Riwaya ya kipelelezi: Wakala wa Siri

siri.jpg


WAKALA WA SIRI 13
Mtunzi; Robert Heriel
0693322300

ILIPOISHIA
Alipanda ghorofa ya pili akiwa kashika bastola yake mkononi, alipofika juu ghafla akasimama baada ya kusikia sauti ya watu wakizungumza. Alitulia kisha akasikiliza;
“ Haiwezekani mpaka sasa hivi hatujaipata Chipu ya Darubini, mwezi sasa umeisha bado mnahangaika bila mafanikio yoyote. Ingekuwa bora kama mngekosa hizi sampo na Cadava kuliko kukosa chipu ya darubini ya hospitalini” Maneno hayo yalimchanganya sana Sajenti akiwa kajificha kwenye korido pembeni ya mlango wa kuingilia kwenye chumba ambacho kulikuwa na kikao cha siri.

INAENDELEA

“ Nafikiri kuna mchezo tumechezewa, na mwenye uwezo wa kucheza mchezo huu ni mtu mmoja. Sasa naweza kuelewa” Sauti nyingine ya mwanaume ilizungumza, Sajenti akiwa makini kusikiliza bila ya kuwaona watu wale.

“ Mtu gani huyo Dokta Binamungu? Nakuahidi donge nono zaidi ikiwa utatufungulia njia ya kumfahamu huyo adui ambaye anavuruga mipango yetu. Tuambie ni nani mtu huyo?” Sajenti aliamini sauti hiyo ilikuwa ya kiongozi wa kikao hicho. Alishtuka pia kusikia jina la Dokta Binamungu, alikuwa akimfahamu kama Daktari wa hospitali ya Boreti ingawaje alikuwa hanamazoea naye. Kufikia hapo Sajenti akaanza kuona mwanga wa kile kinachoendelea, tayari aligundua kuwa Dokta Binamungu ni miongoni mwa wasaliti waliowageuka na kutoa siri za taifa kuhusu hospitali ya Boreti.

“ Nadhani Dokta Beatus atakuwa anafahamu chochote kuhusu kupotea kwa Chipu, yeye ndiye mhusika tuu” Dokta Binamungu alisema.

“ Sidhani..! Ile siku nilivyomzimisha akazirai hakuwa na ujanja mwingine, nilichukua hiyo chipu kwenye darubini na kuondoka” Sauti ya mwanamke iliongea. Sajenti alishtuka kusikia sauti ya kike. Kilichomchanganya zaidi ni kusikia kuwa kumbe Yule mtu aliyevaa kininja aliyemuona siku ile alikuwa ni mwanamke. Sajenti hakudhani kama mtu Yule waliyemuona kwenye Kamera siku ile wakiwa room 66 angekuwa mwanamke. Jinsi alivyokuwa akitembea, alivyomvamia Dokta Beatus na pia alivyoibeba ile Cadava hakuna ambaye angeamini mtu Yule alikuwa ni mwanamke. Watu wote walijua ni mwanaume. Sajenti alitaka kumuona Yule mwanamke aliyekuwa akiongea angalau sura yake.

Habari za Dokta Beatus kutajwa kwenye kile kikao kilimfanya akili yake ikose utulivu. Aliona ipo haja ya yeye kumuwai Dokta Beatus kabla hajafikiwa na wale watu wabaya. Hakutaka kuchelewa kama alivyochelewa kwenye hospitali ya Boreti mpaka Mateka wa Ushahidi akatoroshwa.

Ghafla akiwa bado pale mlangoni alisikia mtu akipanda ngazi kuja ghorofa ya pili kule alipokuwa amesimama. Akajua ni Yule Mzee mlevi aliyekuwa amelala pale sebuleni ndiye aliyekuwa anakuja. Upesi alifyatuka kumfuata kulekule alipokuwa akija, hamadi! Walikutana kwenye ngazi Yule mlevi akiwa anapanda akiwa kashika chupa yake. Mlevi alishtushwa kwa uwepo wa Sajenti mule ndani, alikuwa kama kaona jini wa kaburini aliyesimama mbele yake. Mlevi hakutarajia kutokea kwa Sajenti. Sajenti hakutaka kumchelewesha alimpiga teke la kifua akadondoka na kuanza kubilingita mpaka chini ilipo ngazi ya kwanza. Masikini Mlevi wa watu kabla hajafikiri cha kufanya Sajenti alimzima kwa buti la kifua kama Mjeshi anayepiga guu pande. Hapo hapo Mlevi akapoteza fahamu.

Sajenti alitoka akaenda sebuleni, akakagua kagua lakini hakuona la maana, akatoka nje na kuondoka.

Moja kwa moja aliazimia kwenda nyumbani kwa Dokta Beatus, alichukua pikipiki yake na safari ya Sinza Mori ikaanza. Njia zilikuwa nyeupe pasipo na magari, ilikuwa tayari imehitimu saa kumi na nusu. Ndani ya Lisaa limoja alikuwa kashafika Sinza Mori yapata saa kumi na moja na nusu kukiwa kumekucha, Daladala na magari yakiwa yameshaanza kutembea barabarani. Alipaki pikipiki yake mbele ya geti la Nyumba ya Dokta Beatus. Bila kupoteza muda alizunguka kwa nyuma akaruka ukuta na kuzama ndani. Nyumba ya Dokta Beatus ilikuwa kimya, hii ikamfanya Sajenti kuwa makini zaidi. Alichungulia kwenye dirisha la sebuleni, hakuona mtu yeyote ingawaje taa ya sebuleni ilikuwa inawaka. Punde Sajenti alishtuka kumuona msichana akitokea pale sebuleni, Yule msichana alikuwa akipikicha macho yake yaliyozingirwa na utando wa tongo tongo za usingizi. Msichana Yule bila ya kujua kuna mtu anamtazama alifunua kanga yake ambayo aliifungia kwenye shingo kwa mtindo wa mtu anayetoka kuoga. Woooh! Sajenti soni ilimshika kuona msichana Yule akiwa uchi kama alivyozaliwa. Sajenti hakutaka kuona mambo kama yale, alificha macho yake kwa aibu ili asiuone uchi wa Yule msichana mdogo ambaye kwa umri alionekana anamiaka kumi na nane.

Ghafla Sajenti akiwa kaficha macho yake na viganja vyake, alisikia sauti ya viatu ndani ikitembea, akachungulia. Hapo akamuona Dokta Beatus akitokea chumbani akiwa kavaa kwa umaridadi, Yule msichana alivaa kanga haraka lakini alikuwa ameshachelewa kwani Dokta Beatus alikuwa amemuona. Kwa aibu Yule msichana alifunga kanga yake huku akizuga kwa kuitengeneza sebule. Chakushangaza Dokta Beatus alipofika pale sebuleni alimfuata moja kwa moja Yule msichana na kusimama nyuma yake huku akimkumbatia kwa nyuma. Jambo hili lilimshangaza sana Sajenti. Iweje Dokta mwenye elimu kubwa, na anayeheshimika kwenye jamii afanye mambo kama yale. Jambo hili lilimchukiza sana Sajenti lakini hakuwa na lakufanya zaidi ya kushuhudia aibu ile.

Aliwaona Wakinyonyana ndimi huku wakishikana kwa mahaba mazito, Sajenti aligundua kuwa ule ndio ulikuwa mchezo wao kwani kila mmoja wao alimfurahia mwenzake. Walipinduana mpaka kwenye sofa huku kanga ya Yule binti ikianguka, na hapo akawa uchi kama alivyozaliwa. Hii ilimpa nafasi Dokta Beatus kuufaidi mwili wa msichana Yule ambaye Sajenti alihisi kuwa ni Mfanyakazi wa ndani. “Mtoto mdogo lakini anamambo makubwa jamani” Sajenti alijisemea kimoyo moyo huku uhondo ule ukizidi kupamba moto.

Punde jambo lakushangaza lilimshtua Sajenti, alimuona Yule msichana akiingiza mkono wake kwenye mfuko wa Suruali ya Dokta Beatus, hapa Sajenti akawa macho kushuhudia kile anachotaka kukifanya Yule binti, lakini kabla Yule binti hajatoa mkono wake ndani ya mfuko wa Dokta ghafla sauti ya mlango wa chumbani ikasikika, na wote wakakurupuka huku Yule binti akiiwahi kanga yake pale chini na kujifunga. Dokta Beatus alijiweka sawia na kitambo kidogo alisimama mke wa Dokta Beatus akiwa kavaa nguo za kiofisi na mkoba wake begani huku akijiangalia kwenye kioo. Mke wa Dokta hakuwashtukia, ni wazi alikuwa hajawaona. Waliondoka na kumuacha Yule msichana pale sebuleni akiwa haamini kama hajafumaniwa.

Sajenti alimlaumu sana kimoyomoyo Yule binti kwa yale aliyokuwa anayafanya lakini hata hivyo alimtetea kuwa huenda alikuwa amelazimishwa na Dokta. Hivyo wakulaumiwa ni Dokta Beatus. Bado akiwa dirishani kwa nje alishangaa kuona Yule binti akijibwaga kwenye sofa huku akichekelea kama mtu aliyefanikisha jambo Fulani. Hii iliongeza umakini kwa Sajenti, alitaka kujua ni kwanini Yule binti anacheka kwa namna ile. Hapo akakumbuka muda ule Yule binti akiwa anaingiza mkono katika mfuko wa Dokta Beatus. Akili ya udadisi ikabisha hodi, na macho ya uvumbuzi yakachomoza kama jua la wakati wa kiangazi.

Yule msichana akiwa kakaa pale Sofani alitoa kifaa kilichofanana na Chipu. Sajenti alipagawa alipokiona. Akili yake ilimuambia ndio ileile chipu wanayoitafuta, ndio ileile chipu ambayo kama ataipata inaweza kumfanya akawa huru. Mapigo ya moyo yalienda upesi kama kimbunga, mwili ulimsisimuka mno. Akili yake ilikosa utulivu huku ikipiga kite. Angeachaje kupagawa ikiwa chipu hiyo ndiyo inayodaiwa kuwa yeye ndiye kaiiba. Chipu iliyomgeuza kuwa mkimbizi katika nchi yake mwenyewe. Ingawaje kulikuwa kuna kupotea kwa Cadava, lakini aliona kama angepata ile chipu ingempunguzia mzigo kwa kiasi Fulani. Lakini iweje Yule msichana aibe ile chipu kwenye mfuko wa dokta Beatus, anakazi nayo gani? Kama ametumwa, nani aliyemtuma? Mbona ni msichana mdogo lakini jambo alilolifanya ni kubwa?

Sajenti alivamiwa na msururu wa maswali yasiyo na majibu. “Huyu msichana anamuda gani katika nyumba ya Dr. Beatus? “ Sajenti alinong’ona Wakati huo Yule binti akinyanyuka na moja kwa moja akaelekea chumbani jambo ambalo lilimfanya Sajenti kuangalia anaelekea chumba kipi. Basi baada ya kujua chumba alichoingia Yule msichana, Sajenti akazunguka mpaka lilipodirisha la kile chumba. Alipofika dirishani alimsikia Yule msichana akiongea na simu.

”Ilikuwa kazi rahisi sana tofauti na nilivyotegemea, nilimlaghai na penzi zito mpaka likampofusha, likamlewesha akili yake ikawa chakari. Mke wake ndio alitaka kuwa kigagula lakini kabla hajatokea tayari nilishaiweka mikononi chipu ya Darubini. Nasubiri maelekezo yenu” Yule Binti aliongea kwa wasiwasi huku akiangalia huku na huku kama mtu asiyejiamini licha ya kuwa pekee yake. Hakutaka mtu yeyote ajue yale aliyokuwa akizungumza kwenye simu.

“ Mfanye haraka kabla hajarudi, maana ninauhakika atarudi muda mfupi ujao atakapogundua hana ile chipu. Sawa nawasubiri” Yule Binti aliongea kisha akakata simu. Akaichukua bahasha akaiweka ile chipu kisha akaiingiza ndani ya begi lake la nguo. Kisha akatoka kwenda sebuleni kuendelea na shughuli zake.

Basi Sajenti hakutaka kupoteza muda, hapohapo aliondoka upesi na kwa umakini wa ajabu aliingia sebuleni bila ya Yule binti kumuona wakati huo Yule binti alikuwa akipiga deki, kilichomshtua Yule binti ni mlango wa sebuleni kujigonga lakini alipoutazama aliukuta umefungwa.

ITAENDELEA

OFA hii isikupite!

MLIO WA RISASI HARUSINI

Kitauzwa Kwa Tsh 10,000 badala ya Tsh 15,000.

Mwisho WA OFA ni tarehe 14/10/2021

TUMA PESA KWA NAMBA

0693322300
Airtelmoney
Robert Heriel
 
WAKALA WA SIRI 14
Mtunzi; Robert Heriel
0693322300

ILIPOISHIA
Basi Sajenti hakutaka kupoteza muda, hapohapo aliondoka upesi na kwa umakini wa ajabu aliingia sebuleni bila ya Yule binti kumuona wakati huo Yule binti alikuwa akipiga deki, kilichomshtua Yule binti ni mlango wa sebuleni kujigonga lakini alipoutazama aliukuta umefungwa.

INAENDELEA

Aliutazama kwa kitambo kama mtu mwenye mashaka lakini baadaye aliupuuzia. Kumbe kishindo cha mlango kilisababishwa na Sajenti alivyoingia na kuurudishia ule mlango.

Sajenti kwa upesi bila ya kupoteza muda, huku akijua kuwa wale watu waliokuwa wanaongea na Yule binti kuwa wapo njiani wanakuja hivyo wasije wakafika kabla hajaitia ile chipu mikononi mwake. Akafika kwenye ule Mlango wa chumba cha Yule msichana,. Looh! Haikuwa rahisi kama alivyotarajia, alikuta mlango umefungwa kabisa. Aling’ata meno kwa hasira, huku akijiona kama Yule msichana kamzidi ujanja.

Sajenti alirudi kwa kunyata mpaka sebuleni bila ya kuonekana, kama paka anayewinda alipeleka macho yake huku na huku akitafuta mahali ilipofunguo. Aliziona funguo nyingi juu ya meza ya kulia chakula. Akili yake ikamuambia pale hakuna funguo za kile chumba cha Yule msichana. Alitazama zaidi na zaidi lakini hakuona dalili ya kuwepo kwa funguo za kile chumba. Sasa akili yake ilikaribia kukata tamaa, mwili ulianza kupata joto, aliona kama anaenda kushindwa kuipata ile chipu ya darubini. Akili yake ikamuambia amfuate Yule binti na kumuweka chini ya ulinzi aseme wapi ilipofunguo ya chumba chake. Kabla hajafikia maamuzi akiwa anawaza jambo hilo punde simu ya Yule msichana iliita. Sajenti alishtushwa sana na sauti ya mlio wa ile simu. Sijui nini kilimshtua, labda akili yake iliamua kumshtua tuu.

Yule binti aliacha kupiga deki akaenda kupokea simu, kumbe simu ilikuwa juu ya meza ya kuwekea luninga. Sajenti alishtuka kuona funguo kwenye meza yakuwekea luninga, kumbe ile funguo ya kile chumba Yule binti aliiweka pamoja na simu. Basi Yule binti baada ya kupokea simu aliongea kwa sauti ya chini kisha akatoka nje. Sajenti kagundua kuwa mule ndani hakuwa binti pekee yake, kwani kama angekuwa pekee yake asingeongea kwa sauti ya chini. Yule msichana alitoka nje na hapo hapo Sajenti akaitumia hiyo nafasi kuichukua ile funguo. Moja kwa moja akaenda kwenye kile chumba cha Yule msichana, akafungua upesi bila kupoteza muda. Akafungua lile begi na kuchukua ile chipu. Moyo wake ulifurahi sana, ile chipu ilikuwa ni ukombozi wake, ilikuwa ndio funguo la gereza lake ambalo limemfanya kuwa mfungwa asiyehuru.

Baada ya kuichukua akaondoka kuelekea sebuleni. Punde akiwa sebuleni akasikia Geti la nje likifunguliwa, hapo akaenda kuchungulia dirishani. Alimuona Yule binti akiwa anaingia getini akifuatana na mwanaume mweusi. Yule mwanaume alibaki pale getini kisha Yule msichana akaingia ndani. Sajenti alijificha kumpisha Yule msichana apite bila ya kumuona. Kisha kwa upesi akarudi dirishani kuchungulia; alimuona Yule mwanaume mweusi akichungulia mara kwa mara nje ya geti. Uso wa Yule mwanaume mweusi ulikuwa na wasiwasi ulioficha hila na uovu wa siku nyingi.

Kitambo kidogo Yule Msichana alitoka, Sajenti akajibanza bila kuonekana. Kisha akawahi dirishani kuwaangalia; alimuona Yule mwanaume mweusi akitabasamu baada ya kumuona Yule msichana akija. Yule msichana baada ya kufika na kusimama mbele ya Yule mwanaume mweusi, aligeuka nyuma kutazama dirisha la sebuleni, hali iliyomfanya Sajenti kujificha kwa haraka kama umeme huku akipumua kwa pupa mithili ya panya aliyekoswa na mtego. Baadaye Sajenti alichungulia tena, akamuona Yule binti akiendelea kuangalia huku na huko kama mtu anayehakikisha kuwa hakuna anayemuona. Baadaye Yule binti alipohakikisha hali ni shwari akafungua ile kanga yake akaitoa ile bahasha yenye chipu akamkabidhi Yule mwanaume mweusi; Wote wakatabasamu, kisha Yule mwanaume mweusi akaingiza mkono kwenye ile bahasha akatoa ile chipu ya darubini ya maabara kuu ya Boreti. Sajenti akatabasamu, kitendo cha Sajenti Warioba kuipata ile chipu ya Darubini kilifufua upya nguvu ya uhai katika mifupa yake; tumaini lililokuwa limepotea likarejea.

************************************************

ITAENDELEA

OFA hii isikupite!

MLIO WA RISASI HARUSINI

Kitauzwa Kwa Tsh 10,000 badala ya Tsh 15,000.

Mwisho WA OFA ni tarehe 14/10/2021

TUMA PESA KWA NAMBA

0693322300
Airtelmoney
Robert Heriel
 
WAKALA WA SIRI 15
Mtunzi; Robert Heriel
0693322300

ILIPOISHIA
Baadaye Yule binti alipohakikisha hali ni shwari akafungua ile kanga yake akaitoa ile bahasha yenye chipu akamkabidhi Yule mwanaume mweusi; Wote wakatabasamu, kisha Yule mwanaume mweusi akaingiza mkono kwenye ile bahasha akatoa ile chipu ya darubini ya maabara kuu ya Boreti. Sajenti akatabasamu, kitendo cha Sajenti Warioba kuipata ile chipu ya Darubini kilifufua upya nguvu ya uhai katika mifupa yake; tumaini lililokuwa limepotea likarejea.

************************************************

INAENDELEA

Usiku wa saa sita, Fernanda aliamka kutoka usingizini; hakuona haja ya kuendelea kulala kwa raha zote ilhali yupo katika majanga. Kuendelea kulala ni kuwapa adui zake nafasi ya kumuangamiza jambo ambalo hakutaka litokee. Akaingia bafuni akakoga kisha akarudi chumbani kujiandaa. Kutokana hakuwa na nguo zingine alizobeba, alivaa nguo zilezile alizokuja nazo. Alijitazama kwenye kioo akaridhishwa na jinsi alivyojipodoa. Ni kweli kuwa alikuwa amependeza licha ya kuwa alivaa nguo zilezile. Uzuri wake ulichangia kwa sehemu kubwa. Fernanda alikuwa mwanamke mzuri kupita kiasi.

Alitoka nje ya ile lodge, kisha akaende mahali alipoegesha gari lake, akiwa anatembea alikagua huku na huku kuangalia usalama wake. Hali bado ilikuwa shwari kabisa, hakuona dalili yoyote ya hatari ingawaje haikumfanya aamini eneo lile ni salama kwa asilimia zote, hivyo Bastola yake aliiweka mahali rahisi ambako kama hatari ikitokea angeweza kuichukua kwa haraka. Aliingia ndani ya gari kisha akaondoka eneo lile na kupotea katika barabara za Bagamoyo akiitafuta barabara inayoenda Dar es salaam.

Akiwa njiani alipata wazo la kwenda kwa Meja Jenerali, Mr Venance Kagoda, ambaye alikuwa akiishi na familia yake maeneo ya Masaki. Kutokana na mwendokasi aliokuwa akiendesha gari haikuchukua saa moja tayari alikuwa kashaingia Bunju, Dar es salaam. Ilimchukua dakika arobaini kufika maeneo ya Masaki akiitafuta nyumba aliyokuwa anaishi Meja Venance Kagoda. Haikumchukua muda akaiona, ilikuwa nyumba ya kisasa iliyozungushiwa uzio wa tofali zilizopakwa chokaa. Ndani yake zilikuwepo bustani za maua mazuri na miti kadhaa ya hapa na pale iliyozidisha uzuri wa mandhari ile.

Fernanda aliendesha Gari yake polepole akapita Geti la ile nyumba ya Meja Venance Kagoda akaenda kusimamisha gari mbele umbali wa hatua mia moja, akaegesha gari pembezone kabisa mwa barabara. Kisha akachungulia nyuma na mbele kuona usalama wa eneo lile. Bado eneo lilikuwa tulivu, nyumba za eneo lile zilikuwa kimya zikiwaka taa, huku wadudu wa usiku wakisherekea kwa sauti za nyimbo walizozijua wao. Fernanda akashuka, hapo akiwa kava koti la rangi ya ugoro, kichwani akiwa kavaa Kapero, alitembea kwa tahadhari mwendo wa kilimbwende kama paka. Alipotembea hatua hamsini akiwa nusu kwa nusu kati ya alipoegesha gari lake na ile nyumba ya Meja Venance, alishtushwa na sauti ya gari lililokuwa linakuja upande wa nyuma alipoliacha gari lake.

Kwa upesi alikimbia akajificha kwenye mti upande wa kulia wa ile barabara. Ile gari iliyokuwa inakuja ikasimama kule alipoegesha gari lake. Moyo wa Fernanda ukaanza kupiga kwa hofu, huku mwili ukipandisha joto la woga. Fernanda akachungulia kule liliposimama lile gari, akaona wanaume wawili wakishuka kwenye lile gari. Wanaume wale walivalia nguo nyeusi, mikononi wakiwa wamebeba bastola na mmoja alikuwa ameshika kurunzi akimulika gari la Fernanda. Wakalisogelea gari la Fernanda kwa tahadhari kubwa wakiwa wamelielekezea bastola walizokuwa wamezishikilia.. Yule mwanaume mwenye kurunzi alipomulika kwa ndani hakuona mtu, akajaribu kufungua milango ya gari lakini hakuweza kwani ilikuwa imefungwa. Hapo akageuka na kumulika mbele alipokuwa amejificha Fernanda, ule mwanga wa kurunzi ulimkosa kosa Fernanda, kama sio Fernanda kujificha kwa upesi basi wangeweza kumuona, lakini Fernanda alikuwa mwepesi kama chui. Hata hivyo moyo wake ulipiga kite kwa hofu ya kutaka kuonekana.

Wale wanaume wawili ambao mpaka muda huo Fernanda alikuwa hawaelewi ni akina nani walianza kumulika mulika upande huu na upande huu wakimtafuta aliyeegesha lile gari pale. Waligawana upande, mmoja akaende upande aliopo Fernanda, mwingine akaenda upande lilipokuwa linaelekea gari la Fernanda. Mwanaume mwenye kurunzi ndiye aliyekuwa anakuja kule alipokuwa kajificha Fernanda. Mwanga wa Kurunzi ulikuwa ukizichanga mirindimo ya moyo wa Fernanda, Yule mtu alikuwa akimulika mulika bila mpangilio, mara juu mara chini, mara kushoto na kulia hali iliyowashtua mbwa wa eneo lile na kuwafanya waanze kubweka. Yule mwanaume tayari alikuwa amekaribia pale alipokuwa amejificha Fernanda, ni kama hatua tano tuu. Fernanda aliitoa bastola yake mafichoni akaishikilia mkononi tayari kujihami na kushambulia.

Yule Mwanaume mwenye kurunzi alipunguza hata zake kama mtu aliyehisi kuwa eneo lile lina mtu, polepole akawa anasogea.. anasogea mpaka usawa wa alipojificha Fernanda, kwa upesi akageuka kulia akimulika na kurunzi yake pale alipokuwa amejificha Fernanda lakini hapakuwa na mtu. Fernanda alikuwa kahama eneo lile muda mfupi tuu uliopita usiozidi sekunde thelasini. Mtu Yule alipoona hakuna mtu akarudi kule alipokuwa mwenzake.

Kisha wale wanaume wawili wakapanda gari lao wakaondoka, wakipita palepale alipokuwepo Fernanda,

Fernanda alishangaa kusoma maandishi yaliyoandikwa kwenye lile gari yaliyosomeka TK SECURITY, kumbe walikuwa walinzi wa kampunzi za Tk Security. Fernanda alidhani wanaume wale walikuwa ni watu wabaya waliokuwa wakiwasaka kwa udi na uvumba. Fernanda akaondoka pale mtini alipokuwa amejificha akatembea kama hatua ishirini akawa amefika kwenye nyumba ya Meja Venance, nyumba ilikuwa giza, hata taa za nje zilikuwa hazijawashwa; Fernanda akapanda juu ya ukuta kama paka kwa tahadhari, kisha alipofika juu ya ukuta akaziruka zile nyaya za umeme na kutokea upande wa pili ndani ya ukuta. Moja kwa moja akaisogelea ile nyumba ya Meja Venance ambayo ilikuwa na giza la kutisha lisilo na dalili ya uhai wowote.

Akazunguka kwa nyuma, kisha akachungulia ndani Kupitia dirisha la kioo lakini giza lilimfanya asione chochote, akapasua kioo na kitako cha bastola, alafu akapitisha mkono akafungua dirisha na kuingia ndani. Alisimama kwa muda akijaribu kuzoea giza la mule ndani, macho yake yalipozoea giza la mule chumbani akaiona kitanda kilichotandikwa shuka lenye midoli midoli na mto wake, juu ikiwepo chandarua iliyokuwa imening’inia. Pembeni ya kitanda kulikuwepo na kijikabati kidogo na pembeni yake ilikuwepo meza na kiti cha watoto cha kusomea, hapo akajua kuwa chumba kile alikuwa akilala mtoto mdogo mwenye umri usiozidi miaka kumi, Hakuona la maana ambalo lingemsaidia, akaufuata mlango wa kile chumba akaufungua, ulikuwa upo wazi, akatoka kuifuata korido iliyokuwa ikimtazama, akakata kushoto bado giza likiwa limeshamiri eneo lile. Upande wake wa kulia ulikuwepo mlango uliokuwa umefungwa, akaenda kushika kitasa cha mlango ule akakitekenya ukafunguka, akatembea polepole huku akiyapa masikio yake umakini wa kuweza kusikia chochote ambacho kingetoa sauti. Fernanda akawasha taa na kufanya giza likimbie na kukiacha chumba kile kwa aibu, huku mende wakikimbia huku na huku kushangaa ugeni ule wa dharura ambao hawakuutegemea.

Sasa Fernanda aliweza kukiona vizuri chumba kile. Kilikuwa chumba kikubwa zaidi ya kile cha awali. Aliona kitanda kikubwa kabisa cha kisasa, pembeni ya kile kitanda kulikuwa na sofa la mtu mmoja, mbele ya sofa kulikuwa na meza ndogo ya kioo, pembeni kabisa lilikuwepo sofa jingine dogo lililotazamana na ile meza. Upande wa pili ilikuwepo Luninga bapa kubwa ya inchi arobaini na nne iliyofungwa ukutani kwa ustadi wa hali ya juu. Chini ya ile Luninga ilikuwepo seti ya sabufa za muziki za kisasa kabisa. Kwenye pembe kabisa karibu na Ile Luninga bapa Lilikuwepo Jokofu kubwa kiasi, kilikuwa chumba kikubwa kilichokamilika.

Upande mwingine wa chumba kile ulikuwepo mlango tofauti na ule mlango alioingilia Fernanda. Akili yake ikamtuma aufuate ule mlango, akatembea muda huu alikuwa na wasiwasi mno, alishikilia bastola yake akasonga polepole kwa umakini wa hali ya juu, akatekenya kitasa cha ule mlango lakini haukufunguka, ulikuwa umefungwa. Hiyo ikaongeza hamu ya kutaka kujua ndani ya kile chumba kuna nini. Fernanda akaangaza macho yake huku na huku akikagua chumba kile kama mtu anayetafuta jambo Fulani, macho yake yakatua ilipodroo ya kile kitanda. Upesi akaenda kwenye ile droo akaifungua, kwa bahati ilikuwa wazi. Alipoifungua macho yake yalikutana na makarabrasha na bahasha ya kaki, akapekua pekua kwenye yale makarabrasha lakini hakuona la maana, kisha akaichukua ile bahasha ya kaki, nayo akaipekua hakukuta cha maana, alipokuwa akirudisha yale makarabrasha na bahasha alishtuka kuona kitu mfano wa chipu yenye muundo wa funguo ikianguka pale chini. Akaiokota ile chipu, akaikagua, kisha akageuka kuutazama ule mlango uliokuwa umefungwa, akaachia tabasamu kama mshindi.

Alafu akaufuata ule mlango akiwa kabeba ile chipu, alipofika kwenye ule mlango akaiingiza ile chipu kwenye ule mlango, akaachia tena tabasamu mlango ulipofunguka. Ndani alipokelewa na harufu kali ya vumbi, hii ilionyesha kuwa chumba kile kilikuwa na muda mrefu hakijafunguliwa. Aliiona korido iliyonyooka moja kwa moja mpaka kilipo choo na bafu, Fernanda akatembea kufuata kile choo na bafu alipofika alishangaa kuona mlango mwingine mkono wa kulia, akaghairi uelekeo wa chooni na bafuni, akaugeukia ule mlango uliokuwa mkono wa kulia, akakitekenya kile kitasa lakini haukufunguka, Fernanda akashusha pumzi kama mtu aliyechoka. Akatazama kwa umakini ule mlango alafu akajaribu kuingiza ile chipu lakini mlango haukufunguka, akajaribu kukorokocha lakini bado mlango ukagoma, Hiyo ilimfanya akate tamaa. Akapata wazo la kuigeuza ile chipu na kuiingiza kinyume, alipoiingiza alishangaa kuona mlango ukifunguka. Hiyo ikamfanya atoe tabasamu la kujipongeza. Akaingia ndani ambapo alipokelewa na giza totoro na harufu ya uvundo, Fernanda alipapasa ukutani mpaka alipoikuta swichi ya kuwashia taa ya chumba kile. Alipowasha chumba chote kilikuwa uchi mbele ya macho yake. Kilichukuwa chumba cha kubadilishia nguo, kilichokuwa na kabati kubwa la nguo pamoja na Birika la kuoshea uso na kioo cha kujiangalizia. Upande wa nyuma ya mlango Fernanda aliona nguo chafu zilizokuwa zinatoa harufu mbaya ya uvundo, harufu ile ilikuwa inakera jamani mpaka akawa anahisi kutapika,

Bila kupoteza muda Fernanda akalisogelea lile kabati la nguo na kuanza kuzipangua pangua zile nguo, kama mtu anayetafuta kitu Fulani. Hapo akaona Sare ya kijeshi akajua ilikuwa ni sare ya Meja Venance kagoda, akaichukua ile sare na kuanza kuipekua lakini hakuona la maana, aliendelea kupekua karibu nguo zote bila mafanikio ya namna yoyote yale. Sasa nguo zote zilikuwa zimetapakaa pale chini, kabati lilikuwa tupu, macho ya Fernanda yalikereka kuona mende wakikimbia kimbia huku wengine wakiruka na kumparua na kucha zao kwenye mikono yake. Kama kuna wadudu ambao Fernanda alikuwa hawapendi basi ni mende, alichukizwa na tabia za wadudu hao, lakini muda ule ilimpasa ajikaze tuu.

Fernanda akaachana na lile kabati baada ya kuona halina maana yoyote ile. Akaangaza macho yake huku na huku ndani ya kile chumba, akakinaiwa na kile chumba kwani hakikuwa na jambo lolote la maana zaidi ya kero ya ile harufu ya uvundo, Fernanda akaamua kutoka kwenye kile chumba, alipofika mlangoni ili atoke, akili yake ikamtuma azikague zile nguo zinazotoa Uvundo, aone harufu ile inatokana na nini. Akafuata akili yake, akaenda nyuma ya ule mlango wenye zile nguo zenye harufu inayotapisha. Akaziengua pale juu, zilikuwa ni Suruali ya Kijeshi na tisheti ya kijeshi pamoja na koti lake.

Fernanda alishtuka kuona nguo zile zikiwa na damu nzito iliyooza inayotoa mafinyo finyo, Fernanda alivozichangua zile nguo harufu ndio ilizidi kuongezeka maradufu; akashika pua yake huku akipata shida kupumua. Kwa kinyaa na kujilazimisha aliibeba ile suruali juu chini kisha akaanza kuikung’uta ili kama kuna vitu vipo mfukoni viweze kuanguka chini. Alipokuwa akikung’uta alishuhudia funza wakianguka chini ya sakafu kama kumbikumbi, wale funza walikuwa wamenona haswa, Fernanda alipoona ile suruali haina la maana, akachukua lile koti la kijeshi, nalo akalikung’uta kwa nguvu mara kadhaa, punde alishtushwa kusikia kitu cha chuma kikianguka sakafuni kikitokea katika lile koti; lakini hakukiona kimeangukia wapi. Akaacha kulikung’uta na kuanza kukitafuta hicho kilichoanguka, aliangaza macho yake huku na huku, upande huu na upande huu lakini hakuweza kukiona kitu hicho ambacho alikisikia kimeanguka wakati akiwa anakung’uta lile koti. Fernanda akahisi huenda alisikia vibaya, akapuuza lakini kabla hajaendelea kukung’uta alihamaki kukiona kitu mfano wa funguo karibu na miguu yake, akajua ndio kile kitu alichokisikia kikianguka,

ITAENDELEA

OFA hii isikupite!

MLIO WA RISASI HARUSINI

Kitauzwa Kwa Tsh 10,000 badala ya Tsh 15,000.

Mwisho WA OFA ni tarehe 14/10/2021

TUMA PESA KWA NAMBA

0693322300
Airtelmoney
Robert Heriel
 
WAKUU MKIWA MNAENDELEA KUBURUDIKA NA RIWAYA HII, NAPENDA KUWATANGAZIA OFA KABAMBE YA RIWAYA YA "MLIO WA RISASI HARUSINI"

WAHI OFA UPATE UHONDO
zodo.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom