The Sunk Cost Fallacy 2

JF-Expert Member
Nov 8, 2022
8,757
10,218
My Take
Mlisema Samia ameuza Bandari Kuna bango lenu hili hapa, ni spana tuu Kwa kwenda mbele.

=======

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea mfano wa Hundi kama ...jpg

Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imevunja rekodi kwa kutoa jumla ya Shilingi za Kitanzania 153.9 Bln kama gawio kwa Serikali kuu kwa mwaka wa fedha Mwaka 2023/2024.

Gawio hilo limeifanya TPA, kuongoza kwa kutoa gawio kubwa zaidi kuliko taasisi zote za Serikali hapa nchini, “....na haya ni matunda ya uwekezaji uliofanywa katika Bandari ya Dar es Salaam”, amasema Mkurugenzi Mkuu, Bw. Prasduce Mbossa.

======


“TPA (Mamlaka ya Bandari Tanzania) mwaka jana (2023) nina hakika kiwango chenu hakikuwa hiki, lakini kwa mageuzi yaliyotokea bandarini mmeweza kufikia kiwango hiki na mwakani tunatarajia kiwango kikubwa zaidi pengine mara mbili yake ya hiki mlicholeta leo, hakuna sababu kama mtaendesha bandari na sekta iliyopo pale na pale kuna watu wawili ambao tumeshawaruhusu.

Mmeomba maombi zaidi lakini hata wale wawili mwakani mnaweza kuleta mara mbili ya hiki kiwango na huko ndiko tulikuwa tunaelekea ndugu zangu . Wale waliopiga kelele mama kauza bahari sijui mama kauza bandari mama kauza nini mama kauza..mauzo yale faida yake ni hii hapa leo, na huu ni mwanzo tutatarajia kutapata faida kubwa zaidi kwa bandari zetu zote kubwa ambazo zipo ndani ya nchi”- Dkt. Samia.

Pia soma:

- Rais Samia unadanganywa, DP World hajaleta tija yoyote kwenye Bandari ya Dar es Salaam

- TPA imesifiwa sana kwa kutoa Gawio la Bilioni 153.9 wakati 2018/19 Gawio lilikuwa Bilioni 480. Je, Rais Samia kasahau?

- Ufafanuzi kuhusu Gawio la Tsh. Bilioni 153.9 lililotolewa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania TPA kwa Serikali
 
Ndio manake na ndio maana ya kuamua kupiga Mnada

..mbona bandari ya Mombasa wamekuwa wakifanya vizuri kutuzidi bila kujiuza kwa Dp World?

..kuna uwekezaji mkubwa ulifanyika wakati wa Jpm kwa kutumia mkopo wa World Bank je uwekezaji huo amechangia kiasi gani?

..uwekezaji ambao tuliambiwa Dp world atafanya haukuwa mkubwa kusema Tanzania haiwezi kukusanya nguvu yenyewe.

..maamuzi yameshafanyika kwa hiyo hakuna namna tena. Tuombe tu mambo yasije kuharibika mbele ya safari.
 
..mbona bandari ya Mombasa wamekuwa wakifanya vizuri kutuzidi bila kujiuza kwa Dp World?

..kuna uwekezaji mkubwa ulifanyika wakati wa Jpm kwa kutumia mkopo wa World Bank je uwekezaji huo amechangia kiasi gani?

..uwekezaji ambao tuliambiwa Dp world atafanya haukuwa mkubwa kusema Tanzania haiwezi kukusanya nguvu yenyewe.

..maamuzi yameshafanyika kwa hiyo hakuna namna tena. Tuombe tu mambo yasije kuharibika mbele ya safari.
Hawafanyi vizuri kama unavyosema wewe, wana underperform kulingana na uwezo wa Bandari Yao.

Pili sio sawa kulinganisha Kenya na Tanzania, wale ni business minded siku nyingi huku Tanzania ni wezi na wabinafsi.

Tatu hata nao wanatafuta wawekezaji vile vile
 
Mh yaani hao DP world ndiyo kwanza wametia timu mama tiyari keshahesabu faida?

Hiyo faida kama ipo ni ya TPA yenyewe na ni ushahidi kuwa tulikuwa hatuhitaji DP world kuiendesha hiyo bandari. Sisis wenyewe tunaweza
DP World walianza kitambo, makabidhiano rasmi ndio yamefanyika mwezi Jana ila toka mwaka Jana DP World wapo kazini, waulize importers.
 
Back
Top Bottom