Rais wa Afghanistan kakimbia nchi!

Nyani Ngabu

Platinum Member
May 15, 2006
94,114
121,723
Rais wa Afghanistan, Ashraf Ghani, amekimbilia Tajikistan, kwa mujibu wa Al Jazeera!

Taliban wameshinda!

Taliban wamechukua nchi!

Mwezi mmoja uliopita, Rais wa Marekani alisema bila kumung’unya maneno kuwa Taliban kuchukua nchi hakuwezekani kwa sababu jeshi la Afghanistan liko imara.

Hahahaa. Well, tayari Taliban wameshachukua nchi na Rais wa Afghanistan kala kona.

===

Rais wa Afghanistan Ashraf Ghani ameikimbia nchi yake leo jioni baada ya wanamgambo wa Taliban kuuzingira mji mkuu wa Kabul.

Maafisa wawili wa serikali ambao hawakutaka majina yao kutajwa wameliambia shirika la habari la Associated Press kuwa Ghani ameondoka Afghanistan na inaarifiwa amekimbilia taifa jirani la Tajikistan.

Mkuu wa Baraza la Maridhiano ya Taifa nchini Afghanistan Abdullah Abdullah pia amethibitisha habari hizo kupitia mkanda wa video.

Kuondoka kwa Ghani kunatoa taswira halisi ya uwezekano wa kundi la Taliban kuchukua madaraka nchini Afghanistan wakati wowote kuanzia sasa.

Wapiganaji wa kundi hilo waliingia kwenye viunga vya pembezoni mwa mji mkuu wa Kabul leo Alfajiri baada ya kupata mafanikio makubwa katika siku za karibuni kwa kuikamata miji mingi nchini humo.
 
Biden alikurupuka kuondoa majeshi sasa imekula kwake. Halafu wamechukua nchi kirahisi sana sehemu nyingi hilo jeshi la Serikali hata kupigana hawakupigana waliishia kukimbia na kwenye makambi mengi hawakuwa na chakula.
Wamarekani sijui walijenga jeshi gani tu huko Afghanistan!

Majamaa hayajakumbana na resistance yoyote ile!

Shame.
 
Biden alikurupuka kuondoa majeshi sasa imekula kwake. Halafu wamechukua nchi kirahisi sana sehemu nyingi hilo jeshi la Serikali hata kupigana hawakupigana waliishia kukimbia na kwenye makambi mengi hawakuwa na chakula.
Serikali ile ilishakua mufilisi
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Biden kaenda Camp David atakuwa huko hadi Jumatano na wapambe wake kudeal na hizi crisis tatu. COVID-19, Afghanistan na Wazamiaji ambao wanazidi kumiminika mpakani na Mexico.
Wamarekani sijui walijenga jeshi gani tu huko Afghanistan!

Majamaa hahaha kum bana na resistance yoyote ile!

Shame.
 
Afghanistan
Taliban fighters pose on the back of a vehicle in the city of Herat, west of Kabul, Afghanistan, Saturday, Aug. 14, 2021, after they took this province from Afghan government. The Taliban seized two more provinces and approached the outskirts of Afghanistan’s capital. (AP Photo/Hamed Sarfarazi)
 
Nchi yoyote marekani akitia guu lake tu kwisha. Ni heri taliban waongoze nchi, na amani itakuwepo.
Nmemuonea huruma mama mmoja alikuwa waziri wa elimu ila anasema kutokana na hatu hiyo ya rais kukimbia nchi itamgharimu yeye mama kwa kuwa aliiunga mkono serikali.

Taliban siyo wabaya ila mibaya ni ile misimamo yao mfano wanawake hawatakiwa hata kwenda shule
 
Mhh...

Kile kikosi cha wanajeshi 5000 wa marekani waliotumwa leo kwenda Afghanistan kuwaokoa diplomats sio kwamba kimeshiriki kufanya hujuma kweli?

They camouflage as American soldiers kumbe ndio mataliban wenyewe
Smooth transition of power,wakienda kuwahakikishia Taleban kuingia afresh na kumtisha Ghan akimbie nchi Ili asife .

Hiyo means imetoa fursa kwa wageni kuondoka na kupunguza maafa kwa raia,si unaona wataleban wameingia mjini kushika doria Ili uporaji usiwe mkubwa.
 
Back
Top Bottom