Sababu za kuanguka kwa majengo

greater than

JF-Expert Member
Sep 22, 2018
973
1,610
MAKALA YA 9
Leo tuangazie janga ambalo limekuwa likitokea katika nchi yetu kila baada ya miaka kadhaa. Kuanguka kwa Majengo

1.Sababu kuu za Kuanguka kwa Majengo ni kama zifuatazo
MSINGI WA JENGO KUWA DHAIFU
  • Tabia za ardhi za maeneo/Miji na mitaa hutofautiana.
  • Maeneo ya kutuwamisha maji,Mfinyanzi huitaji msingi imara zaidi.
  • Lakini kwa kukwepa gharama wala haifanyiki hivyo
  • Jengo la ghorofa 4,mjini Kigali Rwanda ,liliporomoka kisa udhaifu wa msingi.
    _89597149_rwandabuildinggettyimages-168784961.jpg
2. UTUMIZI WA MATILIO DHAIFU
  • Kutumia Nondo ,Nyaya za kufunga zisizo na ubora.
  • Utumizi wa matofali,mabovu,mchanga wenye chumvi,kokoto zenye alkali.
  • Jengo la ghorofa 6,Jijini Kampala lilianguka kisa utumizi wa matilio mbovu.
3. UZITO MKUBWA JENGO
  • Unakuta Ghorofa lilitakiwa Liwe na floor 4,Ila kwa tamaa tu,mmiliki anaamuru liwe la ghorofa 6.
  • Hapa hatakama Msingi ulijengwa vizuri,utaelemewa na kuangusha Jengo.
  • Jengo la Ghorofa ,Mtaa wa Indira Gandhi, lilianguka kisa hiki.
  • Jengo lilikuwa la Ghorofa 12,mmiliki Bwana RAZA DAMJI akaamuru na kuhonga na kuongeza ghorofa zingine 4.
    images (30).jpeg
4. KUTOFANYIKA KWA VIPIMO VYA UBORA
  • Sheria zinataka Majengo yote yawe yanafanyiwa ukaguzi na vipimo katika kila hatua ya ujenzi
  • Maghorofa mengi ya Kigamboni,Goba,Makabe,Chanika,Buyuni,Pugu, Toangoma hayafanyiwi ukaguzi.
  • Mjenzi hutakiwa kuwasilisha sample ya zege kwenye ofisi za viwango,lakini haifanyiki hivyo
  • Wakaguzi wa ujenzi kutoka manispaa, huenda site kupata hongo na kuondoka .
5. KUTOTUMIA WATAALAM
  • Mteja anapakua Ramani mtandaoni anapita njia za panya kugonga muhuli na kupata kibali
  • Ramani haijafanyiwa tathmini ya mfumo wa mhimili/structure
  • Anampa kazi fundi,
  • Jengo Laanza kujengwa bila hata kuwa na sanifu ya mhimili
  • Aisee,siyo kila jengo huwa na aina sawa ya msingi
  • Siyo kila jengo nguzo zitaachana kwa mita 4 au 5
  • Jengo la ghorofa 1,Goba kwa awadhi lilianguka kisa hiki.
6. TAMAA
  • Hapa Mtaalam/Fundi,wanaingia tamaa ,wanaanza kuiba matilio za ujenzi
  • Wanabadilisha viwango vya ujenzi
  • Utumizi wa vifaa duni vya kazi
  • Kuwaisha ujenzi bila kujali ubora wa kinachojengwa.
7. UCHAKAVU
  • Zanzibar na Bagamoyo ndiyo wahanga wa Kipengele hiki.
  • Hiji miji mikongwe, majengo yake mengi ni yana zaidi ya miaka 100.
  • Hayafanyiwi ukarabati wa kutosha
  • Yanakuja yanaagnuka yenyewe
images (32).jpeg

8. Nini kifanyike kuondokana na Janga hili
  • Mteja kusanifiwa Ramani yenye kuendana na eneo lake
  • Kuandaliwa na nyara za mhimili
  • Ujenzi ufanyike kwa kufuata viwango
  • Wakaguzi wajitume na kufuata sheria
  • Wato kutoishi katika magofu
  • Kutakuwa na Tamaa
  • Sheria na Taratibu zifuatwe katika hatua za ujenzi
9. Unataka Jenga Ghorofa la millioni 200 kwa kutumia fundi wa millioni 1,duh...
-umakini wahitajika

10.Hata ukitumia fundi,basi tafuta mtaalam awe anakuja kukagua Ujenzi katika kila hatua kubwa ya Ujenzi,,,ole miaka minne/mitano ya shule usichukulie poa.....

Kwa yule mwenye huitaji wa ukaguzi wa jengo lake. Mwenye shaka juu ya tatizo lolote la jengo lake,asisiste kuwasiliana. Wahi kabla ya mwezi wa 5 kuingia

Nakaribisha maswali na Maoni.....
 
vp kuhusu wanaojenga mabondeni karibu na mito jengo haliwezi kuathilika
 
vp kuhusu wanaojenga mabondeni karibu na mito jengo haliwezi kuathilika
Kujenga kwenye Mabonde ya Mto ni hatari kwani.
  • Maeneo hayo mara nyingi huwa na udongo wa kichanga, kwahiyo ardhi inakuwa siyo imara, mmominyoko hutokea na Majengo huanguka...mfano: Mto Mbezi upande wa Kawe Makao mapya,nyumba nyingi zimesombwa...
  • Mto hubadili njia,ambazo unaweza kuja na kusomba jengo lako.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom