupata formal ajira maishani mwake..., au amepata ajira za kampuni za kubangaiza ambazo ndani ya miaka mitano zinakuwa zimefirisika na mwajiri hakuwahi kupeleka mafao ?
 
Back
Top Bottom